Utetezi wa uumbaji kimahesabu na kifizikia: Mathematician's and theoretical physicist appeal to creation

Utetezi wa uumbaji kimahesabu na kifizikia: Mathematician's and theoretical physicist appeal to creation

Siwezi kukosoa coz unatumia kitabu ambacho wewe una amini hakuina shaka leta hoja kifalsafla ikosolewe kifalsafla , mambo ya dini zenu nitakosoaje akati mmeambiwa ni sahihi kwa matumizi yenu?
Kwanza tu mpaka hapa hakuna hata hoja moja niliyo ijibu kwa mujibu wa imani yangu.

Bali nimekosoa hoja zenu kwa kutumia uhalisia, mawanda ya lugha na elimu ya uhakiki wa habari.

Mimi Falsafa naijua siyo kwa kuambiwa bali kwa kuisoma, najua madhaifu yake na najua msingi wake ndiyo maana hapa nahoji kwa uhalisia na hoja za kiakili.
 
Wewe umeona tu utofauti wa idadi vitabu kuwa ni tatizo , hauoni utofauti wa idadi ya din , kuna dini zaidi ya 40000 kila dini one ego yake , malizeni tofauti zenu kwanza mpate din moja yenye majibu sawa ndo uje upinge MUNGU ni energy au super intelligence
Sisi tunajua mpaka sababu za kuwepo hizi dini nyingi na misingi yake na uongo wa dini husika.

Kulingana na asili ya hizi dini, jambo hilo haliwezekani na wala si lazima.
 
Kwanza tu mpaka hapa hakuna hata hoja moja niliyo ijibu kwa mujibu wa imani yangu.

Bali nimekosoa hoja zenu kwa kutumia uhalisia, mawanda ya lugha na elimu ya uhakiki wa habari.

Mimi Falsafa naijua siyo kwa kuambiwa bali kwa kuisoma, najua madhaifu yake na najua msingi wake ndiyo maana hapa nahoji kwa uhalisia na hoja za kiakili.
Kila mtu akili yake ipo tofauti umejuaje hayo unayozungumza yanapatana na akili ya kila mtu ? Sioni cha kukujibu coz sijaona mahali umekanusha MUNGU ni energy au super intelligence , mm nmeona wewe umeweka tu mahubiri ya dini yako ili mimi nione ni nzuri zaidi ya nyingne
 
Sisi tunajua mpaka sababu za kuwepo hizi dini nyingi na misingi yake na uongo wa dini husika.

Kulingana na asili ya hizi dini, jambo hilo haliwezekani na wala si lazima.
Si mliambiwa ninyi mna dini yenu na wao wanadini yao , unaonaje ukiyaishi hayo maandiko mbona yapo kma kuepusha migongano kama hyo unayoitaka wewe?
 
Si mliambiwa ninyi mna dini yenu na wao wanadini yao , unaonaje ukiyaishi hayo maandiko mbona yapo kma kuepusha migongano kama hyo unayoitaka wewe?
Maana ya aya iliongelea kuabudu na si kuwaacha watu wakosee, au kuuficha ukweli.
 
Kwa hiyo kupitia formula yako ya hesabu ni wazi kwamba njia hiyo inathibitisha Mungu Yehova na habari za utatu mtakatifu ambao haukubaliki na jamii ya kiislamu?

Najua point yako ilikuwa kuweka hoja ku challenge atheists lakini since umemtaja Yesu na utatu umejikuta upo katika nafasi ya kujibu maswali ya waislamu wenye itikadi kali

Kwa hiyo sio atheists tu ambao watapinga kanuni yako, kuna waislamu pia. Hiyo inakupa tafsiri gani?

So unashaurije?

Kwanini tusiwape nafasi nyinyi kwa nyinyi believers mkae chini mfikie muafaka wa pamoja kukubaliana jibu moja ambalo mtasimamia kwa pamoja kwenye mjadala dhidi yetu?
Kwani atheist mmewahi kukubaliana kutowepo Mungu? Kama jibu ni ndiyo hawa Academic Atheists, Activist Atheist/Agnostics, Seeker Agnostics, Antitheists, Non-Theists, and the Ritual Atheists

Wanatokea wapi?
Ndo ujue kwamba binadamu hatutokaa tukubaliane kwenye kitu chochote kile .
 
Kwani atheist mmewahi kukubaliana kutowepo Mungu? Kama jibu ni ndiyo hawa Academic Atheists, Activist Atheist/Agnostics, Seeker Agnostics, Antitheists, Non-Theists, and the Ritual Atheists

Wanatokea wapi?
Ndo ujue kwamba binadamu hatutokaa tukubaliane kwenye kitu chochote kile .
Huwa mda mwingine nahisi hizi battle za asili ya uhalisia/Mungu/Uwepo na kila kitu zitaendeleaga milele na milele.

Maana naamini wote kutoka dini zote kulingana na ukweli baadhi yao wataqualify kuingia mbinguni. Na kutokana na asili ya Mungu ataendelea kuwa infinity kwao so lazima mijadala itaendelea kuhusu ibada mwanzo mwisho.

The basic truth itabaki 'We are of God and we live for mankind' which is actually a single repeating statement.

Just like: “ ‘Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote na kwa akili yako yote’. Hii ndiyo amri kuu na ya kwanza. Ya pili inafanana na hiyo: ‘Mpende jirani yako kama unavyojipenda wewe mwenyewe’. Sheria yote ya Mose na mafundisho ya manabii vinategemea amri hizi mbili.”
 
Hiki ulichokiandika kimemili katika falsafa zaidi kuliko uhalisia. Yaani umejibu swali bila kujua wazo ni nini, hii imekupekea kukosea katika kujibu swali.

Hujaonyesha mimi nawezaje kuwa wazo ? Mimi ni nafsi ambaye nimeundwa au ni mjumuiko wa roho na mwili.

Labda tujadili kwanza maana ya tamko wazo. Sababu hiki mnachokiandika kwanza ni matumizi mabaya ya tamoo wazo, kwa maana lugha inakataa matumizi haya ya tamko hili wazo kulipa sifa za uhai yaani kiumbe chenye akili.

Naomba utusaidie au unisaidie kitu kimoja, naomba unipe maana ya tanko "Wazo".
Wazungu wana msemo unasema: Let us not get caught up in semantics.

Na hata kama kungekuwa na tafsiri rasmi za hivi 'vitu' vilivyo katika hali za ki-wazowazo bado lazima tutapwaya kwa sababu sio vitu. Vitu kama akili, utambuzi, wazo, idea, concept havikamiliki bila kupelekea circular reasoning kadha wa kadha.

Moja kati ya vitu hatujavitafsiri vizuri ni akili/intelligence na utambuzi/consciousness hivi ndivyo ninavyovizungumzia kila ninaposema wazo hai. Katika kuichambua na wenzangu tukakuta kuna nishati fulani inayopower mawazo yaliyo katika hali hiyo. Ni kama entity moja tu hivi.............. ndicho kinachozungumziwa humu.

Kwani nikikuuliza unaposema wewe ni nafsi- hicho 'kinafsi' kipo katika hali gani? Hata roho nayo ipo katika hali gani? Nikisema vipo kiwazowazo roho ikiwa in essence wazo pure toka kwa Mola na nafsi ikiwa ni wazo hai unaloendelea kulijenga kwa mchakato unaoitwa kuishi na kuwa 'being'. Hapo vipi?
Hapa itabidi unipe ushahid au kuonyesha wapi falsafa imekusaidia kuujia ukweli na uhalisia. Maana yake ingekuwa hivyo basi kina Plato, Socrates, Aristotle, Pythagoras wote wangepatia katika kuelezea chanzo cha ulimwengu na maisha, au wana Atomu kadhalika.

Nachokijua mimi kuhusu falsafa na Wanafalsafa ni kuwa walikuwa na maswali sahihi ila walikosa njia za kuwapa majibu sahihi.
Philosophy faster definitions: Tafsiri za harakaharaka😂😂
1. the study of the fundamental nature of knowledge, reality, and existence, especially when considered as an academic discipline.
2.a theory or attitude that acts as a guiding principle for behaviour.

Waliotutangulia wakubwa ikiwamo mitume na manabii wamekuwa wakituelekeza elimu ya uhalisia upojepoje - moja kati ya tafsiri ya wanafalsafa.

Popote ninapoona mtu anajaribu kuuelewa ukweli wa uwepo wetu ulivyo naona anatumia falsafa, kuna muda tunakosa vipande fulani vya ukweli basi Mola anatupatia mafunuo kuzikamilisha falsafa zetu tunazoendelea kujifunza. Inaweza kupitia kwa Roho mtakatifu aliye ndani yako, kupitia mtu mwingine ambaye tutamuita nabiy/mtume.

Falsafa ikimtambua Mungu hiyo huitwa dini [my take hii sentensi ya mwisho]
 
Kwa hiyo kwako wewe wazo la Mungu unalipata kupitia assumption baada ya kujiuliza maswali kadhaa ambayo ukakosa majibu?
Siwezi kusema nikakosa majibu, bali kutokana na kwamba uhalisia umeambaa uwanda mpana nitasema nikayapata majibu kwa Mungu☺

Mkuu unaweza kuhisi haya mambo yametenganaaaa kumbe wala. Ni kitu kimoja kinachoendelea. Ukitaka watu watawanyike muite mfizikia, tena yule wa experimental physics kabisa muulize ni kwavipi kuna phenomenon kama;

Why does observation collapse the wave function

Wanaokosa majibu hapa ni ambao hawajakubali kuitambua cosciousness, ila walioitambua wanayo majibu tayari. Sema wewe unaweza kuwashutumu kusema wamekosa majibu basi ndo wakaamua kurukia 'concepts' ambazo hazipo kutokana na uvivu.
 
Cheka ujinga wako mi nakuelekeza unaniona Joker

Mimi nikosoe tena?

Au umesahau wewe ndio ulikuwa una hilo jukumu la kukikosoa biblia na tumefika hapa kwasababu hujataka kufata kanuni zilizowekwa?

Hiyo paragraph ya mwisho hapo ni dua ukituombea kwa Allah? Una hakika amejiunga JF a umeamua kujichosha tu?
Paragraph ya mwisho nimecheka sana, difinisheni ya kuvurugwa na kuvurugikwa😂😂.

Nikasema hizi sasa ni bhangi zipunguze, hivi Mr. Scars unataka kusema hata difinisheni ya Mungu tu huijui? Ni kwamba anao ujuzi wote wa tunayoyafanya popote. In fact hapo tunapofanya hayo mambo yupo na anatuwezesha. So akiandika dua yake humu JF ishasikika.

Sasa usichanganye huo uwepo wake: Ukiwa na watoto watatu ukawapa wazo la 'kutafuta mali kwa bidii'. Popote watakapokuwa hao wanao watakuwa na wazo lako, wazo ni moja, lipo sehemu tatu na hawezi mtu akasema 'ninalo hilo wazo huku, so halipo huko...... wazo sio kitu

Na nikupongeze kitu kimoja: umetambua kwamba kitu/mambo yanaweza kuwa sahihi au kuwa na mantiki kulingana na mfumo ulioukubali. Ni kweli kabisa ukijikita katika dini moja unaweza kuukataa ukweli mwingine kisa tu,.... lakini ukabaki kuwa kweli. Safi sana kwa kumuelekeza Kisai asiwe analeta mahubiri halafu anang'ang'ana ndio uhalisia. Uhalisia wenyewe upo mwingi tu kuna uislamu, uhindu, ukristu, ub....... many many realities. Fuata ushauri wa draga ondoa kwanza ego hizo. Fanaticism is real
 
Kwani atheist mmewahi kukubaliana kutowepo Mungu? Kama jibu ni ndiyo hawa Academic Atheists, Activist Atheist/Agnostics, Seeker Agnostics, Antitheists, Non-Theists, and the Ritual Atheists

Wanatokea wapi?
Ndo ujue kwamba binadamu hatutokaa tukubaliane kwenye kitu chochote kile .
Atheists unawahusishaje na hayo makundi mengine?
 
Siwezi kusema nikakosa majibu, bali kutokana na kwamba uhalisia umeambaa uwanda mpana nitasema nikayapata majibu kwa Mungu☺

Mkuu unaweza kuhisi haya mambo yametenganaaaa kumbe wala. Ni kitu kimoja kinachoendelea. Ukitaka watu watawanyike muite mfizikia, tena yule wa experimental physics kabisa muulize ni kwavipi kuna phenomenon kama;

Why does observation collapse the wave function

Wanaokosa majibu hapa ni ambao hawajakubali kuitambua cosciousness, ila walioitambua wanayo majibu tayari. Sema wewe unaweza kuwashutumu kusema wamekosa majibu basi ndo wakaamua kurukia 'concepts' ambazo hazipo kutokana na uvivu.
Ukisema umepata majibu kwa Mungu hilo ni jambo la mwishoni ambalo lilitanguliwa na wewe kujua Mungu yupo

Swali langu limezungumzia kabla hujamjua Mungu, ulitumia njia gani kama sio kukosa kwako majibu ya maswali ambayo yalikupelekea ufikirie kipo kisababishi ambacho ukakipa jina la Mungu?
 
Ukisema umepata majibu kwa Mungu hilo ni jambo la mwishoni ambalo lilitanguliwa na wewe kujua Mungu yupo

Swali langu limezungumzia kabla hujamjua Mungu, ulitumia njia gani kama sio kukosa kwako majibu ya maswali ambayo yalikupelekea ufikirie kipo kisababishi ambacho ukakipa jina la Mungu?
Kwa kweli mzeebaba hapo kabla kulikuwa na situation tata: Nilishakuambia na mwanzo hakuna sababu kabla ya hii point zero, in fact hii pointi ndiyo inadefine sababu zote mbele yake.

Nilikuwa na nipo full data kuhusu Mungu hayupo na zilimake sense kabisa, pia nilikuwa na data full za kwamba Mungu yupo nazo zilimake sense kabisa. Zote zilianza na affirmation ya a-priori yake bila sababu kabla yake.

Kwa kutopenda kukosea nilitamani nipate japo kijisababu kimoja cha kuupendelea upande mmoja na sio mwingine na nilikosa.

Basi one moment nikakaa nikajiambia neno moja tu 'FREE WILLL' halafu nikaamua kuchagua upande mmoja ambao ninauishi hata sasa. That is how it works.
 
A lakini ukabaki kuwa kweli. Safi sana kwa kumuelekeza @Kisai asiwe analeta mahubiri halafu anang'ang'ana ndio uhalisia.
Naanzia hapa kwa sababu hili umelileta kwa ufupi. Mahubiri ni nini ? Je mahubiri hayawezi kuwa uhalisia au lini mahubiri hayajawahi kuwa uhalisia ?

Mfano naposema acheni zinaa, lini zinaa ilikuwa nzuri ? Kuacha zinaa ni uhalisia au ni kinyume chake ?

Sasa naomba unionyeshe wapi nimeleta mahubiri.

Jaribuni kuchambua hoja na msikimbie hoja. Mfano kuna sehemu nimekuomba uelezee maana ya tamko "wazo" matokeo yake hukufanya hivyo ukaanza kuongelea mambo mengine yasiyo husiana na swali nililo kuuliza, huku ni kutokuwa makini na hoja ya aliye dhidi yako.
 
Na hata kama kungekuwa na tafsiri rasmi za hivi 'vitu' vilivyo katika hali za ki-wazowazo bado lazima tutapwaya kwa sababu sio vitu. Vitu kama akili, utambuzi, wazo, idea, concept havikamiliki bila kupelekea
Kivipi ?
Moja kati ya vitu hatujavitafsiri vizuri ni akili/intelligence na utambuzi/consciousness hivi ndivyo ninavyovizungumzia kila ninaposema wazo hai.
Nani haja tafsiri vizuri tamko hili ? Kwangu mimi ni kinyume nimeshaelezea zaidi ya mara mbili maana ya tamko "AKILI" tena kwa maana yenyekujitosheleza.

Nipe maana ya neno wazo na utupe msingi wake.
Katika kuichambua na wenzangu tukakuta kuna nishati fulani inayopower mawazo yaliyo katika hali hiyo. Ni kama entity moja tu hivi.............. ndicho kinachozungumziwa humu.
Mlitumia marejeo gani katika huo uchambuzi wenu huo ? Hiyo nishati mliijuaje na inaitwaje au ina sifa gani ? Sababu maelezo yako haya. yameishia juu juu.
AnyaKwani nikikuuliza unaposema wewe ni nafsi- hicho 'kinafsi' kipo katika hali gani?
Nafsi ni roho na mwili. Roho ni kitu kisocho onekana chenye mafungamano ya moja kwa moja mwili na kuufanya mwili kuwa hai.
Nikisema vipo kiwazowazo roho ikiwa in essence wazo pure toka kwa Mola na nafsi ikiwa ni wazo hai unaloendelea kulijenga kwa mchakato unaoitwa kuishi na kuwa 'being'. Hapo vipi?
Hili ni kosa sababu umeandika ya uongo na kinyume na uhalisia.
 
Waliotutangulia wakubwa ikiwamo mitume na manabii wamekuwa wakituelekeza elimu ya uhalisia upojepoje - moja kati ya tafsiri ya wanafalsafa.
Popote ninapoona mtu anajaribu kuuelewa ukweli wa uwepo wetu ulivyo naona anatumia falsafa....... kuna muda tunakosa vipande fulani vya ukweli basi Mola anatupatia mafunuo kuzikamilisha falsafa zetu tunazoendelea kujifunza. Inaweza kupitia kwa Roho mtakatifu aliye ndani yako, kupitia mtu mwingine ambaye tutamuita nabiy/mtume. Falsafa ikimtambua Mungu hiyo huitwa dini [my take hii sentensi ya mwisho]
Hujajibu hoja yangu ya msingi, umesema ya kuwa Falsafa inamsaidia mtu kuujua ukweli, nikajenga hija ya kuwa tuonyeshe kwa namna gani falsafa humfanya mtu kuujua ukweli na utupe ushahidi. Hili ndiyo swali langu la msingi. Sasa ulichokifanya wewe ni ndiyo kama wanachokifanya Atheists kila silu kukimbia hoja. Mambo hayaendi hivyo.
 
Back
Top Bottom