Utalii: Simba 17 wahamishiwa katika hifadhi ya taifa ya Burigi - Chato

Utalii: Simba 17 wahamishiwa katika hifadhi ya taifa ya Burigi - Chato

Mlima Kilimanjaro unahamishwa lini ?

Kati ya hifadhi zote Kilimanjaro ndio inaingiza fedha nyingi ikifuatiwa na Serengeti.

Serengeti inatembelewa na watalii wengi kuliko hifadhi zote lakini kimapato kilimanjaro inaongoza.

Kwanini Kilimanjaro inaongoza kimapato wakati inazidiwa idadi ya wageni wanaotembelea Serengeti?.

Ipo hivi mtalii anayetembelea Serengeti anaweza kutumia siku moja au mbili baada ya hapo ataondoka either kwa gari au ndege.Mtalii anayepanda mlima atatumia siku 7 hakuna usafiri wa gari ni miguu so siku atakazo tumia hifadhini ni nyingi na hizo siku maana yake ni fedha nyingi zaidi.

Nilikuwa namshangaa sana tena sana Waziri wa Utalii alipokuja na wazo la kutumia magari ya nyaya (sijui kama ni lugha sahihi) maana yake mtalii atatumia siku chache na ajira ya wabeba mizigo itaondoka.
 
Jumla ya Simba 17 wamehamishiwa katika hifadhi ya taifa ya Burigi huko Chato ikiwa ni hatua ya kuimarisha vivutio vya utalii Kanda ya Magharibi.

Simba hao wamepokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kagera Brigedia Jenerali Gaguti ambaye amewataka wananchi wa maeneo hayo wawe wakarimu wakati wa kuwapokea na kuwahudumia watalii.

Source: ITV habari!
p
 
Kati ya hifadhi zote Kilimanjaro ndio inaingiza fedha nyingi ikifuatiwa na Serengeti.

Serengeti inatembelewa na watalii wengi kuliko hifadhi zote lakini kimapato kilimanjaro inaongoza.

Kwanini Kilimanjaro inaongoza kimapato wakati inazidiwa idadi ya wageni wanaotembelea Serengeti?.

Ipo hivi mtalii anayetembelea Serengeti anaweza kutumia siku moja au mbili baada ya hapo ataondoka either kwa gari au ndege.Mtalii anayepanda mlima atatumia siku 7 hakuna usafiri wa gari ni miguu so siku atakazo tumia hifadhini ni nyingi na hizo siku maana yake ni fedha nyingi zaidi.

Nilikuwa namshangaa sana tena sana Waziri wa Utalii alipokuja na wazo la kutumia magari ya nyaya (sijui kama ni lugha sahihi) maana yake mtalii atatumia siku chache na ajira ya wabeba mizigo itaondoka.
Wazo la waziri lilikuwa bovu na nilipingana nalo hata sasa sikubaliani nalo.
 
Na huko watawamaliza Sokwe wote wa Mlima virunga!

Simba Hawaii kwenye Misitu minene kama ya Biharamulo, Gombe au Virunga. Wanaishi sehemu zenye mvua chache, nyasi ndefu na vichaka vya hapa na pale.

Sasa Burigi Chato itakuwaje? ....Mungu tupe Maarifa zaidi ya Matamanio ya mioyo yetu.
Nafikiri hata swala, nyumbu na nyati hawawezi kuishi huko ile mbuga ni ya sokwe, tumbili, twiga, nyani, ndege, vipepeo nk.
 
Na lengo hasa ni wahamie Rwanda ili ale commission yake huko mbele ya safari. Enzi za JK na kina Nyalandu wao walipeleka wanyama uarabuni, huyu anawapeleka Rwanda kwa mahesabu makali.

Wanyama hao wako njiani kwenda ulaya na Uarabuni kupitia Rwanda ambako Watanzania hamuwezi kuhoji.

Hiyo ni hesabu kali ya kuiba wanyama hai.
 
Trust me baada ya miezi sita nusu yake watahamia Rwanda

Jr[emoji769]
Hao Simba ni wengi sana kwa idadi najua wanyama Wala majani watapunguzwa kwa kasi sana kabla ya hao Simba hawajatoroka kwenda eneo litakalo wapa fever katika uwindaji,wanahitaji eneo la wazi kwa ajili ya kuwinda,vichaka vifupi na nyasi ndefu,pamoja na mawe makubwa yenye mapango kwa ajili ya kupumzika,kufanya mazalia na kuhifadhia vitoto pindi vinapozaliwa.
Hao Simba Kama wamechukuliwa Ngorongoro au manyara wataweza kukaa,ila Kama Ni Serengeti na Tarangire Ni ngumu
 
Siyo kweli, kama lugha zinazoongewa sehemu ilipo Chato-Burigi zina jina kwa mnyama simba, basi mnyama huyo aliwahi kuishi huko - "Entare"!
Hao Simba walienda wapi Kama walikuwepo?.
Fatilua,huwenda walihama au kutoroka na kwenda sehemu zngine ama walikufa Kama eneo halikuwa na mazngira mazuri ya uwindaji.
 
Acha uchawi bwashee!
Sio uchawi ni ukweli, angalia maeneo yenye idadi kubwa ya simba nchini, ni uwanda wa wazi. Hata uwabebe uwapeleke wapi, kama wako huru wataondoka tu na kurudi savannah, wakiwa njiani wataua mifugo ya watu pengine pamoja na watu.
 
Back
Top Bottom