Uteuzi: January Makamba ateuliwa kuwa Waziri wa Nishati. Ndugulile, Kalemani, Chamuriho na AG Kilangi watenguliwa, Feleshi ateuliwa

Uteuzi: January Makamba ateuliwa kuwa Waziri wa Nishati. Ndugulile, Kalemani, Chamuriho na AG Kilangi watenguliwa, Feleshi ateuliwa

Kagoma kuachia hiyo Wizara huyo gaidi.
Wizara zote nyeti wamepewa wanawake, afya ,ulinzi,tamisemi, elimu,[emoji18][emoji18]mwigulu namshauri aachie wizara ya fedha mapema[emoji33][emoji33]
 
Wachaga tulio tanesko tutapumua kidogo. Loh ilikua Kama mchaga unaongoza kitengo Fulani Basi tulikua tunajua anytime 't' naweza zushiwa jambo
 
Mbarawa ndani ya Nyumba nilisikitika Sana mwendazake kumwacha huyu maana ni mchapakazi Sana Magufuli kusema kweli hakuipenda ZANZIBAR na alikuwa na UKABILA SANAA
 
Ndio hivyo tulivyoambiwa usiku huu , kwamba kuna wateule na watenguliwa wapya wako njiani kuja tena baada ya hawa wa leo kuapishwa .

Tunaambiwa hii ni mbinu mpya ya kubadili viongozi .

Tuendelee kusubiri tuone wateule wapya wanaokuja .
 
Ndungilile alikuwa hana uwezo wa kuongoza ile wizara, ilishmshinda, chamuriho huyo ndo kabsa kati ya mawaziri ambao hawafahamik kabsa huyu ndo wa kwanza, ujenzi kunahekaheka ye yupo tu..kalleman timu Chato imemtoa pale..AG huyu hpana kwa kweli mama umefanya vizuri,
Tukianza tena umeme wa mgao lazima kuna atakayewajibu watanzania nini kinaendelea
 
Mkuu tunajadili bila kutukana, Kama hauni tunavyoyumba fumba macho kidg, halafu fumbua utaelewa... Yaan unaona sa iv kila siku teuzi teuzi hakuna la maana sa makamba nae wazir jamani hii nchi inavituko vikuu
Makamba ni mara yake ya kwanza hii kuwa Waziri?
 
Rais Samia Suluhu kafanya mabadiliko madogo kwenye baraza la Mawaziri na mwanasheria mkuu wa Serikali kama ifuatavyo

  1. Rais Samia Suluhu amemteua Dkt. Stergomena Tax kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la kujenga Taifa, anachukua nafasi ya marehemu Elias Kwandikwa
  2. Dkt. Ashatu Kijaji ameteuliwa kuwa waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya habari kuchukua nafasi ya Dkt. Faustine Ndugulile ambae uteuzi wake umetenguliwa
  3. January Makamba anachukua nafasi ya Merdard Kalemani wizara ya Nishati
  4. Makame Mbarawa anachukua nafasi ya Chamuriho wizara ya ujenzi na uchukuzi
  5. Dkt. Feleshi anachukua nafasi ya Kilangi kuwa Mwanasheria mkuu wa Serikali


View attachment 1935268
View attachment 1935270
Weekend njema wapendwa.
Nawasalimu kwa jina la Jamhuri wa Tanzania.
Hii ndio Tanzania, au sio ndugu zangu!!!!
 
Ha ha ; hakuna cha kuchange mzee whether kuna jambo lipo sawa au lah : kubalini tu hadi 2025. Na mkikaa vibaya anaendelea au atamkabidhi mwinyi.

Mwinyi anakuja kuwapigisha kwato. Nchi inatema cheche ...... checheee. Mtaishia ku comment tu but mambo ndiyo yapo hivo Fire Fire [emoji91].

Makanja wameshaanza kusogea jikoni na wote watakuja jikoni ni suala la muda tu.

Komboeni nchi yenu; acheni kupoteza poteza muda kwa social media ; fanyeni maamuzi sahihi.

Hopefully unayajua maamuzi sahihi ni yapi.

Mzee wa Msoga, from a disant ..... Mzee yule kwake ana Warehouse kabjsa Ina USD kama bank; yaani humo ndani unaingia Na Forklifts hatari sana.

Mama ni Ubavu wa Mzee wa Msoga. Hawezi kupindua chochote hata akitaka kupindua.

Mama anaupiga mwingi safi sana
General, ulimwengu alisema Kuna uwezekano Yale ya guinea yanafika EA, ukwel mama anaupinga mwingiiiiiiiiii...
 
Kalemani amepambana sana umeme vijijini
Kuna Uzi upo humu ulitabir haya makamba atachukua nafasi kipindi ile ya mifumo ya luku kusimama
Aliyepambana sana na umeme wa vijijini ni Muhongo!! Usema ovyo wa Muhongo ulisaidia sana, kwa sababu wakati hili zoezi linaanza watu walishaanza habari za kulipwa sehemu zitakopita nguzo! Muhongo kama kawaida yake, akasema "halipwi mtu", na tukiona kijiji kinaleta mambo ya kutaka kulipwa, tunawaruka, tunaenda kule wanakohitaji umeme. Hili Muhongo sitamsahau hata chembe kwa sababu nakumbuka Bush kwetu tulitaka kuwekewa umeme mwaka 1995, lakini ikashindikana baada ya kijiji cha kabla yetu watu wake kugoma kukatwa miti yao (wanafanya sana kilimo cha miti) hadi walipwe! Zoezi likaishia hapo, tukaja kupata 2015.
 
Back
Top Bottom