Utafiti kwa kusoma Hukumu za Divorce Tanzania Ndoa nyingi zina migogoro sababu ya Dharau, Financial reasons ( Pesa) Na extended Family hasa mama wakwe

akili kumkichwa kaka hapa maisha yetu ya mviziano. Mnyenkanda huyu ni mbishi, dharau, kibri sijapata kuona
We subili kwanza utosheke. Maana utakuta unafokewa wewe, unafyonzwa wewe, unaulizwa kama una akili timamu! Daaadeki. Unajiuliza siku unamfata fata na kuomba namba na kumtoa out ulikuwa na akili kweli?! Ila, kuliko kesho ujikute unapata kesi ya mauaji!!? Bora ukaanze maisha upya mkoa mwingine. Kubali hasara.
 
tuna mtoto mmoja ana mwaka sasa. Hapa nawaza kibanda changu cha mbavu nikichukulie mkopo NMB harafu nitalala mbele nimwache na jeuri yake. ni mke wng wa ndoa kbs ya kiislam tumekaa sana vikao vya usuluhishi lkn mabadiliko hamna
 
tuna mtoto mmoja ana mwaka sasa. Hapa nawaza kibanda changu cha mbavu nikichukulie mkopo NMB harafu nitalala mbele nimwache na jeuri yake. ni mke wng wa ndoa kbs ya kiislam tumekaa sana vikao vya usuluhishi lkn mabadiliko hamna
Brazaaaa, babu na bibi zetu walivumiliana,kwa sababu hakukuwa na chochote. Siku hizi,kitanda kikubwa,nyuma yenye vigae,magari,bia na makolokolo kibao. Enzi hizo kulikuwa na nini!!!
Miaka hiyo,unamuoa binti bikra. Unavuruga mwenyewe. Leo hii,unadumbukia kwenye handaki la urusi. Wewe una nini? Kama umechokwa,kubali umechokwa. Usitueleze kila kitu humu,lakini we mwenyewe ukweli unaujua.
Swali langu kabla ya ushauli wa mwisho: mlikutana wapi!? Katika mazingira gani!
 
mazingira ya kazini kwangu
 
Kuna wanawake wanaficha makucha kipindi cha uchumba wakishapata cheti cha ndoa tu mwanaume ndio utajua ujui
 
Aisee..
Na kama mchepukaji ni mke je?
 
Mengi yatasemwa ila chanzo cha kuvunjika kwa ndoa ni mambo makuu matatu.

1.Not choosing the right patner
2.Changamoto za kiuchumi
3.Kufifia kwa upendo baina ya wenza.

1.Right patner
Ni muhimu kuchagua mtu ambaye unaona itikadi zenu zinakwenda kwa asilimia nyingi zaidi hasa smartness. Kama wewe ni mchangamfu tafta mtu aliyechangamka ili muende sawa. Hobbies ziwe zinaendana kwa kiasi flani. Awe na tabia ambazo zinaendana na za kwenu kimalezi. Wengi tunachaguaga wanawake wenye shepu na sura tukijidanganya eti watatumia akili zetu ila unakuta adabu ni 0 shabash!!! Mbali na yote hakikisha mwanamke huyo anakupenda zaidi kuliko wewe unavyomhitaji.

2.Uchumi
Huu una play part kwenye sehemu kubwa kimaisha. Kabla hujaoa hakikisha una income streams za ku sustain maisha basic yale. Kula iwe kwa wepesi, kuvaa na kulipa kodi in case hujajenga. Hapa pakiwa hamna shida mwanamke anakuwa hasumbui. Tunachofeli sikuhizi wengi tunawaachia wanawake nao watoe fungu lao kusongesha gurudumu ila sio wote ni smart kichwani. Wale smart wanatambua kuwa sterling anaweza kuzidiwa sometimes ila wapuuzi wataanza kejeli na dharau just to demolish your manhood. Kama hukuoa right patner lazma akukaange hapo.

3. Upendo
Kitu hiki ni kama kamba inayoshikilia ndoa yenu. Regardless ya magumu mtakayopitia hii kamba ndio itawaunganisha na kujipa moyo kesho mtakuwa pazuri zaidi. Kufifia kwa upendo ni kama kuoza kwa kamba anytime inaweza kukatika na ikikatika maana hamko tena pamoja kila mtu anfanya analojua yeye. Upendo ndio huleta hali ya kuvumiliana na kuvumilia changamoto na hitilafu zote ndoani. Kama hujaoa mtu anayekupenda na kukuhitaji zaidi eti kisa ulimlaghai na pesa zako nikusihi tu kijana mwenzangu pambana sana changamoto zisikukute huko ndoani. Usifukuzwe kazi wala usiishiwe nguvu za kiume maana utateseka mno.😂 Huwezi kupat upendo kama ulichagua matako na shepu kisa una hela za wizi ofisini.
 
Nunua Fanta kubwa nakuja kulipa
 
tuna mtoto mmoja ana mwaka sasa. Hapa nawaza kibanda changu cha mbavu nikichukulie mkopo NMB harafu nitalala mbele nimwache na jeuri yake. ni mke wng wa ndoa kbs ya kiislam tumekaa sana vikao vya usuluhishi lkn mabadiliko hamna
Hahaha..
Kumbuka kama una mke wa ndoa huwezi kuchukua mkopo kwa siri kwa dhamana ya nyumba mnayoishi. Mke atatakiwa kutoa ridhaa yake, ata sign. Akikataa hupewi
 
Kitu kimoja watu hawaelewi kwenye ndoa hamuwezi kufanana. Ambaye hana pesa ndio anatakiwa kuwa mnyonge. Anayechagua mtu wa kuingia naye kwenye ndoa ni mwenye pesa. Kama hauna pesa hautakiwi kuchagua. Inabidi uchukue ambaye hakupi stress. Suala la mama mkwe linatokana na kuwa anayelalamikw wxa hana hela. Maana angekuwa na hela asingechagua kuingia kwenye ndoa na mtu mwenye mama mkorofi.Huku ulaya wanawake wanataka mwanaume anayejua kupika na mwenye gym body. Kwa sababu nguvu ya kuchagua (pesa) wanayo. Namalizia kwa kusema sio kila mwenye pesa anajua kuzitumia. Kuna mfanyabiashara mmoja alifuatilia paspoti pale kurasini miezi sita kisa alikuwa hataki kutoa kitu kidogo.
 
Kifupi usasa umetuharibu sana. Hii taasisi haitaji ulimbokeni sana, na pia tuna shindwa kujua haki na wajibu wa kila mtu kwenye taasisi hii.
Kama alivyo sema mjumbe mmoja hapo juu hii ni taasisi kama taasisi nyingine, sema changamoto ya hii taasisi tumeacha maadili na miongozo yake iliyowekwa na makabila yetu kwa maana mila na desturi lkn pia ile ya dini kwa imani ya kila mtu.
Yote kwa yote ndoa ni mhimu sana kwa ustawi wa jamii iliyo starabika.
Kuzaa pasipo ndoa ndio kuna ongeza janga la migogoro ya ndoa kwa kuwa hao watoto wanakosa malezi thabiti na hivyo kupelekea migogoro kwenye ndoa za baadae.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…