Utakaa barabarani mpaka ufikishe miaka 90?

Utakaa barabarani mpaka ufikishe miaka 90?

Lack of exposure ni tatizo kubwa kwa Watanzania. Niliangalia documentary ya Mghana alikwenda kutafuta maisha Ulaya, alizamia meli akaishia Italy. Alipata kazi kwenye mashamba ya nyanya.

Alibeba idea ile ya kilimo, alipotoboa alikwenda Ujerumani, alinunua matrekta na lorry. Amerudi Ghana sasa hivi anafanya commercial farming ya nyanya.
Hii ninaiona hata kwangu inavyonitafuna kidogokidogo. Hatuna ubunifu kabisa. Tazama siku hizi nyumba zote zikijengwa eti zinawekwa fremu. Mtaa mzima ni fremu tupu. Yani kuchungulia fursa tofauti imekuwa changamoto sana.

Lakini, pamoja na juhudi binafsi kuhitajika, serikali pia ina nafasi katika hili,kuanzia "elimu hai" mpaka kujenga mifumo mizuri ya kiutawala na uchumi.
 
Kwahiyo solution ni kupoteza nguvu za ujana wako pembezoni mwa barabara? Hahaha
Kwao ni solution maana hawana haja na career kwa kazi wanazofanya, wametoka maisha ya jamii yao ya Bora liende hivyo vilimo vya kisasa na biashara rasimi nizawatu wanaojiweka kwenye mfumo wa kuwa na career zinazotambulika na nini wanafanya Ili kujiingizia kipato ila hao wakukaa barabarani wao walichagua kuishi nje ya mfumo wa rasimi na career mpaka kufa.
 
Hii ninaiona hata kwangu inavyonitafuna kidogokidogo. Hatuna ubunifu kabisa. Tazama siku hizi nyumba zote zikijengwa eti zinawekwa fremu. Mtaa mzima ni fremu tupu. Yani kuchungulia fursa tofauti imekuwa changamoto sana.

Lakini, pamoja na juhudi binafsi kuhitajika, serikali pia ina nafasi katika hili,kuanzia "elimu hai" mpaka kujenga mifumo mizuri ya kiutawala na uchumi.
Uchoyo pia unatunyima nafasi, Wazungu wanakaribisha vijana wenye mawazo mapya na pesa ya mitaji kuanzia €250,000 wanapewa visa katika nchi zao.

Pia wanaomaliza na first class wanalengwa kuwa mameneja wa makampuni.
 
Uchoyo pia unatunyima nafasi, Wazungu wanakaribisha vijana wenye mawazo mapya na pesa ya mitaji kuanzia €250,000 wanapewa visa katika nchi zao.

Pia wanaomaliza na first class wanalengwa kuwa mameneja wa makampuni.
Hhaha! Sisi mpaka tubadilike kifikra aisee. Tuwaoga kishenzi.Na uoga unaletwa na huu ujinga tulionao.
 
Kwao ni solution maana hawana haja na career kwa kazi wanazofanya, wametoka maisha ya jamii yao ya Bora liende hivyo vilimo vya kisasa na biashara rasimi nizawatu wanaojiweka kwenye mfumo wa kuwa na career zinazotambulika na nini wanafanya Ili kujiingizia kipato ila hao wakukaa barabarani wao walichagua kuishi nje ya mfumo wa rasimi na career mpaka kufa.
Maamuzi yao yanafanya miundombinu iliyojengwa kwa kodi zetu kuharibika, na watu kushindwa kutumia hiyo miundombinu ipasavyo. Sehemu zile ni za watembea kwa miguu ila hawaruhusiwi kupita kwenye maeneo yao waliopangiwa kwasababu ya watu ambao ni wavivu.
 
Hii ninaiona hata kwangu inavyonitafuna kidogokidogo. Hatuna ubunifu kabisa. Tazama siku hizi nyumba zote zikijengwa eti zinawekwa fremu. Mtaa mzima ni fremu tupu. Yani kuchungulia fursa tofauti imekuwa changamoto sana.

Lakini, pamoja na juhudi binafsi kuhitajika, serikali pia ina nafasi katika hili,kuanzia "elimu hai" mpaka kujenga mifumo mizuri ya kiutawala na uchumi.
We acha tu watu hawataki kufikiri zaidi na kupanua mawazo.
Eti kuna watu kwenye huu uzi wananiomba fursa ili watoke barabarani. Mhmm ukisikia maajabu ya dunia utayakuta Tanzania.
 
Nyerere, pamoja na matatizo yake yote alikomboa maskini kwa njia ya redistribution of resources. (ingawa angefanya kwa njia nyingine) Hakuwa na watendaji wazuri na viongozi wenzake wakati ule hawakumulewa (ni ngumu sana kumuelewa idealist na mtu mwenye vision ya miaka zaidi ya 100 ijayo).

Ninachotaka kusema kwamba yasingefanyika yale yaliyofanyika miaka hio, leo hii mwenye nacho angebaki nacho na asiyenacho asingekuwa na namna yoyote yakufanya ili na yeye awe nacho.

Pamoja na matatizo yote tuliyonayo Watanzania bado tuna uwezo wa kutafuta na kupata (social mobility). Hii ni kwa sababu rasilimali kama vile ardhi bado vipo mikononi mwa wananchi. Sisi siyo kama Kenya, Nigeria au mataifa yaliyoendelea ambapo wenye ardhi ni watu wachache sana na wanaobakia wanateseka na inabidi watafute njia nyingine ya kuingiza kipato. Ardhi ni ya thamani sana hatujui tu.

Huku Tanzania watu wengi wana ardhi za kurithi za mababu zao. Sipendi kujumlisha watu kwenye category moja lakini ukweli lazima usemwe tu. Vijana wengi wa Kitanzania na Watanzania kwa ujumla ni wavivu. Yaani wewe mtu na akili zako na nguvu zako unaondoka shambani unafuata mkumbo wa kwenda mjini eti kwa kisingizio cha kutafuta kipato. Unafika unaenda kukalisha makalio yako kibandani kwenye njia ya wapita miguu unauza dodoki. Eti na wewe unatafuta riziki. Huwezi hata kujiuliza hii shughuli ninayofanya hapa inasaidia vipi katika kuimarisha uchumi wa nchi.

Unamuacha mzee kijijini alime, wewe kijana mwenye nguvu unaenda kujikalisha mjini. Unashindwa kweli kufanya kilimo? Hapa najua majibu yenu ni kwamba kilimo ni kigumu blah blah blah nyingi. Ni hivi hakuna kitu kirahisi na kama unataka njia za mkato utaishia pabaya tu. Mpe hiyo ardhi uliyoikimbia Mnigeria au Mkenya akuoneshe. Au unyanganywe ndio utaelewa umuhimu wake?

Haya basi umelazimisha kuhamia mjini. Wakati wa Kikwete masoko ya machinga yalijengwa yakutosha ili wafanyabiashara wadogo wafanye kazi. Waliyakataa. Yaani mtu unakimbia sehemu ambayo ni rasmi ambapo ungetambulika kwenye mifumo yote ya nchi? Upo tayari kufanya biashara ambayo hata ukiumwa huwezi kuingiza kipato? Mnajua umuhimu wa kutambulika? Mnafahamu kwamba mngeweza kujikusanya na kupata mikopo ya vijana isiyo na riba halmashauri na kwenye baadhi ya mabenki?

Unakaa barabarani huna ujuzi wowote, hata kwenda VETA? Ukiingiza bando la mtandaoni ni kushinda kwenye udaku na kubeti hamna unachojifunza ili kuboresha maisha yako. Unaoa na kuolewa na unapata watoto. Unategemea kuwalisha kwa biashara za barabarani? Ukiumwa au mkitimuliwa inakuwaje? Ukizeeka utabaki kulalamika na kutamani urudishe miaka nyuma

Narudia tena hakuna kitu kirahisi lazima ujitume kimwili na kiakili. Kuwepo kwenye mifumo rasmi ni muhimu sana. Leo na kesho ukiumwa au ukifa bado biashara yako itaendelea. Watoto wako watarithi kibanda chenye uhakika. Mnafikiri familia zenye pesa (naongelea old money siyo hawa new money wanaorudi kwenye umasikini baada ya kizazi kimoja) muda wote wanapesa tu hawaishiwi? Wanaishiwa, lakini kwa sababu wanatambulika kwenye mifumo wana kopesheka na wana bima za kutosha hawawezi kuwa masikini. Uliyejikalisha hapo barabarani una hata bima ya afya?

Ninachosema hapa hakiwezi kutatua tatizo la umaskini katika jamii, umasikini ni mfumo na kinachohitajika ni jitihada za kutosha zikiongozwa na serikali kulitatua tatizo hili.

Ninachosema ni hatua mtu binafsi anazoweza kuchukua ili kuhakikisha anaboresha maisha yake yeye na ya watoto wake. Mifumo inafanya tajiri aendelee kuwa tajiri na masikini aendelee kuwa masikini. Hakikisha unakuwa katika mfumo rasmi ili uondokane na hili janga la umasikini. Tupo kwenye nchi ambayo bado matabaka kwenye jamii hayajakomaa. Huko baadaye yakikomaa utajutia kweli ujana wako na kwa nini hukutaka kuhangaika.

Na serikali nayo imelala sijui imekufa. Mipango miji ilitenga maeneo ya huduma za jamii ikiwemo masoko madogo kwenye maeneo ya makazi ya watu. Hayo maeneo yako wapi? Mliwauzia watu binafsi au?
Mwenye masikio na asikie.
Kwa maelezo yako inaonekana umekulia mjini dada,tuliokulia kijijini tunaelewa urahisi na ugumu wa maisha ya kijijini.
Yes,kula kijijini kama unajituma utakula maana unalima mwenyewe.kasheshe inakuja pale unapotakiwa kuvaa,kupelekea watoto shule.unajikuta mazao ya kuuza unayo ila bei mgogoro,ref.gunia la mahindi elfu 30-50

Kwenda hospitali endapo utaumwa,hakuna anayekubali kupokea mazao akupe dawa,ukienda kuuza unakutana na mkono wa walanguziref.bkb mkungu mkubwa wa ndizi ijulikanayo kama mtwishe sh.elfu tano na wanunuzi hakuna na bado zinaiva na kuozaTukitaka vijana wake vijijini tuboreshe masoko na kujenga viwanda vya kuyaongezea mazao thamani hapo tutavuka
 
awajaamua kua serious na kuchakata ubongo..wengi hawapendi kujichosha wanapenda mteremko kitu ambacho hakiwezi wafikisha popote
 
Back
Top Bottom