Utaratibu wa wafiwa kuwalisha waombolezaji wengine umerasimishwa Tanzania?

Utaratibu wa wafiwa kuwalisha waombolezaji wengine umerasimishwa Tanzania?

Dah nimecheka utadhani mazuri, yaani mnakua hamlali. Mnachangishana Hadi kukopa kisa kuwalisha Watu wanaokuja kuwafariji! Si heri ukodi Watu wa kukufariji ujue Moja, msiba ukiisha unalipa invoice maisha yanaendelea
Hayo maisha yapo kwenye jamii hii tuliyopo?
 
Habari za leo wanajamvi? bila shaka mapambano yanaendelea kama kawaida!
Tuendelee kupambana sana na kusaka michuzi kwa udi na uvumba kana kwamba hatufi, na tuendelee kumuomba na kumwabudu Mungu kana kwamba tunakufa kesho!

Kwanza kabisa napenda kutoa masikitiko yangu kama mwananzengo kwa sintofahamu ambayo imeendelea kuikumba jamii ya kitanzania kwa sehemu kubwa kama si yote.

UMUGHAKA nimekuwa nikijiuliza huu utaratibu wa kipumbavu ni nani/akina nani waliyo urasimisha? Kumekuwa na kasumba ambayo sidhani kama nikiita ni upumbavu/ushenzi kama nitakuwa nakosea.

Misiba mingi kama si yote niliyowahi kuhudhuria, nimekua nikiona utaratibu wa wale waliofikwa na msiba ndiyo ambao wanahaha kuwalisha watu ambao wamekuja msibani kutoa pole/kufariji.

Na lazima niwe mkweli ya kwamba,hata sisi kwetu pia tumepata misiba mingi tu ya ndugu zangu na utaratibu huwa ni huo huo!,hili suala limekaaje wapendwa? Yaani unakuta waliofikwa na msiba ndiyo wanaumiza vichwa namna ya kuwalisha wanaokuja kuwafariji badala ya waliokuja kuwafariji wenye matatizo wao ndiyo ilipaswa wakae wakusanyane wananzengo ili kuwalisha waliofikwa na msiba!

Huu utaratibu ni mbovu sana na siungi mkono kabisa! Ni kwanini tusiwe na utaratibu tunapoenda misibani kuwafariji wafiwa kusiwe na utaratibu wa kuwalisha wafiwa pamoja na watakao hudhuria msibani? Yaani unakutwa watu wengi wanaoenda misibani ni kupiga soga tu na kusubiri kunawishwa wakati wa kula huku wanafurahia maisha kana kwamba ni sherehe.

Watu wengi wanaenda misibani si kufariji bali kupiga soga na kula!,huu ndiyo ukweli ukubali au ukatae!

Yaani mtu amefiwa na mpendwa wake halafu bado aumize na kichwa namna ya kuwalisha wananzengo!,hii kitu iko sawa kweli?,hivi hizi nguvu unadhani atakuwa nazo?,hii imepelekea hasa watu wenye kipato cha chini wanabaki kusimangwa na wananzengo hata bila aibu!,unakuta kabisa majirani wanaongea " Msiba wenyewe hata vyakula hauna,naona watu wamechungulia tu wamesusa",kabisa?

Lakini misiba ya watu wenye uwezo utasikia "Jamaa wanapika vyakula vizuri asikwambie mtu,unakula mpaka unasaza".

Hata kama mfiwa anao uwezo,ndiyo alishe wananzengo badala ya wananzengo kumlisha yeye?.

JE,huu utaratibu ni nani aliyeuanzisha?

Je,makabila yote ya Tanzania hufanya hivi?

Wenzetu mliotembea tembea huko ughaibuni,je hali huwa iko hivi kama huku kwetu.

Unakuta "Mijitu" inaenda misibani kwa ajili ya kula tu,ikishakula hiyoooooo inalala mbele!,hata aibu haioni!,unakuta jitu badala liende hata ndani kusalimia wafiwa lenyewe linakomea getini linapiga msosi halafu linalala mbele!!

HUU UTARATIBU HAUKUBALIKI

#USIPOBADILIKATUTAKUBADILISHA
#TIGHABHATEMWE
Yego chimura siga omururu ouja ukwita abhanu nomweko
 
Kwa kweli ustaarabu wetu ni mgumu sana jamii zetu za kitanzania.

Mtu kafiwa bila shaka katumia gharama nyingi tu kuuguza pia bado ana kibarua kigumu tu katika kusitiri marehemu.

Kiubinadamu nzengo ilipaswa kuwa na jukumu la kufariji na kushiriki mazishi kwa mwenzao huyo. Msiba ni jambo gumu sana kwa mwanadamu hivyo nzengo inapaswa kuwajibika effectively kwa kila hali na mali.

Wananzengo tunapaswa kusitiri marehemu ikiwemo na kuficha aibu ya umasikini lakini leo hii utakuta wananzengo wanaohudhuria msibani wako 200 lakini mchango wanaotoa kwa mfiwa hauzidi hata 200k na hapo wapo msibani si chini ya siku tatu hadi mazishi aisee inasikitisha sana.

Lakini hili ni suala la mindset tu ndugu zangu tunapaswa kubadilika. Hizo changes huanzia kwako wewe na mimi tuhurumiane na kuchukuliana matatizo na madhaifu yetu hapo jamii inaweza kubadilika.
 
Kwa kweli ustaarabu wetu ni mgumu sana jamii zetu za kitanzania.

Mtu kafiwa bila shaka katumia gharama nyingi tu kuuguza pia bado ana kibarua kigumu tu katika kusitiri marehemu.

Kiubinadamu nzengo ilipaswa kuwa na jukumu la kufariji na kushiriki mazishi kwa mwenzao huyo. Msiba ni jambo gumu sana kwa mwanadamu hivyo nzengo inapaswa kuwajibika effectively kwa kila hali na mali.

Wananzengo tunapaswa kusitiri marehemu ikiwemo na kuficha aibu ya umasikini lakini leo hii utakuta wananzengo wanaohudhuria msibani wako 200 lakini mchango wanaotoa kwa mfiwa hauzidi hata 200k na hapo wapo msibani si chini ya siku tatu hadi mazishi aisee inasikitisha sana.

Lakini hili ni suala la mindset tu ndugu zangu tunapaswa kubadilika. Hizo changes huanzia kwako wewe na mimi tuhurumiane na kuchukuliana matatizo na madhaifu yetu hapo jamii inaweza kubadilika.
Nimekuelewa sana[emoji1666][emoji1666]
 
Habari za leo wanajamvi? bila shaka mapambano yanaendelea kama kawaida!
Tuendelee kupambana sana na kusaka michuzi kwa udi na uvumba kana kwamba hatufi, na tuendelee kumuomba na kumwabudu Mungu kana kwamba tunakufa kesho!

Kwanza kabisa napenda kutoa masikitiko yangu kama mwananzengo kwa sintofahamu ambayo imeendelea kuikumba jamii ya kitanzania kwa sehemu kubwa kama si yote.

UMUGHAKA nimekuwa nikijiuliza huu utaratibu wa kipumbavu ni nani/akina nani waliyo urasimisha? Kumekuwa na kasumba ambayo sidhani kama nikiita ni upumbavu/ushenzi kama nitakuwa nakosea.

Misiba mingi kama si yote niliyowahi kuhudhuria, nimekua nikiona utaratibu wa wale waliofikwa na msiba ndiyo ambao wanahaha kuwalisha watu ambao wamekuja msibani kutoa pole/kufariji.

Na lazima niwe mkweli ya kwamba,hata sisi kwetu pia tumepata misiba mingi tu ya ndugu zangu na utaratibu huwa ni huo huo!,hili suala limekaaje wapendwa? Yaani unakuta waliofikwa na msiba ndiyo wanaumiza vichwa namna ya kuwalisha wanaokuja kuwafariji badala ya waliokuja kuwafariji wenye matatizo wao ndiyo ilipaswa wakae wakusanyane wananzengo ili kuwalisha waliofikwa na msiba!

Huu utaratibu ni mbovu sana na siungi mkono kabisa! Ni kwanini tusiwe na utaratibu tunapoenda misibani kuwafariji wafiwa kusiwe na utaratibu wa kuwalisha wafiwa pamoja na watakao hudhuria msibani? Yaani unakutwa watu wengi wanaoenda misibani ni kupiga soga tu na kusubiri kunawishwa wakati wa kula huku wanafurahia maisha kana kwamba ni sherehe.

Watu wengi wanaenda misibani si kufariji bali kupiga soga na kula!,huu ndiyo ukweli ukubali au ukatae!

Yaani mtu amefiwa na mpendwa wake halafu bado aumize na kichwa namna ya kuwalisha wananzengo!,hii kitu iko sawa kweli?,hivi hizi nguvu unadhani atakuwa nazo?,hii imepelekea hasa watu wenye kipato cha chini wanabaki kusimangwa na wananzengo hata bila aibu!,unakuta kabisa majirani wanaongea " Msiba wenyewe hata vyakula hauna,naona watu wamechungulia tu wamesusa",kabisa?

Lakini misiba ya watu wenye uwezo utasikia "Jamaa wanapika vyakula vizuri asikwambie mtu,unakula mpaka unasaza".

Hata kama mfiwa anao uwezo,ndiyo alishe wananzengo badala ya wananzengo kumlisha yeye?.

JE,huu utaratibu ni nani aliyeuanzisha?

Je,makabila yote ya Tanzania hufanya hivi?

Wenzetu mliotembea tembea huko ughaibuni,je hali huwa iko hivi kama huku kwetu.

Unakuta "Mijitu" inaenda misibani kwa ajili ya kula tu,ikishakula hiyoooooo inalala mbele!,hata aibu haioni!,unakuta jitu badala liende hata ndani kusalimia wafiwa lenyewe linakomea getini linapiga msosi halafu linalala mbele!!

HUU UTARATIBU HAUKUBALIKI

#USIPOBADILIKATUTAKUBADILISHA
#TIGHABHATEMWE
Sisi wengine DINI yetu inakataza kabisa kitendo cha mtu ambaye si mfiwa kula msibani,usahihi ni kwamba wale wanao enda msibani ndiyo wanatakiwa kuwahudumia wafiwa.

Tangu nilipopata hii Elimu kwenye dini yangu sikuwahi tena kula msibani na sitokula tena,huwa wakati wa kula ukifika natoka kidogo.
 
Mkuu wewe hayajakufika bila shaka
Mantiki ya post yangu ilikuwa naijibu commemt #44 si vinginevyo!

Angalia alichoandika hiyo comment, ndiyo nilicholenga kujibu.

Kunifika yalishanifika sana, hata mwaka jana yalinifika pia.
 
Kwa waislamu swala la ndowa na mazishi dini yao imewapa maekekezo mazuri sana.

Hizi shida waachieni wakristo lakini kwa mwislamu kupata shida hizi ni kujitakia.

Dini ya kiislamu inaelekeza mtu akifa azikwe haraka.

Familia haiwezi kuumia kwa kuwapikia uji na sukari inatosha kabisa, mambo ya catering waachieni wakristo.
 
Back
Top Bottom