Utabiri wangu: Rais Samia awe makini na sakata la Mbowe, litamaliza kabisa kibali kidogo alichobakiwa nacho kwa Watanzania

Nchi hakika ina watu fulaniwachache wanaishi kwenye fikra za tofauti sana. Huyu anaamini kwamba mbowe anaweza geuza mstakabali kisiasa wa samia wakati mbowe hana uungwaji mkono na watanzania isipokua wachache wenye kasumba ya ubwanyenye na ukabila.
Sasa umeandika nini??
 

Unazungumzia watanzania gani mkuu. Naona unajiongeza mno. Mbowe hana lolote. Mwaka 2013 nilikuja Tz. Dr. Slaa wananchi wengi walimwelewa sana.
 
Wewe nakuonaga Kama mwehu msomi.
 
Kama - ni suala la mahakama kuamua kama ambavyo shauri lililopelekwa huko kusikilizwa.
Muda ndio utakamua kama ni kweli au si kweli.
Kitu kingine ni kuwa epuka kumuingiza Mh. Rais na Amir Jeshi Mkuu kwenye sentensi usizokuwa na uhakika nazo.
 
Amalizwe mara ngapi.
Hata kama akijitahidi 2025 atoboi.
Ccm hawawezi msimamisha saa nne asubui.
Tozo na Mbowe vishammaliza achomoki.
 
Mbowe sio popular kama wanavyoaminisha kuna wakati mpaka unasahau kama huyu mzee Yuko jela
 
Kwani Mbowe ana ushawishi gani wa kisiasa uliopindukia kiasi utampunguzia Samia ubora wake?

Mkipata taabu Viongozi na wana Chadema, wana CCM wanashangilia, sioni kitu cha upekee kwa Mbowe mbali ya kumkweza asipostahili.
 
Mama yuko makini kweli kweli asikudanyanye mtu. Yuko macho kisawasawa kuna mengi hatuyajui.
 
Kirusi cha ugaidi kimejibadili na kipindi hiki kinajivika koti la uanasiasa!
 
Mara mbili kaka.... 2025 hatoboi hata kama akibana katiba mpya....CCM wana mkakati hatari.

Hajui kucheza na karata zake vzr kuzoa credit za makosa ya mwendazake.....ashafeli mapemaaa


.
 
Hii ni vita dhidi ya Ukristu, magaidi wote waliachiwa iweje mbowe aitwe gaidi?
 
Apo mama kapania kifungo cha maisha
UHUJUMU uchumi na ugaidi na ile ya kuuwa viongozi wa juu ni life sentence
 
kila mtu atavuna alichokipanda! Kama alifanya ugaidi ,hatma ya matunda ya ugaidi ni mwisho mbaya !, Ova. Siasa za kipuuzi kwa Sasa hatuzitaki! mahakama itatoa majibu tunaendelea kusbl mwisho wa hili Jambo!
 
Kwa dhati kabisa ya moyo wako wewe unaamini Mbowe anaweza kuwa gaidi?!
 
Kama ilikuwa lazima mama azungumzie suala la mbowe angesema tu kesi iko mahakamani tuache sheria ifuate mkondo wake lakini maelezo yake ya ziada yamemuweka pabaya mno. Watanzania wanajua mbowe sio gaidi. Mama anachoshindwa kuelewa au wasaidizi wake wa karibu hawampelekei taarifa ni kuwa ana vita vikubwa na team mwendazake na sio kikundi kidogo, mfano kiduchu amemsikia slow slow , Gwaji anauma na kupuliza lkn ukweli ndio team yenyewe, alipaswa kulinda imani ya wananchi wengi waliokuwa wanamuunga mkono alipochukua madaraka , vinginevyo anaingizwa chaka.
 
Nchi hakika ina watu fulaniwachache wanaishi kwenye fikra za tofauti sana. Huyu anaamini kwamba mbowe anaweza geuza mstakabali kisiasa wa samia wakati mbowe hana uungwaji mkono na watanzania isipokua wachache wenye kasumba ya ubwanyenye na ukabila.
Tena wa mitandaoni,ni kama alivyosema Rais kwamba kawaulize wananchi wa kawaida kama shida yao ni Katiba au uhakika wa maisha.

Tena kasema yuko tayari kujadiliana Katiba kama mwanasiasa maana hiyo Katiba ni ya kufaidisha wanasiasa kuliko wewe na mimi.

Ukweli ni kwamba kwani huyo Mbowe na machadema wengine wakiingia madarakani ndio wataongeza ugali mezani kwangu? Jibu ni hapana kwa hiyo upuuzi wao usiwe kero kwa wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…