Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Hakika umeona vzr ,huyu jamaa nimemnoti anaiba na wala hana uhandishi huu ,muandiko wake naufahamu mno anakop na kupaste huku [emoji38]

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
Sasa wewe kama sio kilaza basi ni zwazwa.
Jf kuanzia majina nk ni fake lkn unatafuta uhalisia kwenye story ya mtu mwenye jina na utambulisho fake!
Una akili kweli?
Humu tunaburudika na kupunguza msongo na kusonga mbele...tambaa zako
 
Venye nna hasira hii simulizi ntaiweza kweli? Mtu amekukatia line mpk unafikia kuwa nesi wa zamu bado anakuja unampa ela?! Haya we apo ulikua mpitaji utasemaje eti kuaga kuondoka utaonekana umedharau?

Acha tu lemutuz atudharau atudanganye chuma alitaka kumpa uteuzi akamjibu ukitaka tugombane unipe huo uteuzi. Nimegafirika sana
 
Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 03



Nilisimama pale kando ya lile jengo la Ubungo Plaza huku nikiendelea kuwa makini sana,baada ya muda wa nusu saa kuna namba nisiyoifahamu ikanipigia.

Mimi "Hallo"

Yeye "Hallo,mambo vipi"

Mimi "poa,nani?"

Yeye " Ah mh! Wewe si ndiye mgeni wa Mzee Nicolaus?"

Mimi "Ndiyo"

Yeye "Ameniambia upo Ubungo Plaza nije nikuchukue"

Aliendelea "Umesimama eneo gani?"

Mimi "Nipo mbele ya hili jengo kaka,mbele kabisa ya mlango wa kuingia"

Yeye "Ok sasa vuka barabara uje upande wa pilipili unaiona hii gari nyeusi Prado imepaki hapa pembeni?"

Aliendelea "wewe si ndo umevaa shati la damu ya mzee na suruali ya kaki?"

Mimi "Ndiyo kaka,umeniona?"

Yeye "Nishakuona,vuka uje nakusubiri"

Nilivuka ile barabara kwa umakini mkubwa huku nikiendelea kushangaa magari namna yalivyokuwa mengi barabarani,wakati nimefika jiji la Dar es salaam hii barabara ya kutoka Manzese hakukuwa imejengwa miundombinu ya Mwendokasi,hivyo haikuwa rahisi kuivuka ile barabara kwasababu magari yalikuwa rafu sana!.Nilipofika kwenye ile gari jamaa aliyonielekeza niliisogelea kisha nikamgongea kioo akawa amekishusha.

Jamaa "Shwari?"

Mimi "Swari kaka"

Jamaa "Ok Ingia twende"

Nilipanda kwenye ile gari nikaa mbele ili iwe rahisi kuyatazama maeneo ya jiji kwa uzuri zaidi.Wakati tupo kwenye gari hatukuwa na stori sana kwasababu jamaa muda wote alikuwa akiongea na simu.

Baada ya dakika kadhaa tukawa tumefika kwenye nyumba nzuri mno iliyokuwa na geti,ndipo jamaa alipiga honi akawa amefunguliwa geti,baada ya mimi kutelemka jamaa aliondoka na ile gari.Kiukweli ile nyumba ilikuwa nzuri sana na nilipokuwa mwenyeji ndipo niligundua Anko Nico alikuwa akiishi eneo la Ununio -Bahari beach.

Historia fupi ya Anko Nico.

Kiukweli mimi tangu nimekuwa,wajomba zangu nimekuwa nikiwaona Tarime wakiwa wamepita kumsalimia dada yao(Mama yangu),sikuwahi kuzifahamu familia zao na hata makao yao,na mara zote wakati wanapita hapo Tarime huwa wanakuja wenyewe.Hivyo ilikuwa tu ni eidha mama atuambie kuna mjomba wako anaishi sehemu fulani na mwingine yupo sehemu fulani.

Kaka zake mama ambao ni wajomba zangu,wapo wanne(4),Mmoja yupo Serengeti ni muajiliwa wa Tanapa,Mwingine ni Mwanajeshi aliwahi kuwa hapo Lugalo lakini sikuhizi amehamishiwa Kigoma,mwingine anaishj na familia yake huko Botswana,na mwingine ndiye huyu ambaye nilikuwa kwake,kwa bahati nzuri wote nimewahi kuwaona ila sikuwahi kuishi nao.

Kumekuwa na sintofahamu mara zote katika familia mbili na huwa sifahamu shida ni nini,kwa upande wa kina Baba nilikuwaga nikizingua au kufanya kosa lolote,wakati baba akiniadhibu alikuwa akiniambia nimechukua akili za kipumbavu za ujombani,vilevile mama nae alikuwa akisema upande wa kina baba wana roho mbaya na tabia za kipumbavu,sasa sikuwahi kufahamu ni kitu gani kilikuwa kinaendelea kati ya familia hizi mbili.

Anko nico alikuwa ni Contractor na Mkewe hadi leo ninapoandika yupo anafanya kazi wizara ya Afya,Anko Nico kwasasa ni marehemu,hivyo mkewe ndiyo kila kitu kwenye familia yake kwasasa.

Nimeona nitoe historia fupi kidogo ili huko mbele maswali yapungue.

Basi baada ya kuachwa pale ndani ya fensi kulikuwa na ukimya wa ajabu,ni ndege tu ambao nilisikia wanalia kwenye miti,kiukweli mazingira yale ungedhani wanakaa mawaziri au viongozi wenye vyeo vikubwa serikalini kwasababu kulikuwa kuzuri na kutulivu mno!.Baada ya muda nikiwa nashangaa,mlango ulifunguliwa akawa ametoka nje binti mmoja aliyekuwa amevalia mavazi ya jikoni(Yale mavazi yanavaliwa na wapishi wakiwa jikoni wanapika).

Yule binti "Karibu"

Mimi " Ahsante"

Yule binti "Unaitwa nani?"

Mimi "Umughaka"

Yule binti "Kumbe ndiyo wewe!"

Tulipofika ndani nikaa kwenye kochi nikawa nashangaa namna watu walivyokuwa wakiishi,wakati naendelea kushangaa mara simu ya mezani ikawa inaita,yule binti akawa amekuja kuipokea.

Yule binti " Eeh amefika baba"

Aliendelea "sawa baba"

Baada ya yale maongezi yule binti akawa ameikata ile simu na kuondoka kwenda kuendelea na alichokuwa anakifanya.

Yule binti alipoivishwa chakula kilitengwa na kunitaka niende nikajisevie,nilinyanyuka zangu nikaenda kupakua msosi na kuanza kula,nilipomaliza kula yule binti alinionyesha chumba ambacho nilipaswa kwenda kuoga na ndipo ningelala kwa siku hiyo,sasa nilipofungua na kuingia ndani nilimkuta mzee mmoja akiwa amelala huku ikionekana kabisa afya yake imedhoofika kwasababu nilikuta amewekewa mpira wa kukojolea,yaonyesha hata kokojoa mwenyewe tu alikuwa hawezi.

Nilipoufungua ule mlango na kuingia ndani akawa ameshituka na kugeuka kwa shida kunitazama.

Mimi "Shikamoo"

Mzee "Marhaba"

Baada ya salamu sikuwa na stori zaidi ya kuendelea kumshangaa mzee huku na yeye akinitazama kwa umakini.Kwakuwa alikuwa amewekewa mpira wa kukojolea nilifahamu kabisa ni mgonjwa na hivyo ikabidi nimpe Pole.

Mimi "Pole sana mzee wangu"

Mzee "Pole ya nini mwanangu!"

Mimi "kwa maumivu mzee"

Mzee "Aaah haya nilishayazoea muda tu"

Aliendelea "wewe ni nani?"

Mimi "Mimi naitwa Umughaka,Nicolaus ni mjomba wangu"

Mzee "Oooh sawa"

Kwa namna mzee alivyokuwa akiongea alionyesha kabisa ni mtu kutokea pande za kaskazini mwa nchi yetu.

Nilivua nguo nikawa nimeingia bafuni kuoga,sasa wakati nikiwa bafuni nikawa nasikia simu yangu inaita mpaka ikakata,nilipomaliza kuoga moja kwa moja nilienda kuitazama na ndipo nikakuta ni mtoto wa baba mkubwa Kileri alikuwa akinipigia.Nilibadili nguo kisha nikampigia.

Kileri "Mwanangu nisamehe sana,uko wapi?"

Mimi "Nipo kwa Anko Nico"

Kileri "Maeneo gani kaka nije kukuchukua"

Mimi "Usijali niko salama kabisa kaka,nadhani nikitoka huku nitakufahamisha"

Kileri "Daaah nisamehe sana kaka,simu yangu huwa inasumbua betri,jana ilizima"

Mimi "Ungetumia hata simu ya mtu kaka"

Kileri "Tatizo namba yako sijaikariri kaka!"

Mimi "Usijali kaka hakuna kilichoharibika"

Kileri "Poa mwanangu lakini hakikisha huchelewi ili tupambane"

Mimi "Nikitoka huku nitakushitua"

Baada ya yale maongezi na kileri nilitoka mle chumbani nikarudi zangu sebuleni.Nilikaa pale sebuleni huku nikiendelea kutazama luninga,mida ya saa 9 alasiri kuna mabinti wawili waliingia ndani,mmoja akiwa mkubwa na mwingine mdogo,japo kuwa wote walikuwa na miaka zaidi ya 18 lakini kuna mmoja alikuwa mkubwa kuliko mwenzie,wale mabinti walikuwa watoto wa mjomba Niko na kiukweli sikuwahi kuwafahamu na wao walikuwa hawanijui,waliniangalia na mmoja akanisalimia ila mmoja alikula buyu na kuzama ndani!.

Ilipofika mida ya saa 1 usiku,kuna gari iliingia ndani ya fensi ya ile nyumba na haukupita muda akawa ameingia ndani mke wa Anko Nico ambaye nimewahi kumuona mara moja tu pale Tarime wakiwa wamekuja mmewe kumsalimia mama.

Mke wa Anko "Habari ya siku"

Mimi "Nzuri,shikamoo"

Mke wa anko "Marhaba"

Aliendelea "Tarime wazima?"

Mimi "Wazima kabisa"

Mke wa anko "Wifi yupo?"

Mimi "Yupo mzima kabisa"

Mke wa anko "Karibu"

Baada ya salamu yule mke wa anko alizama ndani kwake huko.Ile familia ilikuwa ni familia ambayo ilikuwa haijali kabisa na kila mmoja alijali mambo yake.

Ilipofika mida ya saa 2 mjomba nae akawa amefika.Tuliongea mambo mengi sana na Anko Nico na alitaka kufahamu nimekuja Dar es salaam kufanya shughuli gani kwasababu aliniambia huu mji bila kuwa na kazi ni vema ningerudi Tarime kuliko kudhani kungekuwa na mteremko wa maisha mazuri.Baada ya kumwambia kilichokuwa kimenileta alielewa na akawa kimya.

Maisha ya hapo nyumbani kwa Anko yaliendelea kama kawaida na sasa nikaambiwa niwe namuangalia yule mzee na kumbadilishia mpira,kumuogesha na hata kwenda chooni nihakikishe niwe namtazama,ingawa alikuwa akijiweza kwa kujikokota lakini alihitaji uangalizi,sasa kumbe yule mzee alikuwa ni baba yake na mke wa mjomba Nico.
Niliona nikiondoka pale kwa Anko na kwenda kwa Kileri nitakuwa kama nimewadharau na niliona naweza kupata tatizo halafu ikala kwangu kwasababu ya kuondoka kwa ujuaji,nilisubiri Anko aniambie sasa ni muda wa kuondoka nikaendelee na shughuli zangu baada ya kunifadhili kwa makazi kwa muda.

Kwakuwa muda na siku zilikuwa zimekwenda,Kileri aliniambia kama inawezekana nimuelekeze maeneo nilipokuwa aje achukue ile hela ili akanunue mzigo wa kutosha aongeze kwenye duka kama tulivyokuwa tumekubaliana ili biashara iendelee kufanyika,sikuwa kabisa na shaka kwasababu niliamini ni mtoto wa baba yangu mkubwa na kwetu anafahamika na mimi kwao nafahamika,hivyo niliona ni vema nimwambie aje mpaka Ununio kuchukua ile hela akaendelee kufanya biashara na faida tuwe tunagawana.

Mipango yote ya ufanyaji wa biashara na upatikanaji wa faida tulikuwa tumeisuka tangu nikiwa Tarime,basi jamaa alikuja nikawa nimempatia ile yote milioni 9 akawa ameondoka.

Maisha yalisonga na jamaa akawa ananipa mrejesho kuhusu biashara na kiukweli kwa mujibu wa maelezo yake ilikuwa inachanganya vibaya hivyo sikuwa na shaka.

Pale kwa Anko walikuwa wakiondoka asubuhi nilikuwa ninabaki mimi na yule binti wa kazi huku mimi nikiendelea kumuangalia yule mzee na kuwa kama mtu wa usafi nje ya nyumba.Kadiri siku zilivyokuwa zinasonga ndipo na mambo yalianza kubadilika,kuna siku nilikuwa nikimsalimia mke wa anko anajifanya hajasikia salamu anasepa,nilidhani uenda ilikuwa ni kawaida kwa mtu mzima kuwa na mawazo kumbe haikuwa kama nilivyodhani.

Kuna siku aliporudi kutoka kazini kwake nikawa nasikia anamgombeza sana mjomba huko chumbani kwao na sikufahamu ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.

Itaendelea....
Kuishi na ndugu kazi Sana ni heri upange ama ubaki kwenu Tu ndugu hapana
 
Nimeanza kuyaona yale ninayoamini. Yaani mke wako huwa hapendi uishi na ndugu zako Ila ndugu zake tu sema Kama hao waliosoma na wanaojua hela.

Yaani ukifanikiwa na ukaoa Kilimanjaro na umetokea huko Kama kyasaka ndipo utajua. Jamani mke wangu adhubutu kunyanyua mdomo kujibizana namie.

Bora niishi single
 
Nisikuchoshe na usinichoshe, tusichoshane!.

Kwanza kabisa nipende kuwashukuru wote ambao mmeendelea kuwa na mimi bega kwa bega tangia mwanzo wakati naanza kusimulia visa vya maisha yangu ambayo nimeyaishi na kuyapitia kama mwanadamu.

Simulizi yangu ya kwanza kabisa hapa JF imefahamika kama "TULICHOMFANYA YULE MCHAWI HATOKUJA KUSAHAU KAMWE" hii inapatikana kwenye jukwaa hili la Entertainment,simulizi hii iliangazia namna tulivyopata shuruba ya ushirikina wakati ambao nilienda kumsalimia baba yangu mdogo aliyekuwa mwalimu katika shule moja ya sekondari huko mkoani Tabora,kiukweli ni mkasa ambao sitokuja kuusahau kamwe kwasababu ndipo niliamini wachawi wapo na uchawi upo!

Simulizi ya pili ilikuwa ni muendelezo baada ya hiyo ya kwanza,simulizi hii ya pili niliona nianze kusimulia baada ya mimi kwenda shule ya upili(Advance)na wakati nilipo maliza matokeo yangu hayakuwa mazuri hivyo nikatimuliwa na Mzee(Baba)yangu nyumbani nikaingia mtaani kupambana,simulizi hii inafahamika kama "NILIVYONUSURIKA KIFO BAADA YA MZEE KUNITIMUA NYUMBANI" na inapatikana kwenye jukwaa la Habari na Hoja Mchanganyiko.

Sasa leo nimeona niwaletee na niendelee na masimulizi ya maisha yangu ili kuwapa hamasa vijana wenzangu kuweza kupambana na kutokata tamaa mapema!,dhumuni la masimulizi yangu ni kutoa funzo kwa watu,na sipo hapa ili kujipatia fedha kwa njia ya ulagahai,mimi binafsi ninajiweza kwasababu ni mpambanaji na sihitaji hata mia mbovu ya walalahoi wenzangu!.

Mimi binafsi nimfanyabiashara, nimejiajiri kwa kutoa huduma ya usafirishaji wa abiria almaarufu kama Bodaboda, shughuli zangu huwa nazifanyia hapa Bunju, ingawa ki makazi naishi mbezi Inn ila kikazi nafanyia Bunju. Sasa kama mtakumbuka kwenye simulizi ya mwisho nilisema ya kwamba,baada ya kuwa tumeuza lile duka la vipodozi ambalo tulikuwa tumefungua na rafiki yangu kipenzi Mtatiro (Kwa sasa anaishi nchini Uganda), tuliamua kugawana fedha kila mtu afe na chake, mimi niliamua kurudi zangu Tarime-Sirari, baada ya kukaa kule kuna ndugu yangu(Mtoto wa Baba yangu mkubwa) tuliwasiliana naye akaniambia nije Dar es salaam ili tufanye biashara ya uuzaji wa vyombo vya ndani kwasababu kwa wakati huo ilikuwa na pesa(Kwa maelezo yake).

Niliianza safari ya kuja Dar es salaam, sasa nilipofika Dar es salaam pale Ubungo(Kipindi stendi bado haijaamia mbezi), ile nimefika mida ya saa 5 usiku nikampigia simu mwenyeji wangu lakini majibu toka kwenye simu ni kwamba "Namba unayopiga kwasasa haipatikani,jaribu tena baadae", niliendelea kuipiga ile simu lakini majibu yalikuwa ni hayi hayo!.

Kwakuwa nilikuwa nimechoka,niliamua kumsikiliza moja ya watu ambao walikuwa wakinisumbua ili wabebe mzigo wa begi langu ili niwalipe posho, mpaka wakati huo nilikuwa makini sana kujilinda mimi binafsi pamoja na mzigo wangu, kilichofanya nikawa makini kupita kiasi ni stori ambazo mara zote nimekuwa nikizisikia kuhusu Jiji la Dar es salaam na vioja vyake.

Mimi " Mwanangu vipi!?"

Jamaa " Poa bro"

Mimi "Mbona mnavurugu,shida ni nini?"

Jamaa " Si huyu msenge,nimemwambia wewe ni wakwangu lakini hataki kusikia"

Mimi "Ok mnasemaje"

Jamaa "Bro we nipe begi mi nikubebee,achana na huyu muhuni atakuibia"

Mimi " Sasa wote mnang'ang'ania mzigo,nimpe nani na nimwache nani?"

Mimi "Sa sikia,begi langu nitalibeba mwenyewe,achaneni na mimi"

Baada ya kusikia rafudhi yangu na namna nilivyochukia nadhani waliamua kutii sheria bila shuruti,waliondoka wakiwa wananiangalia kwa uchungu na maumivu makali ya kukosa posho!.Kiukweli muda huo nilichokiongea ndicho nilichokuwa nikikimaanisha, kutokana na sifa mbaya za mkoa wa Dar es salaam nilikuwa nimesema yeyote ambaye angejitia kimbelembele kunikaba au kuniibia,basi siku hiyo ndiyo ingekuwa mwisho wa maisha yake!,Jeuri na kiburi cha kikurya vilinitia morali maradufu na niliwaona wale vijana wa pale stendi ni kama wanawake tu wasiokuwa na uwezo wa kunifanya chochote!.

Niliamua kujisogeza mpaka kwenye geti la kutoka nje,nilipotoka nje nilikuwa nikiendelea kushangaa pilika pilika namna zilivyokuwa za kutosha pale stendi,kiukweli sikuwahi kuona mji uliokuwa na pilika nyingi kama Dar es salaam,Mwanza nimekaa lakini hakukuwa na harakati za kutosha kama Dar es salaam.Nilichukua simu yangu nikawa nampigia tena mwenyeji wangu lakini simu yake ikawa haipatikani.Nilichukia sana kwasababu nakumbuka nilivyofika Singida alinipigia simu nikamwambia ya kwamba nimefika Singida na akawa amesema ikifika mida ya saa 2 usiku angekuwa amekuja pale stendi ili anisubiri nikifika tuondoke wote.

Kuna jamaa mmoja alikuwa kando ya geti la kutokea nje ya stendi pale Ubungo nilimsogelea nikawa namuuliza kuhusu Guest House yeyote iliyokuwa karibu ili niende nikalale na ikiwezekana asubuhi niendelee kumtafuta jamaa.

Jamaa "Sasa tutafanyaje ndugu!"

Aliendelea "Mwenyeji wako hajatokea?".

Mimi "Nimempigia simu lakini hapatikani!"

Jamaa "Duuuu mbona ni hatari!"

Aliendelea "Sasa sikia,wewe nyooka na hii barabara,unaona kwenye ile njia?"

Mimi "Ndiyo"

Jamaa "Hebu subiri"

Jamaa " Hassaniiiiiii"

Baada ya ya kuita hilo jina muhusika alifika


Jamaa "Hassani hebu nenda kampeleke huyu jamaa pale kwa Asteria,ukifika mwambie jamaa anataka chumba"

Aliendelea "Kaka nenda na jamaa atakupeleka kwenye Lodge ambayo kuna usalama na vyumba vipo vya kutosha,ila utamlipa maana kuna umbali"

Mimi "Hakuna tatizo"


Basi yule jamaa aliyeitwa Hassan akanichukua akanivusha barabara tukaikamata njia ya Ubungo Maziwa kuelekea kwenye hiyo lodge ambayo nimeambiwa kuna usalama na vyumba vya kutosha.Wakati tunakwenda na Bwana Hassan tulikuwa tunapiga stori za hapa na pale huku mikono yangu ikiwa bize imeng'ang'ania begi kwasababu ndilo lililokuwa na hela pamoja na nguo za kubadilisha,kiukweli nilikuwa nimesema endapo yeyote angejipendekeza kunikaba angejuta kuzaliwa.

Baada ya mwendo mrefu kidogo hatimaye tukawa tumefika kwenye Bar moja iliyokuwa inapiga mziki kwa sauti kubwa huku kukiwa na watu wengi.

Hassan " Nisubiri hapa nakuja"

Nilimsubiri Hassan pale nje baada ya kufika kwenye hiyo Bar na baada ya dakika 15 akawa amekuja kunichukua na kuongozana nae kuingia ndani.Tulipofika ndani ambako kulikuwa na kaunta,Hassan alinichukua tena kuelekea Uani ambako nilikuta kuna vyumba vingi ambavyo vilikuwa havipungui 10.

Sasa baada ya kufika pale Uani alikuja mwanamke mmoja mweusi mnene na ndiye aliyekuwa akiitwa Asteria,alimuita Hassan Pembeni wakawa wanaongea,sikufahamu kitu walichokuwa wanazungumza kwa wakati huo.Baada ya yale mazungumzo Hassan alirudi kwangu.


Hassan "Sasa bro,mimi nadhani nikuache wewe upumzike,niangalizie basi ustaarabu"

Mimi "Chumba changu cha kulala ni kipi?"

Hassan "Atakuonyesha Asteria,wala usijali kaka hapa ni nyumbani"

Baada ya maneno ya kutia moyo ya Hassan nikachomoa shilingi elfu 5 nikawa nimempatia kama posho ya kunipeleka hapo Guest.

Hassan "Aaah kaka hela gani hii?"

Mimi "Hela gani kivipi?"

Hasaan "Aaaah Kaka yaani nikutoe kule stendi na nimeacha shughuli zangu halafu unanipatia buku tano?,hebu ongeza ongeza kaka angalau kesho niamkie supu"


Sikutaka mambo mengi na yule Jamaa ikabidi nizame tena mfukoni nikatoa elfu 5 nyingine nikampatia,hivyo kufanya jumla kuwa elfu 10.

Baada ya jamaa kuondoka lile eneo nikamfuata yule demu aliyeitwa Asteria ili aje anionyeshe chumba niingie kulala kwasababu nilikuwa nimechoka.

Asteria "Kaka ina maana Hujaambiwa huu si muda wa kulala?"

Mimi "Si muda wa kulala?"

Mimi "Si muda wa kulala kivipi?"

Asteria "Kaka hapa huwa hatulazi watu ila tunakodisha!"

Aliendelea "Hivi vyumba vinakodishwa kwa dakika na masaa,labda usubiri mpaka saa 9 wateja wakipingua ndipo tutakukodishia ulale"

Kiukweli baada ya ile kauli niliishiwa nguvu ghafla,sasa baada ya kuniambia maneno yale yeye aliondoka akaenda kuendelea na shughuli zake akaniacha pale Uani nikiwa sijui cha kufanya,sasa ndipo nilikuja kugundua ya kwamba,vile vyumba vilikuwa vinatumika kwenye biashara ya short time(Biashara ya Ngono),sasa kumbe ile Bar niliyopelekwa,pale nje kulikuwa na wanawake wanaouza miili yao(Dada Poa) na vile vyumba vilitumika kwa shughuli ya short time.

Itaendelea.
Safi Umughaka is back[emoji120]

Sent from my Infinix X665 using JamiiForums mobile app
 
Kwahiyo kwakua wewe haujaingi kwenye hiyo contract, una uhakika wa kuishi zaidi ya hiyo miaka 10?

Mimi naamini kuna madhara mengine ambayo huwa wanapitia yanayowaumiza kuliko hilo la kifo, kwasababu kifo kipo kwa wote.
Maumivu ya Kisaikoloji thus Wana KILA kitu lakini hawapo happy, zaidi ya kufake.
Kuna kifo cha faida na kifo cha hasara
 
Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 03



Nilisimama pale kando ya lile jengo la Ubungo Plaza huku nikiendelea kuwa makini sana,baada ya muda wa nusu saa kuna namba nisiyoifahamu ikanipigia.

Mimi "Hallo"

Yeye "Hallo,mambo vipi"

Mimi "poa,nani?"

Yeye " Ah mh! Wewe si ndiye mgeni wa Mzee Nicolaus?"

Mimi "Ndiyo"

Yeye "Ameniambia upo Ubungo Plaza nije nikuchukue"

Aliendelea "Umesimama eneo gani?"

Mimi "Nipo mbele ya hili jengo kaka,mbele kabisa ya mlango wa kuingia"

Yeye "Ok sasa vuka barabara uje upande wa pilipili unaiona hii gari nyeusi Prado imepaki hapa pembeni?"

Aliendelea "wewe si ndo umevaa shati la damu ya mzee na suruali ya kaki?"

Mimi "Ndiyo kaka,umeniona?"

Yeye "Nishakuona,vuka uje nakusubiri"

Nilivuka ile barabara kwa umakini mkubwa huku nikiendelea kushangaa magari namna yalivyokuwa mengi barabarani,wakati nimefika jiji la Dar es salaam hii barabara ya kutoka Manzese hakukuwa imejengwa miundombinu ya Mwendokasi,hivyo haikuwa rahisi kuivuka ile barabara kwasababu magari yalikuwa rafu sana!.Nilipofika kwenye ile gari jamaa aliyonielekeza niliisogelea kisha nikamgongea kioo akawa amekishusha.

Jamaa "Shwari?"

Mimi "Swari kaka"

Jamaa "Ok Ingia twende"

Nilipanda kwenye ile gari nikaa mbele ili iwe rahisi kuyatazama maeneo ya jiji kwa uzuri zaidi.Wakati tupo kwenye gari hatukuwa na stori sana kwasababu jamaa muda wote alikuwa akiongea na simu.

Baada ya dakika kadhaa tukawa tumefika kwenye nyumba nzuri mno iliyokuwa na geti,ndipo jamaa alipiga honi akawa amefunguliwa geti,baada ya mimi kutelemka jamaa aliondoka na ile gari.Kiukweli ile nyumba ilikuwa nzuri sana na nilipokuwa mwenyeji ndipo niligundua Anko Nico alikuwa akiishi eneo la Ununio -Bahari beach.

Historia fupi ya Anko Nico.

Kiukweli mimi tangu nimekuwa,wajomba zangu nimekuwa nikiwaona Tarime wakiwa wamepita kumsalimia dada yao(Mama yangu),sikuwahi kuzifahamu familia zao na hata makao yao,na mara zote wakati wanapita hapo Tarime huwa wanakuja wenyewe.Hivyo ilikuwa tu ni eidha mama atuambie kuna mjomba wako anaishi sehemu fulani na mwingine yupo sehemu fulani.

Kaka zake mama ambao ni wajomba zangu,wapo wanne(4),Mmoja yupo Serengeti ni muajiliwa wa Tanapa,Mwingine ni Mwanajeshi aliwahi kuwa hapo Lugalo lakini sikuhizi amehamishiwa Kigoma,mwingine anaishj na familia yake huko Botswana,na mwingine ndiye huyu ambaye nilikuwa kwake,kwa bahati nzuri wote nimewahi kuwaona ila sikuwahi kuishi nao.

Kumekuwa na sintofahamu mara zote katika familia mbili na huwa sifahamu shida ni nini,kwa upande wa kina Baba nilikuwaga nikizingua au kufanya kosa lolote,wakati baba akiniadhibu alikuwa akiniambia nimechukua akili za kipumbavu za ujombani,vilevile mama nae alikuwa akisema upande wa kina baba wana roho mbaya na tabia za kipumbavu,sasa sikuwahi kufahamu ni kitu gani kilikuwa kinaendelea kati ya familia hizi mbili.

Anko nico alikuwa ni Contractor na Mkewe hadi leo ninapoandika yupo anafanya kazi wizara ya Afya,Anko Nico kwasasa ni marehemu,hivyo mkewe ndiyo kila kitu kwenye familia yake kwasasa.

Nimeona nitoe historia fupi kidogo ili huko mbele maswali yapungue.

Basi baada ya kuachwa pale ndani ya fensi kulikuwa na ukimya wa ajabu,ni ndege tu ambao nilisikia wanalia kwenye miti,kiukweli mazingira yale ungedhani wanakaa mawaziri au viongozi wenye vyeo vikubwa serikalini kwasababu kulikuwa kuzuri na kutulivu mno!.Baada ya muda nikiwa nashangaa,mlango ulifunguliwa akawa ametoka nje binti mmoja aliyekuwa amevalia mavazi ya jikoni(Yale mavazi yanavaliwa na wapishi wakiwa jikoni wanapika).

Yule binti "Karibu"

Mimi " Ahsante"

Yule binti "Unaitwa nani?"

Mimi "Umughaka"

Yule binti "Kumbe ndiyo wewe!"

Tulipofika ndani nikaa kwenye kochi nikawa nashangaa namna watu walivyokuwa wakiishi,wakati naendelea kushangaa mara simu ya mezani ikawa inaita,yule binti akawa amekuja kuipokea.

Yule binti " Eeh amefika baba"

Aliendelea "sawa baba"

Baada ya yale maongezi yule binti akawa ameikata ile simu na kuondoka kwenda kuendelea na alichokuwa anakifanya.

Yule binti alipoivishwa chakula kilitengwa na kunitaka niende nikajisevie,nilinyanyuka zangu nikaenda kupakua msosi na kuanza kula,nilipomaliza kula yule binti alinionyesha chumba ambacho nilipaswa kwenda kuoga na ndipo ningelala kwa siku hiyo,sasa nilipofungua na kuingia ndani nilimkuta mzee mmoja akiwa amelala huku ikionekana kabisa afya yake imedhoofika kwasababu nilikuta amewekewa mpira wa kukojolea,yaonyesha hata kokojoa mwenyewe tu alikuwa hawezi.

Nilipoufungua ule mlango na kuingia ndani akawa ameshituka na kugeuka kwa shida kunitazama.

Mimi "Shikamoo"

Mzee "Marhaba"

Baada ya salamu sikuwa na stori zaidi ya kuendelea kumshangaa mzee huku na yeye akinitazama kwa umakini.Kwakuwa alikuwa amewekewa mpira wa kukojolea nilifahamu kabisa ni mgonjwa na hivyo ikabidi nimpe Pole.

Mimi "Pole sana mzee wangu"

Mzee "Pole ya nini mwanangu!"

Mimi "kwa maumivu mzee"

Mzee "Aaah haya nilishayazoea muda tu"

Aliendelea "wewe ni nani?"

Mimi "Mimi naitwa Umughaka,Nicolaus ni mjomba wangu"

Mzee "Oooh sawa"

Kwa namna mzee alivyokuwa akiongea alionyesha kabisa ni mtu kutokea pande za kaskazini mwa nchi yetu.

Nilivua nguo nikawa nimeingia bafuni kuoga,sasa wakati nikiwa bafuni nikawa nasikia simu yangu inaita mpaka ikakata,nilipomaliza kuoga moja kwa moja nilienda kuitazama na ndipo nikakuta ni mtoto wa baba mkubwa Kileri alikuwa akinipigia.Nilibadili nguo kisha nikampigia.

Kileri "Mwanangu nisamehe sana,uko wapi?"

Mimi "Nipo kwa Anko Nico"

Kileri "Maeneo gani kaka nije kukuchukua"

Mimi "Usijali niko salama kabisa kaka,nadhani nikitoka huku nitakufahamisha"

Kileri "Daaah nisamehe sana kaka,simu yangu huwa inasumbua betri,jana ilizima"

Mimi "Ungetumia hata simu ya mtu kaka"

Kileri "Tatizo namba yako sijaikariri kaka!"

Mimi "Usijali kaka hakuna kilichoharibika"

Kileri "Poa mwanangu lakini hakikisha huchelewi ili tupambane"

Mimi "Nikitoka huku nitakushitua"

Baada ya yale maongezi na kileri nilitoka mle chumbani nikarudi zangu sebuleni.Nilikaa pale sebuleni huku nikiendelea kutazama luninga,mida ya saa 9 alasiri kuna mabinti wawili waliingia ndani,mmoja akiwa mkubwa na mwingine mdogo,japo kuwa wote walikuwa na miaka zaidi ya 18 lakini kuna mmoja alikuwa mkubwa kuliko mwenzie,wale mabinti walikuwa watoto wa mjomba Niko na kiukweli sikuwahi kuwafahamu na wao walikuwa hawanijui,waliniangalia na mmoja akanisalimia ila mmoja alikula buyu na kuzama ndani!.

Ilipofika mida ya saa 1 usiku,kuna gari iliingia ndani ya fensi ya ile nyumba na haukupita muda akawa ameingia ndani mke wa Anko Nico ambaye nimewahi kumuona mara moja tu pale Tarime wakiwa wamekuja mmewe kumsalimia mama.

Mke wa Anko "Habari ya siku"

Mimi "Nzuri,shikamoo"

Mke wa anko "Marhaba"

Aliendelea "Tarime wazima?"

Mimi "Wazima kabisa"

Mke wa anko "Wifi yupo?"

Mimi "Yupo mzima kabisa"

Mke wa anko "Karibu"

Baada ya salamu yule mke wa anko alizama ndani kwake huko.Ile familia ilikuwa ni familia ambayo ilikuwa haijali kabisa na kila mmoja alijali mambo yake.

Ilipofika mida ya saa 2 mjomba nae akawa amefika.Tuliongea mambo mengi sana na Anko Nico na alitaka kufahamu nimekuja Dar es salaam kufanya shughuli gani kwasababu aliniambia huu mji bila kuwa na kazi ni vema ningerudi Tarime kuliko kudhani kungekuwa na mteremko wa maisha mazuri.Baada ya kumwambia kilichokuwa kimenileta alielewa na akawa kimya.

Maisha ya hapo nyumbani kwa Anko yaliendelea kama kawaida na sasa nikaambiwa niwe namuangalia yule mzee na kumbadilishia mpira,kumuogesha na hata kwenda chooni nihakikishe niwe namtazama,ingawa alikuwa akijiweza kwa kujikokota lakini alihitaji uangalizi,sasa kumbe yule mzee alikuwa ni baba yake na mke wa mjomba Nico.
Niliona nikiondoka pale kwa Anko na kwenda kwa Kileri nitakuwa kama nimewadharau na niliona naweza kupata tatizo halafu ikala kwangu kwasababu ya kuondoka kwa ujuaji,nilisubiri Anko aniambie sasa ni muda wa kuondoka nikaendelee na shughuli zangu baada ya kunifadhili kwa makazi kwa muda.

Kwakuwa muda na siku zilikuwa zimekwenda,Kileri aliniambia kama inawezekana nimuelekeze maeneo nilipokuwa aje achukue ile hela ili akanunue mzigo wa kutosha aongeze kwenye duka kama tulivyokuwa tumekubaliana ili biashara iendelee kufanyika,sikuwa kabisa na shaka kwasababu niliamini ni mtoto wa baba yangu mkubwa na kwetu anafahamika na mimi kwao nafahamika,hivyo niliona ni vema nimwambie aje mpaka Ununio kuchukua ile hela akaendelee kufanya biashara na faida tuwe tunagawana.

Mipango yote ya ufanyaji wa biashara na upatikanaji wa faida tulikuwa tumeisuka tangu nikiwa Tarime,basi jamaa alikuja nikawa nimempatia ile yote milioni 9 akawa ameondoka.

Maisha yalisonga na jamaa akawa ananipa mrejesho kuhusu biashara na kiukweli kwa mujibu wa maelezo yake ilikuwa inachanganya vibaya hivyo sikuwa na shaka.

Pale kwa Anko walikuwa wakiondoka asubuhi nilikuwa ninabaki mimi na yule binti wa kazi huku mimi nikiendelea kumuangalia yule mzee na kuwa kama mtu wa usafi nje ya nyumba.Kadiri siku zilivyokuwa zinasonga ndipo na mambo yalianza kubadilika,kuna siku nilikuwa nikimsalimia mke wa anko anajifanya hajasikia salamu anasepa,nilidhani uenda ilikuwa ni kawaida kwa mtu mzima kuwa na mawazo kumbe haikuwa kama nilivyodhani.

Kuna siku aliporudi kutoka kazini kwake nikawa nasikia anamgombeza sana mjomba huko chumbani kwao na sikufahamu ni kitu gani kilikuwa kikiendelea.

Itaendelea....
Imeanza kunoga.

#MaendeleoHayanaChama
 
Back
Top Bottom