JPM alikuwa na msimamo gani kuhusu UN?
nasikitika kukutaarifu kuwa nafasi zote za uteuzi zimejaa.
Upuuzi mtupu! Tuna wizara husika, tuna ubalozi UN, kikao Cha UNGA Kiko kwenye calendar ya UN kila mwaka; walishindwaje kufanya maandalizi husika kupata mkalimani?! Wacha kutetea ujinga,
Bado uko hai wewe, kabla ya kupost taarifa yako ipitie kwanza.Wanabodi,
Baada ya Rais Samia kuhutubia Kikao cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa jijini New York nchini Marekani kwa kutumia lugha ya Kiingereza safi kilichonyooka, kuna wajinga fulani huku kwenye mitandao ya Kijamii, walimpongeza Rais Samia kwa kuhutubia kwa Kiingereza safi na huku wakimponda mtangulizi wake kuwa alikacha kukanyaga UN kwasababu ya lingua, kitu ambacho sii kweli.
Leo katika pita pita yangu, nikatembelea website ya UN, ndio nikakutana na hii kitu ambayo si wengi nyumbani tuliijua
Kumbe Rais Samia alitaka kuhutubia UN kwa kutumia lugha ya Kiswahili ila hii maana yake ni kuwa, sababu zilizomfanya mtangulizi wa Samia asikanyage UN kuhutubia, sio issues za lingua. Mimi mwenyewe, kama mwandishi wa habari wa kujitegemea, nimehudhuria vikao vya Baraza Kuu la UN mara kibao nikiwa na Ben na JK, kuna viongozi kibao, wanahutubia UN kwa kutumia lugha zao, kitu kinachofanyika ni kwa ubalozi wa nchi husika hapo UN, kuarifu rasmi Secretariat, na kulipia gharama za mkalimani, Rais wa nchi husika, atahutubia kwa lugha yake, halafu kutakuwa na wakalimani wanne, ambao wataitafasiri hiyo hotuba kwa zile lugha 4 rasmi za UN.
Hivyo hata kama ingekuwa ni kweli, Kiingereza cha kiongozi wa taifa lolote, hakijasimama kuhutubia UN kwa Kiingereza, angeweza kuhutubia kwa lugha nyingine yoyote, hivyo naomba kuwahakikishia wajinga hao, sababu za mtangulizi wa Samia kutohutubia UN, sio lugha.
Pili naomba kuchukua fursa hii kuwatangazia trends za hotuba ijayao ya Rais Samia kwenye 77 UNGA, itatolewa kwa lugha ya Kiswahili. Kitendo hicho, sio tuu kitaipaisha sana lugha ya Kiswahili kimataifa, bali rais Mama Samia, ataacha legacy ya kukipaisha Kiswahili, kukiingiza UN na kukifanya Kiswahili kuwa ni moja ya lugha kuu za dunia.
Hongera sana in advance rais wetu Mama Samia, Chief Hangaya kutaka kuhutubia UN kwa Kiswahili. Ukisikia uzalendo wa kweli kwa nchi yako, sasa ndio huu, huwezi kuwa mzalendo, Mkuu wa machifu wa kiasili, halafu uendelee kuhutubia kwa lugha za watu, uzalendo wa kweli ni pamoja na kuuenzi utamaduni wako, na lugha ndio kielelezo cha kwanza cha utamaduni wa jamii.
Kwa sasa Kiswahi tayari ndio lugha ya Afrika, Mama Samia atakipaisha kuwa moja ya lugha kuu za dunia.
2025 Tusifanye Makosa!.
Paskali.
Wachina na waarabu mbona wanatumiaga lugha zao?Watu wengine mnakaaga wapi, Yaani ufike katika Baraza la UN katika mkutano utumie lugha yako, si ungebaki nyumbani kwako
Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Ile mida ya hongera hizi ndio imewadia, her this time Mama atahutubia UNGA kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili, au tutaendeleza ile kasumba ya mkoloni aliotuachia?.Wanabodi,
Hongera sana in advance rais wetu Mama Samia, Chief Hangaya kutaka kuhutubia UN kwa Kiswahili. Ukisikia uzalendo wa kweli kwa nchi yako, sasa ndio huu, huwezi kuwa mzalendo, Mkuu wa machifu wa kiasili, halafu uendelee kuhutubia kwa lugha za watu, uzalendo wa kweli ni pamoja na kuuenzi utamaduni wako, na lugha ndio kielelezo cha kwanza cha utamaduni wa jamii.
Paskali.
Mkuu Alvin Slain, wewe mwenzetu umewahi kufika UN kwenye kikao cha Baraza Kuu, ukasikia viongozi wa mataifa wanahutubia kwa lugha gani?. Lugha rasmi za UN ni 6, English, French, Spanish Arabic, Chinese na Russian, je mataifa wasio tumia lugha hizo, jee viongozi wao wanahutubia UNGA kwa lugha gani?Watu wengine mnakaaga wapi, Yaani ufike katika Baraza la UN katika mkutano utumie lugha yako, si ungebaki nyumbani kwako
Sent from my SM-A013G using JamiiForums mobile app
Nilitaka niseme kitu ila nikakumbuka wewe ni mwanasheria, unamhukumu au kumsifia mtu kwa kukusudia. Hapo nikaishiwa cha kusema.
Lakini kuna Rais yeye hata hakukanyaga UNGA, katuma tu video iliyorekodiwa watu wakasikiliza ukumbini.
Kama Chief alikua na nia na alidhamiria kuhutubia kiswahili na hajatekeleza, tubirie siku akifanikisha hiyo adhma.
JPM alikua na mapungufu yake mengi tu, lakini ikifika jambo la kuonyesha msimamo wake alikua vizuri sana kwenye hilo eneo.
Bila kujali msimamo wake uko hasi au chanya ila alijitahidi kuhakikisha msimamo wake unajulikana bayana.
Binafsi napenda mtu mwenye maamuzi na kusimamia maamuzi yake ( shida yanapokua na matokeo hasi).@The Monk a real man is who stands alone
HBD Rais Samia!.Wanabodi,
Zawadi yangu kwa Birthday ya Mama nilipanga kumpa wiki ya mwisho ya October 2025,
Ili zawadi hii iwe na manufaa kwake, nikisubiri mpaka hiyo 2025, it might be a bit too little too late, kuna ubaya hiyo zawadi, kutolewa mapema mwaka huu ili iweze kutumika mwaka kesho?.
Zawadi yenyewe ni Salaam tuu za Birthday zenye ki parcel fulani!
HBD Mhe. Rais Samia kwa kutimiza miaka 64!, nakupongeza sana na kukuombea afya njema!.
Mwakani 2025 utakuwa unatimiza umri wa miaka 65 na 2030 utakuwa na umri wa miaka 70, hivyo zawadi yangu ya pekee kwako ni HII na kukusisitizia, sio lazima kuizingatia saana kivile, ila ni muhimu kuisikiliza na kujisikilizia kama na wewe pia uliambiwa kama nilivyoambiwa mimi, kwasababu yule YEYE, sometimes ana tabia na mtindo wa kuwaambia watu wake, kupitia kwa watu wengine!, hivyo just listen and try to make sense of this, a think about it, if makes any sense to you, ikitokea it doesn't make any sense to you, then dismiss it as just another set of crap!.
Ila ikitokea na wewe pia uliambiwa, but you are not very sure kama ni YEYE au ni yeye, then don't take a chance!, usipuuze!, maana hicho kitu chenyewe, is nothing compared!.
If this being the case, then tunakuomba sana sana sana, ututekelezee haya mambo tunayokulilia nayo tangu umeingia kwenye usukani, tekeleza tuu yale yaliyomo ndani ya uwezo wako, maana kusubiria post 2025, it might be too little too late!. Please Mama!.
Na ikitokea wewe hujaambiwa mpaka 2025 inaingia na hujawahi kuambiwa na mtu mwingine yeyote, then ipuuze HII itakuwa sio sauti yake YEYE bali itakuwa ni sauti ya yeye tuu ambaye sio YEYE!.
Hivyo endelea na ule mpango wako wa 2025!, na Watanzania wanaolitakia mema taifa letu hili, wote tutakuwa Tuko nyuma yako,
Tuko pamoja nawe,
Tuko nawe!.
Mungu Akubariki Sana!.
HBD Mamaa!.
Paskali