Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani

Hii tabia wanazo sana nyumba ambazo wana uwezo hawafundishwi upendo na kuthamini watu au kujali. Ila kama ukienda nyumba hizo una cheo au uwezo utathaminiwa haswa, wanakupita kama hawakuoni, nyumba chache sanaa utakaa vizuri.

Ndio maana sipendi kwenda kwa watu au ndugu kwa sababu umeenda kusalimia na sio kushughulika na mambo ya wagonjwa Kwan wakati haupo alisaidiwa na nani inatakiwa ufanye kwa ridhaa yako na sio Ndio inakuwa kazi yako kumuosha mtu sio ndugu yako sio kazi ndogo ujue wana uwezo walitakiwa kuwe na nesi wa kumshughulikia mzee na kumsafisha.

Acha nijikalie kwangu aisee kwa ndugu ni kazi kuishi
 
Habari za leo wakuu,bila shaka mko poa.

Nitaendelea kusimulia afya yangu ikitengemaa maana siko vizuri,Siku mbili zimepita nimetoka huko Kigamboni sasa nadhani nilipata mdudu (Korona),aisee kanitandika kinoma,sema nimejitahidi sana kutumia virutubisho na hivi sasa naendelea vema japo viungo vya mwili vinauma vibaya sana!.

Msijali nitaendelea nilipoishia,hali itakuwa vema ndugu zangu.

Nawapenda sana.
Pole mkuu Mwenyezi Mungu akufanyie wepesi Amina.
 
Nisikuchoshe na usinichoshe, tusichoshane!.

Kwanza kabisa nipende kuwashukuru wote ambao mmeendelea kuwa na mimi bega kwa bega tangia mwanzo wakati naanza kusimulia visa vya maisha yangu ambayo nimeyaishi na kuyapitia kama mwanadamu.

Simulizi yangu ya kwanza kabisa hapa JF imefahamika kama "TULICHOMFANYA YULE MCHAWI HATOKUJA KUSAHAU KAMWE" hii inapatikana kwenye jukwaa hili la Entertainment,simulizi hii iliangazia namna tulivyopata shuruba ya ushirikina wakati ambao nilienda kumsalimia baba yangu mdogo aliyekuwa mwalimu katika shule moja ya sekondari huko mkoani Tabora,kiukweli ni mkasa ambao sitokuja kuusahau kamwe kwasababu ndipo niliamini wachawi wapo na uchawi upo!

Simulizi ya pili ilikuwa ni muendelezo baada ya hiyo ya kwanza,simulizi hii ya pili niliona nianze kusimulia baada ya mimi kwenda shule ya upili(Advance)na wakati nilipo maliza matokeo yangu hayakuwa mazuri hivyo nikatimuliwa na Mzee(Baba)yangu nyumbani nikaingia mtaani kupambana,simulizi hii inafahamika kama "NILIVYONUSURIKA KIFO BAADA YA MZEE KUNITIMUA NYUMBANI" na inapatikana kwenye jukwaa la Habari na Hoja Mchanganyiko.

Sasa leo nimeona niwaletee na niendelee na masimulizi ya maisha yangu ili kuwapa hamasa vijana wenzangu kuweza kupambana na kutokata tamaa mapema!,dhumuni la masimulizi yangu ni kutoa funzo kwa watu,na sipo hapa ili kujipatia fedha kwa njia ya ulagahai,mimi binafsi ninajiweza kwasababu ni mpambanaji na sihitaji hata mia mbovu ya walalahoi wenzangu!.

Mimi binafsi nimfanyabiashara, nimejiajiri kwa kutoa huduma ya usafirishaji wa abiria almaarufu kama Bodaboda, shughuli zangu huwa nazifanyia hapa Bunju, ingawa ki makazi naishi mbezi Inn ila kikazi nafanyia Bunju. Sasa kama mtakumbuka kwenye simulizi ya mwisho nilisema ya kwamba,baada ya kuwa tumeuza lile duka la vipodozi ambalo tulikuwa tumefungua na rafiki yangu kipenzi Mtatiro (Kwa sasa anaishi nchini Uganda), tuliamua kugawana fedha kila mtu afe na chake, mimi niliamua kurudi zangu Tarime-Sirari, baada ya kukaa kule kuna ndugu yangu(Mtoto wa Baba yangu mkubwa) tuliwasiliana naye akaniambia nije Dar es salaam ili tufanye biashara ya uuzaji wa vyombo vya ndani kwasababu kwa wakati huo ilikuwa na pesa(Kwa maelezo yake).

Niliianza safari ya kuja Dar es salaam, sasa nilipofika Dar es salaam pale Ubungo(Kipindi stendi bado haijaamia mbezi), ile nimefika mida ya saa 5 usiku nikampigia simu mwenyeji wangu lakini majibu toka kwenye simu ni kwamba "Namba unayopiga kwasasa haipatikani,jaribu tena baadae", niliendelea kuipiga ile simu lakini majibu yalikuwa ni hayi hayo!.

Kwakuwa nilikuwa nimechoka,niliamua kumsikiliza moja ya watu ambao walikuwa wakinisumbua ili wabebe mzigo wa begi langu ili niwalipe posho, mpaka wakati huo nilikuwa makini sana kujilinda mimi binafsi pamoja na mzigo wangu, kilichofanya nikawa makini kupita kiasi ni stori ambazo mara zote nimekuwa nikizisikia kuhusu Jiji la Dar es salaam na vioja vyake.

Mimi " Mwanangu vipi!?"

Jamaa " Poa bro"

Mimi "Mbona mnavurugu,shida ni nini?"

Jamaa " Si huyu msenge,nimemwambia wewe ni wakwangu lakini hataki kusikia"

Mimi "Ok mnasemaje"

Jamaa "Bro we nipe begi mi nikubebee,achana na huyu muhuni atakuibia"

Mimi " Sasa wote mnang'ang'ania mzigo,nimpe nani na nimwache nani?"

Mimi "Sa sikia,begi langu nitalibeba mwenyewe,achaneni na mimi"

Baada ya kusikia rafudhi yangu na namna nilivyochukia nadhani waliamua kutii sheria bila shuruti,waliondoka wakiwa wananiangalia kwa uchungu na maumivu makali ya kukosa posho!.Kiukweli muda huo nilichokiongea ndicho nilichokuwa nikikimaanisha, kutokana na sifa mbaya za mkoa wa Dar es salaam nilikuwa nimesema yeyote ambaye angejitia kimbelembele kunikaba au kuniibia,basi siku hiyo ndiyo ingekuwa mwisho wa maisha yake!,Jeuri na kiburi cha kikurya vilinitia morali maradufu na niliwaona wale vijana wa pale stendi ni kama wanawake tu wasiokuwa na uwezo wa kunifanya chochote!.

Niliamua kujisogeza mpaka kwenye geti la kutoka nje,nilipotoka nje nilikuwa nikiendelea kushangaa pilika pilika namna zilivyokuwa za kutosha pale stendi,kiukweli sikuwahi kuona mji uliokuwa na pilika nyingi kama Dar es salaam,Mwanza nimekaa lakini hakukuwa na harakati za kutosha kama Dar es salaam.Nilichukua simu yangu nikawa nampigia tena mwenyeji wangu lakini simu yake ikawa haipatikani.Nilichukia sana kwasababu nakumbuka nilivyofika Singida alinipigia simu nikamwambia ya kwamba nimefika Singida na akawa amesema ikifika mida ya saa 2 usiku angekuwa amekuja pale stendi ili anisubiri nikifika tuondoke wote.

Kuna jamaa mmoja alikuwa kando ya geti la kutokea nje ya stendi pale Ubungo nilimsogelea nikawa namuuliza kuhusu Guest House yeyote iliyokuwa karibu ili niende nikalale na ikiwezekana asubuhi niendelee kumtafuta jamaa.

Jamaa "Sasa tutafanyaje ndugu!"

Aliendelea "Mwenyeji wako hajatokea?".

Mimi "Nimempigia simu lakini hapatikani!"

Jamaa "Duuuu mbona ni hatari!"

Aliendelea "Sasa sikia,wewe nyooka na hii barabara,unaona kwenye ile njia?"

Mimi "Ndiyo"

Jamaa "Hebu subiri"

Jamaa " Hassaniiiiiii"

Baada ya ya kuita hilo jina muhusika alifika


Jamaa "Hassani hebu nenda kampeleke huyu jamaa pale kwa Asteria,ukifika mwambie jamaa anataka chumba"

Aliendelea "Kaka nenda na jamaa atakupeleka kwenye Lodge ambayo kuna usalama na vyumba vipo vya kutosha,ila utamlipa maana kuna umbali"

Mimi "Hakuna tatizo"


Basi yule jamaa aliyeitwa Hassan akanichukua akanivusha barabara tukaikamata njia ya Ubungo Maziwa kuelekea kwenye hiyo lodge ambayo nimeambiwa kuna usalama na vyumba vya kutosha.Wakati tunakwenda na Bwana Hassan tulikuwa tunapiga stori za hapa na pale huku mikono yangu ikiwa bize imeng'ang'ania begi kwasababu ndilo lililokuwa na hela pamoja na nguo za kubadilisha,kiukweli nilikuwa nimesema endapo yeyote angejipendekeza kunikaba angejuta kuzaliwa.

Baada ya mwendo mrefu kidogo hatimaye tukawa tumefika kwenye Bar moja iliyokuwa inapiga mziki kwa sauti kubwa huku kukiwa na watu wengi.

Hassan " Nisubiri hapa nakuja"

Nilimsubiri Hassan pale nje baada ya kufika kwenye hiyo Bar na baada ya dakika 15 akawa amekuja kunichukua na kuongozana nae kuingia ndani.Tulipofika ndani ambako kulikuwa na kaunta,Hassan alinichukua tena kuelekea Uani ambako nilikuta kuna vyumba vingi ambavyo vilikuwa havipungui 10.

Sasa baada ya kufika pale Uani alikuja mwanamke mmoja mweusi mnene na ndiye aliyekuwa akiitwa Asteria,alimuita Hassan Pembeni wakawa wanaongea,sikufahamu kitu walichokuwa wanazungumza kwa wakati huo.Baada ya yale mazungumzo Hassan alirudi kwangu.


Hassan "Sasa bro,mimi nadhani nikuache wewe upumzike,niangalizie basi ustaarabu"

Mimi "Chumba changu cha kulala ni kipi?"

Hassan "Atakuonyesha Asteria,wala usijali kaka hapa ni nyumbani"

Baada ya maneno ya kutia moyo ya Hassan nikachomoa shilingi elfu 5 nikawa nimempatia kama posho ya kunipeleka hapo Guest.

Hassan "Aaah kaka hela gani hii?"

Mimi "Hela gani kivipi?"

Hasaan "Aaaah Kaka yaani nikutoe kule stendi na nimeacha shughuli zangu halafu unanipatia buku tano?,hebu ongeza ongeza kaka angalau kesho niamkie supu"


Sikutaka mambo mengi na yule Jamaa ikabidi nizame tena mfukoni nikatoa elfu 5 nyingine nikampatia,hivyo kufanya jumla kuwa elfu 10.

Baada ya jamaa kuondoka lile eneo nikamfuata yule demu aliyeitwa Asteria ili aje anionyeshe chumba niingie kulala kwasababu nilikuwa nimechoka.

Asteria "Kaka ina maana Hujaambiwa huu si muda wa kulala?"

Mimi "Si muda wa kulala?"

Mimi "Si muda wa kulala kivipi?"

Asteria "Kaka hapa huwa hatulazi watu ila tunakodisha!"

Aliendelea "Hivi vyumba vinakodishwa kwa dakika na masaa,labda usubiri mpaka saa 9 wateja wakipingua ndipo tutakukodishia ulale"

Kiukweli baada ya ile kauli niliishiwa nguvu ghafla,sasa baada ya kuniambia maneno yale yeye aliondoka akaenda kuendelea na shughuli zake akaniacha pale Uani nikiwa sijui cha kufanya,sasa ndipo nilikuja kugundua ya kwamba,vile vyumba vilikuwa vinatumika kwenye biashara ya short time(Biashara ya Ngono),sasa kumbe ile Bar niliyopelekwa,pale nje kulikuwa na wanawake wanaouza miili yao(Dada Poa) na vile vyumba vilitumika kwa shughuli ya short time.

Itaendelea.
Umekaribishwa mjini
 
Oa ndio uone mziki wake. Watu wengi hawajui Mana ya kuoa wao wanajua hisia ama wanaongozwa na hisia Mana muda huo unakuta Dickson amechachamaa kinyama. So uoe huko kwenu manchi Moto ndio Kuna Koo unazijua tokea babu wa babu yake.wewe unakutana na manka mjini umesoma umekuwa let say lecturer unamuona amewaka unazama. Cheki story ya Jackal Daniel yule mama anaona wivu mmewe kusomesha tu mtt wa Kaka yake. Yaani Bora usomeshe wa mchepuko haitamuuma Ila was ndugu yako inauma mno.

Unapooa unaleta mtu Kuja kumpanda kwenye Koo yako ,je atakubali kuota ama ndio mama yangu akitoka keisangora na like tope jekundu na magaga akiingia kwenye nyumba ya spanisha tiles atakuwa anaona kuwa anaichafua.


Kuna dokta mmoja anaitwa machela alioa mhaya mmoja Tena mziba wale walizopata first contact na wamisheni. Huyu jamaa bana siku mama yake alipokuja kumsalimia mke wake akamwambia kuwa huyu mama yako Ni mchafu mpeleke kwa rafiki yako alale na kweli akampeleka
Waziba n noma bora wamachame
 
Utajiri wa rafiki yangu ulivyofanya nikamuamini Shetani - 04.




Sasa muda ambao mke wa anko anafika pale nyumbani mimi nilikuwa nyuma ya nyumba ambapo kulikuwa kuna kama kibustani kidogo ndani yake kulikuwa kumepandwa miwa ambayo ilikuwa imekuwa mikubwa na hakukuwa na walaji,niliona nikate zangu muwa nikaa chini nikaanza kutafuna,kumbe aliingia chumbani anakolala yule mzee ambaye ni baba yake na akakuta amejisaidia kitandani na hakukuwa na mtu aliyemwangalia na kumjali,kwa mawazo yake yeye alidhani mimi nimemuona yule mzee na nikamuacha kama alivyo ili aendelee kuteseka!.
Akili na mawazo yake yalimtuma vibaya kwasababu sikuwa nimeingia mle chumbani tangia mchana,pia yule mzee alikuwaga kama na kakiburi fulani hivi ambako kalikuwa ka kijinga,anaweza kuwa amebanwa na haja kubwa wala asiite mtu yeyote,utakuta ameinyanyuka ameingia chooni na amechafua vibaya bila hata kuflashi.Inawezekana alifanya makusudi siku ile ili kunikomoa.

Kumbe muda huo Anko anapewa makavu laivu ilikuwa ni hiyo ishu na bahati mbaya sana Anko wangu alikuwaga akoromi kwa yule mwanamke bali hasira za kugombezwa na mkewe zilikuwaga zinaishia kwa wanae au mimi kwa wakati ule nipo kwake.

Muda huo ambao nipo zangu natafuna miwa sina habari,kumbe alimwambia yule mfanyakazi akaingia mle ndani akatoa yale mashuka akawa amemnyanyua mzee akampeleka bafuni mzee akajisafisha kisha akatandika shuka safi na kuweka mazingira ya chumba poa.

Mimi sikufahamu chochote kwasababu nilipomaliza kula miwa nikazunguka kule mbele ya nyumba ndipo nikakuta gari ya mke wa anko ikiwa imepaki nikajua atakuwa amerudi,sikutaka kuingia ndani kwasababu ilikuwa bado mapema,niliingia stoo nikachukua fagio la nje nikaanza kufagia pale nje.

Nilipomaliza niliingia ndani kuoga na kubadili nguo ili nije nikae sebuleni nitazame luninga,wakati naingia mle ndani nilikuta mzee amelala na kitandani kukiwa na shuka nyingine,sikufahamu kumbe dakika chache zilizopita hali ya mle ndani haikuwa nzuri,sasa huo usiku anko alivyorudi ndipo mkewe akamuamshia mtiti!.


Baada ya hayo malumbano Anko alivyorudi sebuleni alikuwa amebadirika na sikutaka kusema chochote mimi niliendelea kutazama luninga,chakula kilipotengwa alielekea kula na alipomaliza aliingia chumbani kwake!.Mkewe yeye sikuonana nae kwa siku hiyo.

Asubuhi kama kawaida wao waliondoka wakawa wamelekee kazini,pale nyumbani nikawa nimebaki mimi,yule binti wa kazi pamoja na mtoto mkubwa wa anko ambaye naye aliondoka ilipofika mida ya saa 3 asubuhi.Sasa baada ya yule mtoto wa Anko kuondoka,yule binti wa kazi alikuja kuniita nikanywe chai,muda huo nilikuwa nje napambana kungolea nyasi kwenye maua yaliyokuwa kando ya fensi.

Binti wa kazi " Hivi jana ulikuwa wapi?"

Mimi "Jana?,Jana saa ngapi?"

Binti wa kazi " Aliporudi Mama"

Mimi "Nilikuwa kule Bustanini"

Binti wa Kazi "Jana mama kagomba"

Mimi "Alikuwa anagomba kuhusu nini?"

Binti wa kazi "Aliporudi aliingia chumbani kwa babu akakuta babu kajinyea,alikuwa anakuulizia mi nikajua labda umetoka!"

Mimi "Alijenyea saa ngapi?,mbona mchana nilipotoka ndani alikuwa tu vizuri"

Binti wa kazi "Alikusema maneno mabaya sana,we acha tu"

Mimi "Mimi siyo mjinga nimuone huyo mzee akiwa anashida niache kumsaidia,mbona siku zote namuosha na kumpeleka chooni na mpira nambadilishia!"

Mimi "Jana nilikuwa bustanini na sikutoka nje kabisa"

Mimi "Kwani kabla sijaja hapa nani alikuwa akimuangalia mzee?"

Binti wa kazi "Nani zaidi yangu?wanae tu wala hawana time na babu yao"

Baada ya mazungumzo ya muda kadhaa nilinoti kitu kwa yule dada wa kazi ambacho hakutaka kabisa kuniambia,kwa kifupi yule mke wa anko inaonekana alitoa shiti nyingi dhidi yangu,niliamua kutulia na kutafakari.
Sikwenda kwa Anko uenda kwakusema nimepigwa na maisha ili anifadhili la hasha,nilienda pale kwasababu wakati nafika mjini mwenyeji wangu alikuwa hapatikani,sasa kuna muda nilikuwa nashangaa wanavyonichukulia ni kana kwamba nimepigwa na maisha!.

Baada ya kupata kifungua kinywa niliamua nimsubiri Anko akitoka kazini ile jioni nimuage na kesho yake nisepe niwaache wapambane na matatizo yao na roho zao mbaya.Kweli,usiku ule kabla ya kula tukiwa pale sebuleni tukiangalia taarifa ya habari,nilimwambia kesho mimi nitaondoka.

Anko Nico " Utaondoka kwenda wapi?"

Mimi "Nitaenda kwa yule mtoto wa baba mkubwa"

Anko Nico " sawa siye tupo"

Baada ya hayo mazungumzo niliona kabisa nilikuwa sitakiwi.Ukiachilia Anko,lakini mkewe na watoto wa Anko walikuwa ni watu ambao hawana time na mtu,tangia nimefika hapo hawakuwahi hata kusema na mimi wala kujua hali ya maisha ya shangazi yao,walikuwa ni watu ambao hawakuwa na muda kabisa,pengine uzungu uliwaharibu au walilithi tabia za kwao mama yao.

Kesho yake nilimuaga yule mzee pamoja na yule binti wa kazi nikaondoka zangu,nilipotoka nje nilitembea hadi kituo cha daladala nikapanda kuelekea tegeta.

Kwakuwa nilikuwa nimeshawasiliana na Kileri akawa ameniambia anakaa Kivule na hivyo ilipaswa nipande magari yatakayonifikisha ubungo stendi ya daladala na nikifika hapo nipande za gongo la mboto nikashukie banana kisha nichukue za kivule.

Namshukuru Mungu nikawa nimefika na jamaa akaja kunichukua tukaelekea kwake.Nilipofika kwa jamaa nilikuta anakaa kwenye nyumba ambayo bado haijaisha na nilikuta mafundi wakiwa wanaweka vigae kwenye vyumba baadhi.


Kileri "Karibu wa kwetu,hapa mimi ndipo naishi na familia yangu"

Mimi "Hongera kaka umejitahidi"

Kileri "Kawaida tu,naipeleka mdogo mdogo mpaka itaisha,mjini hapa ukiwa na kwako unaepuka usumbufu wa kodi"


Baada ya mazungumzo ya hapa na pale,jamaa akawa ameniambia kesho yake tungeenda Tandika ambako alidai ndiko anakofanyia biashara ili nikajionee namna biashara ilivyo shamiri.

Ilipofika asubuhi tuliondoka kuelekea huko Tandika kama alivyokuwa ameniambia.Tulipofika hapo Tandika kuna duka moja la vyombo tuliingia lakini kuna kitu kikanishangaza.


Itaendelea......
Milioni 9 yako mhuni kamalizia tiles [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Hii story imenikumbusha mara ya kwanza mimi kufika dar

kUna kaka angu mtoto wa baba mkubwa aliwah kuja kuishi kwetu kijijin mikoani alikaa muda mrefu sana na pale nyumbani kwetu walimtunza vizuri sana,nakumbuka hadi mama angu alikuwa anamfulia nguo

Sasa kuna kipindi nilkuwa nipo chuo morogoro,nilkuwa nikipata likizo narudi nyumbani kanda ya ziwa,sasa wakati fulani huyo kaka akawa ananipigia simu mara kwa mara na kunisihi siku nyingine nikiwa na likizo niende kwao dar badala ya kwenda huko mbali kanda ya ziwa

nIlipopata likizo nikamtaarifu kuwa siku fulani nitakuja,siku napanda gari nikiwa msamvu nikampigia akaahidi kunipokea,safari ikaanza,nimefika mlandizi napiga simu haipatikani,piga sana haipatikan,bahat nzuri kuna jamaa yangu nilisoma nae o level alikuwa nae yupo dar nae alikuwa ananiomba sana niende dar siku nikipata nafasi,kwahyo kwenda dar nilipata msukumo kutokana na watu wawili

Nilivyokaribia kabisa kufika bila kufanikiwa kumpata huyo kaka angu ikabidi nimpigie dada angu wakati huo alikuwa ni mwanachuo ifm ila akawa anaishi kigamboni,jamaa yangu niliesoma nae olevel yeye kila wakati alikuwa ananipigia simu kuniuliza nimefika wapi,kwahyo dada angu ikabid aje ubungo kunipokea pia jamaa yangu pia alikuwepo,jamaa yangu alikuwa akiishi tabata kimanga na kwa baba mkubwa ni tabata shule,kwavile nilipata mwenyeji wa tabata ikabid dada awahi chuo akaniacha na jamaa yangu ila ikabidi ampigie mama mkubwa kumjulisha ujio wangu pia akamwambia mbona simu ya kaka angu haipatikani,kaka angu kuambiwa ndo akaiweka simu hewani

Tumetoka ubungo tumefika tabata shule tukashuka tukategemea kaka tutamkuta kituoni lakin hatukumkuta ikabid tuanze kumpigia simu ilituchukua kama dk 30 kumsubiri,wakat kutoka kituo cha daladala mpaka nyumban hata sio mbali,basi alivyofika tukaongozana nae mpaka nyumban,yeye mbele mimi na jamaa yangu nyuma na begi letu.

Nilikaa pale kwa baba mkubwa kwa wiki 3 lakin niliona ni kama nimekaa miezi 6
Ilikuwaje
 
Back
Top Bottom