Utajiri wa Magofu ya Rapta

Utajiri wa Magofu ya Rapta

Hivi nilipo waambia nikaingia jikoni kupika hamkujiuliza nimeenda kupika nini? Haaa ahaha hahah.

Aisee nilikua napika chakula fulani hivi maarufu kama chelow kebab kwa huku Iran. Chakula hiki kinahusisha mchele ndani yake au watoto wa uswahilini wanaita cha mtume. Basi bwana nchi ya Iran wanapenda mpunga balaa warabu wale, huko kwetu mchele classic na wakunukia si tumezoea unatokea kyela.

Sasa ukifika Iran kuna chimbo linaitwa Mazandaran, yaani hiyo ndio kama kyela ya Iran. Mpunga wa Mazandaran unanukia na mtamu balaa, kwa upande wangu chakula changu kikuu ni KIBURU kwani ni chakula kilichonikuza na kinapendwa sana nyumbani kwetu.


Lakini ukiacha kiburu basi hunitoi kwenye mchele hivyo siku hiyo nilipania kufanya wonders pale jikoni kiasi kwamba fatemeh akiamka akute tayari nimerekebisha.

Nilichagua kupika chelow kebab kwakua mara zote nilipokua jikoni na fatemeh alionekana kukipenda sana chakula hiki. Lakini pia alinifundisha ni namna gani naweza pika chakula hicho hivyo siku hiyo nilitaka kuitumia kumuonyesha fatemeh kama sikuwa nyuma kwenye mapishi.

Nilitumia masaa kama matatu hivi jikoni mpaka msosi wetu wa chelow kebab kuwa tayari kwa ajili ya kuliwa. Baada ya kuivisha nilibeba msosi mpaka bedroom ya fatemeh ambako nilimkuta tayari ameamka na amekaa tu kitandani ni dhahiri kuna kitu alikua akiwaza muda huo.

MIMI: You are awake dear
( Umeamka mpenzi)

Nilisogea na msosi mpaka kitandani ambako alikua amekaa fatemeh, lakini wakati wote huo alikua kimya zaidi hakunisemesha chochote zaidi ya kuachama baada ya kujua nataka kumlisha.

FATEMEH: whao!!! you know how to cook
( Aisee kumbe unajua kupika)

Nilitamani kumuuliza fatemeh ilikuaje ametapika sana na kupoteza nguvu na mwisho kudondokea kwenye usingizi mzito baada tu ya kutumia dawa zile. Ila niliona naweza kutulia nikasubiri kesho yake ndipo ataweza kunielezea vizuri na sio usiku huo.

Alijitahidi kula japo sio sana kwani hakua na appetite kabisa hivyo kwa kiasi alichokula ni wazi alijitahidi sana.

Kwa mujibu wake alidai mara nyingi akiwa kwenye situation hiyo hukosa appetite ila anashangaa siku hiyo licha ya kukosa appetite ( hamu ya kula) ila alijitahidi kwa kula kiasi kingi cha chakula.

FATEMEH: what did shahzad say about the ancient city you are looking for.
( Leo shahzad amesemaje kuhusu mji wenu wa kale mnaoutafuta)

Nilijitahidi kumueleza yote niliyoambiwa na shahzad kwa siku hiyo lakini kubwa zaidi ni lile la nguvu kazi, mtaji wa pesa na technology pia kwani zoezi hilo lilihitaji vyote hivyo ilikufanikisha project nzima.



Kwa mujibu wa fatemeh Alisema mtaji sio changamoto kabisa, yeye alidai ataweka mkono wake kwenye mambo yote yanayohusu pesa kikubwa tuwe na bajeti ya uhakika ya project nzima.

Mpaka hapo niliona tayari nimemaliza jambo la muhimu na la msingi hivyo kesho napoenda kukutana na shahzad nitaenda nimevimba kwani tayari nina uhakika wa pesa ya ku finance mradi wote.

FATEMEH: of course you are a good driver
( Bilashaka wewe ni dereva mzuri)

MIMI: It's true but I don't have a license
( Ni kweli lakini sina leseni)

FATEMEH: don't worry, just prepare yourself, there is a place to go
( Usijali nenda kajiandae kuna sehemu twende)

Kwakua ulikua ni mtoko wa usiku nilijipigilia kijanja zaidi kupitia nguo ambazo ziliongezeka kwenye chumba changu lakini fatemeh alidai hakununua yeye zaidi ya kuchagua tu.

Sijisifu ila kiukweli nina mwili wa nguo au kwa lugha rahisi tu niseme nina damu ya nguo yaani ata nikivaa gunia hua napendeza hahahahah.

Nilitumia dakika chache sana kujiandaa lakini wakati natoka chumbani na kufika sitting room nilimkuta fatemeh yeye alishamaliza kujiandaa mapema sana na kwenye hili fatemeh na msifu sana alikua wa tofauti sana na wanawake wengine.

Sikua najua tunapoelekea zaidi ya kufuata maelekezo ya mwenyeji wangu tena ukizingatia ilikua ni usiku hivyo nilikua mpole kusubiri maelekezo.

Tuliingia kwenye lifti na kushuka mpaka chini kabisa kwenye eneo linalofahamika kama basement ambapo huko basement nilikuta chuma moja inaitwa Renault.

Fatemeh alinikabidhi funguo za gari ile akimaanisha ndio naenda kuwa dereva kuelekea kwenye safari yetu hiyo ya usiku huo.

Gari ile ilikua mpya kabisa na kama iliendeshwa basi haikuzidi ata mwezi toka inanunuliwe na kisha kutelekezwa huko basement. Siunajua tena ukiwa na binti lazima uoneshe unachokijua, hivyo niliona sasa huo ni wakati sahihi wa kuonyesha talent yangu kwa fatemeh.



Kwani toka tumefahamiana mimi na fatemeh hakuna sehemu fatemeh amewahi kunitegemea au kuniamini. Hivyo nikasema apa kwenye driving ndio sehemu pekee ya kuonyesha kama na mimi kuna vitu najua ili nipate point 3 muhimu.

Safari yetu kwa usiku huo tulielekea eneo moja ambalo lilikua na watu wengi sana kwa usiku huo. Idadi ya watu ilikua kubwa lakini na shughuli za apa na pale zilikua nyingi kuzunguka maeneo hayo yote.

Tuliegesha gari maeneo ya mbali na eneo lile kisha tukatembea kuingia ndani ndani zaidi kwenye mitaa ile. Sikutarajia kama ndani ya mji huo kuna sehemu kwa usiku ule itakua na watu wengi kiasi hicho.

Kwa maelezo ya fatemeh alidai eneo lile linaitwa 30-Tir Street ni eneo maarufu sana ndani ya mji huo na hutembelewa sana na watu hususani nyakati za usiku kama muda ule ambao mimi na yeye tukifika hapo.
Kulikua na vibanda vingi vya biashara huku misosi iliyouzwa ilikua local sana na bei za kawaida kabisa. Ukiacha vibanda au viosk vilivyopo eneo hilo kulikua na magari yaliyogeuzwa kama maduka pia.

Hhhhhmmm hapa kwenye magari yaliyogeuzwa maduka hivi mmenielewa kweli?!!!.

Ok ni hivi kuna muvi moja watoto wa uswahilini walikua wanaita kipanya msosi (kwa mujibu wa lufufu) ila jina la hii muvi iliitwa WHEELS ON MEALS ni muvi ya miaka ya 1980's.

Sasa mfano wa lile gari kwenye muvi hii ambalo linaweza kufanywa duka pia ndio magari tuliyoyakuta eneo lile yakiuza snacks na vitu vingine kama mishkaki mazagazaga mengine mengi.

nilichogundua kwa fatemeh kuja pale ni kwamba alitaka ku refresh kwa kuona watu na kufanya matembezi ya usiku ili tu kupunguza mzigo aliokuwa nao kichwani.


Ila eneo ilo nililipenda sana toka nimefika mji huo sikutarajia kukutana na eneo kama lile japo lilikua mbali lakini ilionekana fatemeh alitaka tutoke tu no matter tunaenda wapi.

Fatemeh alidai anapendelea sana kufika hapo mara nyingi hususani nyakati anazohisi ni ngumu kwenye maisha yake hivyo hufika apo kwa lengo la kupoteza muda na mawazo pia kwa kufanya matembezi ya hapa na pale.

Tulienda kwenye moja ya vibanda ambavyo vilikuwepo eneo lile na kuagiza juice ambayo ilionekana ni moja ya vinywaji pendwa na sio kwa fatemeh tu bali na watu wengi eneo lile.

Tulikaa kwenye viti vilivyokua chini ya mwamvuli karibia na kibanda kile. Baada ya kuketi kwenye viti vile nilimuuliza fatemeh kwanini ametaka kwenda hapo kwa muda huo.
Jibu lake lilikua ni kwamba maeneo hayo alikua anapenda sana kuja na aliyekua mlezi wake wa hapo mwanzo ambaye aliitwa Zahra. Kama mnakumbukumbu huyu Zahra ndiye mlezi wake aliyewekewa sumu na kufariki lakini Sababu haijulikani hadi leo.

Aliendelea kusema kitendo cha kufika maeneo yale hujikuta anamkumbuka Zahra na anamkumbuka kama mzazi wake pekee ambaye alimlea toka akiwa kichanga mpaka kufika umri huo.

Zahra hakuwahi kumuambia fatemeh ilikuaje akafika kwenye kituo kile na hilo ni jambo lililokua linamuumiza kichwa sana fatemeh kwani aliamini Zahra angekuwepo basi angeweza kujua pa kuanzia ili kujua ni wapi ipo origin yake.

Hivyo basi fatemeh alinipeleka eneo lile kwani mimi ndio faraja pekee iliyobaki na ndio mtu pekee ambae tunaweza ku share story na kila kitu kuhusu maisha yake.

Eneo lile lilikua changanyikeni sana lakini kwa mujibu wa fatemeh ni kwamba alichopenda zaidi kwenye eneo hilo ilikua ni chakula local kinachopatikana eneo hilo ambacho mara nyingi pia kilipendwa na Zahra.

Sasa mpaka hapo kwenye ile misheni yangu ya kuchunguza maisha ya Zahra nilipata pa kuanzia. Yaani nilishajua tayari kwamba mzazi wake wa pekee au mlezi wake aliitwa Zahra.

Nilimuuliza fatemeh kuhusu ni wapi alipozikwa Zahra lakini pia kuhusu ndugu wa mwanamama huyo Zahra.

Fatemeh kwa huzuni sana alisema kwa bahati mbaya hakuwahi kujua ndugu wa Zahra na wala hakuwahi kumuuliza Zahra kuhusu ndugu zake. Lakin alisema hilo lilitokana na yeye kuwa kwenye umri mdogo kiasi kwamba asingeweza kukumbuka au kujua umuhimu wa swali hilo.

Lakini pia aliendelea kusema kuna uwezekano mkubwa wa Zahra kutokua na ndugu kabisa kwenye mji huo kwani hakuwahi kumsikia akizingumzia ndugu zake kabisa pamoja na kwamba yeye alikua mdogo.

Kuhusu ni wapi alipozikwa alidai hakuwahi kupajua kwani yeye alipewa tu taarifa akiwa kituoni na sababu nyingine ni kwamba jinsia yao hawakuruhusiwa kwenda kushiriki mazishi kulingana na tamaduni zao.

Je! Fatemeh Alifahamu vipi kama Zahra aliuawa kwa sumu? Huyu Zahra ni nani na kwanini aliuawa. Ni kweli Zahra hana ndugu? Je Zahra aliwahi kupata watoto?

Tuendelee huko mbele tutamjua vizuri mwanamama huyu anayefahamika kwa jina la Zahra.

Nilimuuliza fatemeh vipi wakati anakua hakuwahi kumuuliza Zahra kuhusu baba yake kwani ni kawaida sana watoto kuuliza maswali haya wakati wanakua.

Fatemeh alijibu kuwa yeye alichelewa sana kuongea, kwani wakati watoto wengi wanaanza kuongea kwenye umri usiopungua miezi 18 kwa fatemeh ilikua tofauti sana yeye alianza kuongea akiwa na miaka 2 kuelekea 3 kabisa.

Wengi walihisi anaweza kuwa bubu lakini mtu wake wa karibu ambaye alikua ni Zahra yeye peke ake ndiye alikua anamuelewa fatemeh na ndio mtu pekee aliyekua anawasiliana na fatemeh wakati fatemeh akiwa bado mdogo.

Kwa mujibu wa fatemeh baada ya kifo cha Zahra alichukuliwa na shirika ambalo hakulitaja jina na shirika hilo likaanza kumsomesha hii ni baada ya kuona uwezo wake mkubwa wa darasani japo alikabiliwa na changamoto kadhaa za kiafya.

Hivyo huo ndio ulikua mwanzo wa safari ya masomo ya fatemeh mpaka anakwenda Russia na kurudi na taaluma anayoitumikia wakati huo.

Alidai baada ya kutoka Russia alifikishwa chuo kimoja kilichoitwa Imam Mohammad Bagher University in Tehran. Na kwa mara ya kwanza akapewa akafanya majaribio ya kujiunga na taasisi au shirika analohudumu hivi sasa.

Kwa mujibu wa fatemeh tests hazikuishia pale Mohammad Bagher pekee bali waliendelea mpaka Intelligence Bureau iliyopo Hamedan, magharibi ya Iran.
Na walichopimwa kingine kwa huko ilikua ni intelligence na personality pekee kwa upande huu wa huku hawakujali sana physical strength kikubwa waliangalia akili.

Fatemeh alidai kwake yalikua ni majaribio marahisi sana hususani yale ya physical kwani yeye alikua na fitness ya ajabu sana na ni kama alishaandaliwa kuhudumu huko bila yeye kujua.

Alidai alihisi ameandaliwa kutokana na aina ya maisha aliyokua anaishi toka atoke kwenye kituo kile ambacho alilelewa.

Kuhusu katabia ka kuwalala wadada wenzie alidai katabia ako kalikuja baada ya kuyatambua rasmi maumbile yake ( Apa nikama ujasiri ulipotea kwani alianza kua na aibu).


Nilitamani kujua sana kuna nini kwenye maumbile ya fatemeh kwani mara kadhaa amekua akiyazungumzia lakini kwa kukosa kujiamini kabisa. Na nilipo muona anapata shida kujibu swali hilo niliamua kuingiza swali lingine ili kumfanya apate amani kidogo.

MIMI: would you marry me
( Naweza kukuoa)

FATEMEH: I'm tired of staying here, please lets leave
( Nimechoka kukaa apa naomba tuondoke)

Ni wazi fatemeh taratibu alitaka nimfahamu yeye ni nani hivyo alianza kunipa background yake taratibu taratibu.



MUONEKANO WA ENEO LA 30-Tir STREET KWA NYAKATI ZA USIKU.

[emoji116][emoji116][emoji116][emoji116]
📴
 
A young boy, aliyefukuzwa secondary aombe kwenda Iran kwa issue simple ya kuonana na Shahzad tena majasusi wa Iran ninaowajua kdg wamkubalie, aishi na jasus wao 1 room? asafiri na top spies of Iran kwa ndege yao achilia mbali magari yao? alipiwe everything in VIP mode kwa kazi ipi haswa???? Jasus smart amuelezee mambo mengi mpk ya chumbani easily? a cheap african boy easy to buy?

Halafu...all trip hasa za nje mhusika anafanya mambo kibao halipi hata mia, analipiwa tu?(at least mpk epispde niliyoishia) Asee ana bahati kuliko hata majasusi....

Tuisome kwa kuichukulia kama normal Riwaya tu like ya VIPEPEO WEUSI but haina uhalisia. Few aspects can be verified but the story has above 95% fiction side!

Watakaoamini kuwa ni ya kweli nao wana haki hiyo kikatiba!


Lakini nakupongeza Msimuliaji...punguza tu kuitetea kama eti ni story ya kweli, ipo vzr na inavutia wengi kusoma!

Pia una akili zaidi ya super computer kukalili series yooote ya matukio... u are good dude!
Upo sahih
 
TUNAENDELEA WAKUU

Fatemeh hakutaka kujibu swali langu, na mimi nilimuuliza kwa makusudi ili tu nimtoe kwenye mood aliyokuwa nayo kuhusu kile tulichokua tunakiongelea. Kitu kingine alichokua anataka ku enjoy fatemeh ni kile kitendo cha kutembea umbali mrefu kidogo kwa mguu.

Hivyo kutokana na ka umbali kalikokuwepo kutoka eneo lile mpaka tulipo egesha gari tulitumia dakika kadhaa kutembea na huku tukiongea mambo mengi. Kwa upande wangu nilimsimulia japo kwa uchache Kuhusu baadhi ya mambo kwenye maisha yangu ambayo niliamini hayajui.

Bilashaka tulienjoy sana siku hiyo kwa upande wangu nilifurahia mazingira yale lakini pamoja na vinywaji vilivyopatikana eneo hilo. Tulibeba kwenye vifungashio vitu kadhaa na wakati tukitembea kuelekea tulipo egesha gari ni wazi yoyote angetuona angeamini tulikuwa wapenzi.

Tukiwa kwenye gari tunaelekea nyumbani fatemeh aliilaza kabisa siti yake na jambo hili lilifanya niweze kuiona vyema shape au umbile lake.

Fatemeh alianza kunizoea kiasi kwamba ata ile desturi ya kijistiri sana akiwa na mimi ilipungua tofauti na kama ilivyokua hapo awali wakati ndio tunafika kutokea haullaga.

Ulikua ni usiku ulioenda sana japo sikumbuki ilikua ni saa ngapi, ila kwa hakika nilimuona fatemeh akiwa amefurahia mtoko ule kwani ulimpunguzia baadhi ya mambo yaliyokua yamejaa kichwani mwake.

Tulikaribia jengo ambalo ndilo lilikua na apartments ambazo alikua anaishi fatemeh, hivyo tulipitiliza moja kwa moja mpaka eneo la basement ambapo tulitakiwa kuegesha gari ile.



Baada ya kufika eneo la basement nilimshtua fatemeh ambae alionekana kuanza kutekwa na usingizi nadhani sababu ya uchovu wa usiku ule.

Fatemeh alinyanyua siti ili aweze kutoka ndani ya gari lakini alikutana na mdomo wangu moja kwa moja na kama kawaida yake hajawahi kupinga zaidi ya kunikimbia ikitokea amepata nafasi.

Tukiwa kwenye moment ile kuna mambo mengi yanabadalika kwenye mwili wa fatemeh hususani joto la mwili na mapigo ya moyo hubadilika ghafla na kupanda wakati huo huo.

Kitu cha tofauti kwa siku ya leo ni kwamba fatemeh alitumia nguvu kubwa kunivuta na kunishikilia ikiwa ni ishara hakutaka tuwahi kumaliza jambo lile haraka haraka ni kwamba alihitaji tutumie muda kidogo.

Jinsi mwili wa fatemeh ulivyokuwa mlaini huwezi amini ukiambiwa alikuwa ni ninja wa kike na kiukweli nilikua natamani sana siku moja nimuone akiwa kwenye harakati hizo za kininja anafananaje.

Siku hiyo tulijitahidi kwenda mbali kwani nilifanikiwa kutoa koti lake refu kwa upande wa juu hivyo nikiwa nakaribia kuitoa blazia. Tulisikia Bonnet inagongwa kwa nyuma na mtu ambaye hatukumjua ni nani.

MIMI: what the f**k
( Ujinga gani huu )

Na wakati ule fatemeh pia alistuka ni kama mtu aliepotelewa na fahamu na hivyo hapo ndio zilikua zinamrudia.

Nilishuka kuonana na mtu huyo wakati fatemeh akijirudishia nguo zake ambazo hakumbuki zilivuliwaje ndani ya dakika chache zile.

Aliyekua anagonga ile bonnet alikua ni askari wa eneo lile na aliongea lugha ambayo siku ifahamu na nilipo muuliza kama anaongea kingereza alijaribu na jambo lake lilikua ni kusisitiza tume park gari sehemu ambayo sio sahihi na ata mimi baada ya kuangalia niligundua ni kweli.

Nilirudi ndani ya gari ili kuhakikisha naiegesha sehemu niliyoelekezwa na yule askari lakini nikiwa Ndani ya gari fatemeh aliuliza niliwezaje kuzitoa nguo hizo kwa dakika chache vile. Sikumjibu zaidi ya kutabasamu tu huku nikiwa makini kuhakikisha sikosei kwa kile nilichokua nakifanya.

Tulishuka na kuelekea eneo la lift ambapo ndani ya muda mchache tulikua tayari ndani ya apartment yetu. Tukiwa ndani nilikumbuka kuwa tumesahau vile vifurushi vilivyokua na bidhaa tulizo rudi nazo toka 30-Tir Street.

Hivyo nililazimika kurudi tena kwenye basement kwa ajili ya kuchukua mizigo ile lakini bado nilimkuta yule askari akiwa maeneo yaleyale.

ASKARI: sorry the new guy, is that your wife?
( Samahan kijana mgeni yule ni mke wako?)

MIMI: no! we friends
( Hapana sisi ni marafiki)

ASKARI: what do we call friends who kiss?
( Tunawaitaje marafiki wanao kiss)

Mpaka hapo nilitabasamu tu nikiamini jamaa kumbe aliona wakati namnyonya fatemeh hivyo ilitosha yeye kusema tulikua wapenzi na hakuna namna ningepinga.

Yule askari alinisifia kwa kusema kama nimeweza kung'oa yule mtoto basi mi ni hatari sana kwani binti huyo hakuwahi kuonekana na mtu yoyote toka ameanza kumjua.

Sio kuonekana kimapenzi tu bali ata kuonekana akiongea na mtu yoyote kwani ni binti ambaye yupo cool masaa 24 siku 7 za wiki. Jamaa alidai yeye pamoja na kukaa hapo sikuzote hajawahi ata kusalimiwa na binti huyo hivyo alijiuliza m'bongo mimi nina nini cha ziada.

Yule askari alikua anaongea maneno mengi sana lakini sikuyatilia maanani zaidi nilitoa snacks zilizo kwenye vile vifungashio na nikampatia asogeze masaa.

Wakati naondoka aliniambia anaitwa Mohamed na ikitokea siku nimepatwa na changamoto yoyote yupo pale nimuone lakini sio changamoto ya pesa wala mapenzi.

Nilirudi kwenye floor yetu chap na moja kwa moja nilienda kwenye room ya fatemeh ambapo nilimkuta ametoka kuoga akiwa na taulo tu. Na aliponiona alishangaa kwanini hakufunga mlango mpaka ameruhusu the African rude boy nimeingia.

Sikujali alichokua anaongea zaidi nilienda moja kwa moja bafuni kuweka mwili sawa na kuondoa uchovu. Fatemeh alisisitiza nisitoke uchi tu kwani hana mpango wa kuona linyoka langu.

Nilipotoka bafuni moja kwa moja nilijitupa kwenye kitanda na fatemeh alisimama kama mtu aliyesusa kulala mpaka niondoke. Nilichofanya pale baharia ni kujifunika shuka vizuri nikimaanisha ndio nimefika apo kama atataka ahame chumba na leo.



Nilipotelea usingizini mpaka asubuhi ambapo nilistuka na kukuta kuna mstari mreefu wa mito ukitutenganisha nilipo lala mimi na alipolala fatemeh. Niliishia kucheka tu na kumchungulia upande wa pili wa mito alipokua amejifunika mwili mzima na kuacha sura tu.

Alipogundua na muangalia alinionyesha ngumi akimaanisha nikimsogelea atanichakaza.

MIMI: you want to break my neck like a gringo in the mine
( Unataka univunje shingo kama mzungu wa mgodini)

FATEMEH: No! Damião lied to you
( Damião alikuongopea)



Nilimwambia haina shida ata kama ni kweli mi nipo tayari kwa lolote ata kama ataniua ni kama nzi kufia juu ya kidonda tu.

Hapo niligundua kuwa fatemeh hakuwa anajua kama nilikua na CV yake ya kimapigano ambayo nilipewa na bwana Damião.

Alinikurupusha kwamba natakiwa kwenda kwa shahzad hivyo nitoke kitandani nisiendelee kumpigisha stories. Nadhani alijua kuwa namlia timing na kama angeruhusu niendelee kuwepo pale dakika tano mbele zingekua nyingi sana na zingenitosha kuhakikisha anabaki kama alivyozaliwa.

Siku hiyo nilijipigilia kanzu yangu moja safi na expensive sana kwa sehemu za ukanda ule wote wa Tehran. Fatemeh alinisindikiza mpaka mlangoni nikapigwa good-bye kiss lakini alinisisitiza niache utoto na nisilete usumbufu mara nyingine kwa dereva.

Apo nikajua kumbe bwana dereva alishtaki tayari kama namzingua japo nilimzingua mara moja tu. Kama kawaida tulitumia mda mchache tu kwa speed kali ya gari ile mpaka Tunaingia kwa shahzad.


Nilipofika nyumbani kwa shahzad nilikaribishwa ndani na nikakaa sebuleni kumsubiri mzee mkongwe, na wakati huo nilimbatiza jina nilimuita mjanja wa mzizima.

Hakika shahzad alifurahi sana mara zote alizokua ananiona na furaha yake ilikamilika zaidi tulipokua tunaongea kiswahili.

Shahzad alitokea eneo lile la sebuleni na kumpatia kitu mjukuu wake kisha akiniambia tuelekee chimbo letu ili akanipe nondo za kutosha kwani alidai siku hiyo atakua na muda mchache sana wa kukaa kwenye chumba kile.

Sasa bwana kitu alichotoa shahzad kumpa mjukuu wake ilikua ni kikopo kidogo cheupe kimeandikwa RITALIN kikopo hiki ni kama kile alichokichukua fatemeh siku ile kwenye chumba changu.

Hivyo nilipanga tukiingia ndani ya chumba kile cha maktaba nimuulize ile dawa ilihusiana na nini japo sikupanga kumwambia nimeiona wapi.

MIMI: mzee Samahani ile dawa uliyompa mjukuu wako inaitwaje maana leo sio mara ya kwanza kuiona, nimeshaiona au kukutana nayo mara kadhaa siku za nyuma.

SHAHZAD: ile dawa inaitwa Methylphenidate, inatumika kwenye matibabu ya ugonjwa unaojulikana kama Attention-Deficit Hyperactivity Disorder. Au kifupi huitwa ADHD mara nyingi wataalamu wanatumia jina la psychostimulant kuitaja dawa hii.

MIMI: huo ugonjwa unakuaje maana mjukuu wako namuona ni mzima kabisa hajawahi kuonyesha dosari yoyote tokea nimefika hapa.

Shahzad alidai ugonjwa ule umekaa kisaikolojia sana hivyo ni ngumu kuona dalili kwa mtu mzima ambae ameanza tiba mpaka ukae nae karibu kwa muda mrefu lakini kwa mtoto unaweza kuona dalili hizo mapema.

Kwa mtoto mdogo unaweza kugundua mapema kupitia vitu kama,
  • mtoto anakua careless kiasi cha kutokuweza kutambua hatari, unaweza kuta mtoto anasogelea jiko nakushika moto kwa mikono na ata akiungua huweza kusahau na kurudia tena jambo lile lile.
  • kama yupo lika la shule apa unakuta mtoto kila siku akirudi nyumbani amepoteza aidha daftari au kalamu au begi zima. Mtoto wa hivi utapiga mpaka utamng'oa meno lakini tatizo linatokana na ugonjwa huo tajwa apo juu.
  • jambo lingine mtoto huchelewa sana kuongea ukilinganisha na watoto wengine ambao hawana shida hii.

Shahzad aliuliza nimeiona wapi dawa ile kwani haitolewi kiholela kama dawa nyingine kwa sababu tu Methylphenidate ina pharmacological effects ambazo ni sawa kabisa na cocaine.

Hivyo hupelekea watu wengi kuzitafuta kwa njia zisizo za halali kwa ajili ya matumizi yao binafsi na sio kwa ugonjwa kama inavyotumika na wenye shida hiyo ya ADHD.
 
TUNAENDELEA WAKUU

Fatemeh hakutaka kujibu swali langu, na mimi nilimuuliza kwa makusudi ili tu nimtoe kwenye mood aliyokuwa nayo kuhusu kile tulichokua tunakiongelea. Kitu kingine alichokua anataka ku enjoy fatemeh ni kile kitendo cha kutembea umbali mrefu kidogo kwa mguu.

Hivyo kutokana na ka umbali kalikokuwepo kutoka eneo lile mpaka tulipo egesha gari tulitumia dakika kadhaa kutembea na huku tukiongea mambo mengi. Kwa upande wangu nilimsimulia japo kwa uchache Kuhusu baadhi ya mambo kwenye maisha yangu ambayo niliamini hayajui.

Bilashaka tulienjoy sana siku hiyo kwa upande wangu nilifurahia mazingira yale lakini pamoja na vinywaji vilivyopatikana eneo hilo. Tulibeba kwenye vifungashio vitu kadhaa na wakati tukitembea kuelekea tulipo egesha gari ni wazi yoyote angetuona angeamini tulikuwa wapenzi.

Tukiwa kwenye gari tunaelekea nyumbani fatemeh aliilaza kabisa siti yake na jambo hili lilifanya niweze kuiona vyema shape au umbile lake.

Fatemeh alianza kunizoea kiasi kwamba ata ile desturi ya kijistiri sana akiwa na mimi ilipungua tofauti na kama ilivyokua hapo awali wakati ndio tunafika kutokea haullaga.

Ulikua ni usiku ulioenda sana japo sikumbuki ilikua ni saa ngapi, ila kwa hakika nilimuona fatemeh akiwa amefurahia mtoko ule kwani ulimpunguzia baadhi ya mambo yaliyokua yamejaa kichwani mwake.

Tulikaribia jengo ambalo ndilo lilikua na apartments ambazo alikua anaishi fatemeh, hivyo tulipitiliza moja kwa moja mpaka eneo la basement ambapo tulitakiwa kuegesha gari ile.



Baada ya kufika eneo la basement nilimshtua fatemeh ambae alionekana kuanza kutekwa na usingizi nadhani sababu ya uchovu wa usiku ule.

Fatemeh alinyanyua siti ili aweze kutoka ndani ya gari lakini alikutana na mdomo wangu moja kwa moja na kama kawaida yake hajawahi kupinga zaidi ya kunikimbia ikitokea amepata nafasi.

Tukiwa kwenye moment ile kuna mambo mengi yanabadalika kwenye mwili wa fatemeh hususani joto la mwili na mapigo ya moyo hubadilika ghafla na kupanda wakati huo huo.

Kitu cha tofauti kwa siku ya leo ni kwamba fatemeh alitumia nguvu kubwa kunivuta na kunishikilia ikiwa ni ishara hakutaka tuwahi kumaliza jambo lile haraka haraka ni kwamba alihitaji tutumie muda kidogo.

Jinsi mwili wa fatemeh ulivyokuwa mlaini huwezi amini ukiambiwa alikuwa ni ninja wa kike na kiukweli nilikua natamani sana siku moja nimuone akiwa kwenye harakati hizo za kininja anafananaje.

Siku hiyo tulijitahidi kwenda mbali kwani nilifanikiwa kutoa koti lake refu kwa upande wa juu hivyo nikiwa nakaribia kuitoa blazia. Tulisikia Bonnet inagongwa kwa nyuma na mtu ambaye hatukumjua ni nani.

MIMI: what the f**k
( Ujinga gani huu )

Na wakati ule fatemeh pia alistuka ni kama mtu aliepotelewa na fahamu na hivyo hapo ndio zilikua zinamrudia.

Nilishuka kuonana na mtu huyo wakati fatemeh akijirudishia nguo zake ambazo hakumbuki zilivuliwaje ndani ya dakika chache zile.

Aliyekua anagonga ile bonnet alikua ni askari wa eneo lile na aliongea lugha ambayo siku ifahamu na nilipo muuliza kama anaongea kingereza alijaribu na jambo lake lilikua ni kusisitiza tume park gari sehemu ambayo sio sahihi na ata mimi baada ya kuangalia niligundua ni kweli.

Nilirudi ndani ya gari ili kuhakikisha naiegesha sehemu niliyoelekezwa na yule askari lakini nikiwa Ndani ya gari fatemeh aliuliza niliwezaje kuzitoa nguo hizo kwa dakika chache vile. Sikumjibu zaidi ya kutabasamu tu huku nikiwa makini kuhakikisha sikosei kwa kile nilichokua nakifanya.

Tulishuka na kuelekea eneo la lift ambapo ndani ya muda mchache tulikua tayari ndani ya apartment yetu. Tukiwa ndani nilikumbuka kuwa tumesahau vile vifurushi vilivyokua na bidhaa tulizo rudi nazo toka 30-Tir Street.

Hivyo nililazimika kurudi tena kwenye basement kwa ajili ya kuchukua mizigo ile lakini bado nilimkuta yule askari akiwa maeneo yaleyale.

ASKARI: sorry the new guy, is that your wife?
( Samahan kijana mgeni yule ni mke wako?)

MIMI: no! we friends
( Hapana sisi ni marafiki)

ASKARI: what do we call friends who kiss?
( Tunawaitaje marafiki wanao kiss)

Mpaka hapo nilitabasamu tu nikiamini jamaa kumbe aliona wakati namnyonya fatemeh hivyo ilitosha yeye kusema tulikua wapenzi na hakuna namna ningepinga.

Yule askari alinisifia kwa kusema kama nimeweza kung'oa yule mtoto basi mi ni hatari sana kwani binti huyo hakuwahi kuonekana na mtu yoyote toka ameanza kumjua.

Sio kuonekana kimapenzi tu bali ata kuonekana akiongea na mtu yoyote kwani ni binti ambaye yupo cool masaa 24 siku 7 za wiki. Jamaa alidai yeye pamoja na kukaa hapo sikuzote hajawahi ata kusalimiwa na binti huyo hivyo alijiuliza m'bongo mimi nina nini cha ziada.

Yule askari alikua anaongea maneno mengi sana lakini sikuyatilia maanani zaidi nilitoa snacks zilizo kwenye vile vifungashio na nikampatia asogeze masaa.

Wakati naondoka aliniambia anaitwa Mohamed na ikitokea siku nimepatwa na changamoto yoyote yupo pale nimuone lakini sio changamoto ya pesa wala mapenzi.

Nilirudi kwenye floor yetu chap na moja kwa moja nilienda kwenye room ya fatemeh ambapo nilimkuta ametoka kuoga akiwa na taulo tu. Na aliponiona alishangaa kwanini hakufunga mlango mpaka ameruhusu the African rude boy nimeingia.

Sikujali alichokua anaongea zaidi nilienda moja kwa moja bafuni kuweka mwili sawa na kuondoa uchovu. Fatemeh alisisitiza nisitoke uchi tu kwani hana mpango wa kuona linyoka langu.

Nilipotoka bafuni moja kwa moja nilijitupa kwenye kitanda na fatemeh alisimama kama mtu aliyesusa kulala mpaka niondoke. Nilichofanya pale baharia ni kujifunika shuka vizuri nikimaanisha ndio nimefika apo kama atataka ahame chumba na leo.



Nilipotelea usingizini mpaka asubuhi ambapo nilistuka na kukuta kuna mstari mreefu wa mito ukitutenganisha nilipo lala mimi na alipolala fatemeh. Niliishia kucheka tu na kumchungulia upande wa pili wa mito alipokua amejifunika mwili mzima na kuacha sura tu.

Alipogundua na muangalia alinionyesha ngumi akimaanisha nikimsogelea atanichakaza.

MIMI: you want to break my neck like a gringo in the mine
( Unataka univunje shingo kama mzungu wa mgodini)

FATEMEH: No! Damião lied to you
( Damião alikuongopea)



Nilimwambia haina shida ata kama ni kweli mi nipo tayari kwa lolote ata kama ataniua ni kama nzi kufia juu ya kidonda tu.

Hapo niligundua kuwa fatemeh hakuwa anajua kama nilikua na CV yake ya kimapigano ambayo nilipewa na bwana Damião.

Alinikurupusha kwamba natakiwa kwenda kwa shahzad hivyo nitoke kitandani nisiendelee kumpigisha stories. Nadhani alijua kuwa namlia timing na kama angeruhusu niendelee kuwepo pale dakika tano mbele zingekua nyingi sana na zingenitosha kuhakikisha anabaki kama alivyozaliwa.

Siku hiyo nilijipigilia kanzu yangu moja safi na expensive sana kwa sehemu za ukanda ule wote wa Tehran. Fatemeh alinisindikiza mpaka mlangoni nikapigwa good-bye kiss lakini alinisisitiza niache utoto na nisilete usumbufu mara nyingine kwa dereva.

Apo nikajua kumbe bwana dereva alishtaki tayari kama namzingua japo nilimzingua mara moja tu. Kama kawaida tulitumia mda mchache tu kwa speed kali ya gari ile mpaka Tunaingia kwa shahzad.


Nilipofika nyumbani kwa shahzad nilikaribishwa ndani na nikakaa sebuleni kumsubiri mzee mkongwe, na wakati huo nilimbatiza jina nilimuita mjanja wa mzizima.

Hakika shahzad alifurahi sana mara zote alizokua ananiona na furaha yake ilikamilika zaidi tulipokua tunaongea kiswahili.

Shahzad alitokea eneo lile la sebuleni na kumpatia kitu mjukuu wake kisha akiniambia tuelekee chimbo letu ili akanipe nondo za kutosha kwani alidai siku hiyo atakua na muda mchache sana wa kukaa kwenye chumba kile.

Sasa bwana kitu alichotoa shahzad kumpa mjukuu wake ilikua ni kikopo kidogo cheupe kimeandikwa RITALIN kikopo hiki ni kama kile alichokichukua fatemeh siku ile kwenye chumba changu.

Hivyo nilipanga tukiingia ndani ya chumba kile cha maktaba nimuulize ile dawa ilihusiana na nini japo sikupanga kumwambia nimeiona wapi.

MIMI: mzee Samahani ile dawa uliyompa mjukuu wako inaitwaje maana leo sio mara ya kwanza kuiona, nimeshaiona au kukutana nayo mara kadhaa siku za nyuma.

SHAHZAD: ile dawa inaitwa Methylphenidate, inatumika kwenye matibabu ya ugonjwa unaojulikana kama Attention-Deficit Hyperactivity Disorder. Au kifupi huitwa ADHD mara nyingi wataalamu wanatumia jina la psychostimulant kuitaja dawa hii.

MIMI: huo ugonjwa unakuaje maana mjukuu wako namuona ni mzima kabisa hajawahi kuonyesha dosari yoyote tokea nimefika hapa.

Shahzad alidai ugonjwa ule umekaa kisaikolojia sana hivyo ni ngumu kuona dalili kwa mtu mzima ambae ameanza tiba mpaka ukae nae karibu kwa muda mrefu lakini kwa mtoto unaweza kuona dalili hizo mapema.

Kwa mtoto mdogo unaweza kugundua mapema kupitia vitu kama,
  • mtoto anakua careless kiasi cha kutokuweza kutambua hatari, unaweza kuta mtoto anasogelea jiko nakushika moto kwa mikono na ata akiungua huweza kusahau na kurudia tena jambo lile lile.
  • kama yupo lika la shule apa unakuta mtoto kila siku akirudi nyumbani amepoteza aidha daftari au kalamu au begi zima. Mtoto wa hivi utapiga mpaka utamng'oa meno lakini tatizo linatokana na ugonjwa huo tajwa apo juu.
  • jambo lingine mtoto huchelewa sana kuongea ukilinganisha na watoto wengine ambao hawana shida hii.

Shahzad aliuliza nimeiona wapi dawa ile kwani haitolewi kiholela kama dawa nyingine kwa sababu tu Methylphenidate ina pharmacological effects ambazo ni sawa kabisa na cocaine.

Hivyo hupelekea watu wengi kuzitafuta kwa njia zisizo za halali kwa ajili ya matumizi yao binafsi na sio kwa ugonjwa kama inavyotumika na wenye shida hiyo ya ADHD.
Kwa hiyo fatemeh anaitumia hiyo ADHD kimagendo
 
"Aisee nilikua napika chakula fulani hivi maarufu kama chelow kebab kwa huku Iran"

"Huku" badala ya "huko/kule" ina maana bado upo Iran mzee?
 
"Aisee nilikua napika chakula fulani hivi maarufu kama chelow kebab kwa huku Iran"

"Huku" badala ya "huko/kule" ina maana bado upo Iran mzee?
Nadhani kaongelea kwa wakati uliopo na yeye ni muhusika mkuu hata alipo kua haulaga alikua anaongelea kwa wakati uliopo as if ni kitu kinachoendelea mda huu. Ni sehemu nyingi hasimulii kama ni wakati uliopita labda aliya nukuu matukio.
 
Wiki imeisha toka utume Last episode[emoji848][emoji848]
Broo story inapoteza mvuto kabisa ndio maana hata watu hawaulizii kama mwanzoni .
 
Back
Top Bottom