Utapeli wa kuagiza gari Japan

Utapeli wa kuagiza gari Japan

Naomba kuwasilisha hili kwa faida ya wengi,Mimi niliagiza gari japan kupitia Real motor japan ni miezi kama mitatu sasa.

Kila kitu kikawa kinaenda sawa, nikajulishwa gari imepakiwa nkapewa na jina la meli itafika tarehe ngapi nikawa naitrack fresh kabisa.

Nikaambiwa wanaandaa documents wanitumie through DHL,nimesubiri mpaka hakuna document inayotumwa.

Nimawasumbua sana hapo imebaki one week meli ifike Tanzania wananipanga tu tutatuma tutatuma.mwisho wakaniambia you can cancel the order.

Nikakubali nikacancel ili wanirefund hela yangu.nkatuma details zote za account yangu, up to now kimya natuma message wamenichunia.

Tuwe waangalifu ndugu zangu ntaleta mrejesho zaidi.

Naombeni anayejua hatua za kuchukua

NB: Nilituma pesa kwenye account yao ya Tanzania shillings.
Inaelekea kuna matapeli wengi na wao wamewapa tahadhari wateja wao.

Hebu share number ulizokuwa unafanya nao mawasiliano pamoja na bank details.

Nimetembelea website yao nmekutana na hii.

Screenshot_20231002_211606_Chrome.jpg
 
Naomba kuwasilisha hili kwa faida ya wengi,Mimi niliagiza gari japan kupitia Real motor japan ni miezi kama mitatu sasa.

Kila kitu kikawa kinaenda sawa, nikajulishwa gari imepakiwa nkapewa na jina la meli itafika tarehe ngapi nikawa naitrack fresh kabisa.

Nikaambiwa wanaandaa documents wanitumie through DHL,nimesubiri mpaka hakuna document inayotumwa.

Nimawasumbua sana hapo imebaki one week meli ifike Tanzania wananipanga tu tutatuma tutatuma.mwisho wakaniambia you can cancel the order.

Nikakubali nikacancel ili wanirefund hela yangu.nkatuma details zote za account yangu, up to now kimya natuma message wamenichunia.

Tuwe waangalifu ndugu zangu ntaleta mrejesho zaidi.

Naombeni anayejua hatua za kuchukua

NB: Nilituma pesa kwenye account yao ya Tanzania shillings.
Tatizo mnapokuwa na pesa mnajifanya wajuaji ununue kimyakimya uje kuwashangaza rafiki zako.

Ungeuliza awali ungesaidika.

Hiyo pesa huipati tena.
Beforward.jp wapo wamejaa, waaminifu why ununue vichochoroni?

Nilitumia Beforward wakaniletea kabla ya muda walioniahidi
 
Tatizo mnapokuwa na pesa mnajifanya wajuaji ununue kimyakimya uje kuwashangaza rafiki zako.

Ungeuliza awali ungesaidika.

Hiyo pesa huipati tena.
Beforward.jp wapo wamejaa, waaminifu why ununue vichochoroni?

Nilitumia Beforward wakaniletea kabla ya muda walioniahidi
Acha mipasho kijana. Kama huna msaada kwake unakausha tu...
 
Ujapigwa ila Kuna tatizo limetokea.Je wanaofisi zao hapa tz.
Mbona Mimi ni shaagiza mashine kubwa ujerumani na ikafika.
Ishu ni wewe kuangalia umetimia site Gani ya kampuni
Kuwa na ofisi, usajili brela, TRA nk Sio kigezo Cha kutopigwa hata kama ofisi ipo Ikulu maadamu tu ni mbongo don't try this at home.
Online business, viwanja lipa kidogo maadamu ni mswahili ingia na mguu mmoja
 
Kuna utapeli Fulani wamefunzwa na wanigeria wabongo.
Wanafungua ofisi, documents zote halali vibali vyote hadi bank account then wanafungua biashara hata za kimataifa mwanzoni wanaenda vizur kuvuta wateja wakishafikia mzunguko wa bilioni moja mnapigwa,mtafungua kesi mahakamani kufuatilia haki zenu mchakato wa kesi mtakula danadana hadi mpotee mmoja mmoja.
Mswahili hajawahi kuwa seriously kwenye biashara.anaangalia 500 ya Leo anaacha laki Tano ya kesho.
 
Dah pole Boss wangu nakumbuka kuna jamaa week kadhaa nyuma tulimsanua kuhusu Real motor wanampa vitisho na tulimwambia wateme hao kwa mantiki hiyo website makini bila kufumba maneno ni;-

1.Beforward-Jamaa yangu kaagiza kapata gari ontime na ni mala ya kwanza.
2.Sbtjapan-Nimeagiza namimi nimelipata gari ontime na ni mala ya kwanza.

*Huko kwengine lolote linaweza kukutokea.

Jaribu kwenda Ubalozi wa JAPAN kama ni kweli Real Motors unaweza pata muongozo wa kufatilia hiyo kitu na kuona wanakusaidia vipi kuhusu kampuni yao kukutapeli.

Jemedaree
 
Inaelekea kuna matapeli wengi na wao wamewapa tahadhari wateja wao.

Hebu share number ulizokuwa unafanya nao mawasiliano pamoja na bank details.

Nimetembelea website yao nmekutana na hii.

View attachment 2770004
Niliona hili onyo pia. Kwa kuwa ni la hivi karibuni (July 2023), huenda hivi karibuni kumekuwa na matukio ya watu kutapeliwa kupitia jina la Real Motor Japan.
 
Real Motors hawa hawa? Ebu share email yao tuone.
Na mm nashangaa, perhaps jamaa wengine ambao walijifanya real Motors na web site ikawa kama real motors lkn ilikuwa sio hawa Real Motors tunaowajua!
 
Back
Top Bottom