KENZY
JF-Expert Member
- Dec 27, 2015
- 32,529
- 76,691
Waswahili wanasema "Kata mti panda mti!".
Huu msemo usiulete kwenye mapenzi utakuja kufa ulimi nje!.
Baada yakubwagana na mpenzi wangu chapchap kuuponya moyo,roho na nafsi yangu nikaamua kutafuta mpenzi harakaraka ili ku cover nafasi iliyoachwa wazi!.
alikuwa binti fulani hivi ndembendembe, kuanzia juu mpk chini mwili wake ulihubiri uzuri ama ufundi stadi wa muumbaji!.
muhuni wa watu nikatopea penzini hapo nikiwa na siku tatu tu toka nibwagane na mchuchu wa awali!.
Sasa penzi jipya likiwa na mwezi tu, nilikuwa siambiliki tayari nilikuwa nimezama nginjanginja mtoto alinidatisha na mwili wake laini halafu kitandani alikuwa na miondoko yakiufundi ukizubaa unaweza kupoteza uhai kitandani!!.
Siku isiyona jina sina hili wala lile nikafuma li sms la mahaba kwenye simu yake!!, nikaona isiwe tabu kabla sijapiga kelele wacha nifatilie.
walahi walahi katika kufatilia nikakuta kumbe kuna njemba linamfaidi na mbaya zaidi nilipata chati yao demu kanipondea kwa mshikaji ati wananiita mimi "Karungu yeye!" mara sijui mapenzi ati nampakampaka mate tu kama litoto linalojifunza kunyonya!.
wakati nayasoma hayo ye alikuwa amelala fofofo, machozi fulani hivi yakawa kama yanataka kunitoka lkn nikajikaza!. hawakuishia hapo kumbe walikuwa wanajua niliachwa na ndo nikamtafuta yeye sasa walivyokuwa wanahadithiana kuhusu mimi kuachwa kwangu ati
"ndo maana aliachwa akakonda kama ndama aliekosa lishe!"
hasira zilinipanda nikatamani hata niimeze simu yake ili akiamka hata asiione tena!. hii ndo hatua ilinifanya mpk nimkumbuke mpenzi wangu wa awali alivyokuwa mnyenyekevu,mcheshi na mzuri, nilitamani aje anitoe kwenye hii hali lkn isingewezekana maana nayeye alikuwa ashapata mpenzi mwengine!.
Niliamua kutoka kwenye hayo mahusiano na sikuamua kuanzisha tena mahusiano haraka haraka maana nilijiona kabisa kama huku nimeitwa karungu yeye huko niendako ningeitwa nani..??
Hivyo ndugu zangu kama utaachana na mtu usitumie haraka kupata mpenzi mwengine watu hawana adabu!, tulia jitafutie mpenzi wako taratibu.
Huu msemo usiulete kwenye mapenzi utakuja kufa ulimi nje!.
Baada yakubwagana na mpenzi wangu chapchap kuuponya moyo,roho na nafsi yangu nikaamua kutafuta mpenzi harakaraka ili ku cover nafasi iliyoachwa wazi!.
alikuwa binti fulani hivi ndembendembe, kuanzia juu mpk chini mwili wake ulihubiri uzuri ama ufundi stadi wa muumbaji!.
muhuni wa watu nikatopea penzini hapo nikiwa na siku tatu tu toka nibwagane na mchuchu wa awali!.
Sasa penzi jipya likiwa na mwezi tu, nilikuwa siambiliki tayari nilikuwa nimezama nginjanginja mtoto alinidatisha na mwili wake laini halafu kitandani alikuwa na miondoko yakiufundi ukizubaa unaweza kupoteza uhai kitandani!!.
Siku isiyona jina sina hili wala lile nikafuma li sms la mahaba kwenye simu yake!!, nikaona isiwe tabu kabla sijapiga kelele wacha nifatilie.
walahi walahi katika kufatilia nikakuta kumbe kuna njemba linamfaidi na mbaya zaidi nilipata chati yao demu kanipondea kwa mshikaji ati wananiita mimi "Karungu yeye!" mara sijui mapenzi ati nampakampaka mate tu kama litoto linalojifunza kunyonya!.
wakati nayasoma hayo ye alikuwa amelala fofofo, machozi fulani hivi yakawa kama yanataka kunitoka lkn nikajikaza!. hawakuishia hapo kumbe walikuwa wanajua niliachwa na ndo nikamtafuta yeye sasa walivyokuwa wanahadithiana kuhusu mimi kuachwa kwangu ati
"ndo maana aliachwa akakonda kama ndama aliekosa lishe!"
hasira zilinipanda nikatamani hata niimeze simu yake ili akiamka hata asiione tena!. hii ndo hatua ilinifanya mpk nimkumbuke mpenzi wangu wa awali alivyokuwa mnyenyekevu,mcheshi na mzuri, nilitamani aje anitoe kwenye hii hali lkn isingewezekana maana nayeye alikuwa ashapata mpenzi mwengine!.
Niliamua kutoka kwenye hayo mahusiano na sikuamua kuanzisha tena mahusiano haraka haraka maana nilijiona kabisa kama huku nimeitwa karungu yeye huko niendako ningeitwa nani..??
Hivyo ndugu zangu kama utaachana na mtu usitumie haraka kupata mpenzi mwengine watu hawana adabu!, tulia jitafutie mpenzi wako taratibu.