Utaratibu wa wafiwa kuwalisha waombolezaji wengine umerasimishwa Tanzania?

Utaratibu wa wafiwa kuwalisha waombolezaji wengine umerasimishwa Tanzania?

Habari za leo wanajamvi? bila shaka mapambano yanaendelea kama kawaida!
Tuendelee kupambana sana na kusaka michuzi kwa udi na uvumba kana kwamba hatufi, na tuendelee kumuomba na kumwabudu Mungu kana kwamba tunakufa kesho!

Kwanza kabisa napenda kutoa masikitiko yangu kama mwananzengo kwa sintofahamu ambayo imeendelea kuikumba jamii ya kitanzania kwa sehemu kubwa kama si yote.

UMUGHAKA nimekuwa nikijiuliza huu utaratibu wa kipumbavu ni nani/akina nani waliyo urasimisha? Kumekuwa na kasumba ambayo sidhani kama nikiita ni upumbavu/ushenzi kama nitakuwa nakosea.

Misiba mingi kama si yote niliyowahi kuhudhuria, nimekua nikiona utaratibu wa wale waliofikwa na msiba ndiyo ambao wanahaha kuwalisha watu ambao wamekuja msibani kutoa pole/kufariji.

Na lazima niwe mkweli ya kwamba,hata sisi kwetu pia tumepata misiba mingi tu ya ndugu zangu na utaratibu huwa ni huo huo!,hili suala limekaaje wapendwa? Yaani unakuta waliofikwa na msiba ndiyo wanaumiza vichwa namna ya kuwalisha wanaokuja kuwafariji badala ya waliokuja kuwafariji wenye matatizo wao ndiyo ilipaswa wakae wakusanyane wananzengo ili kuwalisha waliofikwa na msiba!

Huu utaratibu ni mbovu sana na siungi mkono kabisa! Ni kwanini tusiwe na utaratibu tunapoenda misibani kuwafariji wafiwa kusiwe na utaratibu wa kuwalisha wafiwa pamoja na watakao hudhuria msibani? Yaani unakutwa watu wengi wanaoenda misibani ni kupiga soga tu na kusubiri kunawishwa wakati wa kula huku wanafurahia maisha kana kwamba ni sherehe.

Watu wengi wanaenda misibani si kufariji bali kupiga soga na kula!,huu ndiyo ukweli ukubali au ukatae!

Yaani mtu amefiwa na mpendwa wake halafu bado aumize na kichwa namna ya kuwalisha wananzengo!,hii kitu iko sawa kweli?,hivi hizi nguvu unadhani atakuwa nazo?,hii imepelekea hasa watu wenye kipato cha chini wanabaki kusimangwa na wananzengo hata bila aibu!,unakuta kabisa majirani wanaongea " Msiba wenyewe hata vyakula hauna,naona watu wamechungulia tu wamesusa",kabisa?

Lakini misiba ya watu wenye uwezo utasikia "Jamaa wanapika vyakula vizuri asikwambie mtu,unakula mpaka unasaza".

Hata kama mfiwa anao uwezo,ndiyo alishe wananzengo badala ya wananzengo kumlisha yeye?.

JE,huu utaratibu ni nani aliyeuanzisha?

Je,makabila yote ya Tanzania hufanya hivi?

Wenzetu mliotembea tembea huko ughaibuni,je hali huwa iko hivi kama huku kwetu.

Unakuta "Mijitu" inaenda misibani kwa ajili ya kula tu,ikishakula hiyoooooo inalala mbele!,hata aibu haioni!,unakuta jitu badala liende hata ndani kusalimia wafiwa lenyewe linakomea getini linapiga msosi halafu linalala mbele!!

HUU UTARATIBU HAUKUBALIKI

#USIPOBADILIKATUTAKUBADILISHA
#TIGHABHATEMWE
Mimi naongelea kwa Upande wa Uislamu
Sheria ya kiislamu inasema wafiwa ndo wanatakiwa wapelekewe chakula kwa muda wa siku 3 na majirani ili kuonesha upendo bcz kwa mda ule wafiwa wanakua kwenye huzuni kubwa na majonzi

Na nyumba ya mfiwa haitakiwi kutoka moshi ndani ya siku hizo 3 kwa mafundisho sahihi kabisaa ya Uislamu.

Uislamu haujaacha kitu ambacho m.damu anakiishi sasa ivi na atakiishi hapo baadae

Ila kuna watu wanafnya mambo kimazoea lkn si kma mafundisho.yasemavyo

Ukienda misiba ya kiislamu usitarajie kwenda kula bali ww nenda ukashiriki kwenye mazishi na urudi kwako au kwenu ukale.

#Dini ya haki#
 
Usipowalisha ndio utajua wamekuja zika au kula. Yaani ni lawama Kila sehemu. Jamaa alifanya kusudi akawalisha wali Chinese na ana uwezo mkubwa wa kupika nyama, hawakumchelewesha walimfuata na kumpaka pale pale kabla ya maziko, ilibidi wengine tuangue kicheko huku pembeni wanalalamika siku nyingine akitulisha majani kama mbuzi hatuji tena
Ungewachapa makofi. Ila kwa vijijini kwetu kule kaskazini magharibi Kuna utofauti kidogo. Ukitokea msiba majirani kwanza wanakuja na chochote immediately. Na Kuna vyama vya kuchangiana, wanamchangia vyakula, mboga na kufanya kazi.
 
Mimi naongelea kwa Upande wa Uislamu
Sheria ya kiislamu inasema wafiwa ndo wanatakiwa wapelekewe chakula kwa muda wa siku 3 na majirani ili kuonesha upendo bcz kwa mda ule wafiwa wanakua kwenye huzuni kubwa na majonzi

Na nyumba ya mfiwa haitakiwi kutoka moshi ndani ya siku hizo 3 kwa mafundisho sahihi kabisaa ya Uislamu.

Uislamu haujaacha kitu ambacho m.damu anakiishi sasa ivi na atakiishi hapo baadae

Ila kuna watu wanafnya mambo kimazoea lkn si kma mafundisho.yasemavyo

Ukienda misiba ya kiislamu usitarajie kwenda kula bali ww nenda ukashiriki kwenye mazishi na urudi kwako au kwenu ukale.

#Dini ya haki#
Msiba ni msiba tu kwa kweli aidha ndugu ama jamaa wasipochangia kuuendesha ama ofisi ya marehemu basi jua tu kuwa wahusika hela itawatoka tu!
 
Na hapo wamekuja rundo hawana hata rambirambi wamefuata nguo za marehemu, nilizigawa kwa hao ndugu na nauli nikawapa.

Mkuu acha tuyaache.

Tamaduni nyingi nu.za.kutupa hata kuchangushana harusini pia si sawa
Daaah mkuu umenena. Mimi sichangii harusi. Za ndugu mpaka huwa naongea kwerikweri.
 
Tuachane na yoooote, kwanini Wali wa kwenye msiba hua mtamu namna ile???? Hua una ladha flani hivi amazing wakikuwekea na Maharage na kachumbari, alooooooo, [emoji39]

Btw, hua sipendi kula Nyama msibani yaani siwezi kabisa.
 
Ungewachapa makofi. Ila kwa vijijini kwetu kule kaskazini magharibi Kuna utofauti kidogo. Ukitokea msiba majirani kwanza wanakuja na chochote immediately. Na Kuna vyama vya kuchangiana, wanamchangia vyakula, mboga na kufanya kazi.
Si mmoja NI wengi na ni watu anafahamiana nao ndio maana wakamwambia ila wengine walilalamika pembeni
 
Kuna baadhi ya vijiji mpaka leo majirani ndio huwa wanapeleka chakula kwa wafiwa...unakuna kila mtu kabeba chochote kitu..hasa mahindi.!
 
Habari za leo wanajamvi? bila shaka mapambano yanaendelea kama kawaida!
Tuendelee kupambana sana na kusaka michuzi kwa udi na uvumba kana kwamba hatufi, na tuendelee kumuomba na kumwabudu Mungu kana kwamba tunakufa kesho!

Kwanza kabisa napenda kutoa masikitiko yangu kama mwananzengo kwa sintofahamu ambayo imeendelea kuikumba jamii ya kitanzania kwa sehemu kubwa kama si yote.

UMUGHAKA nimekuwa nikijiuliza huu utaratibu wa kipumbavu ni nani/akina nani waliyo urasimisha? Kumekuwa na kasumba ambayo sidhani kama nikiita ni upumbavu/ushenzi kama nitakuwa nakosea.

Misiba mingi kama si yote niliyowahi kuhudhuria, nimekua nikiona utaratibu wa wale waliofikwa na msiba ndiyo ambao wanahaha kuwalisha watu ambao wamekuja msibani kutoa pole/kufariji.

Na lazima niwe mkweli ya kwamba,hata sisi kwetu pia tumepata misiba mingi tu ya ndugu zangu na utaratibu huwa ni huo huo!,hili suala limekaaje wapendwa? Yaani unakuta waliofikwa na msiba ndiyo wanaumiza vichwa namna ya kuwalisha wanaokuja kuwafariji badala ya waliokuja kuwafariji wenye matatizo wao ndiyo ilipaswa wakae wakusanyane wananzengo ili kuwalisha waliofikwa na msiba!

Huu utaratibu ni mbovu sana na siungi mkono kabisa! Ni kwanini tusiwe na utaratibu tunapoenda misibani kuwafariji wafiwa kusiwe na utaratibu wa kuwalisha wafiwa pamoja na watakao hudhuria msibani? Yaani unakutwa watu wengi wanaoenda misibani ni kupiga soga tu na kusubiri kunawishwa wakati wa kula huku wanafurahia maisha kana kwamba ni sherehe.

Watu wengi wanaenda misibani si kufariji bali kupiga soga na kula!,huu ndiyo ukweli ukubali au ukatae!

Yaani mtu amefiwa na mpendwa wake halafu bado aumize na kichwa namna ya kuwalisha wananzengo!,hii kitu iko sawa kweli?,hivi hizi nguvu unadhani atakuwa nazo?,hii imepelekea hasa watu wenye kipato cha chini wanabaki kusimangwa na wananzengo hata bila aibu!,unakuta kabisa majirani wanaongea " Msiba wenyewe hata vyakula hauna,naona watu wamechungulia tu wamesusa",kabisa?

Lakini misiba ya watu wenye uwezo utasikia "Jamaa wanapika vyakula vizuri asikwambie mtu,unakula mpaka unasaza".

Hata kama mfiwa anao uwezo,ndiyo alishe wananzengo badala ya wananzengo kumlisha yeye?.

JE,huu utaratibu ni nani aliyeuanzisha?

Je,makabila yote ya Tanzania hufanya hivi?

Wenzetu mliotembea tembea huko ughaibuni,je hali huwa iko hivi kama huku kwetu.

Unakuta "Mijitu" inaenda misibani kwa ajili ya kula tu,ikishakula hiyoooooo inalala mbele!,hata aibu haioni!,unakuta jitu badala liende hata ndani kusalimia wafiwa lenyewe linakomea getini linapiga msosi halafu linalala mbele!!

HUU UTARATIBU HAUKUBALIKI

#USIPOBADILIKATUTAKUBADILISHA
#TIGHABHATEMWE
Wengine wanaomba mpaka nauli ya kuwarudisha makwao
 
Tuachane na yoooote, kwanini Wali wa kwenye msiba hua mtamu namna ile???? Hua una ladha flani hivi amazing wakikuwekea na Maharage na kachumbari, alooooooo, [emoji39]

Btw, hua sipendi kula Nyama msibani yaani siwezi kabisa.
Chakula chochote cha shughulini kina.ladha ya tofauti [emoji3][emoji3], nimeamua nisijiendekeze nikienda kwenye mgao naomba kachumbali tu tena nione ilivyotengenezwa vinginevyo sili nakula kidogo sana labda tonge mbili basi, hiki chakula ukikizoea unaweza kuwa na tabia ya kutafuta maturubai yalipotundikwa ukakunje mguu na kapilipili na ndiziI yako mfukoni [emoji3][emoji3][emoji3]
 
Kila watu na tamaduni zao
Maadamu hawajavunja katiba ya nchi wewe inakuhusu nini?
Kwani utaratibu wa kupokea rambirambi kutoka kwa waombolezaji umeruhusiwa na nani?
 
Msiba ni msiba tu kwa kweli aidha ndugu ama jamaa wasipochangia kuuendesha ama ofisi ya marehemu basi jua tu kuwa wahusika hela itawatoka tu!
Ayo ni mazoea yenu lkn Uislamu ndo unatufundisha ivo
 
Unakuta "Mijitu" inaenda misibani kwa ajili ya kula tu,ikishakula hiyoooooo inalala mbele!,hata aibu haioni!,unakuta jitu badala liende hata ndani kusalimia wafiwa lenyewe linakomea getini linapiga msosi halafu linalala mbele!!
 
Binadamu tumeumbiwa shida ambazo inabidi tukabiliane nazo, na msiba nao ni sherehe ambayo inaambatana na majonzi ndani yake.
Je ni jukumu la nani kulisha wanaouzulia msiba ?
Kumbuka wafiwa wanapewa rambi rambi, pia watu hufika na vyakula mbali mbali , sukari, chumvi, mafuta , blanket na vingine vingi tu kwa ajili ya wafiwa ,
Je wageni utawatoa na njaa, wachimbaji utawatoa na njaa, unajikuta uwezi watoa na njaa inabidi uwapikie baada ya kukufanyia shughuli mbali mbali hapo kwako.
Na siku izi ugali hatutaki tunataka wali.
Ukiona unawachukia wanao kula msibani ujue wewe ni mnyimi
Vingi vya vyakula vinavyoliwa kwenyi baadhi ya misiba(mingi) ni kafara.
Baadhi yavyo ni maelekezo ya kishirikina yaliyoelekezwa kwa wanufaika na kifo cha mhusika.
Sisemi yote ila baadhi. Na katika hii baadhi kama wewe ni mgeni kwani ugeni wako ni mwaliko wa harusini hata uhudumiwe kwa vyakula? Kama kuna ulazima wa kula kwa nini kila mtu asiende na chakula chake?
 
Habari za leo wanajamvi? bila shaka mapambano yanaendelea kama kawaida!
Tuendelee kupambana sana na kusaka michuzi kwa udi na uvumba kana kwamba hatufi, na tuendelee kumuomba na kumwabudu Mungu kana kwamba tunakufa kesho!

Kwanza kabisa napenda kutoa masikitiko yangu kama mwananzengo kwa sintofahamu ambayo imeendelea kuikumba jamii ya kitanzania kwa sehemu kubwa kama si yote.

UMUGHAKA nimekuwa nikijiuliza huu utaratibu wa kipumbavu ni nani/akina nani waliyo urasimisha? Kumekuwa na kasumba ambayo sidhani kama nikiita ni upumbavu/ushenzi kama nitakuwa nakosea.

Misiba mingi kama si yote niliyowahi kuhudhuria, nimekua nikiona utaratibu wa wale waliofikwa na msiba ndiyo ambao wanahaha kuwalisha watu ambao wamekuja msibani kutoa pole/kufariji.

Na lazima niwe mkweli ya kwamba,hata sisi kwetu pia tumepata misiba mingi tu ya ndugu zangu na utaratibu huwa ni huo huo!,hili suala limekaaje wapendwa? Yaani unakuta waliofikwa na msiba ndiyo wanaumiza vichwa namna ya kuwalisha wanaokuja kuwafariji badala ya waliokuja kuwafariji wenye matatizo wao ndiyo ilipaswa wakae wakusanyane wananzengo ili kuwalisha waliofikwa na msiba!

Huu utaratibu ni mbovu sana na siungi mkono kabisa! Ni kwanini tusiwe na utaratibu tunapoenda misibani kuwafariji wafiwa kusiwe na utaratibu wa kuwalisha wafiwa pamoja na watakao hudhuria msibani? Yaani unakutwa watu wengi wanaoenda misibani ni kupiga soga tu na kusubiri kunawishwa wakati wa kula huku wanafurahia maisha kana kwamba ni sherehe.

Watu wengi wanaenda misibani si kufariji bali kupiga soga na kula!,huu ndiyo ukweli ukubali au ukatae!

Yaani mtu amefiwa na mpendwa wake halafu bado aumize na kichwa namna ya kuwalisha wananzengo!,hii kitu iko sawa kweli?,hivi hizi nguvu unadhani atakuwa nazo?,hii imepelekea hasa watu wenye kipato cha chini wanabaki kusimangwa na wananzengo hata bila aibu!,unakuta kabisa majirani wanaongea " Msiba wenyewe hata vyakula hauna,naona watu wamechungulia tu wamesusa",kabisa?

Lakini misiba ya watu wenye uwezo utasikia "Jamaa wanapika vyakula vizuri asikwambie mtu,unakula mpaka unasaza".

Hata kama mfiwa anao uwezo,ndiyo alishe wananzengo badala ya wananzengo kumlisha yeye?.

JE,huu utaratibu ni nani aliyeuanzisha?

Je,makabila yote ya Tanzania hufanya hivi?

Wenzetu mliotembea tembea huko ughaibuni,je hali huwa iko hivi kama huku kwetu.

Unakuta "Mijitu" inaenda misibani kwa ajili ya kula tu,ikishakula hiyoooooo inalala mbele!,hata aibu haioni!,unakuta jitu badala liende hata ndani kusalimia wafiwa lenyewe linakomea getini linapiga msosi halafu linalala mbele!!

HUU UTARATIBU HAUKUBALIKI

#USIPOBADILIKATUTAKUBADILISHA
#TIGHABHATEMWE
Mwanadamu ana sikukuu kuu tatu.
1. Kuzaliwa
2. Kuoa au kuolewa (japo zi wote wanaobahatika kusherehekea sikukuu hii)
3. Kufa
Hivyo chakula ni muhimu kwa sababu ni sikukuu kwa huyo aliyeondoka. Sasa sikukuu unataka nani achangie tena?? ninavyojua watu wanaokuja msibani huwa wanachanga kiasi. Cha maana misiba isiwe ya siku nyingi
 
Back
Top Bottom