Utamkumbuka Edward Lowassa kwa mambo gani?

Utamkumbuka Edward Lowassa kwa mambo gani?

Lowasa alikuwa ni kati ya viongozi waliopata bahati ya kuzaliwa kizazi ambacho wale wachache walioweza kupata elimu kipindi hicho na kuichagua siasa kama sehemu yao ya maisha, wana maisha mazuri sana.
Kwenye siasa kuna kuanguka, kuna kusalitiana kwenye makubaliano, kuna kuogopana katika upana wa maendeleo binafsi, ambapo nashuhudia viongozi wengi wana muelezea Lowasa alivyoanguka kwenye mbio za urais 2015, alivyojiuzulu Uwaziri Mkuu, kama anguko la kisiasa la asha.....matukio hayo mawili ni matukio makubwa katika siasa za Afrika ambapo ni mfano wa kuigwa......bara letu la Afrika kwa ubinafsi na uroho wa viongozi wafia tumbo ni ngumu kiongozi mwenye madaraka ya Uwaziri Mkuu kuandika barua kwa Rais kuomba kujiuzulu ni ishara ya uwajibikaji hili, Mh. Lowasa katufundisha kwa vitendo, inaweza isitokee, lakini kubaki tu kwenye kumbukumbu tu, inatosha.

Misingi ya kusalitiana kwenye makubaliano ya kisiasa, naamini uwoga wa baadhi ya wajumbe wa Chama Cha Mapinduzi kwenye dhana ile ile ya uwajibikaji, ule ushujaa uliogopesha wengi kwasababu wanasiasa wengi wanaogopa kuwajibika, lakini namshukuru Mwenyezi Mungu, kwenye ule msemo mchagua nazi sana mwishowe anachagua koroma ndivyo ilivyotokea alikatwa Mh. Lowasa akaingia Chuma (R.I.P) Dk. magufuli, moto uliwaka na kikubwa ambacho nakumbuka ajenda ya Lowasa ya Elimu bure, Chuma aliiendeleza, Rais wetu Mama wa Taifa naye anaiendeleza hii ni heshima ya kipekee sana, ingawa hawakumoa Urais kwasababu ya uwoga wa baadhi ya watu.

Mimi binafsi nakushukuru sana uliingia mgogoro na serikali ya Misri kwasababu ya watanzania wao wakitetea mto Nile, na wewe ukitetea ziwa Victoria watanzania wafaidike na maji hayo.....leo hii sio kama kipindi chetu darasa moja la watoto 100 wanachaguliwa 3 kuendelea na masomo ya sekondari, siku hizi darasa zima linaendelea adui ujinga anakaribia kwisha ndani ya nchi hii, naamini tuliokuwepo tupambane kwenye kubadili mitaala ya elimu ili iwe msaada kwa watoto....Mh. Lowasa kaacha alama yake.....tuliobaki tuache ya kwetu.
Pumzika kwa Amani Baba yetu......ni kweli bendera zinapaswa kupepea nusu mlingoti, Taifa Lunakulilia..[emoji24][emoji24][emoji24]
Yaani leo amefariki ndio mnasema yote haya,Kwanini hamkusema alipokuwa bado hai?.Anyway sawa.

Sent from my V1901A using JamiiForums mobile app
 
Mtangazaji Mwandamizi wa Clouds media ndugu Mwijaku amesema yeye binafsi amshukuru sana mzee Lowasa kwa kubuni na kujenga shule za Kata

Mwijaku amesema yeye mwenyewe amesoma shule za Kata na sasa amekuwa Mtu Maarufu sana nchini na Duniani

Source: Clouds Radio
 
Mtangazaji Mwandamizi wa Clouds media ndugu Mwijaku amesema yeye binafsi amshukuru sana mzee Lowasa kwa kubuni na kujenga shule za Kata

Mwijaku amesema yeye mwenyewe amesoma shule za Kata na sasa amekuwa Mtu Maarufu sana nchini na Duniani

Source: Clouds Radio
kwamba CCM mlimuibia kura zake za urais
 
Nitamkumbuka kwa kujilimbikizia mali zisizo na maelezo ya kutosha.

Pale Morogoro alivunja Rekodi ya kumega eneo la Jeshi la Magereza na kujenga Hoteli kubwa!!

Ama kweli kifo hakina huruma; unaondoka na nafsi yako tu na unaacha Kila kitu!!

TUJIFUNZE KWA HUYU NA WEZI WENGINE AMBAO NAO WATAKUFA
Mbona wanasema jamaa hajawahi kuiba chochote huko serikalini..
 
Ufisadi wa Richmond amekufa pasipo kutoa siri ya Richmond ilikuwa niyanani kati ya Yeye na Mkwere.Lowassa nikati ya wanasiasa waliochangia umasikini kwa watanganyika kwa ufisadi wao na Mkwere,by Dk Slaa voice.
Hizo ni siasa za majitaka, Dr Lowassa hajawahi kuiba hata pen ya mtu sembuse kuwa fisadi. Achen kumchafua bwana.
 
Namkumbuka kwa ufisadi
kingine nachomkumbuka zaidi ni utapeli aliowafanyia UKAWA.
akawa anajisahaulisha badala ya peoples power! akawa anasema CCM hoyee!
 
Kuna wakati bwawa la mtera lilikauka kupita kiasi.akiwa waziri wa maji alifuatilia jambo hili kwa umakini mkubwa ikagundulika kuwa kuna watu wamechepusha mkondo wa mto Ruaha kwa kuelekeza maji kwenye mashamba ya mpunga
baada ya kufunga hiyo mifereji kuelekea hayo mashamba na maji kurudi kwenye mkondo wake wa kawaida bwawa la mtera lilirudi kwenye ujazo mzuri wa maji.alikuwa akisimamia jambo alikuwa makini na mfuatiliaji
zaidi sana alikuwa na hofu ya Mungu
Na jambo kubwa ninalojifunza kwake ni kukaa kimya hata kama watu wanakusema vibaya katika jamii.
bila kupunguza ukali wa maneno au kuficha mambo, kuna baadhi ya viongozi walifikia hatua ya kumdhihaki Ndugu yetu Lowassa kuwa anajinyea.na kuwa atafia Ikulu.mwingine akafikia kupiga jaramba jukwaani japo sina uhakika kama alikuwa miongoni mwa waliodhihaki.nasema sina uhakika kwa kuwa sikumsikia kwa kauli yake akimtaja ndugu yetu Lowassa kuwa ni mgonjwa.lakini wapo waliofikia kusema kuwa hawapo tayari kufanya uchaguzi wa marudio kwa kumchagua mgombea mgonjwa
Tuwe makini katika kusema
 
Baba wa Taifa Hayati Julius Kambarage Nyerere itakuwa alikuwa Team Jakaya maana alishinikiza Lowassa ajitoe kwny mbio za Urais 1995 otherwise anarudisha kadi ya Chama
Unaonekana wa juzi,1995 alishinda kikwete dhidi ya Mkapa pale Dom.Mwal akaforce kurudisha kadi mgombea akiwa Kikwete
 

Habari Wadau,

Leo Februari 10, 2024 Makamu wa Rais Dkt. Mpango ametangaza kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania na Mgombea Urais wa CHADEMA mwaka 2015 Edward Ngoyai Lowasa

Soma: Edward Lowassa (Waziri Mkuu Mstaafu na Mgombea Urais wa CHADEMA 2015) afariki dunia

Katika mwaka enzi za uhai wake Mzee alipata kuwa na ushawishi Mkubwa nchini kiwango cha kuweza kujaza mikutano katika Uchaguzi wa Urais mwaka 2015.

Binafsi ntamkumbuka sana kwa uthubutu wake wa kuweza kujiuzulu nafasi ya Uwaziri Mkuu alipohusishwa na tuhuma za ufisadi.

Wewe utamkumbuka Lowassa kwa mambo gani?
Kipindi nakaa monduli miaka ya 2010 to 2012 alikuwa anatupa mahindi Bure Kila nyumba
 

Habari Wadau,

Leo Februari 10, 2024 Makamu wa Rais Dkt. Mpango ametangaza kifo cha aliyekuwa Waziri Mkuu wa zamani wa Tanzania na Mgombea Urais wa CHADEMA mwaka 2015 Edward Ngoyai Lowasa

Soma: Edward Lowassa (Waziri Mkuu Mstaafu na Mgombea Urais wa CHADEMA 2015) afariki dunia

Katika mwaka enzi za uhai wake Mzee alipata kuwa na ushawishi Mkubwa nchini kiwango cha kuweza kujaza mikutano katika Uchaguzi wa Urais mwaka 2015.

Binafsi ntamkumbuka sana kwa uthubutu wake wa kuweza kujiuzulu nafasi ya Uwaziri Mkuu alipohusishwa na tuhuma za ufisadi.

Wewe utamkumbuka Lowassa kwa mambo gani?
Nakumbuka aliwahi kusema haya yafuatayo:-

1. Kabla hajafa lazima awe Rais wa nchi hii

2. Aliahidi kutuletea mvua ya kutengeneza toka Thailand baada ya kufanya ziara huko.
 
Back
Top Bottom