Utaratibu wa kuishi na ndugu baada ya ndoa unafaa uwe vipi?

Utaratibu wa kuishi na ndugu baada ya ndoa unafaa uwe vipi?

shalet

JF-Expert Member
Joined
Feb 12, 2013
Posts
3,430
Reaction score
3,547
Habari za siku nyingi watu wa Mungu.

Hivi ni utaratibu gani unafaa kufuatwa katika kuchagua ndugu wa kuishi nao baada ya ndoa. Nakumbuka mwanzo kabisa kipindi namuoa mke wangu nilimjulisha kuwa napenda sana ndugu ila kuishi na ndugu ni mtihani kama mtu ana uhitaji na tuna uwezo wa kumsaidia bora tumsaidie huko huko aliko kukiwa na ulazima sana ndipo ataishi kwetu.

Bahati mbaya huyu mwenzangu na ndugu zake wamefanya nyumba yangu kijiwe ndugu zake wote wapo hapa hapa mjini sasa imekuwa anakuja huyu anakaa wiki anaondoka wanapokezana , likizo watoto zao wanawaleta kwangu na wana vurugu kweli ile likizo ya mwaka mpya walinivunjia side mirror ya gari ikabidi niwafukuze manake walikuwa wakiaanza kukimbizana wanapita mpaka juu ya makochi ilibaki kidogo wakanyage kompyuta niliwafukuza siku hiyo hiyo.

Tatizo la pili kuna ndugu zake hawa watu wazima wakike ambao ni dadazake ni wakubwa kiasi mmoja binti yake ndiyo mwenye watoto niliowafukuza, hawa wanakaa tu nyumbani hawafanyi chochote ni kuangalia tu tamthiliya mpaka kurudi nyumbani sasa naona kero mimi na wife hatujajaliwa watoto sasa hapo nyumbani kuna familia ya watu 4 na wote wanatokea hapo mabibo yaani mimi ndio nimekuwa kama mgeni kwenye familia.

Nikimuambia hawa watu kwanini wasirudi kwenu kwenye nyumba ya familia wakae sisi tutakaa nao mpaka lini anasema soon wataondoka toka mwezi wa pili anasema hivyo soon wataondoka, karibuni mama anataka kuja kwenye matibabu MOI ila kagoma kufikia kwangu hawezi lala kitanda kimoja na mtu mwingine anashida na mifupa.

hapo bado kuna ndugu zake wanakuja tu wikend wakijisikia na wakiondoka hawana nauli wanakuomba tena shemeji nauli hasa namuuliza hawa nao wanakuja kila wikend kufanya nini, anasema kama sitaki ndugu zake waje atawaambia ila tatizo sio kuja tatizo hata nauli hawana ukiwapa ndogo wanakuimbia kuna sehemu ya kupanda bodaboda.

Ajabu wao wenyewe kwa wenyewe hawatembeleani ni kama vile wanaamua kunimalizia pesa hivi. Nipeni busara kudeal na hawa watu nahisi kuanza kukata mahitaji.
 
UNA ROHO YA HURUMA SANA TATIZO, KUWA NA MSIMAMO

Kama huwahitaji nduguze hapo nyumbani kwa sababu ya kipato ni kidogo kuwa muwazi kabisa, angalia sasa hujapata watoto bado unawahudumia watu wengine.. Ukiwazoesha sana kijiji kizima kitakuja hapo maana si wanajua kuna kitonga kwa shemeji

Set boundaries mkuu, hali yenyewe ya maisha kwa sasa ni vuta ni kuvute

Wale wanaokatazaga ndugu nyumbani kwao kuja kukaa nawaelewaga japo wanaitwa mabahili na wakatili...
 
Asee hilo linatakiwa kujulikana mapema kabisa kabla ya kuoana,cha muhimu wapige stop kuja,au kama watakuja na unaunga mkono maoni ya shetani basi ww tafuta mchempuko mpangie chumba wakija ndugu zake ww hamia kwa mchepuko kwa muda na matumizi yako afu mtumie sms "nimewapa nafasi kwanza wakiondoka niambie nirudi"

Bila shaka utakuwa mwisho wao kama mkeo ni mtu wa kujiongeza
 
Hiyo familia ya mkeo ni watu wa jamii ya mkoa gani kwanza hebu tuanzie hapo maana kuna jamii au makabila kwenda kujibweteka kwa ndugu yao ambaye kidogo maisha yamemkalia afadhali ili kwenda kuridhika na kujiachia bila kujali unagharamikaje kuwakirimu kwao ni jambo la kawaida na hawaoni shida.

Ukiwapinga au ukiongea na mkeo kuhusu bugudha hiyo mkeo anawaambia nduguze vizuri tu na unakuja kuonekana wewe ndie tatizo.
 
Hao ndugu watakuvunjia ndoa yako, maana kiuhalisia mkeo hawezi kuwafukuza ataanzaje??? Aambiwe yeye ni mchoyo hataki kusaidia ndugu ndio maana anakutia moyo kuwa wanaondoka na bado wapo, Sasa fanya hivi onyesha msimamo wako japo mtaingia kwenye msuguano lakin baadaye kutatulia na wewe kuendelea na maisha yako Kama kawaida
 
Mkuu kama huna mtoto hapo Anza kufanya hivi ,acha kununua vyakula hapo nyumbani ,acha kulipia king'amuzi ,wakija usiwe na stori nao kabisa wapite kama huwaoni ,wakija nyumbani unaawapotezea na kuendelea na Mambo mengine ,muoneshe mkeo kwa ukali kuwa hutaki Kijiji cha watu hapo kwako ,,,,,badae wenyewe wataondoka tu ....
 
Tubadilike mtu akishaoa au akiolewa waacheni waishi maisha yao,watu wameoana tayari mshaenda kujazana kuishi hapo mara bibi,sijui shangazi,sijui shemeji,acheni wanandoa waishi kwa uhuru mnawabana, mara waletewe mtoto sijui wa nani walee ,acheni wanandoa waishi wenyewe kusalimiana iwe mara moja moja na mtoe taarifa sio kwenda tu kama kwenu.

Ndugu mnachangia sana wanandoa kuachana kwa sababu mkishaenda kukaa mnaanza maneno na chokochoko. Watu wakioana waacheni waishi maisha Yao wapeni uhuru,wapeni nafasi.

Kina mama wengi wanavunja ndoa za watoto wao kwa kuingilia na kuanza kuwapangia wanandoa waishi namna gani ,wazae watoto wangapi? Kina mama kuweni busy na maisha yenu maisha ya wanandoa hayawahusu nyie wabarikini inatosha sio kuanza kuchongoa midomo na wivu wivu usio na maana,eti kisa umemzaa kwa uchungu ndio umpangie maisha haitakiwi
Nimegundua ndoa nyingi huvunjika kisa ndugu,kwenda kujirundika kukaa kaa tu kwa watu wameoana
Tubadilike

Dinazarde i see ya"
 
Mkuu kama huna mtoto hapo Anza kufanya hivi ,acha kununua vyakula hapo nyumbani ,acha kulipia king'amuzi ,wakija usiwe na stori nao kabisa wapite kama huwaoni ,wakija nyumbani unaawapotezea na kuendelea na Mambo mengine ,muoneshe mkeo kwa ukali kuwa hutaki Kijiji cha watu hapo kwako ,,,,,badae wenyewe wataondoka tu ....
Baadae watamuita mchoyo na bahili ila case solved
 
Wewe ni LIJINGA ndio maana unafanywa ndondocha na wakwe zako. Unaonekana ni uchochoro na huna maamuzi ya kiume kila wanalotaka wao wanakupelekesha.

Ukisikia mtu yeyote anasemekana hana shida, mtu wa watu, hana baya ndio kama wewe hapo. Sifa zenu ni kuvumilia ujinga na huwa mnafeli kwenye kusimamia vitu. Mtu mwenye msimamo, asiyevumilia ujinga na mchukua hatua stahiki anaitwa mkorofi na ndio hawa hufanikiwa mambo yao. Kibongobongo ukiendekeza tabia binafsi za watu ya kwako yatakushinda.

Vunja hiyo kambi, kwanza unawafanya wawe tegemezi na maskini milele.
 
Kama mkeo umeongea naye na haoneshi kujali mfanyie roho mbaya. Ndugu zake usiiongee nao kitu, anza kwenye bajeti kama ulikua unanunua vyakula in bulky acha we mpigie bajeti ya siku ndo uache hela na hiyo bajeti iwe ya wawili tu. Halafu kwa hao ndugu acha kabisa kuwajali, wakiiomba nauli wanyime kisiasa au wakikuomba hela wapige kalenda. In short weka mazingira magumu nyumbani kwako. Si unajua nzi hufuata mvvi
 
Kaka yangu alifanya hivi...
Ndugu wakija nyumban kwake kukaa basi ni ndugu wenye faida haijalishi anatoka upande gani hakuwahi kutaka ujinga kabisa na anaishi vizuri mpaka leo kikubwa msimamo tu.

imagine
Ana kila kitu nyumban kaz nzuri, mshahara mnono alichofanya alianza kilimo cha mpunga bondeni kama mnavyojua kaz za mpunga haziishi mwezi wowote ni kazkaz tu kwahyo ndugu wakienda kwake anawasombelea wote kwenda shamban kumsaidia kaz huko maana yye yuko bize ni kutoa maelekezo tu. Walikuwa wakienda kwake ni trip moja tu hawarud tena wanalalamika tu afu maisha frsh tu
 
Kaka yangu alifanya hivi...
Ndugu wakija nyumban kwake kukaa basi ni ndugu wenye faida haijalishi anatoka upande gani hakuwahi kutaka ujinga kabisa na anaishi vizuri mpaka leo kikubwa msimamo tu.

imagine
Ana kila kitu nyumban kaz nzuri, mshahara mnono alichofanya alianza kilimo cha mpunga bondeni kama mnavyojua kaz za mpunga haziishi mwezi wowote ni kazkaz tu kwahyo ndugu wakienda kwake anawasombelea wote kwenda shamban kumsaidia kaz huko maana yye yuko bize ni kutoa maelekezo tu. Walikuwa wakienda kwake ni trip moja tu hawarud tena wanalalamika tu afu maisha frsh tu
Vyema kabisa
 
... kama hawamegi pakubwa ishi nao tu, sometime huwa wanakuwa na baraka zao. Maisha ni haya haya tu na ya kupita. Mapokeo na mtizamo utakaowachukulia ndio itakuwa hivyo...Upande wa pili hiyo ni familia yako una mamlaka kamili ya kuchagua nani wa kuishi naye nje ya mkeo so be straight.
 
Back
Top Bottom