Utajiri wa Magofu ya Rapta

Utajiri wa Magofu ya Rapta

Hahahah [emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] hapana bosi wangu kuna majukumu yalinibana leo nashusha episodes mbili ngoja nifike home chap.

Ata kule Whatsapp nimechelewa kushusha vitu
Huko home haujafika tu?
 
Story ni nzuri, ila sasa imekuwa too much. Free platform but kwa mwendo huu ni some sort of torture.... Waiting and waiting imeanza kuwa wasting. 😡
 
TUNAENDELEA NDUGU ZANGU


Wakati najiuliza ni shughuli gani za kibinadamu zinazoendelea kwenye mji huo uliopotelea baharini nikajikuta naikumbuka kauli ya javier kuhusu uchawi wa afrika ulivyokua na usiri usiona manufaa kwa waafrika wenyewe.

Hakika javier kuna namna alikua sahihi lakini isingekua rahisi mimi kuukubali ukweli huo. Kama tunavyojua ukweli huwa ni mchungu sana hususani ukweli unaogusa sehemu ya maisha yako.

Sasa shahzad baada ya kuendelea kunielezea zile artifacts na ecofacts yeye akaanza kushangaa baadhi ya vitu vyake alivyovihifadhi umo kwa miaka mingi.

Ilionekana wazi ni miaka mingi imepita toka yeye kupekua sanduku lile ambalo ndilo ndani yake kulikua na zile zana.
Kwa mujibu wa shahzad ni kwamba kwenye familia hiyo hakuna yeyote ambaye yupo interested na habari za mji huo wa rapta. Hivyo baadhi ya zana zile ziliwekwa ndani umo kama kumbukumbu kwa ajili ya familia.

SHAHZAD: kijana unabahati sana umekuja kabla sijafa hivyo tarajia kusikia na kujua mengi kuhusu hii dunia.

MIMI: nadhani ni kusudi la mwenyezi mungu kunikutanisha na wewe kabla umauti hauja kukuta.

SHAHZAD: yule hawala yake leo sijamuona,

Yaani huyu mzee kuchanganya mada kwake ni swala la kawaida sana, tunaongelea hili yeye analeta lile tena wakati huo huo nadhani hii ilisababishwa na umri wake.

Mzee huyu wa ki-shiraz alikua na mambo mengi mno, alitoa artifacts moja ambayo ilikua ni shanga ambazo anadai ni miongoni mwa vitu alivyowahi kutoka navyo ndani ya mji huo ukiwa tayari umezama.

Shanga hizo alidai zilitengenezwa kwa mawe yaliyoitwa moss agate stone. Alisema kwa namna alivyokuta shanga hizo zimehifadhiwa ni wazi zilifichwa kama kitu chenye thamani sana.

Alidai aliwahi kumpa Bi Fatma ambaye ni marehemu mke wake avae kama mapambo tu. Lakin kuna kitu wali experience kipya kabisa kwenye maisha yao, alidai bi Fatma tangu aanze kuvaa hiyo moss agate hakuna biashara alishindwa fanya.

Lakini bi Fatma mwenyewe hakujua chochote mpaka pale alipokutana na muhindi mmoja hukohuko bongo ambaye alikua anajua siri ya agate hiyo. Yule muhindi malengo yake yalikua ni kumuomba bi Fatma kama anajua sehemu anaweza kupata agate nyingine ya kufanana na hiyo.

Mwanzoni bi Fatma alijua kuna ushirikina Ndani yake lakini muhindi yule alikanusha akidai hizo ni nguvu za asili zilizo ndani ya jiwe lile. Ila zaidi alimuelekeza namna ya kuchaji jiwe hilo.

Alimuelekeza kuwa anapaswa kuiweka agate hiyo kwenye jua la mchana au usiku wa mbalamwezi kama atataka kuifanya iwe active zaidi au ku activate kwa lugha rahisi.

Shahzad alinikabidhi hiyo shanga iliyotengenezwa kwa hayo mawe ya moss agate akidai kwamba umri wangu bado ni mdogo sana hiyo kitu itanisaidia sana kwenye upambanaji lakini alisisitiza ni upambanaji wa kutafuta pesa na sio vitu vyangu vile ( mzee alikua na masiala mengi).


Kwa kuwa muda ulikua unaenda sana niliamua kumuuliza kuhusu yale machapisho pale mezani kwani yenyewe ndio yalikua ya msingi zaidi ya zile mboyoyo mingi anazoleta.

Lugha ya kwenye machapisho yale ilikua ngumu kwa upande wangu kwani sikuelewa kabisa kilatini. Ila shahzad alikijua vizuri sana na nahisi alijifunza kutokana na uwepo wa machapisho ndani ya maktaba ile.

Alidai machapisho hayo yamechanganyika sio kwamba yote yalihusu history na geography ya dunia hapana. Kuna machapisho matatu yaliyo onekana kufungwa kwa pamoja alidai hayo yalikua ni mashairi tu yaliyoandikwa na warumi wa kale.


Mashairi yale yaliwahusu watu watatu ambao kwa mujibu wa shahzad walikua ni Virgil, Horace, na Ovid. Mashairi mengi Ovid yalikua ya mapenzi wakati huo Virgil akizingumzia matukio ya kihistoria.

Niliona dalili zote za shahzad kutaka kunisomea mashairi yale, na mimi kiukweli sikuwahi kuwa mpenzi wa mashairi kabisa toka enzi nipo shule hivyo niliona ni bora twende kwenye swala letu kwani shahzad kufanya vile ni kama anapoteza muda tu.

Kuna muda nilihisi shahzad ananifanyia makusudi lakini baadae nilikumbuka kuwa wazee hukumbwa na changamoto hizi baada ya kuwa umri umewatupa mkono kwa kiasi Fulani.

Ulifika muda wa kusali na kiukweli shahzad alikua sensitive sana linapokuja swala la ibada kulingana na Imani yake. Hivyo tulielekea msikiti kama kawaida tukifuatana na mjukuu wake ambae alionekana kutokunielewa kabisa.

Nilitamani tukiwa njiani nimuulize maswali kadhaa ambayo yatarahisisha zoezi letu Lakini kwa bahati mbaya huyu mzee akiwa anaelekea msikitini hua hana story zozote zaidi ya kuwa bize na rosary yake mkononi.

Siku hiyo zoezi kwa upande wangu halikua gumu kwani nilipita kwenye sehemu ya ablution tena kama mzoefu. Baada ya hapo tuliingia msikitini nikasimama vyema kwenye safu zile na ibada ikaenda mpaka kufika mwisho.

Nilichokalili ni kwamba tukifika stage tukageuza shingo kulia na kisha kushoto basi huo ndio utakua mwisho wa ibada kwa unit husika. Hapa kwenye unit kiswahili chake sijui lakin kwa mujibu wa fatemeh unit namba ya mzunguko wakati unaendelea na ibada.

Kawaida unit chache ni mbili lakini unit nyingi ni nne ambazo mtu anaweza kusali kwa siku. Wakati tunatoka nje ya msikiti nilimuuliza shahzad kama aliwahi kukutana tena na Schulz baada ya kufukuzwa kwa wajermani nchini humo.

Jibu lilikua aliwahi kukutana nae tena walikutana bongo wote wakiwa na mpango wa kuzamia rapta kwa dhumuni la kutoka na chochote.

Huko nyuma nilielezea matukio mawili, tukio la kwanza lilikua ni namna gani mzee Schulz alikutana na shahzad huko Tehran. Ambapo baadae nikaeleza sababu iliyomrudisha Schulz kutoka Tehran na kisha kurudi kwao Düsseldorf huko ujerumani.

Hapa nadhani tulielewana, in simple terms ni kwamba raia wa ujerumani walifukuzwa na kurudi kwao baada ya kutolewa madarakani kwa aliyekua shah ( emperor) ambaye alisupport uhusiano wa Iran na German.

Nilielezea sababu ya kufukuzwa kwao nikaelezea na mikataba iliyosainiwa baina ya Democratic power na serikali ya Iran kwa wakati huo.

Tukio la pili lililkua ni vita iliyopelekea kupatikana kwa kile tulichoita treasure box ambayo ndani yake kulikua na mambo mengi ya siri na yasiyo ya siri lakini kwa sehemu kubwa yalikua ni machapisho ya warumi wa kale.

Box hili lilipatikana wakati wa battle moja maarufu kama BATTLE OF EDESSA ambapo warumi walikula kichapo cha mbwa koko kutoka kwa wa persia na mwisho wa siku Persian wakaondoka na baadhi ya mali zikiwepo na hizo treasure box.

Hivyo basi apa tumepata picha kuwa ni kwa namna gani waajemi walipata taarifa zile zilizo andikwa na Claudio Ptolemy. Na ni kwa namna gani taarifa hizo zilimfikia Schulz ambae alikuja kukutana na Javier, kwani Schulz yeye alizipata kutoka kwa shahzad ambae walikutana huko Tehran.

Back to the point now,

Shahzad alisema watangulizi wake wa awali kwenye kuutafuta mji huo ni kweli walirahisisha kazi kwa upande wake kwani walikuja na taarifa nyingi ambazo walizishuhudia wenyewe na sio machapisho ya Claudio tena.

Kwa upande wake ilikua rahisi kufika kwani watangulizi walishafika eneo husika na wakafanikiwa kurudi. Hivyo ata yeye hakutumia nguvu kulitafuta eneo husika kama ilivyo kwa wengine ata wataja hapo baadae.

Shahzad aliendelea kusema kuwa baada ya kukutana na john yule bwana wa ushelisheli ni kama alimuongezea kwenye zoezi hilo.

Kivipi john aliongeza nguvu, john kwanza kabisa alikua baharia mzoefu lakini pia uzoefu mkubwa aliupata kwenye kazi zake za kuwinda dhahabu zilizohusishwa na shipwrecks.

Hivyo kwa lugha rahisi ni kwamba john alikua ni mtaalamu linapokuja swala la scuba diving. Shahzad pia hakua nyuma kwa ujanja huo hivyo ata yeye alikua mtaalamu pia japo john alimzidi sana. Nadhani ujanja wa john kwenye maji unasababishwa na mazingira yake aliyokulia huko visiwani ushelisheli.

Sasa basi shahzad wakati anakuja bongo akiwa na ndoto kama walizokua nazo watangulizi wake, yaani ndoto ya kuhakikisha anafika rapta na anakomba kila kitu. Ni wachache ndani ya familia walimsapoti kwenye swala hilo na mtu wa kwanza kumsapoti alikua ni marehemu mke wake bi Fatma.

Ni wazi shahzad alimpenda sana bi Fatma kwani mara zote alizomtaja alikua akimtaja kwa hisia sana na kama mtu anaethamini. Nilidokezewa jambo kuwa toka afariki bi Fatma shahzad hakuwahi kuoa mke mwingine tena yeye alijikita bize na ibada akiamini baada ya kifo chake na yeye basi atakutana na mke wake kipenzi.

Hivyo basi shahzad alifika bongo huku akiwa hana mtu yeye ambae angeweza kusaidiana nae kuhusu jambo hilo. Lakini baada ya kukutana na john wa ushelisheli ni kama ndoto zake aliona zinatimia.

SHAHZAD: hivi mjukuu wangu unakumbuka nilikuuliza kuhusu mtaji wa hii project lakini pia nilikuuliza kuhusu rasilimali watu.

MIMI: nakumbuka mzee

SHAHZAD: basi pamoja na kwamba mimi nilifika kwenye mji huo na nitakueleza nini nilikuta huko.
Ila changamoto kubwa ilikua ni technology, mtaji na nguvu kazi yaani watu. Project ya rapta ni project kubwa mno, kwani ulikua mji mkubwa sana na kama unavyojua miji ya kale ilikua fenced hususani miji iliyotawaliwa na warumi.

Kwa mujibu wa shahzad alisema wakati wanafika kwenye mji huo yeye na john kikubwa walichokuwa nacho ni ujuzi wa scuba diving pekee. Kwa shahzad yeye ujuzi na vifaa alitolea huko ufaransa wakati huo kuhusu John yeye anadai kila kitu alijifunzia kwao ushelisheli.

Shahzad aliendelea kusema hapo kabla alitumia pesa nyingi kuhakikisha anapata ujuzi lakini pia anapata vifaa vya kumsaidia kwenye zoezi hilo. Lakini kwa bahati mbaya sana baada ya kufika kwenye field aligundua kuwa bado hajakamilika.

Namna ambavyo waliwaza kufanikisha zoezi hilo ni kama walikua wanaenda kufanya zoezi hilo kwenye zile zilizoitwa shipwreck.

Kwani shahzad alidai baada ya kufika underground akiwa na mwenzie waligundua kuna uhitaji wa mambo mengi ili kufanikisha zoezi lile.

Alidai kwanza kwa hali jinsi ilivyo wanahitajika wataalamu wa Marine remote sensing kwa kutumia geophysical techniques.

( Hapa sasa nilibidi nitulie sana kwani mzee alianza kutema nondo ambazo ndio niliamini zina msaada kwangu. Na yeye apa alikua anaongea kama mtu ambaye amefika tayari kwenye site hivyo anayajua mazingira yote)

Tusikate tamaa simulizi itaisha, naomba tuendelee kula mtori nyama zipo chini.

0623329512 Whatsapp bei bado ni aftatu [emoji23][emoji23][emoji23] sijaongeza
 
Sio rozary.waislam wanaita tasbihi.kutokana na yale maneno yanayosemwa.kutukuza ni kutasbih.nalo jina likatoholewa kuitwa Tasibihi.
Rozary ni some kind of plastic chain with a sanamu of person.
Nimekusahihisha pale ukisema mzee shahzad anaenda na rosary yake mkonon
 
Sio rozary.waislam wanaita tasbihi.kutokana na yale maneno yanayosemwa.kutukuza ni kutasbih.nalo jina likatoholewa kuitwa Tasibihi.
Rozary ni some kind of plastic chain with a sanamu of person.
Nimekusahihisha pale ukisema mzee shahzad anaenda na rosary yake mkonon
Asante ndugu yangu kwa marekebisho mazuri, ubarikiwe sana
 
Screenshot_20230701-230945.png
 
Hivi bado mnakumbuka yule jamaa wa SUGAR RAY kule temeke ambae ndio anapokeaga mizigo ya Ras inayoletwa na magari ya mizigo yanayoenda stirio.

[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] Tusimsahau anaitwa boni, nimeamua tu niwakumbushe na tukumbuke yeye ndio aliniunganisha na Ras.

Wale ndugu zangu wa Whatsapp kuna mwarabu mwingine anaitwa Rehman, ambaye taarifa zinaonyesha anahudumu kwenye kikosi cha wanamaji nchini Iran NEDAJA lakini pia kuna taarifa wakati huohuo zinasema yupo gerezani huko huko Tehran fashafuyeh.

Mambo mengi muda mchache, tule mtori nyama zipo chini.
 
Hivi bado mnakumbuka yule jamaa wa SUGAR RAY kule temeke ambae ndio anapokeaga mizigo ya Ras inayoletwa na magari ya mizigo yanayoenda stirio.

[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] Tusimsahau anaitwa boni, nimeamua tu niwakumbushe na tukumbuke yeye ndio aliniunganisha na Ras.

Wale ndugu zangu wa Whatsapp kuna mwarabu mwingine anaitwa Rehman, ambaye taarifa zinaonyesha anahudumu kwenye kikosi cha wanamaji nchini Iran NEDAJA lakini pia kuna taarifa wakati huohuo zinasema yupo gerezani huko huko Tehran fashafuyeh.

Mambo mengi muda mchache, tule mtori nyama zipo chini.
Ni ngumu kukumbuka. Hata wewe umeona eeeeh.... Mambo unaandika mengi ambayo hayana msingi. So watu wanashindwa hata kusoma kitu kikaeleweka. Mimi nitakushauri upate mwandishi mzuri. Wewe uwe unatunga yeye ana edit anapost humu. Ila nakusifu kwenye kuandika unaandika sana. Na unapenda kuandika. Issue ni kuandika kitu cha mvuto ndo changamoto. Unatakiwa uwe very smart. Halafu ulichagua kutunga story kwa topic ambayo utaumia sana kuisimamisha iendelee kuwepo. So utajikuta unajichanganya changanya. Weka pia mambo ya uchawi na sex endeleea nayo itakusaidia kiasi.
 
Hivi bado mnakumbuka yule jamaa wa SUGAR RAY kule temeke ambae ndio anapokeaga mizigo ya Ras inayoletwa na magari ya mizigo yanayoenda stirio.

[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3] Tusimsahau anaitwa boni, nimeamua tu niwakumbushe na tukumbuke yeye ndio aliniunganisha na Ras.

Wale ndugu zangu wa Whatsapp kuna mwarabu mwingine anaitwa Rehman, ambaye taarifa zinaonyesha anahudumu kwenye kikosi cha wanamaji nchini Iran NEDAJA lakini pia kuna taarifa wakati huohuo zinasema yupo gerezani huko huko Tehran fashafuyeh.

Mambo mengi muda mchache, tule mtori nyama zipo chini.
Siku hizi hiyo bar ya sugar ray inaitwa kisuma
 
Back
Top Bottom