Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Utajiri wa nchi ni akili za Watu sio rasilimali kama madini na nyinginezo

Watanzania Kodi hatutaki kutoa alafu ndio wakwanza kulalamika.
Lakini pia ukitoa Kodi kuna wenye uroho wanazitumbua kifisadi Kwa mambo Yao binafsi na kujineemesha wenyewe. Hapo ndipo msala Ulipo.

Serikali ilikuwa inahitaji watu sampuli ya kina Nyerere ndio washike nyazifa za juu. Watu wasio na tamaa ya Mali.
Lakini watu sampuli ya kina Nyerere ni wachache Mno sio ajabu nchi nzima wasifike 10.

Watoto wanakuzwa kibinafsi hivyo wakikua nao wanakuwa wabinafsi
Hii Nchi Ina watu wapumbavu Sana na mdomo Sana.Yote yanayojadiliwa Ni Pesa Sasa lijitu hakitaki kutoa risiti Wala kudai risiti ila linataka Hali nzuri,haiwezekani.

Wanatoa visingizio vya kijinga Mara ooh Pesa inaliwa na blaa blaa kibao ila kiuhakisia Pesa inayoliwa haisidi hata 30% na kwenye 30% na zilizosakia pengine nyingi zinaingia kwenye mipango na matumizi yasiyo na tija Sana..

Kwenye kupanga kipinkianze na wapi tupeleke Pesa kunahitaji mjadala ili tuwe na mipango yenye matokeo makubwa zaidi ila kesi ya wizi sio kubwa Sana hapa Tanzania ukilinganisha na Nchi Nyingi..

Nilisoma mahala fulani kwamba hizi NGOs huwa zinatumiq zaidi ya Til.3 kwenye Uchumi wa Nchi,Sasa ukiangalia hizo pesa pamoja na kwamba ni za Private sector ilitakiwa ziwekewe utaratibu yaani wao wa compliment pale Serikali inapoishia lakini huwa zinaiehia kwenye mikono ya wachache hukunzikiharibu Uchumi kwa kuingia kwenye mzunguko bila utaratibu maalumu na hazina tija..
 
Hii Nchi Ina watu wapumbavu Sana na mdomo Sana.Yote yanayojadiliwa Ni Pesa Sasa lijitu hakitaki kutoa risiti Wala kudai risiti ila linataka Hali nzuri,haiwezekani.

Wanatoa visingizio vya kijinga Mara ooh Pesa inaliwa na blaa blaa kibao ila kiuhakisia Pesa inayoliwa haisidi hata 30% na kwenye 30% na zilizosakia pengine nyingi zinaingia kwenye mipango na matumizi yasiyo na tija Sana..

Kwenye kupanga kipinkianze na wapi tupeleke Pesa kunahitaji mjadala ili tuwe na mipango yenye matokeo makubwa zaidi ila kesi ya wizi sio kubwa Sana hapa Tanzania ukilinganisha na Nchi Nyingi..

Nilisoma mahala fulani kwamba hizi NGOs huwa zinatumiq zaidi ya Til.3 kwenye Uchumi wa Nchi,Sasa ukiangalia hizo pesa pamoja na kwamba ni za Private sector ilitakiwa ziwekewe utaratibu yaani wao wa compliment pale Serikali inapoishia lakini huwa zinaiehia kwenye mikono ya wachache hukunzikiharibu Uchumi kwa kuingia kwenye mzunguko bila utaratibu maalumu na hazina tija..

Hata wangeiba 1% ni Haki ya wananchi kulalamika.
Ila walalamika lazima wawe wanaolipa Kodi(walioibiwa) sio jitu halilipi Kodi, halizalishi chochote ndani ya taifa alafu linakuwa la Kwanza kulalamika.
Kwa kweli mtu wa namna hiyo hana uhalali WA kulalamikia wezi au mafisadi.

Kila kitu kinaenda na wajibu, majukumu, na Haki
 
Wapo na wanaakili sana.Sema ubinafsi umewazidi baadhi ya viongozi wetu.Mungu tu ndie atawanyoosha mana wananchi wenyewe tumelewa Moshi wa Mwenge.
 
Mada imekushinda toka mwanzo hadi mwisho! Sasa kama umeficha madini hapo katikati ambapo sikupasoma kwa kukosa uvumilivu na niliyosoma mwanzo mwa mada na mwisho wake, lawama ni yako kwa mtindo wako mbovu wa uandishi.

Niliposoma kichwa cha habari tu, nikavutiwa sana na kutaka kujuwa yaliyomo ndani ya mada yenyewe.

Mstari wa kwanza tu, nikaona mada imepinda. Sikukata tamaa nikajikaza nivute subira. Nikasoma hadi nusu ya andiko; nikaishia hapo. Sikuwa na nguvu tena za kuendelea hadi mwisho wa andiko refu lisilokuwa na mvuto kulisoma.
Lakini nikawa na wasiwasi kwamba pengine nikiruka hadi kule mwisho nitakuta mambo yanayohusiana na kichwa cha mada yenyewe, hata kama itakuwa ni katika mhitasari tu!

Looo, sikuona kitu. Nikaamua kunyanyua hayo niliyobamiza hapo juu kwa kuwa 'disappointed' na mada nzima, isipokuwa kichwa chake cha habari tu basi!

Pole yako ya kuwa na muda wa kupoteza, na pole yetu wasomaji wako kwa kupotezewa muda.
Nimesoma kwa kuruka ruka.
 
Yaani Ng'wigulu waziri wa fedha? Hakika hatujawahi kuwa siriazi.
 
Tatizo hadi leo tuna akina ''Sultani Mang'ung'o" wengi!
Ona awamu ya 4 tulivyoingia mikataba ya kipuuzi kabisa ya gas yetu!
Tena ya kupewa 'shanga' kama alivyofanya mang'ung'o mwenyewe!
 
Kutokujua unachokifanya ndio kukosa akili Kwenyewe huko
Nimesema hao wenye kusaini mikataba mibovu isiyo na faida kwa taifa wanajua vizuri tu wanachokifanya kuwa si sahihi.
Ndio maana watu hutaki katiba mpya yote ni katika kutaka kuweka mifumo mizuri.
 
UTAJIRI WA NCHI NI AKILI ZA WATU, SIO RASILIMALI KAMA MADINI N.K.

Anaandika, Robert Heriel.

Huwaga namshangaa mtu anayesema nchi yetu ni Tajiri. Kwa kweli sio tuu anachekesha Bali pia anaonyesha jinsi alivyokuwa mjinga na asiyeweza kufikiri sawia.

Kama nikiulizwa hivi leo sababu gani inatufanya Waafrika ikiwemo nchi yetu kuwa Masikini, basi jibu litakuwa ni kuwa Sisi tunaakili ndogo Kama sio kuwa hatuna Kabisa.

Taifa ili kiwe Tajiri linahitaji watu wenye akili zaidi kuliko Rasilimali. Utajiri ni Akili na sio wingi wa Rasilimali.
Kuna msemo usemao, penye miti hapana wajenzi.

Akili ndio inaweza kufanya madini kuwa Rasilimali Kwa kuipa Value. Madini kama madini hayajui kama yenyewe ni yathamani, Ila wenye akili ndio wanajua thamani ya madini hayo kutokana na matumizi waliyoyabuni kwayo.

Kidunia Bara la Afrika ndilo bara lenye malighafi nyingi kuliko bara lolote lile. Lakini watu wake wameshindwa kuzigeuza malighafi hizo kuwa Rasilimali Kwa kuzipa thamani.

Ukisikia mtu anakuambia Yeye ni Tajiri Kwa sababu nchi yake inamadini, maziwa na Mito, Ardhi yenye Rutuba, wanyama wa kuvutia, na mambo mengine lakini watu wake ni Hali zao za maisha ni duni jua mtu huyo hajui kufikiri vizuri, na pengine akawa mwendawazimu.

Nchi haiwezi kuwa Tajiri Kama ndani yake inawatu wajinga wengi. Watu wasio na akili wakiwa wengi ndivyo nchi inavyozidi kuwa Masikini.

Mtu asiye na akili Hana tofauti na mnyama wa porini, ni Sawa na tumbili au ngedere anayeishi msituni ananyeshewa mvua na kuchomwa na Jua lakini anashindwa kujenga nyumba hata ya mbao Kwa sababu ya upeo mdogo wa Akili.

Wazungu walivyotuita Waafrika manyani kuna watu walifikiri walimaanisha maumbile yetu yanafanana na nyani😀😀 Kama nawe ulifikiri hivyo basi nawe upo kundi la watu wajinga.

Wazungu walituita manyani mbali na ubaguzi wao lakini walituona akili zetu hazijaachana Sana na tumbili na nduguye ngedere.

Nyani au ngedere ukimpelekea Dhahabu au Almasi wala hataiona inatofauti na jiwe jingine. Kutokana na upeo mdogo wa Akili.

Sisi Watanzania wengi wetu tunaakili ndogo mno na hiyo ndio sababu Sisi sio matajiri. Na tutaendelea kuwa Vivi hivi Kwa Karne kadhaa zijazo.

Watanzania wengi ni Kama wanyama Kwa mambo mengi, kama unavyomuona ng'ombe basi ndivyo wengi wetu tulivyo.

Sio ajabu ukakuta watu kwenye makazi Yao kuna mavi au maji machafu waliyoyasababisha yamewazunguka, yananuka na nzi wamejaa lakini wao hawaoni Shida. Wanalala, wanakula hapohapo, na wanakunya na kukojoa hapohapo.

Hapo ati wanasubiri kiongozi aje awaambie wawe wasafi tena wengine ifikie hatua ya kupelekwa serikali za mitaa kisa anaambiwa asizibue chemba za mavi yake na familia yake, come on!

Sio ajabu jitu linakunya chooni labda cha umma alafu hali-flash uchafu wake. Hivi mtu huyo anatofauti ipi na Mnyama?

Mtu anajua kabisa ili aishi anatakiwa awe na chakula cha kutosha kinachomtosha yeye na familia yake, badala awe na ghala la kuhifadhi chakula kinachomtosha yeye na watoto wake angalau Kwa miaka miwili kulingana na Hali ya hewa.

Yeye anakula Kama mnyama asijue kesho atakula nini. Halafu ikifika kesho anaanza kumlalamikia mtu mwingine labda ni serikali au viongozi. Jamani hivi tunaakili kweli?

Tena wakati mwingine tunazidiwa akili hata na Wanyama.

Hakuna mnyama ambaye atazaa watoto ambao hawezi Kuwatunza. Hakuna na hajawahi kutokea. Mfano Kuku anaouwezo wa kutaga mayai hata Mia moja.

Lakini atataga mayai kumi (10-12) kulingana na uwezo wake wakuyaatamia, sio atage mayai 20 alafu wakati wa kuatamia mengine ashindwe kuyaatamia yajitokeze nje.

Kisha Kwa mayai 10-12 anaouwezo wa kuwachunga na kuwakuza watoto hao.

Halikadhalika na mbwa, ng"'ombe, mbuzi, Simba n.k.

Lakini Sisi unakuta mtu anazaa watoto nje ya uwezo wake wa Kuwatunza, labda watoto 10 alafu ananilaumu serikali kuwa gharama za Shule au hospitali ziondolewe.

Au anaomba msaada Kabisa wa kusaidiwa kulelewa watoto.

Hivi tumelogwa au ni kitu gani?

Mtu unajua kabisa miti ndio huleta hewa Safi, huleta mvua na kivuli kizuri, na Kupunguza joto la nchi. Alafu unakuta watu wamekata miti mtaa mzima ili wajenge nyumba.

Unashangaa mtaa mzima miti ipo 20 Kwa eneo la kilometa moja. Alafu muda huohuo unasikia mwehu akipiga kelele jamani joto Kali, jamani jua linawaka! Mara kiyama kinakaribia.

Kiama ya mavi. Ujinga na wehu wako ndio unaita Kiyama?

Utajiri WA nchi ni akili za watu na sio Rasilimali Kama madini.

Chakufanya;
I. Tujifunze kuwa na Akili ili tuwe nchi yetu itajirike.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kuna nyumba nilikua naishi ya kupanga miaka kadhaa uwezi Amin hadi zamu ya chooni watu wanataka kuwekewa ratiba kama watoto wa secondary

Uwezo wa watanzania ni mdogo sana kwenye mambo mengi kiufupi watanzania hawajitambui
 
Kulaumu viongozi ni sawa ila tatizo ni sisi, kwanza viongozi ni reflection ya watu wake maana hatukodi kutoka nje badi ni sisi wenyewe, kama kiongozi umemuweka madarakani lakini akizingua kumtoa huwezi sasa hapo alaumiwe nani kama sio wewe uliemchagua..
Hii point kubwa sana sababu viongozi ni matunda ya jamii ni kweli wanareflect jinsi tulivyo
 
Enzi zile Amin akawatimua Wahindi 70,000 kwa mkupuo na kuwanyang'anya kila kitu na kuwapa wananchi hawa unaowasema

Hivyo hivyo Mugabe nae kama huyo tu nae akatimua wazungu leo unanunua mkate mmoja million
Walijimikikisha mashamba ya muzungu matokeo yake waliiba matrekta yote na swimming pools wakanyea na kuyafanya dampo

Mwingine akaibuka kwetu akawa anaimba nchi yetu ni tajiri sana, tumeibiwa sana kumbe nyuma ya pazia wanaiba x2
Acha waishi hivyo hivyo ndio wamechagua maisha hayo na wamekataa kutoka
 
Kwangu Mimi hii ni thread ya kufunga mwaka 2022.ni madini tupu ahsante taikon.Unaweza kukuta mtu ni daktari au MWALIMU Lakini anakula ndizi kwenye daladala anarusha maganda dirishani.Hapa taikon unahisi TATIZO ni nini??
Hiki kitu kinanikera sana na unakuta ndani ya gari Kuna kopo/dustibin la kuwekea takataka lakin unakuta mtu anatupa takataka nje
 
Kwangu Mimi hii ni thread ya kufunga mwaka 2022.ni madini tupu ahsante taikon.Unaweza kukuta mtu ni daktari au MWALIMU Lakini anakula ndizi kwenye daladala anarusha maganda dirishani.Hapa taikon unahisi TATIZO ni nini??

Ukosefu wa Akili ni tatizo KUBWA.

Na Hilo tatizo miaka ya hivi karibuni litaingia Uzunguni. Tuombe uzima
 
Pole Sana ndio maana huwa nasema Kama huna taarifa usiongee la hasha unakuwa mpumbavu..

Wizara ya Maji inajenga mabwawa makubwa 31 mwaka huu kwenye maeneo kame achilia mbali mabwawa ya wizara ya kilimo na mabwawa makubwa zaidi yanayoendelea na ujenzi Kama Farkwa na Kidunda.
Hii serikali huwa naifananishaga na bongo movie. Wasanii wa bongo movie hawana ubunifu hufanya mambo kimazoea, hawajui kwamba wako nyuma ya muda wakifanya jambo jipya kwao hutaka wajisifu na kusifiwa hata kama hilo jambo lilitakiwa kufanyika miaka kumi nyuma huko matokeo yake hujiona wamepiga hatua kubwa kana kwamba wameanza juzi hiyo bongo movie. Wasanii wa bongo movie pamoja na kwamba wanaangalia kazi za wenzao waliyoendelea huko ila bado hawajifunzi hata kwa yale yenye kuwezekana wanafikiri ndani ya duara lile lile la siku zote.
 
Nakuunga mkono 100%,hata maofisini wafanyakazi wasio na uwezo wa kuleta ufanisi ndiyo hupewa vyeo!!
Kujipendekeza na unafiki vinaliangamiza taifa hili.

Tanzania Ni masikini kwa sababu tumewaachia waso na akili wafanye maamuzi na ndiyo hushika nyadhifa za kufanya maamuzi.

Nisiposifia nitafukuzwa kazi nifanyaje Mkuu?
 
Back
Top Bottom