Uteuzi: January Makamba ateuliwa kuwa Waziri wa Nishati. Ndugulile, Kalemani, Chamuriho na AG Kilangi watenguliwa, Feleshi ateuliwa

Mimi bibi yangu kizaa baba ni msukuma tena Nyantuzu ila mimi sio Msukuma,Stegomena sio Msukuma
 
Huyo January mnamuona malaika? watz kumbukumbu hakuna.
Usishangae sana, January kawekeza Sana siasa za mitandaoni.
Humu kuna vijana wake wengi Sana. Yeye ndio alikuwa muasisi wa lumumba buku 7, na wale vijana wa IT masaki
 
Katika hao ni nani makini?
Makamba alikuwa waziri Toka enzi za kikwete, hakuna jipya
 
Mimi bibi yangu kizaa baba ni msukuma tena Nyantuzu ila mimi sio Msukuma,Stegomena sio Msukuma
Ukisema sio msukuma, basi tafsiri yake ni mjerumani. Sasa inakuwaje mjerumani anateuliwa kuwa waziri?
Yote kwa yote, kwa wanaCCM hakuna jipya
 
Mini grid ndio nini ? Vyanzo vya uzslishaji vya Tanesco vinazalisha uneme mwingi kuliko tunao utumia.

Uzalishaji uko karibu 2000MW na matumizi yapo karibu 1600MW, tatizo ni usambazaji.
Miundo mbinu ya usambazaji ni hafifu na mingine imechoka mbali ya kutokidhi mahitaji ya wakati huu.
 
Hii nchi inapiga hatua mbili mbele alafu inarudi hatua tatu nyuma, ni ngumu sana kufika huko tunapopafikiria
Mpaka ubadhirifu wa Mali za umma utakapokoma ndio Nchi itapiga hatua nyingi kwenda mbele, lakini hiyo ni ngumu kwa sasa maana watu wanaamini katika "KAZI NA BATA" Hii falsafa hii haiwezi kuipeleka Nchi mbele, Zinatafutwa kisha wengine wanapanga namna ya kuzila, Unaona hata Spika anashangaa safari za Dom - Dar zimezidi, Huo ni mfano mdogo tu, kwa kweli tujitahidi kubana matumizi kama tunaitakia mema nchi yetu,
 
Katika hao ni nani makini?
Makamba alikuwa waziri Toka enzi za kikwete, hakuna jipya
Wote ni makini,uzoefu wa Makamba,Mbarawa,Tax na Wengine utakua na tija kwenye awamu ya 6. Kwa maoni yangu ningependa Mama abadilishe baadhi ya Mawaziri ambao wanaonekana energy yao imeshuka,kuna mambo yanaanza kujirudia,business as usual.Kuna viongozi wamerelax na kusoma upepo
 
Ukisema sio msukuma, basi tafsiri yake ni mjerumani. Sasa inakuwaje mjerumani anateuliwa kuwa waziri?
Yote kwa yote, kwa wanaCCM hakuna jipya
Wote mko sawa kwa 50%. Madame Tax ni Msukuma kwa mama yake lakini Mjerumaniu kwa baba yake, she is more Deutsche oriented cultured, though remains a high breed of both traits
 
Rais wetu Mama Samia Mungu akubariki sana tena sana.
Hakika unaendelea kuwa bora kila kukicha.
Mungu azidi kumlinda.
Teuzi anazo zifanya zimetulia na zinaviwango vya juuu.
 
Sio wasukuma wa ndani kabisa,Stegomena sio Msukuma,Mama yake ndo Msukuma,baba yake alikuwa mjerumani
Yupo MTU mwenye akili timamu anaweza akadharau upande wa mama yake eti tu kwa kuwa baba yake ni wa kutoka mataifa ya nje ? , Hakuna kitu kama hicho Acheni chembe chembe za ubaguzi hizo
 
Hivi hadi Mimi nifike hatua za kupata teuzi kama hizo nifanyeje? au nitumie njia gani wakuu?
 
I think we are missing back ups, alivyofariki Mh Kuandikwa imeshindikana kureplace kutoka kundi la wabunge waliopo mpaka akatafutwa nje yao. Nashauri watu mbadala wawe wanaandaliwa katika hizi nafasi kubwa.
Waliopo ni wabunge wa kuunga mkono hoja tu mkuu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…