Utata wa Kifo Cha Hayati Sokoine

Utata wa Kifo Cha Hayati Sokoine

Una uwezo wa kupekua jambo likapekulika wewe?

Kuna vigezo vingi sana na inategemea mazingira nani anapekuliwa na anapekuliwa na nani na kitu gani kinapekuliwa. Haimzuii LiverpoolFC au mtu mwingine yeyote kupekua jambo, na hata kama halitapekulika haifanyi unachokisema wewe kiwe sahihi au watu waamini hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Chinga one mimi nakumegea yale ambayo ninayafahamu. Sokoine alikuwa anatokea Dodoma kurejea Dar baada ya kumalizika kwa kikao cha Bunge. Msafara wake ulipofika eneo la Wami Sokoine mkoani Morogoro, jirani na palipojengwa makao makuu ya sasa ya Wilaya ya Mvomero, gari yake ilipata ajali kwa kugongwa na gari L/cruiser iliyokuwa inaendeshwa na Mkimbizi raia wa Afrika ya kusini anaitwa Dumisani Dube aliyekuwa anaishi kwenye Kambi ya wanachama wa ANC hapo Dakawa. Dumisani alishitakiwa mahakamani lakini ninadhani kwa sababu za kisiasa zaidi, mahakama ilimwachia na alirudishwa kwao Afrika ya Kusini. Ajali hiyo ilitokea mchana na Sokoine alipofikishwa Hospitali ya mkoa wa Morogoro, madaktari walithibitisha kifo chake. Miaka kumi baada ya kifo chache, Daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Sokoine baada ya kifo, aliweka wazi taarifa ya chanzo cha kifo chake. Sehemu ya taarifa hiyo ilisema kuwa baada ya ajali, Sokoine alivunjika shingo ambayo ilisababisha kubana mshipa wa fahamu (spinal cord) ambayo ilikata mawasiliano kati ya ubongo na sehemu nyingine za mwili. Kumbuka Nyerere na Karume walikuwa maraisi wa nchi, Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na raisi wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, pia waasisi wa mataifa haya, hivyo tunawaenzi kwa sababu hizo kuu tofauti na Sokoine aliyekuwa Waziri mkuu. Mahali alipopatia ajali Sokoine pamejengwa mnara wa kumbukumbu. NINAWASILISHA.
 
Chinga one mimi nakumegea yale ambayo ninayafahamu. Sokoine alikuwa anatokea Dodoma kurejea Dar baada ya kumalizika kwa kikao cha Bunge. Msafara wake ulipofika eneo la Wami Sokoine mkoani Morogoro, jirani na palipojengwa makao makuu ya sasa ya Wilaya ya Mvomero, gari yake ilipata ajali kwa kugongwa na gari L/cruiser iliyokuwa inaendeshwa na Mkimbizi raia wa Afrika ya kusini anaitwa Dumisani Dube aliyekuwa anaishi kwenye Kambi ya wanachama wa ANC hapo Dakawa. Dumisani alishitakiwa mahakamani lakini ninadhani kwa sababu za kisiasa zaidi, mahakama ilimwachia na alirudishwa kwao Afrika ya Kusini. Ajali hiyo ilitokea mchana na Sokoine alipofikishwa Hospitali ya mkoa wa Morogoro, madaktari walithibitisha kifo chake. Miaka kumi baada ya kifo chache, Daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Sokoine baada ya kifo, aliweka wazi taarifa ya chanzo cha kifo chake. Sehemu ya taarifa hiyo ilisema kuwa baada ya ajali, Sokoine alivunjika shingo ambayo ilisababisha kubana mshipa wa fahamu (spinal cord) ambayo ilikata mawasiliano kati ya ubongo na sehemu nyingine za mwili. Kumbuka Nyerere na Karume walikuwa maraisi wa nchi, Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na raisi wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, pia waasisi wa mataifa haya, hivyo tunawaenzi kwa sababu hizo kuu tofauti na Sokoine aliyekuwa Waziri mkuu. Mahali alipopatia ajali Sokoine pamejengwa mnara wa kumbukumbu. NINAWASILISHA.

Shukrani mkuu, wengine wanasema daktari aliye ufanyia postimatamu mwili wa sokoine alisema kua mwili ulikuwa na tundu la risasi mgongoni pia hakuna ndugu wa marehemu aliye ruhusiwa kushiriki kuuandaa mwili wa marehemu,nazidi kuchanganyikiwa hapa.
 
Mimi binafsi kila nikifuatilia movie hii huwa inaniuma sana, yaani unalia kabisaaaaaaa, yaani hii movie ni kama ya Titanic ambayo stering anauwawa.
Kila nkisoma habari za hii movie huwa nakumbuka msemo huu, "Tanzania has lost a rightful hair"
Swali moja nmelipenda can we handle the truth?, kwa wakati ule nadhani isingewezekana.

Na ukizingatia kipindi kile cha utawala wa mwalimu ilikua kuhoji mamlaka ni mwiko.
 
nikiwa mdogo nilisikia tetesi kwamba kuna mganga wa kisangoma anataka kumrudisha Sokoine kwani alisema bado hajaharibwa huko aliko !! lakini uongozi wa juu wa nchi akiwemo baba wa taifa wakasema itakuwa aibu kwa dunia - maana ametangazwa amefariki tena aibuke mzima tutaonekana vipo sisi watanzania!!

Pia nilisikia toka wa wazee kwamba Prof. Shaba wakati ule pale Mifupa Moi ndiyo alimfanyia postmortem - kama bado anaishi anaweza kutujuza kwamba ilikuwaje kuwaje riport yake original kutotolewa mpaka leo; hata familia hawajawahi kuiona
 
Kuna mwanaye wa kiume wa kwanza kama sijakosea alinukuliwa kutaka kufungua kesi mahakamani ili kupata kibali ya kufanya postmortem upya mwili wa baba yake!! Sheria zinasema unaweza kuruhusiwa kufanya hivyo miaka 20 baada ya mazishi - hii nayo imekaaje ? hebu tufafanulieni.
 
nikiwa mdogo nilisikia tetesi kwamba kuna mganga wa kisangoma anataka kumrudisha Sokoine kwani alisema bado hajaharibwa huko aliko !! lakini uongozi wa juu wa nchi akiwemo baba wa taifa wakasema itakuwa aibu kwa dunia - maana ametangazwa amefariki tena aibuke mzima tutaonekana vipo sisi watanzania!!

Pia nilisikia toka wa wazee kwamba Prof. Shaba wakati ule pale Mifupa Moi ndiyo alimfanyia postmortem - kama bado anaishi anaweza kutujuza kwamba ilikuwaje kuwaje riport yake original kutotolewa mpaka leo; hata familia hawajawahi kuiona

Duuh hii nayo kali aisee kwa hiyo kachukuliwa msukule? ha ha ha!
 
Nilikuwa drs la 1 shule ya msingi mtoni kwa mama mary, taarifa hizi nilizupata wakati nacheza na wenzangu wakati wa mapumziko ys saa nne...RIP sokoine, magamba si watu wema
 
Chinga one mimi nakumegea yale ambayo ninayafahamu. Sokoine alikuwa anatokea Dodoma kurejea Dar baada ya kumalizika kwa kikao cha Bunge. Msafara wake ulipofika eneo la Wami Sokoine mkoani Morogoro, jirani na palipojengwa makao makuu ya sasa ya Wilaya ya Mvomero, gari yake ilipata ajali kwa kugongwa na gari L/cruiser iliyokuwa inaendeshwa na Mkimbizi raia wa Afrika ya kusini anaitwa Dumisani Dube aliyekuwa anaishi kwenye Kambi ya wanachama wa ANC hapo Dakawa. Dumisani alishitakiwa mahakamani lakini ninadhani kwa sababu za kisiasa zaidi, mahakama ilimwachia na alirudishwa kwao Afrika ya Kusini. Ajali hiyo ilitokea mchana na Sokoine alipofikishwa Hospitali ya mkoa wa Morogoro, madaktari walithibitisha kifo chake. Miaka kumi baada ya kifo chache, Daktari aliyeufanyia uchunguzi mwili wa Sokoine baada ya kifo, aliweka wazi taarifa ya chanzo cha kifo chake. Sehemu ya taarifa hiyo ilisema kuwa baada ya ajali, Sokoine alivunjika shingo ambayo ilisababisha kubana mshipa wa fahamu (spinal cord) ambayo ilikata mawasiliano kati ya ubongo na sehemu nyingine za mwili. Kumbuka Nyerere na Karume walikuwa maraisi wa nchi, Jamuhuri ya muungano wa Tanzania na raisi wa serikali ya mapinduzi ya Zanzibar, pia waasisi wa mataifa haya, hivyo tunawaenzi kwa sababu hizo kuu tofauti na Sokoine aliyekuwa Waziri mkuu. Mahali alipopatia ajali Sokoine pamejengwa mnara wa kumbukumbu. NINAWASILISHA.

Mh mkuu there you are hebu funguka zaidi hapo kwenye bold. Shingo ilivunjikaje baada ya ajali kutokea na sio kuvunjika kutokana na ajali yenyewe? Au ilivunjwa na wajeda waliombeba kwenye helicopter kumpeleka hospitali? Maana mwandishi wake wa habari Acadoga Chiledi inasemekana aliwahi kusema kuwa Mh. Sokoine alitoka kwenye ajali akiwa hai kabisa. TARATIBU UKWELI UTAJULIKANA TU HATA KAMA ITACHUKUA MIAKA 100.
 
Mh mkuu there you are hebu funguka zaidi hapo kwenye bold. Shingo ilivunjikaje baada ya ajali kutokea na sio kuvunjika kutokana na ajali yenyewe? Au ilivunjwa na wajeda waliombeba kwenye helicopter kumpeleka hospitali? Maana mwandishi wake wa habari Acadoga Chiledi inasemekana aliwahi kusema kuwa Mh. Sokoine alitoka kwenye ajali akiwa hai kabisa. TARATIBU UKWELI UTAJULIKANA TU HATA KAMA ITACHUKUA MIAKA 100.

Mkuu, labda lugha imegongana kidogo tu kwa vile wengine hatuna ujuzi wa kuandika lugha zinazokidhi mahitaji ya kisheria. Tuliaminishwa na watoa taarifa kuwa ajali ndiyo iliyosababisha kuvunjika shingo. Nadhani Acadoga Chiledi bado yuko hai anaweza kutujuza vinginevyo au tunukuu vyombo vya habari vilivyomnukuu huyo Chiledi. Mimi sikuwa shuhuda wa ajali hiyo.
 
Harooo usin'tanie!! Ina maana Mzee Kizota long time alikuwa Mjeda yule? Sa' yale manyama manyama aliyonayo na mengine yaliyojazana sehemu ya kukalia yametoka wapi yale? Au anaumwa?

NAAM! Yaani kionjo chenye kuifanya thread hii iwe na mvuto zaidi ndio hiyo issue ya huyo Mzee Kizota, kama ni kweli!

 
E. Sokoine.jpg
 
Pichani ni gari lililosababisha kifo cha aliyekuwa waziri mkuu wa Tanzania Mhe:Edward Moringe Sokoine mnamo Tar 12 Mwezi 04 Mwaka 1984 wakati akitokea kwenye kikao cha Bunge mjini Dodoma kwenda jijini Dar – Es – Salaam

sokoine.jpg



Hiyo gari aliyopata nayo ajali sokoine imehifadhiwa makumbusho au wapi?

Mkuu unataka kuja kupiga nayo picha? Ipo...
 
Nilikuwa drs la 1 shule ya msingi mtoni kwa mama mary, taarifa hizi nilizupata wakati nacheza na wenzangu wakati wa mapumziko ys saa nne...RIP sokoine, magamba si watu wema

Mkuu Head teacher, umenikumbusha. Mimi nilikuwa darasa la 5, shule ya msingi Katwe, kule Karagwe - Kagera. Pia siku hiyo tulikuwa na ugeni shuleni wa viongozi wa CCM kutoka mkoani, namkumbuka Mzee Pius Ngeze (Mwenyekiti wa mkoa) na Bonifas Njohole ambaye alikuwa katibu wa CCM mkoa wa Kagera. Yaani enzi hizo viongozi wa CCM mkoa walikuwa na nguvu kuliko mkuu wa mkoa. Habari za msiba zilijulikana mida ya saana 7 mpaka 8, hakika yalikuwa ni majonzi makubwa sana.
 
Mkuu, labda lugha imegongana kidogo tu kwa vile wengine hatuna ujuzi wa kuandika lugha zinazokidhi mahitaji ya kisheria. Tuliaminishwa na watoa taarifa kuwa ajali ndiyo iliyosababisha kuvunjika shingo. Nadhani Acadoga Chiledi bado yuko hai anaweza kutujuza vinginevyo au tunukuu vyombo vya habari vilivyomnukuu huyo Chiledi. Mimi sikuwa shuhuda wa ajali hiyo.

Hapana mkuu Shakidinkili, Mzee Acadoga Paul Chiledi aliishatangulia mbele ya haki miaka kadhaa iliyopita na alizikwa kwenye makaburi ya Kinondoni. Lakini kama kweli kulikuwa na conspiracy yoyote katika kifo kile hata Marehemu Chiledi asingeweza kusema waziwazi kwani naye angemalizwa.
 
kwa kifupi kifo cha Sokoine kilipangwa kitaalam kuliko wengi tujuavyo. Sokoine alipigwa lisasi kwanza ndo akagongwa na gari ili kupoteza ushahidi....hata uchunguzi wa dactari ulithibitisha kuwa mwili ulikuwa na tobo ya lisasi, na alivytaka kutoa taarifa akafungwa mdomo, vinginevyo na yeye angemalizwa. Hizi habari huwezi zipata kwa vitabu wala aticles

Ndio sawasawa kabisa alikuwa ni Dr Shaba maana alisema wazi kabisa kwamba kutokana na miiko ya kazi alitakiwa aandike chanzo cha kifo, lakini akapigwapigwa danadana na akaishia kuzuiwa pale Ocean Road.

Dr Shaba aliishia kuwa na maisha ya ajabu ajabu tu.

Nchi hii ina vituko vingivingi tu, na wewe Chinga 1 ni mdogo sana kuweza kuchimba haya.
 
Ndio sawasawa kabisa alikuwa ni Dr Shaba maana alisema wazi kabisa kwamba kutokana na miiko ya kazi alitakiwa aandike chanzo cha kifo, lakini akapigwapigwa danadana na akaishia kuzuiwa pale Ocean Road.

Dr Shaba aliishia kuwa na maisha ya ajabu ajabu tu.

Nchi hii ina vituko vingivingi tu, na wewe Chinga 1 ni mdogo sana kuweza kuchimba haya.

Mkuu mbona unanitishia tena? nina haki ya kutaka kujua mambo haya muhimu ukizingatia mi ni mwalimu wa masomo yanayo landana na matukio ya nchi yetu.
 
Mkuu mbona unanitishia tena? nina haki ya kutaka kujua mambo haya muhimu ukizingatia mi ni mwalimu wa masomo yanayo landana na matukio ya nchi yetu.

La hasha mkuu,

Najaribu kusema tu kwamba hli suala lilikuwa halielezeki si kwa wanafamilia tu bali nchi nzima.

Kuna mambo mengi ambayo hakuna atakaeweka wazi bali ni hadithi tu.
 
Back
Top Bottom