Utawala wa Rais Mwinyi ulileta neno "Mheshimiwa" badala ya "ndugu" kwa viongozi na sasa wamekuwa tabaka lenye kujiona wako juu ya Watanzania wengine!

Utawala wa Rais Mwinyi ulileta neno "Mheshimiwa" badala ya "ndugu" kwa viongozi na sasa wamekuwa tabaka lenye kujiona wako juu ya Watanzania wengine!

Synthesizer

Platinum Member
Joined
Feb 15, 2010
Posts
12,699
Reaction score
22,598
Zamani enzi za utawala wa Nyerere, kila Mtanzania aliitwa ndugu, pamoja na Nyerere mwenyewe akiwa Raisi wa nchi. Nyerere aliitwa "ndugu raisi" sawa tu na mtu wa mtaani. Hata kwa mtu ambae ulikuwa humfahamu, ukitaka kuuliza kitu tulianza kwa kusema "samahani ndugu, sijui basi la kwenda ferry ni lipi".

Watanzania wote tulikuwa ndugu, bila kujali kama wewe ni masikini, muuza karanga mtaani, kiongozi au hata jobless, lofa tu wa mtaani, bado uliitwa "ndugu" kama ambavyo raisi wa nchi aliitwa ndugu raisi. Jambo zuri kabisa lililoondoa matabaka nchini.

Akaingia Raisi Mwinyi na umwinyi kutoka Zanzibar, watu wake ndani ya CCM wakamshawishi kwamba viongozi wa Tanzania hawawezi kuitwa kwa namna moja na wauza karanga mitaani, bali wao waitwe "weheshimiwa", na hata kuanza kuimba bila aibu kuwa CCM ina wenyewe, waheshimiwa. Nyerere akashangaa sana.

Basi leo tunaona matokeo na laana hii ya ubaguzi wa ndani ambao chama hiki kinachotawala, CCM, kiliianzisha. Matokeo sasa ni kwamba Tanzania imezaa tabaka la viongozi (vigogo) ambao wanajiona wako tofauti na hata sheria za nchi haziwahusu. Tuna hili kundi la viongozi, "waheshimiwa" ambao halitaki kusikia maoni ya mtu mwingine ambae haitwi mheshimiwa. Wao wanajiona wanajua kila kitu na hawapaswi kuulizwa, na wako juu ya sheria, na Polisi, Usalama wa Taifa na hata JW wakati fulani, wapo kwa ajili ya kuwalinda wao, nafasi zao na utajiri wao ambao kila mtu anajua umetokana na ufisadi na sio mishahara yao. Wameamua kwamba mtu yeyote asie mheshimiwa, akileta ubishi au maoni tofauti wasiyopenda, atekwe, apigwe hata kuuawa ikibidi!

Hawa "waheshimiwa" na familia zao wamekuwa wakibebana katika nafasi za serikalini, na hata kutengeneza mazingira ili watoto wao waje waurithi "uheshimiwa" hapo baadaye, jambo ambalo limeleta wingu kubwa la vigogo ambao baba zao walikuwa vigogo huko nyuma!

Siku hizi hawa "waheshiwa", hata magari yao yanatofautishwa. Wanapewa ving'ora na taa za blue kwa sababu wao wanajiona hawapaswi kukaa kwenye trafik jam (foleni) kama Watanzania wengine ambao sio waheshimiwa! Wao wana haraka kurudi nyumbani kwa familia zao baada ya kazi, kwa hiyo wapishwe barabarani! Ukikwaruza gari yao au kuwanyima kupita, mara nyingi wanauliza "unajua mimi ni nani?", mentality ya mimi ni mheshimiwa, wewe ni lofa tu!

Sasa nawauliza Watanzania wenzangu, hili linavumilika? Linakubalika? Tufanyeje ili kulikomesha mara moja?
 
Neno "mtukufu Rais " lilitumika enzi ipi??
Je bado linatumika?? Kama halitumiki nani aliliondoa??
 
Halafu hili tabaka la waheshimiwa likazaa tabaka la machawa🤔
Kweli kabisa! Halafu machawa ndio watu wa kudharauliwa sana, wanashangilia waheshimiwa kwa kila kitu kama misukule walioondolewa akili, na wala hakuna wanachofaidika nacho kama mtu mmoja mmoja binafsi au kama raia wa Tanzania!
 
Neno "mtukufu Rais " lilitumika enzi ipi??
Je bado linatumika?? Kama halitumiki nani aliliondoa??
Baada tu ya uhuru, na kwa Raisi Nyerere, ambae alilikataa akisema kuitwa mtukufu ilimfanya awe kama malaika, jambo aliloona linakaribia kuwa kufuru. Akalikataza. Lilikuja kuibuka wakati wa Mwinyi, watu walimwita Mtukufu Raisi na hakuwazuia, na hata sasa, likitumiwa zaidi na machawa
 
Kweli kabisa! Halafu machawa ndio watu wa kudharauliwa sana, wanashangilia waheshimiwa kwa kila kitu kama misukule walioondolewa akili, na wala hakuna wanachofaidika nacho kama mtu mmoja mmoja binafsi au kama raia wa Tanzania!
Pole sana, umeandika kwa Uchungu. Ulikuwepo enzi za Nyerere au Mwinyi ukiwa unajitambua kiakili?
 
Zamani enzi za utawala wa Nyerere, kila Mtanzania aliitwa ndugu, pamoja na Nyerere mwenyewe akiwa Raisi wa nchi. Nyerere aliitwa "ndugu raisi" sawa tu na mtu wa mtaani. Hata kwa mtu ambae ulikuwa humfahamu, ukitaka kuuliza kitu tulianza kwa kusema "samahani ndugu, sijui basi la kwenda ferry ni lipi".

Watanzania wote tulikuwa ndugu, bila kujali kama wewe ni masikini, muuza karanga mtaani, kiongozi au hata jobless, lofa tu wa mtaani, bado uliitwa "ndugu" kama ambavyo raisi wa nchi aliitwa ndugu raisi. Jambo zuri kabisa lililoondoa matabaka nchini.

Akaingia Raisi Mwinyi na umwinyi kutoka Zanzibar, watu wake ndani ya CCM wakamshawishi kwamba viongozi wa Tanzania hawawezi kuitwa kwa namna moja na wauza karanga mitaani, bali wao waitwe "weheshimiwa", na hata kuanza kuimba bila aibu kuwa CCM ina wenyewe, waheshimiwa. Nyerere akashangaa sana.

Basi leo tunaona matokeo na laana hii ya ubaguzi wa ndani ambao chama hiki kinachotawala, CCM, kiliianzisha. Matokeo sasa ni kwamba Tanzania imezaa tabaka la viongozi (vigogo) ambao wanajiona wako tofauti na hata sheria za nchi haziwahusu. Tuna hili kundi la viongozi, "waheshimiwa" ambao halitaki kusikia maoni ya mtu mwingine ambae haitwi mheshimiwa. Wao wanajiona wanajua kila kitu na hawapaswi kuulizwa, na wako juu ya sheria, na Polisi, Usalama wa Taifa na hata JW wakati fulani, wapo kwa ajili ya kuwalinda wao, nafasi zao na utajiri wao ambao kila mtu anajua umetokana na ufisadi na sio mishahara yao. Wameamua kwamba mtu yeyote asie mheshimiwa, akileta ubishi au maoni tofauti wasiyopenda, atekwe, apigwe hata kuuawa ikibidi!

Hawa "waheshimiwa" na familia zao wamekuwa wakibebana katika nafasi za serikalini, na hata kutengeneza mazingira ili watoto wao waje waurithi "uheshimiwa" hapo baadaye, jambo ambalo limeleta wingu kubwa la vigogo ambao baba zao walikuwa vigogo huko nyuma!

Siku hizi hawa "waheshiwa", hata magari yao yanatofautishwa. Wanapewa ving'ora na taa za blue kwa sababu wao wanajiona hawapaswi kukaa kwenye trafik jam (foleni) kama Watanzania wengine ambao sio waheshimiwa! Wao wana haraka kurudi nyumbani kwa familia zao baada ya kazi, kwa hiyo wapishwe barabarani! Ukikwaruza gari yao au kuwanyima kupita, mara nyingi wanauliza "unajua mimi ni nani?"

Sasa nawauliza Watanzania wenzangu, hili linavumilika? Linakubalika? Tufanyeje ili kulikomesha mara moja?
Neno ndugu liko poa sana, Mheshimiwa nikujitweza
 
Zamani enzi za utawala wa Nyerere, kila Mtanzania aliitwa ndugu, pamoja na Nyerere mwenyewe akiwa Raisi wa nchi. Nyerere aliitwa "ndugu raisi" sawa tu na mtu wa mtaani. Hata kwa mtu ambae ulikuwa humfahamu, ukitaka kuuliza kitu tulianza kwa kusema "samahani ndugu, sijui basi la kwenda ferry ni lipi".

Watanzania wote tulikuwa ndugu, bila kujali kama wewe ni masikini, muuza karanga mtaani, kiongozi au hata jobless, lofa tu wa mtaani, bado uliitwa "ndugu" kama ambavyo raisi wa nchi aliitwa ndugu raisi. Jambo zuri kabisa lililoondoa matabaka nchini.

Akaingia Raisi Mwinyi na umwinyi kutoka Zanzibar, watu wake ndani ya CCM wakamshawishi kwamba viongozi wa Tanzania hawawezi kuitwa kwa namna moja na wauza karanga mitaani, bali wao waitwe "weheshimiwa", na hata kuanza kuimba bila aibu kuwa CCM ina wenyewe, waheshimiwa. Nyerere akashangaa sana.

Basi leo tunaona matokeo na laana hii ya ubaguzi wa ndani ambao chama hiki kinachotawala, CCM, kiliianzisha. Matokeo sasa ni kwamba Tanzania imezaa tabaka la viongozi (vigogo) ambao wanajiona wako tofauti na hata sheria za nchi haziwahusu. Tuna hili kundi la viongozi, "waheshimiwa" ambao halitaki kusikia maoni ya mtu mwingine ambae haitwi mheshimiwa. Wao wanajiona wanajua kila kitu na hawapaswi kuulizwa, na wako juu ya sheria, na Polisi, Usalama wa Taifa na hata JW wakati fulani, wapo kwa ajili ya kuwalinda wao, nafasi zao na utajiri wao ambao kila mtu anajua umetokana na ufisadi na sio mishahara yao. Wameamua kwamba mtu yeyote asie mheshimiwa, akileta ubishi au maoni tofauti wasiyopenda, atekwe, apigwe hata kuuawa ikibidi!

Hawa "waheshimiwa" na familia zao wamekuwa wakibebana katika nafasi za serikalini, na hata kutengeneza mazingira ili watoto wao waje waurithi "uheshimiwa" hapo baadaye, jambo ambalo limeleta wingu kubwa la vigogo ambao baba zao walikuwa vigogo huko nyuma!

Siku hizi hawa "waheshiwa", hata magari yao yanatofautishwa. Wanapewa ving'ora na taa za blue kwa sababu wao wanajiona hawapaswi kukaa kwenye trafik jam (foleni) kama Watanzania wengine ambao sio waheshimiwa! Wao wana haraka kurudi nyumbani kwa familia zao baada ya kazi, kwa hiyo wapishwe barabarani! Ukikwaruza gari yao au kuwanyima kupita, mara nyingi wanauliza "unajua mimi ni nani?"

Sasa nawauliza Watanzania wenzangu, hili linavumilika? Linakubalika? Tufanyeje ili kulikomesha mara moja?
Ongezea na ile “Mtukufu” aliitwa “Mtukufu Rais Alhaji Mwinyi” hahaha this mzee was a waste kwa kweli. Yeye ndiye aliyesababisha mfumo wa ufisadi kuota mizizi (ingawa yeye hakiwa fisadi ila wateule wake). Tunahitaji rais mwenye mkono wa chuma kuua mafisadi na wezi wote maana mahakama zetu zinahongeka. Yaani kill all mafisadi kila sehemu then tutakuwa na taifa lililo jaa wazalendo na wanaofuata sheria. Sasa hivi unakuta hakuna haki kama huna hela
 
Pole sana, umeandika kwa Uchungu. Ulikuwepo enzi za Nyerere au Mwinyi ukiwa unajitambua kiakili?
Ni kweli, nasikitishwa sana na jinsi "waheshimiwa" wanavyozidi kujijengea himaya yao na kujitofautisha na Watanzania wengine. Enzi za Nyerere na Mwinyi nilikuwapo kama kijana chipukizi mkereketwa! 😀 😀 😀
 
Neno ndugu liko poa sana, Mheshimiwa nikujitweza
Kweli kabisa. Nakumbuka hadithi kwamba Watanzania wakienda Kenya kutokana na mazoea, waliwaita Wakenya "ndugu", na Wakenya wakawa wanasema, "wee wacha hiyo, mie hapana ndugu yako!"😀
 
Neno "mtukufu Rais " lilitumika enzi ipi??
Je bado linatumika?? Kama halitumiki nani aliliondoa??
Enzi za huyo ruksa. Nilikuwa mdogo lkn lilikuwa linanikwaza sana. Alipokuja mzee mkapa ndio akakataa kuitwa mtukufu rais na kuintroduce neno mheshimiwa.
 
Kundi la Waheshimiwa wamo Wabunge, Mawaziri, Wakuu wa Mikoa/Wilaya na hata Madiwani. Halafu pia kuna Mstahiki/Wastahiki (Ma-Mayor).Wengine wameona u-heshimiwa hautoshi sasa wameongeza na taaluma zao. Utasikia "Mheshimiwa, Dokta, CPA, Arch, Eng, Contractor, Wakili msomi, Mchungaji, Igwe, CBE, CSP, nk..nk..
 
Ongezea na ile “Mtukufu” aliitwa “Mtukufu Rais Alhaji Mwinyi” hahaha this mzee was a waste kwa kweli. Yeye ndiye aliyesababisha mfumo wa ufisadi kuota mizizi (ingawa yeye hakiwa fisadi ila wateule wake). Tunahitaji rais mwenye mkono wa chuma kuua mafisadi na wezi wote maana mahakama zetu zinahongeka. Yaani kill all mafisadi kila sehemu then tutakuwa na taifa lililo jaa wazalendo na wanaofuata sheria. Sasa hivi unakuta hakuna haki kama huna hela
Mzee huyu alikuwa wa kumhurumia tu. Na alipata wakati mgumu sana, maana Nyerere alikuwa hai bado. Ndio maana Mkapa alipoingia alimfanyia Nyerere mambo ya ajabu sana. Kama Nyerere angekuwapo baada ya miaka mitano ya kwanza ya utawala wa Mkapa, CCM ingeandika historia, asingepitishwa tena. Mkapa alijua hilo. Akajiongeza.
 
Kundi la Waheshimiwa wamo Wabunge, Mawaziri, Wakuu wa Mikoa/Wilaya na hata Madiwani. Halafu pia kuna Mstahiki/Wastahiki (Ma-Mayor).Wengine wameona u-heshimiwa hautoshi sasa wameongeza na taaluma zao. Utasikia "Mheshimiwa, Dokta, CPA, Arch, Eng, Contractor, Wakili msomi, Mchungaji, Igwe, CBE, CSP, nk..nk..
Halafu wote wanataka watumie gari kubwa 4 x 4, ndio maana kuna utitiri sana wa haya magari Tanzania. Huenda tunaongoza duniani kwa kuwa na 4x4 nyingi per capita! Kuna mahali nilisoma watu wanaopenda kutumia 4 x 4 wana tatizo la egoism. Mheshimiwa hajioni mheshimiwa bila kuwa na 4 x 4!
 
Ni kweli, nasikitishwa sana na jinsi "waheshimiwa" wanavyozidi kujijengea himaya yao na kujitofautisha na Watanzania wengine. Enzi za Nyerere na Mwinyi nilikuwapo kama kijana chipukizi mkereketwa! 😀 😀 😀
Kwanini Nyerere alikuwa akimskilizasana Thabit Kombo ? Kwa mujibu wa kitabu cha Marehemu Mzee Mwinyi, kabla ya kuteuliwa Rais wa Mpito wa Zanzibar kwenye vikao vya Chama aliamuru Ndege kumfata Thabit Kombo kutoka Moshi mpaka Dodoma na kumuuliza nani anafaa kuwa Rais wa mpito.
 
Kwanini Nyerere alikuwa akimskilizasana Thabit Kombo ? Kwa mujibu wa kitabu cha Marehemu Mzee Mwinyi, kabla ya kuteuliwa Rais wa Mpita wa Zanzibar kwenye vikao vya Chama aliamuru Ndege kumfata Thabit Kombo kutoka Moshi mpaka Dodoma na kumuuliza nani anafaa kuwa Rais wa mpito.
Nyerere akiwa Raisi wa Tanzania ndie Raisi pekee aliekuwa na maamuzi Tanzania, bara na visiwani. Lakini maamuzi yaliyohusu visiwani aliyafanya kwa kuwashirikisha watu kama Thabit Kombo ambao walikuwa ni visima vya ujuzi kuhusu siasa za visiwani
 
Watanzania ni wagonjwa na mbaya zaidi hawatambui kuwa ni wagonjwa.Taifa lina mambo ya kijinga hili,Kuna kundi la vilaza na mazuzu kule makao makuu wanaliita "Bunge tukufu"
 
Nyerere akiwa Raisi wa Tanzania ndie Raisi pekee aliekuwa na maamuzi Tanzania, bara na visiwani. Lakini maamuzi yaliyohusu visiwani aliyafanya kwa kuwashirikisha watu kama Thabit Kombo ambao walikuwa ni visima vya ujuzi kuhusu siasa za visiwani
Ahsante sasa naomba wasifu japo mdogo wa Thabit Kombo. Alikuwa nani hasa?

Mbili Mzee Mwinyi wizara yake ya kwanza katika Serikali ya Muungano iliwahi kuwa ni Waziri wa Mambo ya Ndani na Waziri nchi ofisi ya Rais. Wizara nyeti kabisa, je tofauti na Ualimu Mzee Mwinyi alikuwa na ujuzi mwingine?
 
Kweli kabisa! Halafu machawa ndio watu wa kudharauliwa sana, wanashangilia waheshimiwa kwa kila kitu kama misukule walioondolewa akili, na wala hakuna wanachofaidika nacho kama mtu mmoja mmoja binafsi au kama raia wa Tanzania!
Umenikumbusha chawa lucas mwashamba😀😀
 
Back
Top Bottom