Tetesi: Utata mkubwa ripoti ya CAG , kuna uhariri umefanyika

Tetesi: Utata mkubwa ripoti ya CAG , kuna uhariri umefanyika

Kumbe tupo wengi tulioliona hili!? Hawa jamaa mchezo wanaoufanya tunawacheki tu! Lakini mwisho wao utakuwa wa aibu kubwa! Magu atawatesa zaidi akiwa kwenye raha ya milele na mwanga wa milele kuliko alivyowatesa akiwa na mwili wa nyama! Rip our true son of Africa [emoji174][emoji22], rest in power [emoji123] [emoji120] our true African hero! We won't forget your kindness [emoji4]!
Mataga kazi mnayo siyo mchezo
 
achaneni na CAG....mbona hatukusikia awamu ya nne watu wanamlalakia CAG....Utoh alipokuwa anaibua uozo?.....
 
Ulitaka aulizwe nani?
Sio kuulizwa bali nasema tu kuwa viongozi ambao walikuwepo kwenye awamu ya tano ambapo ndio hayo madudu yamefanyika wao wamekaa kimya kana kwamba sio wao, wenyewe wanasisitiza kuwa hii ni awamu ya sita kwahiyo wao hawawajibiki na yaliyotokea awamu ya tano hayo yote ni madudu ya marehemu tu wao wako safi kabisa.
 
Heri kuwa na mwizi anaefanya vitu vya kuonekana!
Deni la taifa ni kubwa mno. Unalijua hilo?. Isitoshe, miradi hiyo itakufa moja baada ya mwingine. Ni ya umma, hakuna usimamizi. Ikifa, deni hili la taifa litalipwa na nini? Dunia nzima sasa hivi serikali haifanyi uzalishaji. Uzalishaji unafanywa na sekta binafsi huku serikali ikikusanya kodi. Sasa magufuli amefanya kinyume. Ameshaiua nchi hii kama alivyokufa yeye.
 
Kwahiyo utagundua wazi kuwa hii report kama imepikwa ili kuweza kuharibu taswira ya jpm

Hapa ndipo ulipoharibu......Huyo Shujaa wenu wa Africa kajiharibia yeye mwenyewe.....Soma Taarifa ya mbowe ...JIWE alikuwa katili na Mwizi.
 
Ni ngumu mno kufuta legacy ya Magu, halafu hii naiona ni bad timing kwao, watu wametoka kwenye maombelezo, halafu ghafla kukatokea na u-turn kama hii?
Kikawaida, watu waliowengi washajua lengo la hiki kikundi nikutaka kumchafua tu, sijui billion ngapi zimepotea, kwendelea zao huko na unafiki wao.
Hivi wewe utawambia nini watu wa Dodoma, mwanza, dar etc kuhusu kazi za JPM? Vituo vya afya, hospital, madaraja, vivuko, miradi mikubwa ya kimkakati you name it, halafu kitokee kikundi kimoja tu kituambie kupitia report ya kinafiki kama hiyo.
Kumpoteza Magu kwenye mioyo ya watz tuliowengi, nkujidanganya tu, watafute kick nyingine siyo hii report uchwara.
Kwani magu ana mpango wa kugombea tena mpaka watu watumie nguvu kumchafua?

Je umewahi kuona report yoyote ya CAG kabla ya hii ya kichere? unafahamu zinafananaje?

Binafsi wewe kwanini unadhani watu wameamua kumchafua magu ikiwa tayari ameshafariki? Mnazungumzia as if amesafiri watu wanatumia kusafiri kwake kumchafua ili akirudi asikubalike, Ni lini mtaelewa kuwa hakuna anayechafuliwa bali wananchi wamepata wasaa wa kusikia yale yaliofichwa gizani kwa miaka 5. Vitu mnavyovikiria pro Magu havipo practically ni hisia zenu tu zinazotokana na hali ya kuwa katika "denial".
 
Tunaendelea na mjadala mzito juu ya yale yaliyotajwa na CAG ni sahihi ,ndivo yalivo au ni mwendelezo wa juhudi za kufa na kupona kupoteza Legacy ya Jpm.

Nikiendelea kufanya utafiti wangu binafsi ,jana nilikitana na taarifa ya CLOUDS media wakitolea ufafanuzi tuhuma za kwamba walilipwa kiasi cha shiling 629.7m bila wao kutoa Risiti.

Katika mjadala huo Clouds walidai kwamba waliposikia taarifa hiyo ikabidi wafuatilie kwenye makabrasha yao wakagundua kwamba risiti walizitoa TRA (AUTOMATIC EFD) na Wizara.

#Hapa ndipo mjadala unaanza ;
1. Kama risiti zimetolewa TRA na Wizarani huko na Clouds wanaujasiri wakusema hilo ,basi kuna uwalakini katika auditing ya kichere kwamba huenda amelishwa matango pori kwa makudi, kwa madhaifu ya watenda kazi au kupangwa.

2. Kama wizarani au TRA hawakumpa kichere risti hizo basi hapo napo kuna shida , kwani hawakumpa? Kuna nia gani nyuma ya pazia? Kwasababu clouds wao wanadai walitoa.Huenda ndio maana hata Kigwangalla anachekelea kwasabab anajua mchezo unaoendelea.

3.Hili suala la risiti imefanyika mwak 2018, Kichere alipaswa kulisema kwenye ripoti ya mwaka jana na si mwaka huu.

Hapa napo kuna tafakuri kubwa , .Report ya Kichere ni ya matumizi ya serikali 2019/2020, suala la risti ni la 2018 ambalo likitakiwa kutajwa 2018/2019 ,ndio maana nina wasiwasi kwamba huenda report hii imeeditiwa na kupachikwa vitu ambavo watu fulani walikusudia kuvionyesha kwa jamii ili watimize yao.

4. Report ya CAG ukiangalia kwa jicho la mbali utagundua imejikita kwenye mambo fulani ambayo mengine ni ya kwelini.

NA ILI UONGO USIJULIKANE KUWA NI UONGO LAZIMA UCHANGANYWE NA UKWELI.

Yaani unaambiwa juu ya stendi ya mbezi ITASABABISHA FOLENI , TENA KWA MIUNDO MBINU ILE ,YA NYEGEZI AMBAYO IPO KATIKATI YA MJI HATUJAAMBIWA KAMA ITASABABISHA FOLENI, DODOMA HATUJAAMBIWA ITASABABISHA FOLENI KISA INAITWA STEND YA MAGUFULI na ndo bora na kubwa kuriko zote, jitihada za kufuta Legacy ya jpm.
Unaambiwa juu ya SGR, yaani unatajiwa SGR imesababisha hasara zaidi ya 3b hatuambiwi imeingiza faida kiasi gani , mashaka matupu, nilitegemea atuambie na upande wa pili imeingizia faida kiasi gani.

Kwahiyo utagundua wazi kuwa hii report kama imepikwa ili kuweza kuharibu taswira ya jpm

5.Kuna taarifa ya siri kwamba report hii tayari ilikuwa imeshaandaliwa na CAG lakini kuanzia trh 18.3.2021 ,ilianza kufanyiwa editing ,kwa maelekezo/maagizo kutoka juu.
Ingawa taarifa hizi si rasimi lakini ninaweza kuziamini.

-Cag alianza kwa kutoa taarifa nusu ,akagusia suala la ndege watu wakaibuka na kulaumu ,ndege imekula hasara ya 60b ,wakajitokeza watetezi na kusema hio mbona hasara ndogo, ikawa imeisha.
Kama iliandaliwa tangu mwaka jana ,kwanini alitoa taarifa nusu? Au tuseme editing ilikuwa haijakamilika?
-Kama watu wanasema haya yanatokea kwasababu jpm hakutaka kukosolewa ,tujiuliza hii report imeandaliwa lini ? Wakati au baada ya kifo cha jpm? Kama ni kabla ya jpm ,basi tukubali kuna editing ya taarifa kwa maana jpm asingeikubali(kutokana na hoja zenu kuwa hakutaka kukosolewa).
Kama ilieditiwa kwa maagizo ya nani ? Kwamakusudi gani?

KAMA HATUKUSIKIA HIZO HASARA ZA NDEGE MWAKA JANA , LEO HII TENA MUDA MFUPI KWAMBA ZIMESABABISHA HASARA ,KUNA MASHAKA MAKUBWA.
Nataka kusema kwamba Huenda kichere na timu yake kwa maagizo toka juu alichambua MIRADI ILIYOKUWA INAMPAISHA JPM Na kuweka figisu ilimradi kuonyesha haifai , alikulupuka au alipiga hela kutimiza matakwa ya hao walioko juu.
#Kama ni maagizo ya kikwete ,basi ili kutimiza lengo lake kuanzisha mfumo wake wa ponda mali kifo kinakuja.
#Kama ni Samia ni kutaka kufuta kivuli cha jpm kwenye uongozi wake , yaani yeye si kama jpm ,yeye ni bora zaidi.

MWISHO
JPM aliwahi kusema "ukiona adui yako anakushangilia sana rudi nyuma ujiulize umekosea wapi"

NAONA GIZA NENE MBELE YA URAIS WA SSH, NAONA NCHI INARUDI KWENYE KIKWETISM .NAONA MIKATABA MIPYA YA MADINI ,MIKATABA MIPYA BOMBA LA KUTOKA TANGA HADI HOIMA.

LAKINI YOTE KATI YOTE NASEMA KWAMBA " WANANCHI WENGI HASA WANACCM WANAIMANI KUBWA NA JPM NA WAKO TYR KUSIMAMA NAYE MPKA MWISHO".
UPEPO HUU UTAPITA , REPORT ZITASOMWA ZITATAJWA HASARA ZA MABILIONI WATU WATASHANGILIA ,MWISHO WATU WATASAHAU LAKINI MIRADI ALIYOIANZISHA JPM ITADUMU VIZAZI HADI VIZAZI.

Asilimia kubwa ya wanaccm hivi sasa hawana imani tena na SSH ,WENGI WAKO KIMYA ILA WANAJUA WATAFANYA NINI .
Yaani asilolijua SSH na wenzake watu wengi wanamkubali JPM kuriko hata ccm, wapinzani wengi kama kafulila wanamkubali JPM kuriko ccm.Wengi wanaomshangilia ni wa upinzani ambao nao wanamtumia tu.

ASANTE JOHN
toa huu uchafu
 
😂😂😂 mleta uzi kaniacha hoi hapo anaposema SGR imetengeneza hasara ya 3B sasa anauliza kwanini hawasemi faida iliyotengenezwa, jama jama kuna hasara sasa faida inatoka wapi, sasa hiyo faida si wangeitumia kucover hiyo hasara ndugu yangu.
 
Nilivyosoma hapo uliposema kuwa mnaambiwa SGR inatengeneza hasara ya 3B na hamjaambiwa faida nikaamua nipuuze hili bandiko.

Hivi mleta mada maboss zako wakiona huu utetezi watakulipa kweli? Huko Matagani hakuna mwenye akili timamu anayeweza walau kupangua hoja? Jibu ni kuwa hoja za CAG hazipanguliki, mnagusa gusa tu mnaishia kutuletea viroja.
 
Jamani ndugu zangu Wasukuma.. Kubalini ukweli kwamba Meko Kafa.. Jamani Meko Kafa.. Yaani Kafa. Hawezi rudii.. Mbona Hamuaminii? Naona design kama Hamtaki kukubali.. Mlitaka awe Raisi wa malaika? Basi yeye Meko kakataa.. anataka awe Kiranja Kule aliko. Japo baada ya report ya CAG amevuliwa Ukiranja wake.
 
Kwani magu ana mpango wa kugombea tena mpaka watu watumie nguvu kumchafua?

Je umewahi kuona report yoyote ya CAG kabla ya hii ya kichere? unafahamu zinafananaje?

Binafsi wewe kwanini unadhani watu wameamua kumchafua magu ikiwa tayari ameshafariki? Mnazungumzia as if amesafiri watu wanatumia kusafiri kwake kumchafua ili akirudi asikubalike, Ni lini mtaelewa kuwa hakuna anayechafuliwa bali wananchi wamepata wasaa wa kusikia yale yaliofichwa gizani kwa miaka 5. Vitu mnavyovikiria pro Magu havipo practically ni hisia zenu tu zinazotokana na hali ya kuwa katika "denial".
Wenye akili wanajua kua ukiona unapambana na legacy, Basi kunajambo lisilo la kheri linakuja.
Haiwezekani upambane na marehemu!!
Si Alisha kua marehemu hana madhara? Fanta yako yaonekane, watu wakukubali!
Shida ni kua marehemu kaacha viatu vikubwa mno na warithi Wana pima upepo.

Ccm achaneni na Ilani yenu ya uchaguzi na iueni miradi mkakati alio ianzisha Marehem halafu njooni mpambane na nguvu ya walalahoi ambao sikuhizi Wana smart phone.

Naamini hizi ni ngonjera tu Ila legacy ya JPM itamalaki.

Nahisi ccm na TISS wanawaingiza chaka Wapinzani ili kujenga umoja wa kitaifa.

Or otherwise, kunakaburi la ccm linachimbwa.
My own mtazamo(views)
 
Jamani ndugu zangu Wasukuma.. Kubalini ukweli kwamba Meko Kafa.. Jamani Meko Kafa.. Yaani Kafa. Hawezi rudii.. Mbona Hamuaminii? Naona design kama Hamtaki kukubali.. Mlitaka awe Raisi wa malaika? Basi yeye Meko kakataa.. anataka awe Kiranja Kule aliko. Japo baada ya report ya CAG amevuliwa Ukiranja wake.

Ilo ndio linalowaumiza kichwa ,hawaamini kabisa kwamba MEKO KAKATA KAMBA aka KANG'ATA SHUKA.
 
Nilivyosoma hapo uliposema kuwa mnaambiwa SGR inatengeneza hasara ya 3B na hamjaambiwa faida nikaamua nipuuze hili bandiko.

Hivi mleta mada maboss zako wakiona huu utetezi watakulipa kweli? Huko Matagani hakuna mwenye akili timamu anayeweza walau kupangua hoja? Jibu ni kuwa hoja za CAG hazipanguliki, mnagusa gusa tu mnaishia kutuletea viroja.
😂😂 Kiukweli hawana hoja za kumpinga CAG kabisa. Na hii inasababishwa na ukosefu wa data na taarifa sahihi, wanakosoa ripoti kwa kuchomoa taarifa kutoka kwenye hiyohiyo ripoti halafu wanapinga kijanja janja ili kujifariji.

Waipinge kwa kuleta taarifa zao ambazo ni sahihi sio kusema tu sio sahihi na kilichosahihi hamleti.

Mkuu huyu leo atajua atakapokula hapati mgao huyu kajiharibia mwenyewe😂😂
 
Nataka uniambie mwaka ambao CAG ,hakuona madudu sehem yoyote ktk hii nchi,alaf ndio urud uniambie CAG uyu amepewa maelezo kutoka juu

"3.Hili suala la risiti imefanyika mwak 2018, Kichere alipaswa kulisema kwenye ripoti ya mwaka jana na si mwaka huu.



Hapa napo kuna tafakuri kubwa , .Report ya Kichere ni ya matumizi ya serikali 2019/2020, suala la risti ni la 2018 ambalo likitakiwa kutajwa 2018/2019 ,ndio maana nina wasiwasi kwamba huenda report hii imeeditiwa na kupachikwa vitu ambavo watu fulani walikusudia kuvionyesha kwa jamii ili watimize yao.
"
 
Ni ujinga mtupu tu, ina maana CAG hakufanya ukaguzi ofisi ya makamu wa rais? Au huko hakuna madudu? Mungu hafanyiwi unafiki muda utaongea, CAG mwenyewe sura mbaaaya.
 
Wenye akili wanajua kua ukiona unapambana na legacy, Basi kunajambo lisilo la kheri linakuja.
Haiwezekani upambane na marehemu!!
Si Alisha kua marehemu hana madhara? Fanta yako yaonekane, watu wakukubali!
Shida ni kua marehemu kaacha viatu vikubwa mno na warithi Wana pima upepo.

Ccm achaneni na Ilani yenu ya uchaguzi na iueni miradi mkakati alio ianzisha Marehem halafu njooni mpambane na nguvu ya walalahoi ambao sikuhizi Wana smart phone.

Naamini hizi ni ngonjera tu Ila legacy ya JPM itamalaki.

Nahisi ccm na TISS wanawaingiza chaka Wapinzani ili kujenga umoja wa kitaifa.

Or otherwise, kunakaburi la ccm linachimbwa.
My own mtazamo(views)
"Wenye akili" akina nani mataga? Na mimi nikikwambia "wenye akili" wanafahamu hakuna anayepambana na Hayati bali uhuru wa kutoa maoni ambao umepelekea hata report ya CAG kusoma na kuchambuliwa hadharani ndio yameleta haya utanibishia? Ni kipimo kipi kinaonesha ni wapi wenye akili kati ya ninaowazungumzia mimi na unaowazungumzia wewe.

FYI, Hayati hakuwa anatekeleza ilani ya chama, alikuwa na ilani yake kichwani.
 
Back
Top Bottom