Nataka Anza fuga hata kuku wanneMzee kipi ni bora kati ya kufa kifo cha mateso kwa siku 20 na kufa ndani ya dk 1?. Vyote ni Vifo ila kipi kinauma zaidi?
Kweli kabisa ni UKATILI wa hali ya JUU. Wangeuza hata kwa nusu/robo bei kisha wasimamishe uzalishaji kwa muda.Nimeona jana Waziri wa Mifugo katika kauli ya kwamba ile kampuni inatakiwa kufuatiliwa na vyombo vya dola kwa kosa la kuchoma vifaranga. Binafsi imeniuma sana kuona watu wanatoa uhai wa viumbe vya mwenyezi Mungu hadharani tena kwa moto. Pale kuna kitu nyuma ya pazia sio kweli kukosa wateja ndio chanzo. Si bora angevigawa bure kwa watu wengine?
Shida yenu hamuelewi kinachoendelea mtaani, vifaranga kwa sasa wanunuzi hawavitaki hata bure kwa sababu vyakula vya kuku vimepanda bei karibu mara 10-15.
Imagine debe la pumba lililokuwa linauzwa elfu 1, kwa sasa linauzwa elfu 10, maeneo mengine mpaka elfu 15.
Hapo hata kama utapewa vifaranga bure haisaidii maana utaingia hasara tuu maana gharama za uendeshaji zitakuwa kubwa kuliko faida.
View attachment 2446055
Hakusababisha ukatili wa kuvichoma moto.Yote haya yamesababishwa na nchi kuvurugwavurugwa na huyu bibi ambaye ameenda kubembea marekani.kila aina ya takataka aneziruhusu kuingia nchini na matokeo yake viwanda vya ndani vimekosa soko.
Si kweli.Kilichosababisha soko la kuku kuanguka ni sera mbovu za rais wenu Samia za kufungua nchi!
Eti kufungua nchi,
Watu wameuza mazao yote nje ya nchi wakati soko letu la ndani lilikuwa bado halijitoshelezi.
Kilichotokea sasa ni vyakula vya kuku kupanda bei na wafugaji wameacha kufuga maana hawaoni faida ya kufuga.
Mwezi uliopita Samia akiwa arusha eti anawambia watu kwamba kipindi kile vifaranga vimechomwa haikuwa sawa kama vile yeye hakuwa makamu wa rais.
Tumwache aendelee kufungulia nchi huku wakenya wakijaza mavifaranga yao na huku wa ndani wakikosa soko.
Atajifunza akiwa amechelewa sana.
mweusii yulee falaa tuuu hana uzungu wowotee... huwezi kuua vifaranga wote wale tena unawachoma wakiwa hai wakati kiukweli kuna wafugaji wengi ukiwapa bure hawawezi kukataaa.
Hujui chochote!Si kweli.
Ongea na Wafugaji.
Unaweza kuhiari kununua kifaranga kwa bei ya juu ikiwa kimekidhi sifa zote....za Mbegu bora!!
Quality ya baadhi ya Wazalishaji wa ndani iko chini.
Wafugaji wanafanya biashara...Lazima waendane na kinachowapatia faida...
Siyo kweli kwamba Mashamba yote yana ubora unaohitajika...
Kama mtu siyo Mfugaji hawezi kuelewa hiki kitu...!
Wafugaji wakubwa wanajua. .
Wa kati wanajua
Wadogo wanaweza wasijue...!
Mkuu uwape bure alafu watawalisha nini?mweusii yulee falaa tuuu hana uzungu wowotee... huwezi kuua vifaranga wote wale tena unawachoma wakiwa hai wakati kiukweli kuna wafugaji wengi ukiwapa bure hawawezi kukataaa.
wewe tangaza hata bei ndogo uonee kama utakosa watejaaa yani mnafanya overproduction mpaka vifaranga 3000 na bado mnataka muendelee kuzalisha wengine... huyo mtu wa sales nae wakufukuzaa kazi.Mkuu uwape bure alafu watawalisha nini?
Unga tu wa kula nyumbani watu unawashinda sembuse kununua chakula cha kuku ambacho mfuko mmoja una kimbilia laki 1?
Wakishindwa hata kuwafadhili akina mama wenye vikundi na baadae walipwe hata kwa riba ndogo imenisikitisha maana wamelenga hasara ya moja kwa mojaKupitia taarifa ya habari jana Jumatatu saa mbili usiku Azam TV imeripoti habari ya kiwanda kimoja cha kuzalisha vifaranga cha mjini Moshi kuteketeza mamia ya vifaranga kwa kuwatosa kwenye moto mkaili eti kisa tu vifaranga hao wamekosa soko!
Kweli japo kuku wanaliwa kila siku lakini kitendo kilichofanywa na uongozi wa kiwanda hicho ni cha kinyama tena kinyama mno.
Kwa kweli nimepigwa na butwaa baada ya kusikiliza habari ile na kumshuhudia mmoja wa wafanyakazi akitupia box moja baada ya jingine juu ya moto mkali huku vifaranga vikilia kwa uchungu! Aisee imeniuma mno.
Sababu za mkurugenzi:
~ Walivisafirisha vifaranga hivyo hadi Dar ili viuzwe kwa tsh 1000, biashara ikawa ngumu kwa sababu ati kuna watu wengi sasa hivi wana ingiza vifaranga toka nje hivyo soko limetibuka.
Wakaamua washushe bei hadi Tsh 900, bado hawakupata soko. Wakaamua mzigo urudi kiwandani Moshi huko nako wakatangaza bei ya Tsh 900 ikashindikana, uamuzi wao wa mwisho ukawa ni kuwateketeza kwa moto mkali!
Tuiombe serikali kitengo cha watu wa mifugo au kama bado ipo taasisi ya kutetea wanyama iwafuatilie wamiliki wa kiwanda hiki na ikibidi wachukuliwe hatua kali ili iwe onyo kwa wengine watakaofikiria kufanya upuuzi huu.
Maana Mkurugenzi wao ameshasema kuwa vifaranga wengine laki nane na nusu wanatarajiwa hivi karibuni na hajui pa kuwapeleka.
Nimejiuliza kwanini basi hata huku Dar na Moshi wasivigawe kwa mtu yeyote atakayeweza kutunza? Hata kama mtu angechukua 20 mwingine box 4, mwenye vifaranga 60 n.k, wangetangaza tu hadharani, au kuwatangazia hata majeshini, vyuoni pengine wangejaribu kuwakuza vifaranga hao wa nyama na mayai.
Nimalizie kwa kusema kitendo kile ni cha kishetani na hakina budi kulaaniwa na serikali ichukue hatua stahiki na hili lisijirudie.
View attachment 2445992
Lo! hapana nina mabanda hayana vifaranga wagenipatia hata 1000 nigejitahidi kupata chakula .Kweli walishidwa hata kututangazia watu wa Dar hata watuuzie kwa 500 wasingekosa wateja. mm nilitamani kidogo nipige ukunga nilivyoona ule moto. hawakuwaza vyema.yule mmliliki hata sikumuelewa.hapo pana utata inawezekana hata wao hawajapenda ila mazingira yalikuwa ni limited kwao! Maana ilikuwa inatakiwa kuvilisha na kuvitibu kila siku, so kuliko kubiacha vife na njaa wameona bora vichomwe tu