Utalii: Simba 17 wahamishiwa katika hifadhi ya taifa ya Burigi - Chato

Uzalendo kwanza

Chato nayo ni sehemu ya jamhuri
 
Hiyo hifadhi siku zote ilikuwa mkoa wa Kagera. Imekuwaje Chato, Mkoa wa Geita?
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Siyo Barabara zilizowamaliza simba. Ni upungufu wa wanyama ambao ndio chakula cha simba.
Sishabikii mbuga ila natoa taarifa kuwa Simba walikuwepo kabla ya barabara za Muleba Biharamulo na Muleba Chato kuwekwa lami. Wanaoifahamu barabara ya Muleba Biharamulo kuna mlima unaitwa mlima wa Simba.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Simba walikuwepo. Ile mbuga siyo mpya bali ilikuwa imepungukiwa wanyama kwa sababu ya uwindaji haramu, uvamizi wa wafugaji kutoka Rwanda na mabadiliko ya mazingira.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hiyo hifadhi siku zote ilikuwa mkoa wa Kagera. Imekuwaje Chato, Mkoa wa Geita?

Sent using Jamii Forums mobile app

Hata mimi huwa najiuliza swali hilo nakosa jibu! Burigi kwa mfano ni part and parcel ya mkoa wa Kagera tangu ukoloni wa Wajerumani - miaka kama mitatu iliyo pita niliona RPC wa Mkoa wa Kagera na Mkuu wa Mkoa wa Kagera wakisimamia uondoshwaji wa kundi kubwa la ng'ombe wa Rwanda kwenye misitu ya Mkoa wa Kagera pamoja na ziwa Burigi, sikuwahi kusikia Mkoa wa Geita ukihusishwa katka operation hiyo, cha ajabu siku hizi Burigi inahusishwa sana sana na Chato sijui mantiki yake ni nini? Kwa nini isiwe Muleba-Burigi au Biharamulo-Burigi?
 
Nilichogundua watu wengi hamuielewi jiographia ya Burigi vizuri. Burigi sio kile kipande katikati ya Biharamulo na Muleba na Chato. Burigi imeizunguka Wilaya ya Biharamulo inaambaa mpaka kule karibu na Rusumo na inaingia hadi Kimisi.

Hoja ya misitu minene na kwamba hakuna plains ni dhaifu na inaongelewa na watu wasioijua hifadhi bali wapita njia ya Biharamulo - Muleba. Kimisi game reserve haina misitu ni savannah na ni sehemu ya Burigi National park. Ziwa Burigi lenyewe linaonekana kwa urahisi ukipita njia ya Kimisi Benaco - Karagwe. Chato yenyewe haina msitu wowote wa kutisha. Msitu pekee na ambao watu humu wanajua ndio Burigi ni poli la Kasindaga.

Kwa wasiojua mpaka wa Akagera National Park (Rwanda) na Burigi Chato ni mto Kagera. Kama Simba wanaweza kuishi Akagera tunachotakiwa ni study aina ya Simba waliopo kule ndio hao hao waletwe upande wa Burigi.

Hata zamani kabla ya wafugaji kuvamia hifadhi, Burigi ilikuwa na wanyama wengi wakiwamo Simba (Simba hawa walikuwa wembamba warefu), Swala, Twiga etc. Kikichowaondoa na ufugaji na uwindaji haramu.
 
Hapo mimi natofautiana na wewe na kumuunga mkono Waziri.

Kuna aina ya Watalii wengi wanaotaka kujua kama eneo husika kuna miundo mbinu inayorahisisha mambo kabla ya kutumia fedha zao kuja huku..iwapo wanaona ishu ni complicated wanachagua kwenda kwingine.
 
Watanzania bwana soma hapo ili ujue simba wapo huko long time ago mnabishana tu Bure Biharamulo Game Reserve


Ni kweli, ndio uwanda huo huo wa Kimisi kwenda Karagwe hauna tofauti na Serengeti na Ngorongoro ila misitu ya Chato, Biharamulo na Kasindaga ni vigumu Simba kuishi kwenye enviroment zenye misitu minene.
 

 
Hawajui chochote ndg Sina imani Kama haya maamzi yamefanywa na wahifadhi nahisi watakuwa wanasiasa.
Kama wataweza kuishi Hilo eneo ambalo Lina mistu mikubwa Basi hata sokwe wataweza kuishi Serengeti au Tarangire
samahani twende taratibu hapa kuna kitu nataka nijifunze. Kabla ya mnyama kuhamishwa kuna approach zipi zinafanyika ili kuhakikisha au kujiridhisha mahitaji ya mnhama huyu ndani ya ikolojia x ya hifadhi fulani ni sawa na mahitaji yaleyale ya ikolojia y ndani ya hifadhi fulani?
 
Ni vitu vingi,ikiwa Ni pamoja na...

Hali ya hewa joto na upatikanaji was mvua Kama vinaendana x na y.

Uoto wa asili,savanna au equatorial etc Kama vinafanaa na x na y.

Magonjwa ya wanyama wa x na y.
Ndo maana nkasema Kama Ni Simba wa manyara au Ngorongoro wataweza kuishi tofauti na Happ watatoroka maana Mara nyingi Simba huwa wajeuri
 
You are talking of something else. The link has a lot of nonsense information. Biharamulo Game reserve is just part of the larger Burigi Chato.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…