Narumu kwetu
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 1,888
- 4,489
Utafiti uliochapishwa Jumamosi, umeonyesha kuwa watu wengi zaidi nchini Ujerumani, wanaokadiriwa kufikia milioni 17.5 wanaishi katika umaskini kuliko ilivyodhaniwa hapo awali.
Hali hiyo imetokana na viwango vya juu vya kodi na gharama zinazohusiana na kodi za nyumba.
Kulingana na data za Ofisi ya Takwimu, kaya nyingi hutumia zaidi ya theluthi moja ya mapato yao kulipia gharama ya makazi, huku baadhi zikitumia zaidi ya nusu ya pato lao.
Hayo yakiarifiwa, mauzo ya nje ya Ujerumani yamepungua kwa asilimia 2.8 mnamo mwezi Oktoba ikilinganishwa na mwezi uliopita, huku uchumi wake ukitarajia kushuhudia ukuaji mdogo mwaka ujao baada ya kushuka kwa asilimia 0.2 mwaka huu.
Hali hiyo imetokana na viwango vya juu vya kodi na gharama zinazohusiana na kodi za nyumba.
Kulingana na data za Ofisi ya Takwimu, kaya nyingi hutumia zaidi ya theluthi moja ya mapato yao kulipia gharama ya makazi, huku baadhi zikitumia zaidi ya nusu ya pato lao.
Hayo yakiarifiwa, mauzo ya nje ya Ujerumani yamepungua kwa asilimia 2.8 mnamo mwezi Oktoba ikilinganishwa na mwezi uliopita, huku uchumi wake ukitarajia kushuhudia ukuaji mdogo mwaka ujao baada ya kushuka kwa asilimia 0.2 mwaka huu.