Utaratibu na gharama za kupata hatimiliki ya nyumba/kiwanja

Utaratibu na gharama za kupata hatimiliki ya nyumba/kiwanja

Ni hatua ndefu. Kwanza lazima uwe na uthibitisho kuwa hilo eneo la ardhi ni lako. Pili uende wilayani kitengo cha ardhi. Wao watakupa picha yote. Ni lazima waje wapime eneo husika walipeleke wizarani likishakubaliwa watakutengenezea mawe ya pembeni (beacons) yenye namba zao. Baada ya hapo ndio watapeleka waizani ili maandalizi ya hati yaanze. Malipo ya kisheria yapo lakini siwezi kujua ni kiasi gani kwani inategemeana na ukubwa wa eneo na mahali lilipo. Kwa sababu uko nje ya mkoa wa DSM hati utaipata mapema tu!
 
Habarini wadau...naomba kufahamisha ni hatua gani za kufwata ili kupata hati ya kiwanja ambacho hakina hati kabisa lakini mmiliki halali ni mimi.Thanx in advance
 
Jodoki Kalimilo;

Ndugu Jodoki, majibu yako yamenifurahisha sana, inaonyesha unaupeo mzuri katika mambo haya. Mimi niimestushwa sana na kupandishwa kwa gharama ya kodi ya kiwanja changu, maeneo ya Dar. Nimeanziasha thread huku about that. Katika thread hii swali langu kuu lilikuwa ni hili;

Je, hivi inawezekana kweli kodi ya kiwanja chenye ukubwa wa acre moja ikapande kutoka 90,500 (2011/12) mpaka 340,000 (2012/13) tshs? Hivi kodi za viwanja zimepanda au unataharifa zozote za mabadiliko haya?

Tafadhali naomba unisaidie kwa ufahamu wako.
Ni matumaini yangu kwamba mchango wako unaweza kuwasaidia na watu wengine.

Asante sana
Naona comment ya 2013 ndio inaingia tena kwa mara nyingine, nadhani nilishakujibu mkuu
 
Habarini wadau...naomba kufahamisha ni hatua gani za kufwata ili kupata hati ya kiwanja ambacho hakina hati kabisa lakini mmiliki halali ni mimi.Thanx in advance
Nenda kwenye halmashauri uliyopo kitengo cha ardhi watakupa mwongozo wa namna ya kufanya na kama una hela wanakupimia kisha watakupa letter of offer ambapo baadae utatakiwa kwenda ofisi wa kamishina wa ardhi ili kuweza kupata hati yako, ni zoezi linaweza kuchukua kama mwaka hivi kupata hati ila kikubwa ni eneo kupimwa kisha upate letter of offer (hii inakupa uhalali wa kiwanja chako) then baada watu wa halmashauri/manispaa wataipeleka kwa kamishina wa ardhi ili aweze kufanya taratibu zingine
 
Asanteni sana waliotoa majibu na walioongeza maswali ya msingi.....hakika nimejifunza
 
Wanandugu ninaomba kujua procedure nzima ya kufuata ili kupata hati ya kiwanja chako ulichonunua kutoka wizarani. Documents zipo Manispaa ya Kinondoni.

Na pia ninaomba kujua gharama na kodi husika ambazo natakiwa nilipe.

Natanguliza shukurani.
 
Manispaa ya Kinondoni yaani kwa DC mpya ....... Uwiiiiii ingekuwa ilala tungechangia idea hapa jukwaani,,,,,
 
Habarini wadau,mm bado sijaprocess hati ya kiwanja ila nina copy ya certificate ya occupacy na original yake sijafanikiwa kuiona maana kiwanja ni cha urithi na kina jina la mzee kwa sasa nataka nichukue mkopo kwa kutumia kiwanja hcho vipi utaratibu wa kupata certificate of occupacy ambayo ni original?
 
Kuna watu hawana vipaji vya ualimu,hata wakuelekezeje huwezi kuelewa.Mimi nina kiwanja cha urithi nyumbani kijijini kabisa nataka NIKIKATIE HATIMILIKI Naanzaje WADAU.............
 
Kuna kiwanja nimeuziwa nimeambiwa kina Offer na kimepimwa,kimewekewa becoans.Sasa hakina hati nataka kuuliza mchakato wake upoje nipate hati.Hivi kiwanja Halmashauri ndiyo walipima sasa mchakato wa hati miliki nataka kujua upoje
 
Kuna watu hawana vipaji vya ualimu,hata wakuelekezeje huwezi kuelewa.Mimi nina kiwanja cha urithi nyumbani kijijini kabisa nataka NIKIKATIE HATIMILIKI Naanzaje WADAU.............
Mkuu sio hawana kipaji, huu uzi una miaka kadhaa na wengine wameshazeeka (jokes), kwa uzito wa issue ya ardhi nina uhakika ukisoma comments kwenye hizo page utapata jibu though kwa haraka haraka suala lako linaangukia sehemu mbili kwanza mambo ya mirathi kisha ukishakamilisha huko ndio unakuja kuangalia kuhusu umilki wa hicho kiwanja kwa jina lako then hatua za kukatia hati milki kwa kufuata taratibu sawa na watu wengine wanaomilki visivyo vya urithi
 
na kiwanja nimeuziwa kina Offer na kimepimwa,kimewekewa becoans.Sasa hakina hati,nimeshajenga na ninaishi

nataka kuuliza mchakato wake upoje nipate hati?
gharama ni kiasi gani?
 
Kwanza kuna aina mbili za hati..
1.hati ya kawaida
2.hati ya kimila

Hati ya kawaida inatolewa katika eneo ambalo lina mchoro Wa mipangomiji..na limepimwa na kupatiwa namba za viwanja....

Kwa mujibu Wa sheria za ardhi mwenye mamlaka ya umilikishaji ni afisa ardhi Mteule.....
Utaratibu ni kuwa muombaji Wa eneo lililopimwa anawasilisha barua kwa afisa ardhi Mteule Wa halmashauri husika....afisa ardhi Mteule kama Katibu Wa kamati anaratibu maombi ya umilikishaji Wa viwanja na kuingiza maombi husika katika kamati ya ugawaji Wa viwanja na mashamba ambayo mwenyekiti wake ni Mkurugenzi Wa halmashauri husika....maombi yanajadiliwa na waombaji wanabarikiwa au wanakataliwa kupewa viwanja kama viwanja ni vya serikali....
Baada ya maombi kukubalika ofisi ya ardhi inamuandalia gharama ambazo muombaji anatakiwa kulipia ili apate hati na anapewa muda Wa siku 30, ili kufanya malipo ya hati miliki ambayo ni
1.malipo ya mbele ambayo ni asilimia 7.5 ya thamani ya kiwanja

2. Ada ya maombi Tshs 20000/-
3.ada ya usajili Wa hati ambayo ni asilimia ishirini ya kodi ya ardhi

4.ada ya maandalizi ya hati tshs 50000/-

5...ada ya ramani ndogo Tshs 20000/

6.ushuru Wa serikali ambao ni asilimia moja ya kodi ya ardhi kwa Mwaka...

7.kodi ya ardhi ambayo ni bei ya mita ya mraba zidisha na ukubwa Wa kiwanja....
Akishalipia anawasilisha cheti cha kuzaliwa,kiapo au passport ..na picha sita passport size kwa ajili ya kupatiwa hati mmiliki....

Hati inaandaliwa na kufungashwa tayari kwa kwenda kwa kamishna Wa ardhi na baadae kwa Msajili Wa hati Wa kanda husika kwa ajili ya kusajiliwa

Naomba kuwasilisha
Akhsante
 
Kwanza kuna aina mbili za hati..
1.hati ya kawaida
2.hati ya kimila

Hati ya kawaida inatolewa katika eneo ambalo lina mchoro Wa mipangomiji..na limepimwa na kupatiwa namba za viwanja....

Kwa mujibu Wa sheria za ardhi mwenye mamlaka ya umilikishaji ni afisa ardhi Mteule.....
Utaratibu ni kuwa muombaji Wa eneo lililopimwa anawasilisha barua kwa afisa ardhi Mteule Wa halmashauri husika....afisa ardhi Mteule kama Katibu Wa kamati anaratibu maombi ya umilikishaji Wa viwanja na kuingiza maombi husika katika kamati ya ugawaji Wa viwanja na mashamba ambayo mwenyekiti wake ni Mkurugenzi Wa halmashauri husika....maombi yanajadiliwa na waombaji wanabarikiwa au wanakataliwa kupewa viwanja kama viwanja ni vya serikali....
Baada ya maombi kukubalika ofisi ya ardhi inamuandalia gharama ambazo muombaji anatakiwa kulipia ili apate hati na anapewa muda Wa siku 30, ili kufanya malipo ya hati miliki ambayo ni
1.malipo ya mbele ambayo ni asilimia 7.5 ya thamani ya kiwanja

2. Ada ya maombi Tshs 20000/-
3.ada ya usajili Wa hati ambayo ni asilimia ishirini ya kodi ya ardhi

4.ada ya maandalizi ya hati tshs 50000/-

5...ada ya ramani ndogo Tshs 20000/

6.ushuru Wa serikali ambao ni asilimia moja ya kodi ya ardhi kwa Mwaka...

7.kodi ya ardhi ambayo ni bei ya mita ya mraba zidisha na ukubwa Wa kiwanja....
Akishalipia anawasilisha cheti cha kuzaliwa,kiapo au passport ..na picha sita passport size kwa ajili ya kupatiwa hati mmiliki....

Hati inaandaliwa na kufungashwa tayari kwa kwenda kwa kamishna Wa ardhi na baadae kwa Msajili Wa hati Wa kanda husika kwa ajili ya kusajiliwa

Naomba kuwasilisha
Akhsante

Ahsante kwa ufafanuzi huu. Ni jambo ambalo kidogo lina changamoto zake. Sasa kwa mfano mimi nna kiwanja kimoja kipo Kigamboni ambacho nna kila kitu isipokuwa hati.

Kwa hapa Dar es Salaam, ili niweze pata hati natakiwa anzia ofisi zipi?
 
Back
Top Bottom