Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Nadhani umeandika hoja MUHIMU yenye kushika hisia, na hivo kuna hatari ya kuzuia fikra yakinifu, tusipokuwa Makini wote tutashiriki kujilaani, kulaumu watu na kukosa hata mawazo suluhishi.

Katika kuelewa Jambo ili ulihukumu yapaswa akili na fikra yakinifu vishirikiane.
Mimi naungana na wasemao Tanzania ni tajiri sana Kwa minajiri ya rasilimali tulizonazo, bali tunaishi katika umaskini. Nadhani aliyetoa hoja hii na hata wengine walosimamia walibeba lengo jema la kuamsha tujitambue na tutazame tumejikwaa wapi ili ikiwezekana tujisahihishe ili tuanze mkakati wa kuutumia utajiri ghafi wa nchi kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa nchi na watu wake.

Natoa mfano; mwanafunzi ambaye anafeli sana mitihani lakini mwalimu wake akatambua kuwa ni mwenye uwezo mkubwa wa kuweza kufanya vizuri katika masomo yake, ili kumepower huyo mwanafunzi mwalimu atamwambia wewe ni mwanafunzi mwenye uwezo kimasomo, kisha atamweleza wapi anakosea na achukue hatua zipi, wewe usikiaye, tena Kwa kukosa tafakuri utambeza mwalimu Kwa kutazama matokeo ya sasa, ni ujinga Tu unaokuendesha, au wewe mtumwa sehemu fulani na umeaminishwa kwamba jamii yenu ilizaliwa kutumikishwa na kuishi katika hali ya umaskini, kisha anakuja mwenye akili anayetambua ukweli juu ya asili yako kwamba waweza kuwa huru na ukatafuta Mali hata kuwa tajiri na kutawala wengine. Mtu huyu ameenda mbali zaidi akijua historia ya vizazi vyako kwamba walikuwa wafalme, machifu na watu wenye utajiri mkubwa, mtu huyu atakuamsha Kwa kukuambia hivi wewe ndugu unafahamu kwamba WEWE NI MTAWALA WALA SI MTUMWA NA PIA WEWE NI TAJIRI SANA? That is an alert to you to discover yourself it makes you aware na itafanya uanze kujitafuta wapi ulikosea hata kuwa na hali hii, hiyo ni empowering of one self. Inatumika Kwa wachezaji, mwanasiasa mwenye kipaji hicho pasipo kukitambua n.k. Ni Sawa na kuona kipaji cha mtoto juu ya muziki na ukamwambia hivi unafahamu kuwa wewe ni zaidi ya mwanamuziki Fulani ( maarufu na mwenye mafanikio) Sasa ukiwa mjinga utaishia kubisha kwamba yule mtumwa si mtawala wala si tajiri ni masikini tu, au yule mtoto si lolote si chochote katika muziki, na kwa wakati huo ni kweli juu ya Hali zao hao.
Hii ni kukosa akili pembuzi iwezayo kutafsiri na kuchanganua maudhui ya Jambo fulani na nguvu ibebayo kufanikisha Jambo husika. Hiyo ndo akili ndogo, pia ni ujinga.

Hebu fikiria kidogo, tutegemee mawazo yako uliyoandika kukomboa taifa toka umaskini, tunatokaje, hata ukiitwa ushauri utashauri nini zaidi ya kubariki mzungu aliyekulaani Kwa kukufananisha na nyani.

Kuna tatizo kubwa sana juu ya sisi wabeba hoja tudhaniazo ni hoja jadidu na yakinifu, tatizo hili ni kutetea au kulaani jambo pasipo uelewa wa kina, kwa mfano unayoyasema juu ya jamii zetu, kuwa wachafu, wasiojali mazingira, tegemezi, wenye kulaumu laumu tu, walojaa ubinafsi, watesi juu ya jamii yao wenyewe na mwingine mengi. Naandika tena Kwa herufi kubwa, HAKUNA JAMII YOYOTE ISIYOPITIA HAYO, HAIPO DUNIANI HAIPO. Kikubwa wao hawakujilaani, na kwa bahati hakuwepo wa kuwalaani, wakasumbuliwa na hayo huku wakitafuta namna ya kujikwamua.

Cha kusikitisha ni pale mleta hoja nadhani kwa ujinga tu au Kwa hasira juu ya mawazo fulani inatolea mfano jamii zilizoendelea kama kwamba zilizaliwa hivyo, brother kuna kazi imefanyika na ilianzishwa na wachache wenye fikra yakinifu, ndugu yangu HAKUNA JAMII YENYE WATU WAADILIFU NA WENYE AKILI TUUU PASIPO JUHUDI ZA WACHACHE WENYE KUTHUBUTU KUFUTA UJINGA WA WENGI.

Hivi unafahamu waafrika wengesema watu wa jinsia moja waoane kinyume kabisa na nature, tungeitwa hata mavi, Hilo kwako si shida, hawa watu wamepitia mengi maovu, ujambazi ulokithiri, kupigania uongozi, Vita vya kiraia, uuwaji watu wadhaniwao kuwa wachawi, vipindupindu, kunya bila kujisafisha na mengineyo.

Nini kifanyike. HAMNA HAJA YA KUJILAANI. Tunaweza kujikwamua toka ujinga huu na umaskini huu Ila si Kwa kutegemea mikakati ya wengine ambao kimsingi ni wafaidika wakubwa wa rasilimali zetu, tuweke malengo yetu wenyewe kama ni elimu tuwe very selective and serious tukitengeneza mitaala itayolenga utumizi mzuri wa rasilimali zetu, Pia kubadilisha mtazamo juu yetu wenyewe, kuwa na utashi wa kisiasa hili halitafanikiwa over night ni mchakato mfano kuandika au kuigiza mawazo ya namna ambayo yataamsha watu na kujitambua. Sisi waandikaji tuandike pasipo kuchoka, watu watakapochoshwa na kuona hatma ya maisha yao ipo mashakani watajitafuta kwa kurudia maandiko kama haya, historia yao na kutafuta wapi wamejikwaa.

Angalizo: Kwa mitazamo tuliyonayo sasa hasa wasomi na wanaodhani kuwa wanaharakati wa taifa hili, HATUTAMUELEWA KIRAHISI ALIYEBEBA MAONO YA KWELI YA KUJIKWAMUA TOKA MADHILA HAYA. Maana matatizo yetu ni complex alafu tunakazana kuyatatua kwa simple means.

Ukikuta wasomi wanavoainisha mbinu za kufikia maendeleo ya kweli na kufuta umaskini, utaona ni raisi mno, na Kwa mtindo huo basi nchi zote zingekuwa zimejikwamua toka umaskini na kuwa tajiri.

Naamini njia za maendeleo si njia nyeupe na za wazi, na yeyote azijuaye wanyonyaji wetu hupiga kelele usiku na mchana wakituaminisha huyo siye.

Wengi walozitoa nchi zao walau kwa kiwango fulani na kufanya zijitegemee, hawakufuata njia za uchumi kwa mazoea.

NAAMINI SOTE TUNA LENGO MOJA, NA HIZI NDO HARAKATI ZA KUJITAFUTA TUMEJIKWAA WAPI.

Tusijibanze nyuma ya uhasama wa kisiasa, tuwe watumwa wa ukweli tutachambua pasipo kupepesa.

Akili zipi ni akili kweli katika kujikomboa kutoka umaskini na ujinga tuuishio sasa. Hilo nadhani ni swali kwetu.
Niaminivyo hata hawa viongozi wetu huwa nadhamira ya kujiondoa katika MADHILA HAYA Ila hukwama katika njia, na wengi huchagua kukomboa maisha yao Tu. Ili tuendelee tunauhitaji njia zote, huo ndo ukqeli, yaani njia halali na haramu, busara na uwehu, upole na unabe, demokrasia na penginepo pasipo demokrasia, mawazo shirikisho na muda mwengine wazo la kijasri pasipo ushirikiahaji, kufuta Sheria na pengine kuvunja Sheria, ukweli na uwazi na pengine uwongo na uficho, yote yalenge kujenga taifa na watu wake. Maendeleo ni Complex by nature.
 
Bara la Afrika Ina watu takribani billion 1.35 Taifa la Uswis lina watu million 8.97 Taifa la Uswis kiuchumi linabeba bara Zima la Afrika kwasababu Africa imebeba mabilioni ya watu wajinga.

Kiukweli maendeleo ni rasilimali watu wenye ubongo pevu na si vitu
Hongera mleta mada

Nyerere Kwenye moja ya hotuba zake aliwahi kusema kanchi Ka ubeligiji licha ya udogo wake lakini Bars la Afrika nzima likisema lipambane nacho kivita hatutoboi.

Sijui tunatatizo gani
 
Watanzania Kodi hatutaki kutoa alafu ndio wakwanza kulalamika.
Lakini pia ukitoa Kodi kuna wenye uroho wanazitumbua kifisadi Kwa mambo Yao binafsi na kujineemesha wenyewe. Hapo ndipo msala Ulipo.

Serikali ilikuwa inahitaji watu sampuli ya kina Nyerere ndio washike nyazifa za juu. Watu wasio na tamaa ya Mali.
Lakini watu sampuli ya kina Nyerere ni wachache Mno sio ajabu nchi nzima wasifike 10.

Watoto wanakuzwa kibinafsi hivyo wakikua nao wanakuwa wabinafsi
Kwa kesi ya kina mzee Mwamindi!Bado hata yeye Nyerere hakuwa na maono sahihi ya kukuza uchumi kupitia rasilimali watu.
Kitendo cha kutaka watu waliobweteka na wavivu wagawiwe mashamba ambayo mtu ametumia akili na maarifa kuyafanya kuwa na thamani,nao ulikuwa ni kutumia akili vibaya.
Na matokeo yake ndiyo haya ya sasa watu wengi akili zao kuzielekeza kwenye kutafuniwa tu na serikali.
 
Nchi ni nini ?

Kumbuka pia sehemu inhabitable kutakuwa hakuna hata hao watu..., na sehemu ambayo ni hospitable all the brains in the world will go there, (immigrate)...

That's what happened to America when it used to be land of the free / opportunity... (not anymore)

Pili Utajiri ni nini ?

Babu yangu aliyekuwa anaweza kulala nje weather ni nzuri haitaji hata AC; na kuna mto hapo anaweza kupata chakula chake (samaki) na matunda natural yanaanguka yeye anayaokota unaweza kumfananisha kwa utajiri na kipindi hicho mtu aliyekuwepo Egypt (though more advanced hadi anafanya irrigation; necessity being the mother of invention)...,

Au Red Indians waliokuwa wanaishi in an ecosystem na wanyama wengi wanaowapatia nyama kwa kuwavuna (Je walikuwa masikini kuliko the wanyanganyi waliowamarginalize later ?, au hao masikini walitumia unyanganyi kuwapora utajiri wao)?

Just showing you thing are not black or white; lot of grey areas and one happenstance leads to another...., Africa (with resources) is where its at because of a lot of marginalization ; na mizani ya utajiri ina-depend your perspective...
 
UTAJIRI WA NCHI NI AKILI ZA WATU, SIO RASILIMALI KAMA MADINI N.K.

Anaandika, Robert Heriel.

Huwaga namshangaa mtu anayesema nchi yetu ni Tajiri. Kwa kweli sio tuu anachekesha Bali pia anaonyesha jinsi alivyokuwa mjinga na asiyeweza kufikiri sawia.

Kama nikiulizwa hivi leo sababu gani inatufanya Waafrika ikiwemo nchi yetu kuwa Masikini, basi jibu litakuwa ni kuwa Sisi tunaakili ndogo Kama sio kuwa hatuna Kabisa.

Taifa ili kiwe Tajiri linahitaji watu wenye akili zaidi kuliko Rasilimali. Utajiri ni Akili na sio wingi wa Rasilimali.
Kuna msemo usemao, penye miti hapana wajenzi.

Akili ndio inaweza kufanya madini kuwa Rasilimali Kwa kuipa Value. Madini kama madini hayajui kama yenyewe ni yathamani, Ila wenye akili ndio wanajua thamani ya madini hayo kutokana na matumizi waliyoyabuni kwayo.

Kidunia Bara la Afrika ndilo bara lenye malighafi nyingi kuliko bara lolote lile. Lakini watu wake wameshindwa kuzigeuza malighafi hizo kuwa Rasilimali Kwa kuzipa thamani.

Ukisikia mtu anakuambia Yeye ni Tajiri Kwa sababu nchi yake inamadini, maziwa na Mito, Ardhi yenye Rutuba, wanyama wa kuvutia, na mambo mengine lakini watu wake ni Hali zao za maisha ni duni jua mtu huyo hajui kufikiri vizuri, na pengine akawa mwendawazimu.

Nchi haiwezi kuwa Tajiri Kama ndani yake inawatu wajinga wengi. Watu wasio na akili wakiwa wengi ndivyo nchi inavyozidi kuwa Masikini.

Mtu asiye na akili Hana tofauti na mnyama wa porini, ni Sawa na tumbili au ngedere anayeishi msituni ananyeshewa mvua na kuchomwa na Jua lakini anashindwa kujenga nyumba hata ya mbao Kwa sababu ya upeo mdogo wa Akili.

Wazungu walivyotuita Waafrika manyani kuna watu walifikiri walimaanisha maumbile yetu yanafanana na nyani😀😀 Kama nawe ulifikiri hivyo basi nawe upo kundi la watu wajinga.

Wazungu walituita manyani mbali na ubaguzi wao lakini walituona akili zetu hazijaachana Sana na tumbili na nduguye ngedere.

Nyani au ngedere ukimpelekea Dhahabu au Almasi wala hataiona inatofauti na jiwe jingine. Kutokana na upeo mdogo wa Akili.

Sisi Watanzania wengi wetu tunaakili ndogo mno na hiyo ndio sababu Sisi sio matajiri. Na tutaendelea kuwa Vivi hivi Kwa Karne kadhaa zijazo.

Watanzania wengi ni Kama wanyama Kwa mambo mengi, kama unavyomuona ng'ombe basi ndivyo wengi wetu tulivyo.

Sio ajabu ukakuta watu kwenye makazi Yao kuna mavi au maji machafu waliyoyasababisha yamewazunguka, yananuka na nzi wamejaa lakini wao hawaoni Shida. Wanalala, wanakula hapohapo, na wanakunya na kukojoa hapohapo.

Hapo ati wanasubiri kiongozi aje awaambie wawe wasafi tena wengine ifikie hatua ya kupelekwa serikali za mitaa kisa anaambiwa asizibue chemba za mavi yake na familia yake, come on!

Sio ajabu jitu linakunya chooni labda cha umma alafu hali-flash uchafu wake. Hivi mtu huyo anatofauti ipi na Mnyama?

Mtu anajua kabisa ili aishi anatakiwa awe na chakula cha kutosha kinachomtosha yeye na familia yake, badala awe na ghala la kuhifadhi chakula kinachomtosha yeye na watoto wake angalau Kwa miaka miwili kulingana na Hali ya hewa.

Yeye anakula Kama mnyama asijue kesho atakula nini. Halafu ikifika kesho anaanza kumlalamikia mtu mwingine labda ni serikali au viongozi. Jamani hivi tunaakili kweli?

Tena wakati mwingine tunazidiwa akili hata na Wanyama.

Hakuna mnyama ambaye atazaa watoto ambao hawezi Kuwatunza. Hakuna na hajawahi kutokea. Mfano Kuku anaouwezo wa kutaga mayai hata Mia moja.

Lakini atataga mayai kumi (10-12) kulingana na uwezo wake wakuyaatamia, sio atage mayai 20 alafu wakati wa kuatamia mengine ashindwe kuyaatamia yajitokeze nje.

Kisha Kwa mayai 10-12 anaouwezo wa kuwachunga na kuwakuza watoto hao.

Halikadhalika na mbwa, ng"'ombe, mbuzi, Simba n.k.

Lakini Sisi unakuta mtu anazaa watoto nje ya uwezo wake wa Kuwatunza, labda watoto 10 alafu ananilaumu serikali kuwa gharama za Shule au hospitali ziondolewe.

Au anaomba msaada Kabisa wa kusaidiwa kulelewa watoto.

Hivi tumelogwa au ni kitu gani?

Mtu unajua kabisa miti ndio huleta hewa Safi, huleta mvua na kivuli kizuri, na Kupunguza joto la nchi. Alafu unakuta watu wamekata miti mtaa mzima ili wajenge nyumba.

Unashangaa mtaa mzima miti ipo 20 Kwa eneo la kilometa moja. Alafu muda huohuo unasikia mwehu akipiga kelele jamani joto Kali, jamani jua linawaka! Mara kiyama kinakaribia.

Kiama ya mavi. Ujinga na wehu wako ndio unaita Kiyama?

Utajiri WA nchi ni akili za watu na sio Rasilimali Kama madini.

Chakufanya;
I. Tujifunze kuwa na Akili ili tuwe nchi yetu itajirike.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Nadhani umeandika hoja MUHIMU yenye kushika hisia, na hivo kuna hatari ya kuzuia fikra yakinifu, tusipokuwa Makini wote tutashiriki kujilaani, kulaumu watu na kukosa hata mawazo suluhishi.

Katika kuelewa Jambo ili ulihukumu yapaswa akili na fikra yakinifu vishirikiane.
Mimi naungana na wasemao Tanzania ni tajiri sana Kwa minajiri ya rasilimali tulizonazo, bali tunaishi katika umaskini. Nadhani aliyetoa hoja hii na hata wengine walosimamia walibeba lengo jema la kuamsha tujitambue na tutazame tumejikwaa wapi ili ikiwezekana tujisahihishe ili tuanze mkakati wa kuutumia utajiri ghafi wa nchi kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa nchi na watu wake.

Natoa mfano; mwanafunzi ambaye anafeli sana mitihani lakini mwalimu wake akatambua kuwa ni mwenye uwezo mkubwa wa kuweza kufanya vizuri katika masomo yake, ili kumepower huyo mwanafunzi mwalimu atamwambia wewe ni mwanafunzi mwenye uwezo kimasomo, kisha atamweleza wapi anakosea na achukue hatua zipi, wewe usikiaye, tena Kwa kukosa tafakuri utambeza mwalimu Kwa kutazama matokeo ya sasa, ni ujinga Tu unaokuendesha, au wewe mtumwa sehemu fulani na umeaminishwa kwamba jamii yenu ilizaliwa kutumikishwa na kuishi katika hali ya umaskini, kisha anakuja mwenye akili anayetambua ukweli juu ya asili yako kwamba waweza kuwa huru na ukatafuta Mali hata kuwa tajiri na kutawala wengine. Mtu huyu ameenda mbali zaidi akijua historia ya vizazi vyako kwamba walikuwa wafalme, machifu na watu wenye utajiri mkubwa, mtu huyu atakuamsha Kwa kukuambia hivi wewe ndugu unafahamu kwamba WEWE NI MTAWALA WALA SI MTUMWA NA PIA WEWE NI TAJIRI SANA? That is an alert to you to discover yourself it makes you aware na itafanya uanze kujitafuta wapi ulikosea hata kuwa na hali hii, hiyo ni empowering of one self. Inatumika Kwa wachezaji, mwanasiasa mwenye kipaji hicho pasipo kukitambua n.k. Ni Sawa na kuona kipaji cha mtoto juu ya muziki na ukamwambia hivi unafahamu kuwa wewe ni zaidi ya mwanamuziki Fulani ( maarufu na mwenye mafanikio) Sasa ukiwa mjinga utaishia kubisha kwamba yule mtumwa si mtawala wala si tajiri ni masikini tu, au yule mtoto si lolote si chochote katika muziki, na kwa wakati huo ni kweli juu ya Hali zao hao.
Hii ni kukosa akili pembuzi iwezayo kutafsiri na kuchanganua maudhui ya Jambo fulani na nguvu ibebayo kufanikisha Jambo husika. Hiyo ndo akili ndogo, pia ni ujinga.

Hebu fikiria kidogo, tutegemee mawazo yako uliyoandika kukomboa taifa toka umaskini, tunatokaje, hata ukiitwa ushauri utashauri nini zaidi ya kubariki mzungu aliyekulaani Kwa kukufananisha na nyani.

Kuna tatizo kubwa sana juu ya sisi wabeba hoja tudhaniazo ni hoja jadidu na yakinifu, tatizo hili ni kutetea au kulaani jambo pasipo uelewa wa kina, kwa mfano unayoyasema juu ya jamii zetu, kuwa wachafu, wasiojali mazingira, tegemezi, wenye kulaumu laumu tu, walojaa ubinafsi, watesi juu ya jamii yao wenyewe na mwingine mengi. Naandika tena Kwa herufi kubwa, HAKUNA JAMII YOYOTE ISIYOPITIA HAYO, HAIPO DUNIANI HAIPO. Kikubwa wao hawakujilaani, na kwa bahati hakuwepo wa kuwalaani, wakasumbuliwa na hayo huku wakitafuta namna ya kujikwamua.

Cha kusikitisha ni pale mleta hoja nadhani kwa ujinga tu au Kwa hasira juu ya mawazo fulani inatolea mfano jamii zilizoendelea kama kwamba zilizaliwa hivyo, brother kuna kazi imefanyika na ilianzishwa na wachache wenye fikra yakinifu, ndugu yangu HAKUNA JAMII YENYE WATU WAADILIFU NA WENYE AKILI TUUU PASIPO JUHUDI ZA WACHACHE WENYE KUTHUBUTU KUFUTA UJINGA WA WENGI.

Hivi unafahamu waafrika wengesema watu wa jinsia moja waoane kinyume kabisa na nature, tungeitwa hata mavi, Hilo kwako si shida, hawa watu wamepitia mengi maovu, ujambazi ulokithiri, kupigania uongozi, Vita vya kiraia, uuwaji watu wadhaniwao kuwa wachawi, vipindupindu, kunya bila kujisafisha na mengineyo.

Nini kifanyike. HAMNA HAJA YA KUJILAANI. Tunaweza kujikwamua toka ujinga huu na umaskini huu Ila si Kwa kutegemea mikakati ya wengine ambao kimsingi ni wafaidika wakubwa wa rasilimali zetu, tuweke malengo yetu wenyewe kama ni elimu tuwe very selective and serious tukitengeneza mitaala itayolenga utumizi mzuri wa rasilimali zetu, Pia kubadilisha mtazamo juu yetu wenyewe, kuwa na utashi wa kisiasa hili halitafanikiwa over night ni mchakato mfano kuandika au kuigiza mawazo ya namna ambayo yataamsha watu na kujitambua. Sisi waandikaji tuandike pasipo kuchoka, watu watakapochoshwa na kuona hatma ya maisha yao ipo mashakani watajitafuta kwa kurudia maandiko kama haya, historia yao na kutafuta wapi wamejikwaa.

Angalizo: Kwa mitazamo tuliyonayo sasa hasa wasomi na wanaodhani kuwa wanaharakati wa taifa hili, HATUTAMUELEWA KIRAHISI ALIYEBEBA MAONO YA KWELI YA KUJIKWAMUA TOKA MADHILA HAYA. Maana matatizo yetu ni complex alafu tunakazana kuyatatua kwa simple means.

Ukikuta wasomi wanavoainisha mbinu za kufikia maendeleo ya kweli na kufuta umaskini, utaona ni raisi mno, na Kwa mtindo huo basi nchi zote zingekuwa zimejikwamua toka umaskini na kuwa tajiri.

Naamini njia za maendeleo si njia nyeupe na za wazi, na yeyote azijuaye wanyonyaji wetu hupiga kelele usiku na mchana wakituaminisha huyo siye.

Wengi walozitoa nchi zao walau kwa kiwango fulani na kufanya zijitegemee, hawakufuata njia za uchumi kwa mazoea.

NAAMINI SOTE TUNA LENGO MOJA, NA HIZI NDO HARAKATI ZA KUJITAFUTA TUMEJIKWAA WAPI.

Tusijibanze nyuma ya uhasama wa kisiasa, tuwe watumwa wa ukweli tutachambua pasipo kupepesa.

Akili zipi ni akili kweli katika kujikomboa kutoka umaskini na ujinga tuuishio sasa. Hilo nadhani ni swali kwetu.
Niaminivyo hata hawa viongozi wetu huwa nadhamira ya kujiondoa katika MADHILA HAYA Ila hukwama katika njia, na wengi huchagua kukomboa maisha yao Tu. Ili tuendelee tunauhitaji njia zote, huo ndo ukqeli, yaani njia halali na haramu, busara na uwehu, upole na unabe, demokrasia na penginepo pasipo demokrasia, mawazo shirikisho na muda mwengine wazo la kijasri pasipo ushirikiahaji, kufuta Sheria na pengine kuvunja Sheria, ukweli na uwazi na pengine uwongo na uficho, yote yalenge kujenga taifa na watu wake. Maendeleo ni Complex by nature.

Sijakuelewa mkuu,unapinga au unakubaliana na mtoa mada,kuwa hakuna utajiri pasi kuwa na akili?
Utajiri wa Kwanza ni akili,bila akili Unaweza kuwa na ng'ombe 1000 afu ukafungwa kwa deni la 800,000😄😄

Yanatukuta Tanzania leo,nenda Mbeya(tukuyu) ushangae shida ya maji inayokumba wananchi ilhali wamezungukwa na mito kila kona!!Watanzania tunahitaji tubikiri bongo zetu la sivyo tutabaki masikini hata Karne ijayo.
 
Watu, ardhi, siasa safi, na uongozi bora.
Shukrani sana mkuu 'denooJ'.

Mada hii ni kati ya mada nzito sana inayostahiri kujadiliwa kwa kina zaidi, lakini naona wachangiaji tunajirusharusha tu na mambo mengine kabisa yasiyohusiana na mada yenyewe.

Wengi wetu tunakimbilia tu kwa hao "watu", na kuanza kuwashambulia, utadhani hawa ni watu tofauti na watu waliopo kwenye mataifa mengine yaliyoweza kuleta maendeleo kwa kuwatumia watu wao.

Tanzania tuna hazina nzuri sana ya watu, ambao wapo tayari kuongozwa ili walete maendeleo yao wenyewe.

Ardhi safi kabisa tunayo, tena yenye raslimali za kila aina ndani yake,... hao watu wapo tayari kabisa kuzitumia raslimali hizi, ardhi, na vyote vilivyomo ndani yake na juu yake, kuleta mabadiliko katika hali zao za maisha

Vitu ambavyo bado hatujabahatika navyo ni hivyo viwili vya mwisho - "Siasa Safi", na "Uongozi Bora." Ombwe letu lipo hapa.
 
Nchi ili ipate maendeleo Jambo kubwa kuliko yote ni Akili.
Kama Watu hawana akili hata wangeishi peponi lazima pangedorora.
Hao watu wenye akili hupatikana wapi na vipi?
Uliwahi lini kusikia kwamba kuna nchi isiyokuwa na watu wenye akili.

AKILI - kwako ni kitu gani hasa?

Kutokana na mwandiko wako hapa jukwaani nina hakika huna uwezo wa kuyajibu hayo maswali niliyokuuliza.
 
Kwa akili yako unadhani Mimi ni mtu wa kueleweshwa mambo madogo Kama hayo?

Nilichoelez ndicho hichohicho,
Wewe ndio Kwa vile upeo wako ni mdogo huwezi kuelewa ninazungumzia kitu gani.
Dah!

Mkuu 'ROBERT HERIEL', utaniwia radhi, kwani hii ndiyo mara yangu ya kwanza kabisa kukuona na kukusoma humu ndani ya jukwaa hili, kwa hiyo sina uzoefu nawe kabisa.

Kutokana na nilichosoma ndani ya andiko lako, kamwe siwezi kukupa hiyo sifa unayojibinafsisha nayo ya kuwa "melewa wa mambo" kama unavyojitangazia.

Kama kuna kundi la "watu wenye AKILI", ambalo unategemea kuwa ndio wenye uwezo wa kuleta maendeleo, na wewe ukajihesabu kuwa mmoja wa watu hao wenye akili, sina shaka yoyote kwamba nchi hiyo itakuwa ya ujuha mkubwa sana..

Ngoja niishie hapo.
 
😀😀😀
Kamuonyeshe Mchumba wako ulicho-comment alafu mpe na Mada niliyoandika alafu utaona Nani anafaa kuambiwa pole.

Embu kaa, tulia, soma Mada uolewe, kisha Kama umeamua kupinga uje Kwa hoja.
Na sio uje ujivue nguo hapa alafu hujatoa hoja yoyote.

Labda ningekuuliza, Mada hii dhamira yake kuu ni ipi?
Jibu la swali: "Watu wenye Akili".

Hii ni kwa mjibu wa mada yako, mimi sijatunga jibu.

Sasa kama huoni ujinga wa hali ya juu sana juu ya jibu hilo, sitaweza kushangaa kwa sababu ya akili inayokuongoza wewe.
 
Huyo Achana Naye, ni sampuli ya watu wapumbavu ambao wakiwa mbele za watu hasa kwenye mijadala wanajifanya wako na hoja lakini katika maelezo Yao watakayoyatoa hakuna kitu cha maana wanachozungumza.

Yaani ni ili Naye aonekane anauwezo na anakitu chakuongea kumbe hamnazo.
Huyo ndiye mwenye "Akili mwenzio"?
Hivi umesoma aliyobandika hapo na mimi nikamjibu?
, nawe hapa kuja kusifua?

Huna kitu kichwani mkuu, nami huwa sina subira wala wakati wa kuhangaika na takataka kama hizo.
Endelea na akili zako mbovu.
 
Mbaya zaidi waliopo juu kwenye uongozi wengi ni weupe mpaka huruma. Unajiuliza kama kiongozi wao yupo hivi wananchi watakuwaje. Tz haina huo utajiri katika nyanja zote iwe ni siasa, maofisini, michezo nk

Mbaya zaidi awamu ya 5 na 6 watu wanaotumia akili hawatakiwi
Kipngozo mkuu ndo mweupe kwanza akifutiwa na akina nape na januari
 
Ulichokisema ni sahihi mkuu,akili yako huwa inafanya kazi sana,mara nyingi unatemaga madini tu

Kuna vinchi vinategemea bahari tu lakin viko mbali mno,raia wake wanaishi kama wako peponi
 
Hakuna mnyama ambaye atazaa watoto ambao hawezi Kuwatunza. Hakuna na hajawahi kutokea. Mfano Kuku anaouwezo wa kutaga mayai hata Mia moja.

Lakini atataga mayai kumi (10-12) kulingana na uwezo wake wakuyaatamia, sio atage mayai 20 alafu wakati wa kuatamia mengine ashindwe kuyaatamia yajitokeze nje.

Mkuu hapo juu umenichekesha sana,mkuu nakupa salute una akili sana,unawekaga madini sana humu
 
Ukiwachukua watanzania wote kuwahamishia Marekani, na wamarekani wote wahamie Tanzania baada ya miaka kumi, Tanzania itakuwa super power! Na baada ya miaka kumi na tano Marekani itakuwa Third World country!

Tatizo la Waafrica (watanzania) siyo udongo ni UBONGO!
 
Hakuna mnyama ambaye atazaa watoto ambao hawezi Kuwatunza. Hakuna na hajawahi kutokea. Mfano Kuku anaouwezo wa kutaga mayai hata Mia moja.

Lakini atataga mayai kumi (10-12) kulingana na uwezo wake wakuyaatamia, sio atage mayai 20 alafu wakati wa kuatamia mengine ashindwe kuyaatamia yajitokeze nje.

Mkuu hapo juu umenichekesha sana,mkuu nakupa salute una akili sana,unawekaga madini sana humu
Hili la kuku kutaga ni la asili tu (natural). Kuku hapangi idadi ya mayai ya kutaga.
Tusidanganyane na kujisifu wenyewe.
 
Back
Top Bottom