Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Nchi hii ina mambo, mfano kisiwa cha Ukerewe kimezungukwa na maji baridi safi ya ziwa Victoria. Lakini wakaazi wanalalamika ukame, bei ya vyakula kuwa juu n.k

Je uongozi wa mkoa wa Mwanza wameshindwa kukigeuza kisiwa cha Ukerewe kuwa shamba-darasa kwa kuwawezesha wakulima wote kufanya kilimo cha umwagiliaji chanzo kikiwa ni ziwa hilo lilolizunguka kisiwa hicho chote.

Nina uhakika kisiwa hicho kinaweza kuzalisha mazao ya chakula kwa wingi kwa kilimo cha kisasa na cha umwagiliaji, na kutumia tunu alioijalia kisiwa hicho kiwe mfano kwa uzalishaji mkubwa wa nafaka kama nchi ya Ukraine.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe​



Kilimo​

Mazao yalimwayo kwa wingi katika Wilaya ya Ukerewe yenye visiwa 38 japo visiwa 15 vinatumika kama maeneo ya uvuvi ni muhogo, viazi vitamu, mpunga, matunda aina ya machungwa, maembe, mananasi, mapapai, kahawa, migomba, mazao ya

ndizi.jpg
bustani na mazao ya jamii ya kunde kama vile maharage, njugu mawe na kunde. Mazao mengine yanayolimwa kwa kiasi kidogo ni mtama na rosella (choya). Mazao haya yanalimwa katika eneo la Ha.33, 765.5Ardhi iliyopo ni ndogo kuruhusu kilimo cha kupumzisha mashamba. Kwa hali hiyo kilimo kinahitaji kifanyike kwa tija ili uzalishaji wa mazao uweze kukidhi mahitaji ya wananchi wote ambao kulingana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ni 347,145. Zao la alizeti linatiliwa mkazo badala ya zao la pamba ambalo katikamiaka ya 1970 lilikuwa zao maarufu la biashara ambalo lilikuwa linawapatia wakulima kipato. Lakini kutokana na upungufu wa ardhi hasa ukizingatia kuwa zao hili halitakiwi kuchanganywa na mazao mengine pamoja na kushuka kwa bei, zao hili lilionekana kutofanya vizuri.
Idara ya Kilimo ili iweze kutekeleza vyema ilani ya Uchaguzi ya CCM ni lazima ihakikishe inatekeleza majukumu mbalimbali ya msingi ili kuleta tija katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara, kuendeleza na kuboresha huduma za ugani ikiwa ni pamoja na kuwezesha wakulima kuwa na vyama vya ushirika vilivyo hai na vyenye nguvu ya mtaji. Aidha kuwawezesha wakulima kuunda vikundi ili waweze kuwa na umoja wenye nguvu katika kufikisha bidhaa zao katika masoko ya mazao yao. Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ina jumla ya Vyama Vya Ushirika 71 vilivyoandikishwa chini ya Sheria Na.6 ya mwaka 2013 ya Vyama Vya Ushirika. Idadi ya VICOBA vilivyopo ni 150. Vyama vilivyo vingi vinakabiliwa na matatizo mbalimbali ambayo yanapelekea vyama hivyo kutofanya vizuri. halmashauri inakabiliwa na upungufu wa wataalam 4 wa Ushirika kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji wa vyama hivyo ikiwa ni pamoja na kufanya ukaguzi wa mahesabu. Ili haya yaweze kufanyika kwa ufanisi Maafisa Ugani wanatakiwa kuboreshewa mazaingira yao ya kufanyia kazi. Maboresho hayo ni pamoja na kupatiwa nyumba za kuishi katika maeneo yao na kuwezeshwa vyombo vya usafiri hususani pikipiki ili kuwawezesha kuwafikia wakulima kwa urahisi na kwa muda muafaka pale huduma za ugani zinapohitajika.

banio.jpg
Pamoja na Serikali kutilia mkazo juu ya kilimo cha umwagiliaji wakulima bado wanategemea mvua katika kilimo. Hii ni kutokana na kutokamilika kwa miundo mbinu ya umwagiliaji katika skimu za Bugorola na Miyogwezi. Miradi hii imekwamakukamilika kutokana na ukosefu wa fedha licha ya Ofisi hiyo ya Umwagiliaji

Source : Kilimo
 
Ujinga mtupu yaani tuna raw materials za kila aina lakini kutwa tunaomba misaada Ulaya, sababu kubwa ni kukosa akili
Ukitaka kujua hii nchi imejaa wapumbavu , tumeshindwa kutumia hata chuma kule Liganga na mchuchuma kuanza kuzalisha bidhaa za kilimo ,ujenzi nk ili tuondokane na utegemezi wa bidhaa toka nje ya nchi ambapo tunapoteza pesa nyingi za kigeni , wapumbaf huko serikalini ukiwauliza watakupa visingizio vya kiduwanzi mpaka utatamani kulia .
 
Kila binadamu ana akili.

Tutofautishe akili na nyanja za fikara kama kuchakata data, kufanya maamuzi, kuhifadhi kumbukumbu, kukariri maarifa, kuthamanisha vitu, kuvumbua mambo mapya, kujenga taswira kubwa kutoka kwenye mambo madogo au kupata vingi kwa kutumia vichache, na kutumia yote haya kutatua matatizo kwenye maisha kwa ujumla.

Suala ni kuwa akili za watu wetu zimekuzwa na kuendelezwa katika maeneo gani ya fikara?

Tusisahau kuwa binadamu wenzetu waliotangulia kujiendeleza kwenye hizo nyanja kwa sababu ya changamoto za kimazingira walichukua hatua za makusudi kabisa kutudumaza kifikra na mpaka leo, wengi wetu hatujaweza kujikomboa kwenye hicho kifungo. Kinyume chake maelfu ya watu wetu bado wanazidi kujipeleka kwenye hivyo vifungo na kuwashawishi wengine pia waingie huko.

Viwango vya kukua na kuendelea kwa akili vinatofautiana pia ikiwa pamoja na mivuto mbalimbali inayowashawishi watu kuendeleza akili zao kwenye nyanja ambazo zina matokeo tofauti yakiwamo yale ambayo hayana tija ya kweli kwa jamii(nadhani kwa Tanzania hawa wapo wa kutosha).

Kwa maoni yangu,akili za watanzania wengi zimeendelezwa kiasi cha kutosha tu kukidhi mahitaji ya muhimu kama chakula, mavazi, na makazi. Kilichobaki ni akili za kiharamia ambazo hata wanyama wanazo, na zile za kusubiri ujio wa pepo( mbingu)

Kwa kuacha kukuza na kuendeleza akili zetu kufikia viwango stahiki, na kuachia zitawaliwe na watu wa nje na vibaraka wao wa huku kwetu ndio tumefikia hii hatua ya kushindwa kumiliki na kuendeleza rasilimali zilizopo kwenye himaya yetu.

Mkuu Robert Heriel, akili zipo lakini hazijaendelezwa na mbaya zaidi, zinatawaliwa na watu wasio na na nia njema kwa jamii yetu, ndani na nje ya nchi.

Lakini panga pangua, hata kama uletaji wako wa mada hii haujakidhi ladha ya kiuandishi ya baadhi ya wasomaji wako, bado uko sahihi kabisa.

Utajiri wa kwanza kabisa ni akili.
Ukikosa akili hata uwe na rasilimali kiasi gani, utaishia kuwa maskini tu!
 
Asante sana mleta hoja. Naiunga mkono 100% kwani na mie nawaza kama wewe. Waafrika ni wajinga sana yaani dumbs.. hatuamini katika akili. Serikali inategemea watu wasio na akili kuongoza.. watu wasio na akili, au wenye kufanya kazi zisotumia wala kuhitaji akili ndo wanaotumia V8. Wale wenye najukumu ya kutia maarifa na akili kizazi cha sasa kama vile walimu, wahadhili na wanataaluma wengine, hawathaniniwi.. Akili itakuja vipi na utajiri utatoka wapi?
 
Mada imekushinda toka mwanzo hadi mwisho! Sasa kama umeficha madini hapo katikati ambapo sikupasoma kwa kukosa uvumilivu na niliyosoma mwanzo mwa mada na mwisho wake, lawama ni yako kwa mtindo wako mbovu wa uandishi.

Niliposoma kichwa cha habari tu, nikavutiwa sana na kutaka kujuwa yaliyomo ndani ya mada yenyewe.

Mstari wa kwanza tu, nikaona mada imepinda. Sikukata tamaa nikajikaza nivute subira. Nikasoma hadi nusu ya andiko; nikaishia hapo. Sikuwa na nguvu tena za kuendelea hadi mwisho wa andiko refu lisilokuwa na mvuto kulisoma.
Lakini nikawa na wasiwasi kwamba pengine nikiruka hadi kule mwisho nitakuta mambo yanayohusiana na kichwa cha mada yenyewe, hata kama itakuwa ni katika mhitasari tu!

Looo, sikuona kitu. Nikaamua kunyanyua hayo niliyobamiza hapo juu kwa kuwa 'disappointed' na mada nzima, isipokuwa kichwa chake cha habari tu basi!

Pole yako ya kuwa na muda wa kupoteza, na pole yetu wasomaji wako kwa kupotezewa muda.
Ndo kutokuwa na akili kunakuwa hivi.. pole yako sana..
Kwa Tz na Africa kwa ujumla, watu wa jamii yako mko wengi sana..

Akili, akili.... Akili ni utajiri
 
Ndo kukosa akili kwenyewe.. unaweza kuthibitisha hayo mabwawa 31 yako wapi exactly? Yaani utaje location, (kijiji, kata, wilaya, mkoa).. vinginevyo hizi ni propaganda ambazo hutumika kwenye mataifa yenye watu wajinga.. yaani (dumb nation)

Hayo mambo ya Kidunda ni uwongo, uwongo uwongo.. mmekalia uwongo, mnakula uwongo na mnanuka uwongo..
Poor you!
Pole Sana ndio maana huwa nasema Kama huna taarifa usiongee la hasha unakuwa mpumbavu..

Wizara ya Maji inajenga mabwawa makubwa 31 mwaka huu kwenye maeneo kame achilia mbali mabwawa ya wizara ya kilimo na mabwawa makubwa zaidi yanayoendelea na ujenzi Kama Farkwa na Kidunda.
 
Kweli akili ni mali.. ambayo bahati mbaya wewe huna.. ukame katika eneo hili la Africa ni kitu cha kawaida, na kimsingi kila baada ya miaka 5, lazima itokee ukame kwa miaka 2 hadi 3.. hii iko hivyo na inajulikana na watu wenye akili miaka kibao iliyopita.. serikali inaongozwa kwa kiwango kikubwa na watu wasio na akili.. kwa hiyo kwao fact kama hii ni vigumu kuiona, wao na maccm wanajitetea kuwa ukame haujaletea na ccm.. hapo ndo utagundua akili zilivyo chache kabisa..

Lazima kifanyike kitu..
Akili haiji tu kiholela.. lazima watokee watu wachache wenye akili, wafanye mabadiliko ambapo nchi itawekeza katika kukuza akili ya watu wake.. sasa hili halifanyiki kabisa..
V8 moja na gharama za uendeshaji wake kwa miaka 2 ni sawa na gharama za kujenga shule moja nzuri ya msingi.. sasa jiulize zipo V8 ngapi? Hapo ndo ujuwe tunaongozwa na mapopoma.. yaani zero concept


Habari za ukame ziliwnza mwaka Jana ndio bajeti ya mwaka huu ikahusisha hiyo mipango na hata bajeti ijayo itahusisha masuala hayo ya kukabiliana na ukame ,Sasa shida iko wapi?

Changamoto za Sasa Ni kwa vile mifumo iliyopo haikuwa imetake hizo precautions huko tulikotoka but by 2025 hutosikia kelele za sijui maji Mara umeme nk..
 
Nadhani umeandika hoja MUHIMU yenye kushika hisia, na hivo kuna hatari ya kuzuia fikra yakinifu, tusipokuwa Makini wote tutashiriki kujilaani, kulaumu watu na kukosa hata mawazo suluhishi.

Katika kuelewa Jambo ili ulihukumu yapaswa akili na fikra yakinifu vishirikiane.
Mimi naungana na wasemao Tanzania ni tajiri sana Kwa minajiri ya rasilimali tulizonazo, bali tunaishi katika umaskini. Nadhani aliyetoa hoja hii na hata wengine walosimamia walibeba lengo jema la kuamsha tujitambue na tutazame tumejikwaa wapi ili ikiwezekana tujisahihishe ili tuanze mkakati wa kuutumia utajiri ghafi wa nchi kuleta maendeleo ya kiuchumi kwa nchi na watu wake.

Natoa mfano; mwanafunzi ambaye anafeli sana mitihani lakini mwalimu wake akatambua kuwa ni mwenye uwezo mkubwa wa kuweza kufanya vizuri katika masomo yake, ili kumepower huyo mwanafunzi mwalimu atamwambia wewe ni mwanafunzi mwenye uwezo kimasomo, kisha atamweleza wapi anakosea na achukue hatua zipi, wewe usikiaye, tena Kwa kukosa tafakuri utambeza mwalimu Kwa kutazama matokeo ya sasa, ni ujinga Tu unaokuendesha, au wewe mtumwa sehemu fulani na umeaminishwa kwamba jamii yenu ilizaliwa kutumikishwa na kuishi katika hali ya umaskini, kisha anakuja mwenye akili anayetambua ukweli juu ya asili yako kwamba waweza kuwa huru na ukatafuta Mali hata kuwa tajiri na kutawala wengine. Mtu huyu ameenda mbali zaidi akijua historia ya vizazi vyako kwamba walikuwa wafalme, machifu na watu wenye utajiri mkubwa, mtu huyu atakuamsha Kwa kukuambia hivi wewe ndugu unafahamu kwamba WEWE NI MTAWALA WALA SI MTUMWA NA PIA WEWE NI TAJIRI SANA? That is an alert to you to discover yourself it makes you aware na itafanya uanze kujitafuta wapi ulikosea hata kuwa na hali hii, hiyo ni empowering of one self. Inatumika Kwa wachezaji, mwanasiasa mwenye kipaji hicho pasipo kukitambua n.k. Ni Sawa na kuona kipaji cha mtoto juu ya muziki na ukamwambia hivi unafahamu kuwa wewe ni zaidi ya mwanamuziki Fulani ( maarufu na mwenye mafanikio) Sasa ukiwa mjinga utaishia kubisha kwamba yule mtumwa si mtawala wala si tajiri ni masikini tu, au yule mtoto si lolote si chochote katika muziki, na kwa wakati huo ni kweli juu ya Hali zao hao.
Hii ni kukosa akili pembuzi iwezayo kutafsiri na kuchanganua maudhui ya Jambo fulani na nguvu ibebayo kufanikisha Jambo husika. Hiyo ndo akili ndogo, pia ni ujinga.

Hebu fikiria kidogo, tutegemee mawazo yako uliyoandika kukomboa taifa toka umaskini, tunatokaje, hata ukiitwa ushauri utashauri nini zaidi ya kubariki mzungu aliyekulaani Kwa kukufananisha na nyani.

Kuna tatizo kubwa sana juu ya sisi wabeba hoja tudhaniazo ni hoja jadidu na yakinifu, tatizo hili ni kutetea au kulaani jambo pasipo uelewa wa kina, kwa mfano unayoyasema juu ya jamii zetu, kuwa wachafu, wasiojali mazingira, tegemezi, wenye kulaumu laumu tu, walojaa ubinafsi, watesi juu ya jamii yao wenyewe na mwingine mengi. Naandika tena Kwa herufi kubwa, HAKUNA JAMII YOYOTE ISIYOPITIA HAYO, HAIPO DUNIANI HAIPO. Kikubwa wao hawakujilaani, na kwa bahati hakuwepo wa kuwalaani, wakasumbuliwa na hayo huku wakitafuta namna ya kujikwamua.

Cha kusikitisha ni pale mleta hoja nadhani kwa ujinga tu au Kwa hasira juu ya mawazo fulani inatolea mfano jamii zilizoendelea kama kwamba zilizaliwa hivyo, brother kuna kazi imefanyika na ilianzishwa na wachache wenye fikra yakinifu, ndugu yangu HAKUNA JAMII YENYE WATU WAADILIFU NA WENYE AKILI TUUU PASIPO JUHUDI ZA WACHACHE WENYE KUTHUBUTU KUFUTA UJINGA WA WENGI.

Hivi unafahamu waafrika wengesema watu wa jinsia moja waoane kinyume kabisa na nature, tungeitwa hata mavi, Hilo kwako si shida, hawa watu wamepitia mengi maovu, ujambazi ulokithiri, kupigania uongozi, Vita vya kiraia, uuwaji watu wadhaniwao kuwa wachawi, vipindupindu, kunya bila kujisafisha na mengineyo.

Nini kifanyike. HAMNA HAJA YA KUJILAANI. Tunaweza kujikwamua toka ujinga huu na umaskini huu Ila si Kwa kutegemea mikakati ya wengine ambao kimsingi ni wafaidika wakubwa wa rasilimali zetu, tuweke malengo yetu wenyewe kama ni elimu tuwe very selective and serious tukitengeneza mitaala itayolenga utumizi mzuri wa rasilimali zetu, Pia kubadilisha mtazamo juu yetu wenyewe, kuwa na utashi wa kisiasa hili halitafanikiwa over night ni mchakato mfano kuandika au kuigiza mawazo ya namna ambayo yataamsha watu na kujitambua. Sisi waandikaji tuandike pasipo kuchoka, watu watakapochoshwa na kuona hatma ya maisha yao ipo mashakani watajitafuta kwa kurudia maandiko kama haya, historia yao na kutafuta wapi wamejikwaa.

Angalizo: Kwa mitazamo tuliyonayo sasa hasa wasomi na wanaodhani kuwa wanaharakati wa taifa hili, HATUTAMUELEWA KIRAHISI ALIYEBEBA MAONO YA KWELI YA KUJIKWAMUA TOKA MADHILA HAYA. Maana matatizo yetu ni complex alafu tunakazana kuyatatua kwa simple means.

Ukikuta wasomi wanavoainisha mbinu za kufikia maendeleo ya kweli na kufuta umaskini, utaona ni raisi mno, na Kwa mtindo huo basi nchi zote zingekuwa zimejikwamua toka umaskini na kuwa tajiri.

Naamini njia za maendeleo si njia nyeupe na za wazi, na yeyote azijuaye wanyonyaji wetu hupiga kelele usiku na mchana wakituaminisha huyo siye.

Wengi walozitoa nchi zao walau kwa kiwango fulani na kufanya zijitegemee, hawakufuata njia za uchumi kwa mazoea.

NAAMINI SOTE TUNA LENGO MOJA, NA HIZI NDO HARAKATI ZA KUJITAFUTA TUMEJIKWAA WAPI.

Tusijibanze nyuma ya uhasama wa kisiasa, tuwe watumwa wa ukweli tutachambua pasipo kupepesa.

Akili zipi ni akili kweli katika kujikomboa kutoka umaskini na ujinga tuuishio sasa. Hilo nadhani ni swali kwetu.
Niaminivyo hata hawa viongozi wetu huwa nadhamira ya kujiondoa katika MADHILA HAYA Ila hukwama katika njia, na wengi huchagua kukomboa maisha yao Tu. Ili tuendelee tunauhitaji njia zote, huo ndo ukqeli, yaani njia halali na haramu, busara na uwehu, upole na unabe, demokrasia na penginepo pasipo demokrasia, mawazo shirikisho na muda mwengine wazo la kijasri pasipo ushirikiahaji, kufuta Sheria na pengine kuvunja Sheria, ukweli na uwazi na pengine uwongo na uficho, yote yalenge kujenga taifa na watu wake. Maendeleo ni Complex by nature.
...Maendeleo ni Complex by nature....

Umeandika mengi.. na pumba zikiwemo..
Maendeleo ni sayansi na wala siyo complex kama uavyotaka tuamini. Maendeleo ni CHOICE.. ili ufanye 'the right choice' lazima uwe na akili.. jambo ambalo mleta hoja amejikita kwalo.
Tz na Africa kiujumla tunashindwa kufanya right choices kwa sababu communities zetu hazina akili au haziko tayari kutumia hata akili kidogo iliyopo..
 
Kweli akili ni mali.. ambayo bahati mbaya wewe huna.. ukame katika eneo hili la Africa ni kitu cha kawaida, na kimsingi kila baada ya miaka 5, lazima itokee ukame kwa miaka 2 hadi 3.. hii iko hivyo na inajulikana na watu wenye akili miaka kibao iliyopita.. serikali inaongozwa kwa kiwango kikubwa na watu wasio na akili.. kwa hiyo kwao fact kama hii ni vigumu kuiona, wao na maccm wanajitetea kuwa ukame haujaletea na ccm.. hapo ndo utagundua akili zilivyo chache kabisa..

Lazima kifanyike kitu..
Akili haiji tu kiholela.. lazima watokee watu wachache wenye akili, wafanye mabadiliko ambapo nchi itawekeza katika kukuza akili ya watu wake.. sasa hili halifanyiki kabisa..
V8 moja na gharama za uendeshaji wake kwa miaka 2 ni sawa na gharama za kujenga shule moja nzuri ya msingi.. sasa jiulize zipo V8 ngapi? Hapo ndo ujuwe tunaongozwa na mapopoma.. yaani zero concept
Sasa wewe mwenye akili mbona matumizi ya akili yako ni ulalamishi tuu nothing else..

Hizo Ni akili au matope?
 
Ndo kukosa akili kwenyewe.. unaweza kuthibitisha hayo mabwawa 31 yako wapi exactly? Yaani utaje location, (kijiji, kata, wilaya, mkoa).. vinginevyo hizi ni propaganda ambazo hutumika kwenye mataifa yenye watu wajinga.. yaani (dumb nation)

Hayo mambo ya Kidunda ni uwongo, uwongo uwongo.. mmekalia uwongo, mnakula uwongo na mnanuka uwongo..
Poor you!
Wewe Ni mpumbavu nianze kukuthibitishia hujui kwa kupata habari? Sasa una akili gani Kama nimekueleza wizara husika ambako unaweza kupata specific areas bado unaongea ufala..

Mapopoma Kama nyie mna akili za kwendea chooni na kulalamika tuu Hakuna kingine,wakati Serikali unasema imejenga Vituo vya Afya 234 vya Tozo mlikuja na upumbavu Kama huu huu ooh viko wapi mkapewa orodha mkapata aibu na kuanza kutafuta visingizio Mara ooh havifanyi kazi Ni majengo tuu na upuuzi mwingine Kama huu..
 
Ukitaka kujua hii nchi imejaa wapumbavu , tumeshindwa kutumia hata chuma kule Liganga na mchuchuma kuanza kuzalisha bidhaa za kilimo ,ujenzi nk ili tuondokane na utegemezi wa bidhaa toka nje ya nchi ambapo tunapoteza pesa nyingi za kigeni , wapumbaf huko serikalini ukiwauliza watakupa visingizio vya kiduwanzi mpaka utatamani kulia .
Nchi imejaa matapeli tupu
 
Wewe Ni mpumbavu nianze kukuthibitishia hujui kwa kupata habari? Sasa una akili gani Kama nimekueleza wizara husika ambako unaweza kupata specific areas bado unaongea ufala..

Mapopoma Kama nyie mna akili za kwendea chooni na kulalamika tuu Hakuna kingine,wakati Serikali unasema imejenga Vituo vya Afya 234 vya Tozo mlikuja na upumbavu Kama huu huu ooh viko wapi mkapewa orodha mkapata aibu na kuanza kutafuta visingizio Mara ooh havifanyi kazi Ni majengo tuu na upuuzi mwingine Kama huu..
Unaonesha ulivyo first order dumb.. nimekuuliza hayo mabwawa 31 yako wapi exactly?
Anyway sitaki kupoteza muda kujibishana na dumb a§s kama wewe, form four failure flani hivi
 
Unaonesha ulivyo first order dumb.. nimekuuliza hayo mabwawa 31 yako wapi exactly?
Anyway sitaki kupoteza muda kujibishana na dumb a§s kama wewe, form four failure flani hivi
Na Mimi nikakwambia Kama hujui kwa kupata taarifa yaliko Basi Baki na utaahira wako.
 
UTAJIRI WA NCHI NI AKILI ZA WATU, SIO RASILIMALI KAMA MADINI N.K.

Anaandika, Robert Heriel.

Huwaga namshangaa mtu anayesema nchi yetu ni Tajiri. Kwa kweli sio tuu anachekesha Bali pia anaonyesha jinsi alivyokuwa mjinga na asiyeweza kufikiri sawia.

Kama nikiulizwa hivi leo sababu gani inatufanya Waafrika ikiwemo nchi yetu kuwa Masikini, basi jibu litakuwa ni kuwa Sisi tunaakili ndogo Kama sio kuwa hatuna Kabisa.

Taifa ili kiwe Tajiri linahitaji watu wenye akili zaidi kuliko Rasilimali. Utajiri ni Akili na sio wingi wa Rasilimali.
Kuna msemo usemao, penye miti hapana wajenzi.

Akili ndio inaweza kufanya madini kuwa Rasilimali Kwa kuipa Value. Madini kama madini hayajui kama yenyewe ni yathamani, Ila wenye akili ndio wanajua thamani ya madini hayo kutokana na matumizi waliyoyabuni kwayo.

Kidunia Bara la Afrika ndilo bara lenye malighafi nyingi kuliko bara lolote lile. Lakini watu wake wameshindwa kuzigeuza malighafi hizo kuwa Rasilimali Kwa kuzipa thamani.

Ukisikia mtu anakuambia Yeye ni Tajiri Kwa sababu nchi yake inamadini, maziwa na Mito, Ardhi yenye Rutuba, wanyama wa kuvutia, na mambo mengine lakini watu wake ni Hali zao za maisha ni duni jua mtu huyo hajui kufikiri vizuri, na pengine akawa mwendawazimu.

Nchi haiwezi kuwa Tajiri Kama ndani yake inawatu wajinga wengi. Watu wasio na akili wakiwa wengi ndivyo nchi inavyozidi kuwa Masikini.

Mtu asiye na akili Hana tofauti na mnyama wa porini, ni Sawa na tumbili au ngedere anayeishi msituni ananyeshewa mvua na kuchomwa na Jua lakini anashindwa kujenga nyumba hata ya mbao Kwa sababu ya upeo mdogo wa Akili.

Wazungu walivyotuita Waafrika manyani kuna watu walifikiri walimaanisha maumbile yetu yanafanana na nyani😀😀 Kama nawe ulifikiri hivyo basi nawe upo kundi la watu wajinga.

Wazungu walituita manyani mbali na ubaguzi wao lakini walituona akili zetu hazijaachana Sana na tumbili na nduguye ngedere.

Nyani au ngedere ukimpelekea Dhahabu au Almasi wala hataiona inatofauti na jiwe jingine. Kutokana na upeo mdogo wa Akili.

Sisi Watanzania wengi wetu tunaakili ndogo mno na hiyo ndio sababu Sisi sio matajiri. Na tutaendelea kuwa Vivi hivi Kwa Karne kadhaa zijazo.

Watanzania wengi ni Kama wanyama Kwa mambo mengi, kama unavyomuona ng'ombe basi ndivyo wengi wetu tulivyo.

Sio ajabu ukakuta watu kwenye makazi Yao kuna mavi au maji machafu waliyoyasababisha yamewazunguka, yananuka na nzi wamejaa lakini wao hawaoni Shida. Wanalala, wanakula hapohapo, na wanakunya na kukojoa hapohapo.

Hapo ati wanasubiri kiongozi aje awaambie wawe wasafi tena wengine ifikie hatua ya kupelekwa serikali za mitaa kisa anaambiwa asizibue chemba za mavi yake na familia yake, come on!

Sio ajabu jitu linakunya chooni labda cha umma alafu hali-flash uchafu wake. Hivi mtu huyo anatofauti ipi na Mnyama?

Mtu anajua kabisa ili aishi anatakiwa awe na chakula cha kutosha kinachomtosha yeye na familia yake, badala awe na ghala la kuhifadhi chakula kinachomtosha yeye na watoto wake angalau Kwa miaka miwili kulingana na Hali ya hewa.

Yeye anakula Kama mnyama asijue kesho atakula nini. Halafu ikifika kesho anaanza kumlalamikia mtu mwingine labda ni serikali au viongozi. Jamani hivi tunaakili kweli?

Tena wakati mwingine tunazidiwa akili hata na Wanyama.

Hakuna mnyama ambaye atazaa watoto ambao hawezi Kuwatunza. Hakuna na hajawahi kutokea. Mfano Kuku anaouwezo wa kutaga mayai hata Mia moja.

Lakini atataga mayai kumi (10-12) kulingana na uwezo wake wakuyaatamia, sio atage mayai 20 alafu wakati wa kuatamia mengine ashindwe kuyaatamia yajitokeze nje.

Kisha Kwa mayai 10-12 anaouwezo wa kuwachunga na kuwakuza watoto hao.

Halikadhalika na mbwa, ng"'ombe, mbuzi, Simba n.k.

Lakini Sisi unakuta mtu anazaa watoto nje ya uwezo wake wa Kuwatunza, labda watoto 10 alafu ananilaumu serikali kuwa gharama za Shule au hospitali ziondolewe.

Au anaomba msaada Kabisa wa kusaidiwa kulelewa watoto.

Hivi tumelogwa au ni kitu gani?

Mtu unajua kabisa miti ndio huleta hewa Safi, huleta mvua na kivuli kizuri, na Kupunguza joto la nchi. Alafu unakuta watu wamekata miti mtaa mzima ili wajenge nyumba.

Unashangaa mtaa mzima miti ipo 20 Kwa eneo la kilometa moja. Alafu muda huohuo unasikia mwehu akipiga kelele jamani joto Kali, jamani jua linawaka! Mara kiyama kinakaribia.

Kiama ya mavi. Ujinga na wehu wako ndio unaita Kiyama?

Utajiri WA nchi ni akili za watu na sio Rasilimali Kama madini.

Chakufanya;
I. Tujifunze kuwa na Akili ili tuwe nchi yetu itajirike.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kwa kiasi fulani siungi mkono hoja zako. Akili kila mtu anazo, lakini maarifa yaliyopo kwenye hizo akili sio kila mtu anaweza kuyageuza yakawa utajiri. Nchi kuwa na resources au kutokuwa nazo sio hoja, hoja ni uwezo wa watu wa nchi husika kuzigeuza hizo resources kuwa utajiri. Akili +Elimu =Huzaa maarifa.
maarifa +resources =Huzaa utajiri.
Taifa tajiri, ni lile ambalo asilimia kubwa ya wananchi wake ni matajiri ingawa hata huko kwenye taifa tajiri na maskini wapo. Taifa maskini ni namba ya maskini ndani ya taifa kuwa kubwa kuliko matajiri 80/20 or 90/10 rule ndio huwa ina apply huko. Changamoto ya watanzania sio Akili, bali ni uwezo wa kubadili kile kilichopo kwenye akili kwa kushirikiana na resources zilizopo kuwa utajiri.
 
Ndo kutokuwa na akili kunakuwa hivi.. pole yako sana..
Kwa Tz na Africa kwa ujumla, watu wa jamii yako mko wengi sana..

Akili, akili.... Akili ni utajiri
EEeeeeHeeeee!

Sasa wewe hapa umetumia akili gani hasa!
 
Nchi hii ina mambo, mfano kisiwa cha Ukerewe kimezungukwa na maji baridi safi ya ziwa Victoria. Lakini wakaazi wanalalamika ukame, bei ya vyakula kuwa juu n.k

Je uongozi wa mkoa wa Mwanza wameshindwa kukigeuza kisiwa cha Ukerewe kuwa shamba-darasa kwa kuwawezesha wakulima wote kufanya kilimo cha umwagiliaji chanzo kikiwa ni ziwa hilo lilolizunguka kisiwa hicho chote.

Nina uhakika kisiwa hicho kinaweza kuzalisha mazao ya chakula kwa wingi kwa kilimo cha kisasa na cha umwagiliaji, na kutumia tunu alioijalia kisiwa hicho kiwe mfano kwa uzalishaji mkubwa wa nafaka kama nchi ya Ukraine.

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe​



Kilimo​

Mazao yalimwayo kwa wingi katika Wilaya ya Ukerewe yenye visiwa 38 japo visiwa 15 vinatumika kama maeneo ya uvuvi ni muhogo, viazi vitamu, mpunga, matunda aina ya machungwa, maembe, mananasi, mapapai, kahawa, migomba, mazao ya

ndizi.jpg
bustani na mazao ya jamii ya kunde kama vile maharage, njugu mawe na kunde. Mazao mengine yanayolimwa kwa kiasi kidogo ni mtama na rosella (choya). Mazao haya yanalimwa katika eneo la Ha.33, 765.5Ardhi iliyopo ni ndogo kuruhusu kilimo cha kupumzisha mashamba. Kwa hali hiyo kilimo kinahitaji kifanyike kwa tija ili uzalishaji wa mazao uweze kukidhi mahitaji ya wananchi wote ambao kulingana na Sensa ya Watu na Makazi ya mwaka 2012 ni 347,145. Zao la alizeti linatiliwa mkazo badala ya zao la pamba ambalo katikamiaka ya 1970 lilikuwa zao maarufu la biashara ambalo lilikuwa linawapatia wakulima kipato. Lakini kutokana na upungufu wa ardhi hasa ukizingatia kuwa zao hili halitakiwi kuchanganywa na mazao mengine pamoja na kushuka kwa bei, zao hili lilionekana kutofanya vizuri.
Idara ya Kilimo ili iweze kutekeleza vyema ilani ya Uchaguzi ya CCM ni lazima ihakikishe inatekeleza majukumu mbalimbali ya msingi ili kuleta tija katika uzalishaji wa mazao ya chakula na biashara, kuendeleza na kuboresha huduma za ugani ikiwa ni pamoja na kuwezesha wakulima kuwa na vyama vya ushirika vilivyo hai na vyenye nguvu ya mtaji. Aidha kuwawezesha wakulima kuunda vikundi ili waweze kuwa na umoja wenye nguvu katika kufikisha bidhaa zao katika masoko ya mazao yao. Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe ina jumla ya Vyama Vya Ushirika 71 vilivyoandikishwa chini ya Sheria Na.6 ya mwaka 2013 ya Vyama Vya Ushirika. Idadi ya VICOBA vilivyopo ni 150. Vyama vilivyo vingi vinakabiliwa na matatizo mbalimbali ambayo yanapelekea vyama hivyo kutofanya vizuri. halmashauri inakabiliwa na upungufu wa wataalam 4 wa Ushirika kwa ajili ya kufanya ufuatiliaji wa vyama hivyo ikiwa ni pamoja na kufanya ukaguzi wa mahesabu. Ili haya yaweze kufanyika kwa ufanisi Maafisa Ugani wanatakiwa kuboreshewa mazaingira yao ya kufanyia kazi. Maboresho hayo ni pamoja na kupatiwa nyumba za kuishi katika maeneo yao na kuwezeshwa vyombo vya usafiri hususani pikipiki ili kuwawezesha kuwafikia wakulima kwa urahisi na kwa muda muafaka pale huduma za ugani zinapohitajika.

banio.jpg
Pamoja na Serikali kutilia mkazo juu ya kilimo cha umwagiliaji wakulima bado wanategemea mvua katika kilimo. Hii ni kutokana na kutokamilika kwa miundo mbinu ya umwagiliaji katika skimu za Bugorola na Miyogwezi. Miradi hii imekwamakukamilika kutokana na ukosefu wa fedha licha ya Ofisi hiyo ya Umwagiliaji

Source : Kilimo

Shukrani Sana Mkuu
 
Kwa kiasi fulani siungi mkono hoja zako. Akili kila mtu anazo, lakini maarifa yaliyopo kwenye hizo akili sio kila mtu anaweza kuyageuza yakawa utajiri. Nchi kuwa na resources au kutokuwa nazo sio hoja, hoja ni uwezo wa watu wa nchi husika kuzigeuza hizo resources kuwa utajiri. Akili +Elimu =Huzaa maarifa.
maarifa +resources =Huzaa utajiri.
Taifa tajiri, ni lile ambalo asilimia kubwa ya wananchi wake ni matajiri ingawa hata huko kwenye taifa tajiri na maskini wapo. Taifa maskini ni namba ya maskini ndani ya taifa kuwa kubwa kuliko matajiri 80/20 or 90/10 rule ndio huwa ina apply huko. Changamoto ya watanzania sio Akili, bali ni uwezo wa kubadili kile kilichopo kwenye akili kwa kushirikiana na resources zilizopo kuwa utajiri.

Akili lazima zithibitishwe katika Mazingira ya nje. Mtu huwezi kusema kila mtu anaakili wakati hauna uthibitisho.

Uwezo wa kubadili changamoto kuwa fursa ni sehemu ya akili, uwezo wa kukabiliana na matatizo yanayozunguka jamii ndio akili yenyewe hiyo.
Sasa Kama mtu hawezi kukabiliana na matatizo na changamoto zinazomzunguka utasemaje anaakili?

Unapozungumzia Akili tayari umegusa Maarifa, ufahamu, tafakuri, Ujuzi ambayo hayo ndio yanaunda kitu inaitwa Elimu.
 
Sijakuelewa mkuu,unapinga au unakubaliana na mtoa mada,kuwa hakuna utajiri pasi kuwa na akili?
Utajiri wa Kwanza ni akili,bila akili Unaweza kuwa na ng'ombe 1000 afu ukafungwa kwa deni la 800,000😄😄

Yanatukuta Tanzania leo,nenda Mbeya(tukuyu) ushangae shida ya maji inayokumba wananchi ilhali wamezungukwa na mito kila kona!!Watanzania tunahitaji tubikiri bongo zetu la sivyo tutabaki masikini hata Karne ijayo.
Hivi tunatofautishaje kutokuwa na akili za kufanya jambo fulani na kutoku dhamiria tu kufanya hilo jambo?
 
Ukiwachukua watanzania wote kuwahamishia Marekani, na wamarekani wote wahamie Tanzania baada ya miaka kumi, Tanzania itakuwa super power! Na baada ya miaka kumi na tano Marekani itakuwa Third World country!

Tatizo la Waafrica (watanzania) siyo udongo ni UBONGO!
Mbona sioni mkitolea mifano au kulinganisha na waarabu ambao nao wametajirika kwa mafuta yao badala yake inatumika mifano ya wazungu tu au waarabu si mfano sahihi ya watu wenye akili?
 
Back
Top Bottom