Utesaji wa Dola - Agenda kubwa Uchaguzi ujao

Utesaji wa Dola - Agenda kubwa Uchaguzi ujao

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Habari hii iwafikie wote wanaokodolea macho nafasi za uongozi.

Ifahamike kuwa bila tume huru hakuna uchaguzi.

Hatutaangalia mgombea ni mwanamke au mwanaume. Haki zetu za binadamu hazitakuwa na mbadala.

Kama ni mtarajiwa atuambie atafanya nini kuondoa kadhia kama hizi:



Kama alikuwamo madarakani atwambie alifanya nini kuondoa kadhia kama hizo.

Kutesa watu, kuteka watu, kuuwa watu au kuwashikilia watu bila kujulikana walipo kinyume cha utashi wao ni kinyume cha sheria na kinyume cha haki za binadamu.

Tutahitaji kujua wako wapi wote waliopotezwa na dola.

Tutahitaji kujua yuko wapi Moses Lijenje. Tutahitaji kujua alipo Luteni Dennis Urio na kwa nini kama yupo anashikiliwa na kuteswa huko aliko.

Aghalabu hao ni kwa kuanzia kwani orodha yote ya waliotoweka itakuwapo.

Uongozi siyo udhwalimu.

Tunayo haki ya kuishi nchini mwetu kwa furaha itokanavyo na uwepo wa uhuru, haki, usawa na demokrasia.
 
Habari hii iwafikie wote wanaokodolea macho nafasi za uongozi.

Ifahamike kuwa bila tume huru hakuna uchaguzi.

Hatutaangalia mgombea ni mwanamke au mwanaume. Haki zetu za binadamu hazitakuwa na mbadala.

Kama ni mtarajiwa atuambie atafanya nini kuondoa kadhia kama hizi:



Kama alikuwamo madarakani atwambie alifanya nini kuondoa kadhia kama hizo.

Kutesa watu, kuteka watu, kuuwa watu au kuwashikilia watu bila kujulikana walipo kinyume cha utashi wao ni kinyume cha sheria na kinyume cha haki za binadamu.

Tutahitaji kujua wako wapi wote waliopotezwa na dola.

Tutahitaji kujua yuko wapi Moses Lijenje. Tutahitaji kujua alipo Luteni Dennis Urio na kwa nini kama yupo anashikiliwa na kuteswa huko aliko.

Aghalabu hao ni kwa kuanzia kwani orodha yote ya waliotoweka itakuwapo.

Uongozi siyo udhwalimu. Tunayo haki ya kuishi nchini mwetu kwa furaha itokanavyo na uwepo wa uhuru, haki, usawa na demokrasia.

When i watched that video it send a chill on my spine.

Vyombo vya dola ni waonevu sana.
 
Hivi kuna maana gani kumfanyia mwanaume mwenzio kitendo cha hovyo kama hicho? hawaoni kuwafanyia hivyo wenzao ni sawa na kujidhalilisha wao wenyewe?

Hata kama Katiba Mpya itachelewa upatikanaji wake, upuuzi wa aina hii haupaswi kuisubiri mpaka ipatikane, hao wahuni wanaotesa watu, kuwaibia mali zao ( pesa), na kuwapoteza wakiwa chini ya usimamizi wao, wanatakiwa kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Uchunguzi ufanywe na taasisi huru ku expose madhila yote polisi wa nchi hii wanayowafanyia raia wakiwa vituoni, itakapothibitika ushiriki wa polisi, wachukuliwe hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa wote wenye tabia za hovyo kama hizi.

Mwisho CCM na serikali ndio wachochezi wa hizi tabia ovu, ushirikiano wao na polisi kwenye mambo ya kisiasa kwa manufaa yao ndiko kunasababisha polisi wajisahau na kujiona wana haki ya kuwakandamiza wengine, kwasababu wana "urafiki" na serikali iliyopo madarakani.
 
Hivi kuna maana gani kumfanyia mwanaume mwenzio kitendo cha hovyo kama hicho? hawaoni kuwafanyia hivyo wenzao ni sawa na kujidhalilisha wao wenyewe?

Hata kama Katiba Mpya itachelewa upatikanaji wake, upuuzi wa aina hii haupaswi kuisubiri mpaka ipatikane, hao wahuni wanaotesa watu, kuwaibia mali zao ( pesa), na kuwapoteza wakiwa chini ya usimamizi wao, wanatakiwa kuchukuliwa hatua kali za kisheria.

Uchunguzi ufanywe na taasisi huru ku expose madhila yote polisi wa nchi hii wanayowafanyia raia wakiwa vituoni, itakapothibitika ushiriki wa polisi, wachukuliwe hatua kali za kisheria ili iwe fundisho kwa wote wenye tabia za hovyo kama hizi.

Mwisho CCM na serikali ndio wachochezi wa hizi tabia ovu, ushirikiano wao na polisi kwenye mambo ya kisiasa kwa manufaa yao ndiko kunasababisha polisi wajisahau na kujiona wana haki ya kuwakandamiza wengine, kwasababu wana "urafiki" na serikali iliyopo madarakani.

Wakuu wa nchi wanye kuongoza nchi zao na haya wakiyajua kuwa ni sehemu ya utawala wao, hawafai.

Kama wanaongoza nchi haya hawayajui, haiyumkiniki basi hawana udhibiti na hali nzima ya nchi.

Kwamba hawana udhibiti na nchi kwa ujumla? Basi wako madarakani kwa ajili ya nini?

We sincerely owe them a response.
 
Shame on this country ndiomaana wakati mwingine hata mvua hazinyeshi, yote haya ni uroho na uchoyo wa madaraka , Jiwe alikua mbwa sana hivi mtu kama hakukubali ni lazima umtese? kwani haya mavyeo situnayaacha hapa hapa duniani? hii nchi ni ngumu sana
 
Hili swala kwa kweli linaharibu taswila ya taifa na watu kupenda nchi yao

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app

Mateso ya namna hii hayapo kokote katika jamii iliyostaarabika. Haya si ya kufumbia macho.

"Kuunyamazia uovu ni kuubariki kuendelea kuwapo." -- Desmond Tutu.

Hawa ni lazima kwa umoja wetu tuwapigie kelele kweli kweli.

Leo ni kina Adamoo, Ling'wenya, Lijenje, na kina Urio. Kesho itakuwa nani?

Uchumi gani wanasimamisha? Tunataka haki.

Tunamtaka Lijenje akiwa hai.
 
Shame on this country ndiomaana wakati mwingine hata mvua hazinyeshi, yote haya ni uroho na uchoyo wa madaraka , Jiwe alikua mbwa sana hivi mtu kama hakukubali ni lazima umtese? kwani haya mavyeo situnayaacha hapa hapa duniani? hii nchi ni ngumu sana

Rais Samia kama ana mawazo na 2025 ajitenge haraka sana na kwa vitendo na uonevu huu.

Sirro na Majaliwa muda wao wa kupumzishwa sasa na kuchunguzwa uhusika wao na kadhia hizi.

Hili ni la uchunguzi huru.

Jambo hili ni la dharura mno kuliko huo anaodai uchumi wa kusimamisha.

Maisha yetu kwanza!

Wamrejeshe Lijenje akiwa hai.
 
When i watched that video it send a chill on my spine.

Vyombo vya dola ni waonevu sana.

Ni aibu sana kwa Samia, Majaliwa na Sirro. Haya yanafanyika chini yao.

Hayakubaliki.

Huu ni uhalifu dhidi ya binadamu. ICC inawahusu watu hapa kama hatuwezi kuwamudu.
 
Kumekuwa na tabia mbaya kabisa ya ukatili wa baadhi ya watu katika kutafuta au kushikilia uongozi/madaraka katika Tanzania.
Kwa bahati mbaya sana, wananchi masikini wa mali na fikra wameingia kwenye mtego wa kushabikia unyama huu.
Hii siyo sawa na haikubaliki hata kidogo.
Kwa mustakabali mwema wa taifa, watu makatili dhidi ya wenzao wapingwe kwa njia zote.
 

Tupaze sauti zetu wahusika wote wakiwamo Samia, Majaliwa, Sirro na wote wasikie. Haya hayakubaliki!

"If you are neutral in situations of injustice, you have chosen the side of the oppressor."

"If an elephant has its foot on the tail of a mouse, and you say that you are neutral, the mouse will not appreciate your neutrality."

----- Desmond Tutu.

Yuko wapi Commando Moses Lijenje?
 
Kumekuwa na tabia mbaya kabisa ya ukatili wa baadhi ya watu katika kutafuta au kushikilia uongozi/madaraka katika Tanzania.
Kwa bahati mbaya sana, wananchi masikini wa mali na fikra wameingia kwenye mtego wa kushabikia unyama huu.
Hii siyo sawa na haikubali hata kidogo.
Kwa mustakabali mwema wa taifa, watu makatili dhidi ya wenzao wapingwe kwa njia zote.

Hawa si wa kunyamazia. Kwa majina yao tunawajua.

Dhamana zipi watatajwa kuwa nazo kutoka kwetu kama hawawezi kuhakikisha haki zetu?

Yuko wapi Moses Lijenje?
 
Habari hii iwafikie wote wanaokodolea macho nafasi za uongozi.

Ifahamike kuwa bila tume huru hakuna uchaguzi.

Hatutaangalia mgombea ni mwanamke au mwanaume. Haki zetu za binadamu hazitakuwa na mbadala.

Kama ni mtarajiwa atuambie atafanya nini kuondoa kadhia kama hizi:




Kama alikuwamo madarakani atwambie alifanya nini kuondoa kadhia kama hizo.

Kutesa watu, kuteka watu, kuuwa watu au kuwashikilia watu bila kujulikana walipo kinyume cha utashi wao ni kinyume cha sheria na kinyume cha haki za binadamu.

Tutahitaji kujua wako wapi wote waliopotezwa na dola.

Tutahitaji kujua yuko wapi Moses Lijenje. Tutahitaji kujua alipo Luteni Dennis Urio na kwa nini kama yupo anashikiliwa na kuteswa huko aliko.

Aghalabu hao ni kwa kuanzia kwani orodha yote ya waliotoweka itakuwapo.

Uongozi siyo udhwalimu. Tunayo haki ya kuishi nchini mwetu kwa furaha itokanavyo na uwepo wa uhuru, haki, usawa na demokrasia.
Nchi inayojiita ya AMANI Wananchi Wake WANATESWA na KUPOTEZWA na VYOMBO vya DOLA
 
Kiapo cha Kiongozi wa nchi..ni kulinda raia wa Jamhuri..hli ndilo jukuu kubwa no moja. Je Kiongozi mkuu akibarik Unyama huu dhidi ya raia Je hajasalit kiaopo chake?

Ni wakati wa rais Samia kuaza kujihoji mwenyewe kama anatosha.

Kiongozi anayeongoza nchi haya yakiwapo hafai.
 
Back
Top Bottom