Zanzibar kuna Chumbe mbili.... moja ni kisiwa kabla ya kufika Unguja na Chumbe ya pili ipo karibu na Mbweni katika barabara ya kwenda Entebbe.
Master naona kashindwa kabisa kuelezea ni Chumbe ipi alikwenda! Kama ni Chumbe ya barabara ya kwenda Entebbe, hiyo haina msitu na bahari ipo mbali kidogo aidha eneo lote toka Chumbe hadi ufukweni kumejengwa, hivyo basi hakuna msitu wa aina ya simulizi ilivyosema.
Kwa upande wa kisiwa cha Chumbe, ni kisiwa kisichokaliwa na wenyeji, zamani wavuvi walipita hapo baada ya shughuli zao za uvuvi na ndio sababu kuna msikiti kisiwani hapo. Zaidi ya msikiti kuna mnara wa kuongezea meli na vibanda vya hoteli ya kitalii. Ni kisiwa ambacho kipo chini ya uangalizi na kinasimamiwa na kampuni binafsi!
Sijui Master alikwenda Chumbe ipi! Kama kuna mtu anajua ni vema akatufahamisha.