Uteuzi: January Makamba ateuliwa kuwa Waziri wa Nishati. Ndugulile, Kalemani, Chamuriho na AG Kilangi watenguliwa, Feleshi ateuliwa

Hongera kwa wote walio teuliwa hakika ni wachapa kazi hodari.

Makamba na Kijji ni wachapa kazi hodari na makini sana.

AG Mteule Dr. Feleshi Jembe haswaa, mtu makini na mtenda haki kwa wote.
 
Ndio maana yake na nguzo ikichakaa wakija kubadilisha hakuna kuichukua waniachie gogo langu nichanje kuni.
 
Hii nchi inapiga hatua mbili mbele alafu inarudi hatua tatu nyuma, ni ngumu sana kufika huko tunapopafikiria
 
Kazi iendelee.

Hivi mawasiliano ni jambo la muungano? Mbona Makame ameteuliwa kwenye wizara ambayo sio ya Muungano wakati yeye ni Mzanzibari?

Ama ndio zamu ya wazanzibari?
Ila kumbuka alikuwa Waziri katika Wizara hiyo wakati wa Mwendazake.
 
Tanesco ni utility company hawauzi vifaa vya umeme lile ni shirika linalotoa/linalouza huduma na sio shirika linalouza vifaa. Ukielewa hilo hutatoa hoja zako hizo.

Mkuu isiwe inshu Wewe endelea kukomaa hivyo hivyo na hizo gharama unazotaka. Ila Kuna nchi nyingi tu duniani huduma za kuunganishiwa umeme ni bure. Sijawahi kufika South African lakini ni moja wapo ya nchi za hivyo
 
Kuna mdau jn alinusa harufu ya makamba kurudi ulingoni bila shaka jikoni bado kunavuja
 
Bora mzee Chamuriho ametolewa ujenzi maana alikuwa mzigo mzito,
sasa Prof Mbarawa fuatilia ujenzi wa barabara,
 
Usipende kuwaita watanzania wanyonge
 
😤😤😤 Hivi post yangu ya Makamba inahusiana vipi na ili unganisho lako la huu upuuzi

For some reason I can’t see the middle finger ya kukupa.
 
Jk anaupiga mwingi sio kidogo....
Ile safu yake yoote imerudi ulingoni.
Bado sijajua ni PRC au USA ndo atanufaika.
Ila naona USA ndo anaula zaidi.
 
Kabudi, Ndalichako, Mpango wakati wanateuliwa kwa mara ya kwanza hawakuwa wabunge
Ndio shida ya watanzania wanaona sasa tu kisa mama ndio kafanya ila huko nyuma kipindi cha mwendazake akiyafanya haya walikua kimya
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…