Utata wa Kifo Cha Hayati Sokoine

Utata wa Kifo Cha Hayati Sokoine

Waulize Dr Kashimba alie na Siri aina ya majeraha ambayo hata Familia ilikataliwa kuona, pia Muulize Mzee Kizota yule mwenye Bar viwanja vya Saba Saba, alikuwa bodi gadi yake, wakimbizi waliokuwepo maeneo ya karibu na ajali wanadai kuona bodi gadi huyo akifyatua risasi, muda mfupi tu baada ya mheshimiwa kutoka nje ta gari kujaribu kukimbia. Muulize Mwalimu Nyerere aliekuwa Rahisi wa Tanzania

Bila shaka maelezo yako ni majibu tosha juu ya mauaji ya mpendwa wetu na kijana mahiri wa kimasai
 
Asante kwa picha lakini bado hizo picha hazijibu maswali mengi,ukiangalia vizuri hayo maswali yote yame base kwenye kupata reality kwa mfano taarifa ya polisi inasemaje? lazima kulifanyika uxhunguzi wa kina kubaini chanzo cha ajali hiyo kama unafanywa uchunguzi kwa ajali za watu wa kawaida itakua kwa waziri mkuu?

Taarifa za Polisi inaweza kuwa tofauti na hali halisi uliyopewa? Jaribu kuwasiliana n Polisi maana kuna mtu alikamatwa na kushtakiwa kwa kosa hilo.
 
Asante kwa picha lakini bado hizo picha hazijibu maswali mengi,ukiangalia vizuri hayo maswali yote yame base kwenye kupata reality kwa mfano taarifa ya polisi inasemaje? lazima kulifanyika uxhunguzi wa kina kubaini chanzo cha ajali hiyo kama unafanywa uchunguzi kwa ajali za watu wa kawaida itakua kwa waziri mkuu?

Ili iweje?
Vitu vingine ni state matters kwamba ajali yake ilipangwa ama ilikuwa ajali ya kawaida haibadilishi dhana kwamba alikufa!
 
Ila ukweli kabiiisa tu ni kwamba hiki kifo cha SOKOINE kilikuwa na mikono ya watu siyo bure.Haiwezekani wanafamilia wakataliwe hata ile kuuosha tu mwili wa MAREHEMU kama vile hakuwa ndugu yao.CCM hii tabia ya kuuana wameianza kitambo saaana na watanzania wanajua kila mauaji yaliyokuwa yakifanywa na hawa wenzetu ila mikwara iliyokuwa inapigwa na government hapo nyuma iliwafanya watu wasihoji chochote juu ya maovu yaliyokuwa yakifanywa.
 
Nakumbuka ilikuwa ni jumapili ya tarehe 15 April 1984 nikiwa Arusha. tulikuwa kanisani kwenye ibada ya jumapili katika kanisa lilo kando ya barabara ya uhuru ( kwasasa karibu na shoprite) waumini wote tulitoka nje ya kanisa kuangalia mwili wa Sokoine ukipitishwa kuelekea Munduli kwa Maziko, nakumbuka jinsi watu walivyokuwa na simanzi wakati huo


Mkubwa nakwambia umenikumbusha kitu gani tena? Usinilize Mkubwa! Nakumbuka kabisa mvua kubwa ilinyesha pasipo kukatika takrban masaa 7 na RTD enzi hiyo ambayo leo ndiyo TBC ikitangaza moja kwa moja mazishi yake!
Nilikuwa mdogo sana kwani nilikuwa darasa la kwanza ila nilikuja barabarani kuomboleza kifo ya shujaa huyo wa Tanzania mzalendo wa Nchi yetu!
Nakumbuka kabisa wanakijiji wote wababa kwa wamama walijitokeza barabarani na huku vijana karibu wengi wa kabla lake (Maasai) Morani wakiumiza miili yao kwa mori siku hiyo ya mazishi nilikuwa mdogo lakini sitokaa nikasahau msiba huu mchungu kwa Watanzania walio wengi kwa JEMBE huyo Marehemu Edward Moringe Sokoine.
Mwenyenzi MUNGU mwingi wa Rehema na ampe pumziko la milele shambani mwake Bwana wetu!

Ameeen!
 
nakumbuka ilikuwa ni jumapili ya tarehe 15 april 1984 nikiwa arusha. Tulikuwa kanisani kwenye ibada ya jumapili katika kanisa lilo kando ya barabara ya uhuru ( kwasasa karibu na shoprite) waumini wote tulitoka nje ya kanisa kuangalia mwili wa sokoine ukipitishwa kuelekea munduli kwa maziko, nakumbuka jinsi watu walivyokuwa na simanzi wakati huo

mwili wake ulikuwa ktk land rover pick up,jeneza lilipambwa na mauwa ya kutosha na mbele yake iliwekwa picha yake kubwa...black and white .....rtd nyimbo za maombolezo zilipigwa......
 
Waulize Dr Kashimba alie na Siri aina ya majeraha ambayo hata Familia ilikataliwa kuona, pia Muulize Mzee Kizota yule mwenye Bar viwanja vya Saba Saba, alikuwa bodi gadi yake, wakimbizi waliokuwepo maeneo ya karibu na ajali wanadai kuona bodi gadi huyo akifyatua risasi, muda mfupi tu baada ya mheshimiwa kutoka nje ta gari kujaribu kukimbia. Muulize Mwalimu Nyerere aliekuwa Rahisi wa Tanzania
nilikua bado mdogo sana,ila nakumbuka kipindi wanatangaza ndo nilikua natoka RTC kununua sukari ,ndo nikasikia ulikua mshituko na hudhuni sana tulifuatilia mazishi live kupitia RTD.

Kisha nikiwa sec miaka ya 90 tukawa na urafiki na mtoto wa mmoja wa mkuu wa majeshi ambae pia kwao ni butiama karibu kabisa na kwa jk,akawa anatuambia ni siri kubwa ila mwili wa sokoine ulikutwa na jeraha la risasi mgongoni.
Ila sikuwahi kuamini asee.
 
Ila ukweli kabiiisa tu ni kwamba hiki kifo cha SOKOINE kilikuwa na mikono ya watu siyo bure.Haiwezekani wanafamilia wakataliwe hata ile kuuosha tu mwili wa MAREHEMU kama vile hakuwa ndugu yao.CCM hii tabia ya kuuana wameianza kitambo saaana na watanzania wanajua kila mauaji yaliyokuwa yakifanywa na hawa wenzetu ila mikwara iliyokuwa inapigwa na government hapo nyuma iliwafanya watu wasihoji chochote juu ya maovu yaliyokuwa yakifanywa.


Naunga hoja yako mkono IKINGO. Hili ccm ilihusika moja kwa moja.

Ni swali. Mwaka huo 1984 Edward Lowassa alikuwa wapi ndani ya serikali hii?
 
Last edited by a moderator:
Pichani ni gari lililosababisha kifo cha aliyekuwa waziri mkuu wa Tanzania Mhe:Edward Moringe Sokoine mnamo Tar 12 Mwezi 04 Mwaka 1984 wakati akitokea kwenye kikao cha Bunge mjini Dodoma kwenda jijini Dar – Es – Salaam

sokoine.jpg


Picha hapo chini ikimuonyesha Baba wa Taifa ambaye naye ni marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere akilia kwa uchungu baada ya kuona mwili wa aliyekuwa rafiki yake kipenzi Waziri Edward Sokoine ukiwa umelala milele.

soko.jpg


Sokoine alifariki kwa ajali ya gari Jumatano ya Aprili 12, 1984 saa 11:30 jioni wakati akitoka kwenye kikao cha bunge Dodoma kuelekea Dar es Salaam
Mwili wa Edward Moringe Sokoine ulizikwa nyumbani kwao Monduli, mkoani Arusha!
Hayo mengine ni maswali ya hisia tu ambayo kila mwenye hisia zake moyoni hana budi kujiuliza bt all in all apumzike kwa amani milele!


Hiyo green,Ilikuwa siku ya alhamisi saa 7:15 mchana
 
1.Itasaidia nn ukijua leo au unajifunza mbinu mbali mbali za assasination na unajaribu kuvuta theory ipi ili apply.
2.Kama ni ajari ya gari moja tu picha inaonyesha kuwa iligongwa upande wa dereva. Na ni benzi ngumu upande wake yeye aliumiaje kama sio kazi maalum.
3. kumbu kumbu za mahakamni zinaonyesha vp kuhusu debi sijui aliachiwa kwa ground zipi?maana ulikuwa ni msafara na unajulikana gari ipi ni ya waziri mkuu.

Na kama princense Diana alikufa mbele ya makamera na bodyguard si ajabu kama wao wazungu walijifunzia kwetu maana hii ndio TZ ilianza .
5.Kaka zangu walio nizid umri na waliokuwa wanaishi upanga na uhindin kisutu wanadai miaka ile wahindi walikuwa wanaacha mipesa bara barani mnapita mnaokota.
6.Na BOT iliungua mwaka 1984 na mwaka huo huo jk alitangaza kung'atuka sababu aliona usalit wa serikali yake kutoka kwa watu anaowategemea sana.
 
Official version ni kwamba Sokoine alifariki Aprili 12, 1984 Dumila, mkoani Morogoro, baada ya gari lake kugongana na Toyota Land Cruiser pickup (kama hiyo hapo chini) iliyokuwa ikiendeshwa na mkimbizi kutoka Afrika Kusini Dumisani Dube. Mwanachama huyo wa ANC alifikishwa mahakamani akikabiliwa na shtaka la kusababisha kifo kwa uendeshaji hatari, lakini baadae aliachiwa huru.

005.jpg

Siyo Dumila bali jirani na Dakawa(kijiji cha Luhindo). Pamejengwa kumbukumbu ku muenzi.
 
Asante kwa picha lakini bado hizo picha hazijibu maswali mengi,ukiangalia vizuri hayo maswali yote yame base kwenye kupata reality kwa mfano taarifa ya polisi inasemaje? lazima kulifanyika uxhunguzi wa kina kubaini chanzo cha ajali hiyo kama unafanywa uchunguzi kwa ajali za watu wa kawaida itakua kwa waziri mkuu?

RPC wa Morogoro wawakati huo,alipigiwa sim kutoka makoa makuu dakaki kadhaa baada ya tukio kuulizwa kama anajua kinachoendelea(hali ya usalama),binafsi hakuwa na taarifa yoyote mpaka baadae alipokuja kutaarifiwa na vijana wake kuwa waziri mkuu kafariki katika ajali..Utata pia
 
Back
Top Bottom