Utamkumbuka Edward Lowassa kwa mambo gani?

Utamkumbuka Edward Lowassa kwa mambo gani?

Nakumbuka jinsi Msukuma alivyomsema eti anapupu wakati anatembea.

Wanasiasa ni watu wa hovyo sana.
 
Habari Wadau,

Leo Februari 10, 2024 Makamu wa Rais Dkt. Mpango ametangaza kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania na Mgombea Urais wa CHADEMA mwaka 2015 Edward Ngoyai Lowasa

Soma: Breaking News: - Edward Lowassa (Waziri Mkuu Mstaafu na Mgombea Urais wa CHADEMA 2015) afariki dunia

Katika mwaka enzi za uhai wake Mzee alipata kuwa na ushawishi Mkubwa nchini kiwango cha kuweza kujaza mikutano katika Uchaguzi wa Urais mwaka 2015.

Binafsi ntamkumbuka sana kwa uthubutu wake wa kuweza kujiuzulu nafasi ya Uwaziri Mkuu alipohusishwa na tuhuma za ufisadi.

Wewe utamkumbuka Lowassa kwa mambo gani?
Tushawahi cheza mpira wa miguu team magu vs team lowasa 2015 nilikua team lowasa
 
Kusambaza Mtandao wa Maji Mikoa Ya shinyanga Tabora na Mwanza sasa hivi hawana shida ya maji..
Kuanzisha shule za kata Nchi nzima kwa sasa 85-89% ya Vijana wote wamefika Form four..
NA MENGI MAZURI KAFANYA SANA..
 
Hatotokea kiongozi yeyote tanzania akaachia nafasi kubwa kama hiyo kama lowasa alivyo fanya.

Aliwajibika kwa makosa ambayo hakufanya alionesha usomi na uelewa wa kiwango cha juu.

Nilimpigia kampeni ati nilitembea kata zote 19 kwa miguu kuwaelimisha wananchi kuhusu kwa nini aliachia cheo cha waziri mkuu.

Nyie zile pilikapilika za 2015 sio za kusahau.

1.Team lowassa
2. Team ulipo tupo

Lowassaaaaaaaa mabadiliko, mabadilikooooooooooooo lowasa.

Roho nyeupe, ngozi nyeupe, nywele nyeupe mapema asubuhi mpaka Ikulu.🤣

Bibi yangu mimi ilikuwa ni lazima apige kura sasa yeye alicho kuwa akijua ni ccm na nyerere,

Bibi yeye anasema atampigia kura wa chama cha nyerere, sasa tukachukuwa picha ya lowasa tukamuekeza kuwa lowasa ni mtoto wa nyerere, alivyoona zile nywele nyeupe akase, maaaaaaaawe anamfanana baba yake nyerere ona hizo nywele kweli nampigia kura🤣

Siku ya kupiga kura mapema vijana walishamfata na pikipiki mpaka kituo cha kupigia kura, si hajui kusoma, alivyouliza bibi unampigia kura nani akasema wa chama cha nyerere🤣

Wakamuuliza unamjua picha yake? , si alisha oneshwa picha ya lowasa na nywele zake akawaonesha huyu hapa mwenye nywele nyeupe🤣 imeisha hiyo.
RIP BIBI YANGU
RIP LOWASSA
Very interesting. Lini ulihamia kwa Magufuli?
 
Kampeni zake 2015 zilikua zinachekesha sana eti mara masheikh wamfuate mara maaskofu na wachungaji eti wanamtaka awe rais, kuna siku alipanda daladala la kwenda buguruni kaka kiti cha dirishanu.
 
Tunakumbushana tu maneno ya mwendazake Lowasa alipotangaza Kujiuzulu na Bunge zima kushikwa na Mfadhaiko

Mlale Unono 😀😀🔥
 
Hatotokea kiongozi yeyote tanzania akaachia nafasi kubwa kama hiyo kama lowasa alivyo fanya.

Aliwajibika kwa makosa ambayo hakufanya alionesha usomi na uelewa wa kiwango cha juu.

Nilimpigia kampeni ati nilitembea kata zote 19 kwa miguu kuwaelimisha wananchi kuhusu kwa nini aliachia cheo cha waziri mkuu.

Nyie zile pilikapilika za 2015 sio za kusahau.

1.Team lowassa
2. Team ulipo tupo

Lowassaaaaaaaa mabadiliko, mabadilikooooooooooooo lowasa.

Roho nyeupe, ngozi nyeupe, nywele nyeupe mapema asubuhi mpaka Ikulu.[emoji1787]

Bibi yangu mimi ilikuwa ni lazima apige kura sasa yeye alicho kuwa akijua ni ccm na nyerere,

Bibi yeye anasema atampigia kura wa chama cha nyerere, sasa tukachukuwa picha ya lowasa tukamuekeza kuwa lowasa ni mtoto wa nyerere, alivyoona zile nywele nyeupe akase, maaaaaaaawe anamfanana baba yake nyerere ona hizo nywele kweli nampigia kura[emoji1787]

Siku ya kupiga kura mapema vijana walishamfata na pikipiki mpaka kituo cha kupigia kura, si hajui kusoma, alivyouliza bibi unampigia kura nani akasema wa chama cha nyerere[emoji1787]

Wakamuuliza unamjua picha yake? , si alisha oneshwa picha ya lowasa na nywele zake akawaonesha huyu hapa mwenye nywele nyeupe[emoji1787] imeisha hiyo.
RIP BIBI YANGU
RIP LOWASSA
Kiukweli Lowassa alikuwa kiongozi aliyeandaliwa kama alivyosema Ryoba
 
Hatotokea kiongozi yeyote tanzania akaachia nafasi kubwa kama hiyo kama lowasa alivyo fanya.

Aliwajibika kwa makosa ambayo hakufanya alionesha usomi na uelewa wa kiwango cha juu.

Nilimpigia kampeni ati nilitembea kata zote 19 kwa miguu kuwaelimisha wananchi kuhusu kwa nini aliachia cheo cha waziri mkuu.

Nyie zile pilikapilika za 2015 sio za kusahau.

1.Team lowassa
2. Team ulipo tupo

Lowassaaaaaaaa mabadiliko, mabadilikooooooooooooo lowasa.

Roho nyeupe, ngozi nyeupe, nywele nyeupe mapema asubuhi mpaka Ikulu.🤣

Bibi yangu mimi ilikuwa ni lazima apige kura sasa yeye alicho kuwa akijua ni ccm na nyerere,

Bibi yeye anasema atampigia kura wa chama cha nyerere, sasa tukachukuwa picha ya lowasa tukamuekeza kuwa lowasa ni mtoto wa nyerere, alivyoona zile nywele nyeupe akase, maaaaaaaawe anamfanana baba yake nyerere ona hizo nywele kweli nampigia kura🤣

Siku ya kupiga kura mapema vijana walishamfata na pikipiki mpaka kituo cha kupigia kura, si hajui kusoma, alivyouliza bibi unampigia kura nani akasema wa chama cha nyerere🤣

Wakamuuliza unamjua picha yake? , si alisha oneshwa picha ya lowasa na nywele zake akawaonesha huyu hapa mwenye nywele nyeupe🤣 imeisha hiyo.
RIP BIBI YANGU
RIP LOWASSA
Aliacha kwasababu hakuna anachopoteza wadhifa wa waziri mkuu mstaafu kuhudumiwa hadi mwisho uko palepale na pesa kapiga
 
Lowasa alikuwa ni kati ya viongozi waliopata bahati ya kuzaliwa kizazi ambacho wale wachache walioweza kupata elimu kipindi hicho na kuichagua siasa kama sehemu yao ya maisha, wana maisha mazuri sana.
Kwenye siasa kuna kuanguka, kuna kusalitiana kwenye makubaliano, kuna kuogopana katika upana wa maendeleo binafsi, ambapo nashuhudia viongozi wengi wana muelezea Lowasa alivyoanguka kwenye mbio za urais 2015, alivyojiuzulu Uwaziri Mkuu, kama anguko la kisiasa la asha.....matukio hayo mawili ni matukio makubwa katika siasa za Afrika ambapo ni mfano wa kuigwa......bara letu la Afrika kwa ubinafsi na uroho wa viongozi wafia tumbo ni ngumu kiongozi mwenye madaraka ya Uwaziri Mkuu kuandika barua kwa Rais kuomba kujiuzulu ni ishara ya uwajibikaji hili, Mh. Lowasa katufundisha kwa vitendo, inaweza isitokee, lakini kubaki tu kwenye kumbukumbu tu, inatosha.

Misingi ya kusalitiana kwenye makubaliano ya kisiasa, naamini uwoga wa baadhi ya wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi kwenye dhana ile ile ya uwajibikaji, ule ushujaa uliogopesha wengi kwasababu wanasiasa wengi wanaogopa kuwajibika, lakini namshukuru Mwenyezi Mungu, kwenye ule msemo mchagua nazi sana mwishowe anachagua koroma ndivyo ilivyotokea alikatwa Mh. Lowasa akaingia Chuma (R.I.P) Dk. magufuli, moto uliwaka na kikubwa ambacho nakumbuka ajenda ya Lowasa ya Elimu bure, Chuma aliiendeleza, Rais wetu Mama wa Taifa naye anaiendeleza hii ni heshima ya kipekee sana, ingawa hawakumchagua Urais kwasababu ya uwoga wa baadhi ya watu.

Mimi binafsi nakushukuru sana uliingia mgogoro na serikali ya Misri kwasababu ya watanzania wao wakitetea mto Nile, na wewe ukitetea ziwa Victoria watanzania wafaidike na maji hayo.....leo hii sio kama kipindi chetu darasa moja la watoto 100 wanachaguliwa 3 kuendelea na masomo ya sekondari, siku hizi darasa zima linaendelea adui ujinga anakaribia kwisha ndani ya nchi hii, naamini tuliokuwepo tupambane kwenye kubadili mitaala ya elimu ili iwe msaada kwa watoto....Mh. Lowasa kaacha alama yake.....tuliobaki tuache ya kwetu.
Pumzika kwa Amani Baba yetu......ni kweli bendera zinapaswa kupepea nusu mlingoti, Taifa Linakulilia..[emoji24][emoji24][emoji24]
 
Back
Top Bottom