Utajiri wa 'ngende' (ushirikina) una masharti magumu kuliko utajiri wowote ule duniani

Utajiri wa 'ngende' (ushirikina) una masharti magumu kuliko utajiri wowote ule duniani

Acha kutapeli watu mkuu,labda Kama unazungumzia ngende ya mgodini,Ila Kama unazungumzia ngende ya liwale iliyoko Kijiji Cha mpigamiti Basi jua unataka kutapeli watu hapa.

Kiufupi huwezi nificha kitu kuhusu huyo Bibi njumwite,na vibaraka wake,wale wote ni matapeli,ukienda pale wako radhi wakupukitushe Hadi chupi uliyovaa,

Wakuu nashauri msijaribu hata kumfuata huyo bwana PM,Ila Kama mnataka kuibiwa Basi jaribuni,I speak from my experience,nimewahi kufika huko,nilichoambulia ni kutapeliwa kila kitu na hao jamaa wa ngende,hakuna jipya nililoliona.
Yaani had wewe ulobahatika kwenda shule ulienda?? Aisee.
 
Formular ya pesa ni hardworking, nidhamu ya pesa, kuthamini muda, kutafuta na kubuni fursa mpya kila siku, kuhakikisha unadominate soko ya bidhaa yako, uaminifu, kua mkweli, hakikisha huduma au bidhaa yako inakua bora kwa viwango, hakikisha unakua na customer care nzuri, hapo umemaliza mengine ni mbwembwe kwa wasijiamini kwani mganga kama anaweza kukugawia utajiri kwa nini yeye afe fukara unadhani yeye anakupenda sana kuliko anavojipenda,? Wengi wao matapeli tu
 
Hii kitu hii mkuu digba sowey anasema alitapeliwa ngoja nikitulia nije kuelezea stori ya rafiki yangu ambaye ni mmakonde na ilibidi arudi kwao kuadjust.

Edit:

Nimerudi- nina rafiki tulijuana kupitia ishu za kuuza muvi mshkaji akaja akaoa baada ya muda ile ndoa ikawa miyeyusho kwakua binti akajidhihirisha kwamba anataka kuishi maisha ya juu mno.

Mume ana simu ya kawaida yeye anaingia mchezo ili afanye birthday au anunue simu baadaye zikaanza na dharau. Hapo wana mtoto mmoja jamaa akaona asikonde kwenye ndoa akaazimia kumuacha mwanamke.

Haka ni kastori karefu lakini ni kwamba akamuacha na jamaa akawa ameenda kijijini kwao kuadjust ili ofisi imlipe mimi nikaiescape hiyo proposal kwa kusema sina nauli. Mchizi kufika kule akapigwa manyanga akaambiwa kwamba kuna kitu umetumiwa na mwanamke wako kwahiyo tuanze na hilo kwanza.

Wakaanza na hilo kisha ikaja biashara kupigwa ndumba.

Akarudi akatuhadithia yaliyotokea. Biashara yake imeflourish kwa maelezo yake anasema anaweza kutengeneza 30K to 50K siku ambazo siyo J3. J3 anatengeneza kuanzia 50K to 100K.

So nafikiri ina ukweli wake na kuna hiyo chapter ya utapeli kama ya digba sowey
 
Acha kutapeli watu mkuu,labda Kama unazungumzia ngende ya mgodini,Ila Kama unazungumzia ngende ya liwale iliyoko Kijiji Cha mpigamiti Basi jua unataka kutapeli watu hapa.

Kiufupi huwezi nificha kitu kuhusu huyo Bibi njumwite,na vibaraka wake,wale wote ni matapeli,ukienda pale wako radhi wakupukitushe Hadi chupi uliyovaa,

Wakuu nashauri msijaribu hata kumfuata huyo bwana PM,Ila Kama mnataka kuibiwa Basi jaribuni,I speak from my experience,nimewahi kufika huko,nilichoambulia ni kutapeliwa kila kitu na hao jamaa wa ngende,hakuna jipya nililoliona.
Bahati yako ulitapeliwa pesa tu ungefirw* fanyeni kazi vijana pesa za bure hakuna dunia hii.
 
Mambo vipi wazee!

Aisee duniani kuna mambo sana.

Ukienda gende yenyewe original kutafuta utajiri hakika utaupata endapo tu utazingatia masharti yao.

Sharti lao kuu uwe na biashara, hili sharti halihitaji biashara kubwa. Hata biashara ya kuuza nyanya chungu poa tu, hata kuuza mishikaki ya mia mia poa tu.

Jamaa watakupa pesa either ya noti au sarafu ingawa sarafu ndio kipaumbele chao zaidi. Ile pesa utaambiwa kaiweke kwenye mkoba au chombo unachotunzia fedha za mauzo.

Jioni ukipega hesabu utakuta imeji double mara kadhaa.

Kuhusu gharama ya ndagu jamaa kwa ufupi ni Kama wanatoa bure vile maana mara nyingi wanasema utarudi kushukuru wazee ukifanikiwa.

Hapo ndipo utajiri unakujia.

Nitatoa mifano ya watu 4 ninaowafahamu walioshindwa masharti kabla au baada ya utajiri:

1. Huyu jamaa alipewa sharti la kupeleka sh. Mia moja ya sarafu kila mwaka wakati wa kiangazi. Aliweza kupeleka misimu miwili tu akadharau. Aliishia kuwa fukara.

2. Huyu jamaa alipewa sharti la kupeleka sindano ya mkono moja kila mwaka wakati wa kiangazi alipekeka mara moja tu akaona ni ujinga, atoke na gari Iringa mpaka Liwale ngende kupeleka sindano ya sh. Hamsini huku anatumia mafuta ya laki 3 . Sasa ni fukara anaomba mpaka sigara.

3. Alipewa sharti la kutokusalimiana au kupeana mkono na mtu yeyote kutoka Liwale Lindi mpaka Dar. Akaona simple. Nakuambia huyu alichemka vibaya. Akarudi kwa bibi akabadilishiwa sharti. Akatajirika ila mwishowe alichemka sharti la pili la kutokuchepuka. Unaambiwa baada ya kuwa na mipesa mastaa wa Bongo warembo unaowafahamu walimzonga kila kona akachepuka nao wawili watatu akafilisika.

4. Huyu alipewa sharti la kusafiri kwa mguu au baiskeli tu. Akafanikiwa sana mpaka alijenga hoteli za kisasa. Akiangalia meneja wa hotel zake zote mbili wana magari yeye ni mwendo wa baiskeli tu. Akanunua magari ya kutembelea. Akafulia.

Visa ni vingi takuja kusimulia vingine.
Meneja ana gari kali boss anakomaa na baiskeli
 
Naomba rejea mkuu ayo mandiko
Mathayo 12


25 Basi Yesu akijua mawazo yao, akawaambia, Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama.
26 Na Shetani akimtoa Shetani, amefitinika juu ya nafsi yake; basi ufalme wake utasimamaje?


Marko 3


23 Akawaita, akawaambia kwa mifano, Awezaje Shetani kumtoa Shetani?
24 Na ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, ufalme huo hauwezi kusimama;
25 na nyumba ikifitinika juu ya nafsi yake, nyumba hiyo haiwezi kusimama.
26 Na kama Shetani ameondoka juu ya nafsi yake, akafitinika, hawezi kusimama, bali huwa na kikomo.
 
Yaani had wewe ulobahatika kwenda shule ulienda?? Aisee.
Unajua mimi kwa ''ujinga'' wangu nilikuwa sidhani kama kuna binadamu tena kijana aliyesoma anaweza kuamini hayo mambo ya ''ngende'' na utajiri. Kumbe hata meseji za kitapeli zinazotumwa kwenye simu huwa zinapata ''mabwege'' wa kuliwa. Hata huyu mwanzisha thread anatafuta bwege wa kumliza na huenda kabisa akapata wengi. Kweli dunia ni mzunguko.
 
Unajua mimi kwa ''ujinga'' wangu nilikuwa sidhani kama kuna binadamu tena kijana aliyesoma anaweza kuamini hayo mambo ya ''ngende'' na utajiri. Kumbe hata meseji za kitapeli zinazotumwa kwenye simu huwa zinapata ''mabwege'' wa kuliwa. Hata huyu mwanzisha thread anatafuta bwege wa kumliza na huenda kabisa akapata wengi. Kweli dunia ni mzunguko.

Ukweli elimu tuliyoipata haijatusaidia hata kidg...huyu bwana kwa mujibu wa maandiko yake ni mwalimu..duh💣
 
Mambo vipi wazee!

Aisee duniani kuna mambo sana.

Ukienda gende yenyewe original kutafuta utajiri hakika utaupata endapo tu utazingatia masharti yao.

Sharti lao kuu uwe na biashara, hili sharti halihitaji biashara kubwa. Hata biashara ya kuuza nyanya chungu poa tu, hata kuuza mishikaki ya mia mia poa tu.

Jamaa watakupa pesa either ya noti au sarafu ingawa sarafu ndio kipaumbele chao zaidi. Ile pesa utaambiwa kaiweke kwenye mkoba au chombo unachotunzia fedha za mauzo.

Jioni ukipega hesabu utakuta imeji double mara kadhaa.

Kuhusu gharama ya ndagu jamaa kwa ufupi ni Kama wanatoa bure vile maana mara nyingi wanasema utarudi kushukuru wazee ukifanikiwa.

Hapo ndipo utajiri unakujia.

Nitatoa mifano ya watu 4 ninaowafahamu walioshindwa masharti kabla au baada ya utajiri:

1. Huyu jamaa alipewa sharti la kupeleka sh. Mia moja ya sarafu kila mwaka wakati wa kiangazi. Aliweza kupeleka misimu miwili tu akadharau. Aliishia kuwa fukara.

2. Huyu jamaa alipewa sharti la kupeleka sindano ya mkono moja kila mwaka wakati wa kiangazi alipekeka mara moja tu akaona ni ujinga, atoke na gari Iringa mpaka Liwale ngende kupeleka sindano ya sh. Hamsini huku anatumia mafuta ya laki 3 . Sasa ni fukara anaomba mpaka sigara.

3. Alipewa sharti la kutokusalimiana au kupeana mkono na mtu yeyote kutoka Liwale Lindi mpaka Dar. Akaona simple. Nakuambia huyu alichemka vibaya. Akarudi kwa bibi akabadilishiwa sharti. Akatajirika ila mwishowe alichemka sharti la pili la kutokuchepuka. Unaambiwa baada ya kuwa na mipesa mastaa wa Bongo warembo unaowafahamu walimzonga kila kona akachepuka nao wawili watatu akafilisika.

4. Huyu alipewa sharti la kusafiri kwa mguu au baiskeli tu. Akafanikiwa sana mpaka alijenga hoteli za kisasa. Akiangalia meneja wa hotel zake zote mbili wana magari yeye ni mwendo wa baiskeli tu. Akanunua magari ya kutembelea. Akafulia.

Visa ni vingi takuja kusimulia vingine.
duh, ya kweli mkuu!!?
 
Back
Top Bottom