The Assassin
JF-Expert Member
- Oct 30, 2018
- 4,942
- 20,077
Kwamba Rais wa Muungano anaweza mteua mteule wa Rais wa Zanzibar? Hii imekaaje?Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali. Kwa mujibu wa taarifa illyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi Balozi Dkt. Moses Kusiluka, viongozi walioteuliwa ni kama ifuatavyo:-
Mhe. Dkt. Selemani Said Jafo (Mb.) ameteuliwa kuwa Waziri wa Viwanda na Biashara. Kabla ya uteuzi huu, Mhe. Dkt. Jafo alikuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira).
Mhe. Dkt. Ashatu Kachwamba Kijaji (Mb.) ameteuliwa kuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira). Kabla ya uteuzi huu, Mhe. Dkt. Kijaji alikuwa Waziri wa Viwanda na Biashara.
Mhandisi Yahya Ismail Samamba ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa Wizara va Madini. Kabla ya uteuzi huu, Mhandisi Samamba alikuwa Katibu Mendaji wa Tume ya Madini. Mhandisi Samamba anachukua nafasi ya Bw. Kheri Abdul Mahimbali ambaye atapangiwa kazi nyingine.
Bw. Yusuph Juma Mwenda ameteuliwa kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kabla ya uteuzi huu, Bw. Mwenda alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA).
Bw. Alphayo Japan Kidata ameteuliwa kuwa Mshauri wa Rais, Ofisi ya Rais - Ikulu. Kabla ya uteuzi huu, Bw. Kidata alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA)
Wametupa ajenda nyingine tena ya kwenda nayo siku mbili tatu hizi ikiandaliwa nyingine!Bw. Yusuph Juma Mwenda ameteuliwa kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA). Kabla ya uteuzi huu, Bw. Mwenda alikuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Zanzibar (ZRA).
Hamtakaa muelewe kitu,Ujinga upi hapo? Lengo lipi?
Au ndo inanyesha ili tuone panapovuja boss?🤣🤣🤣🤣
TRA ni ya muungano, lakini ZRA siyo. Kutoka ZRA kwenda TRA ni sawa, lakini kinyume chake haipo!Mm sijaelewa naomba msaada hivi inakuwa mzanzibari toka ZRA kwenda TRA kwa hizo ni tasisi za Muungano.?
Basi tufanye ni zubaisha bwege,elewesha Sasa weweHamtakaa muelewe kitu,
Ndio ilivyo wanatumia mbinu za zilizo tumiwa ba Ulaya MasharikiWametupa ajenda nyingine tena ya kwenda nayo siku mbili tatu hizi ikiandaliwa nyingine!
Sasa unamyofoaje mteule wa Rais wa Zanzibar?TRA ni ya muungano, lakini ZRA siyo. Kutoka ZRA kwenda TRA ni sawa, lakini kinyume chake haipo!
Mwenda si Mzanzibari,Mm sijaelewa naomba msaada hivi inakuwa mzanzibari toka ZRA kwenda TRA kwa hizo ni tasisi za Muungano.?
Kwani kuna waziri yeyote anayefanya chochote cha maana kwenye wizara yake? Wote wanaishia kupiga picha tu na kuonesha tai zao.Jaffo na biashara wapi na wapi labda wampe michezo
Kabla hakujakucha utapata ukweli woteRc chalamila naye?
Huenda walishazungumza nyuma ya pazia.Kwamba Rais wa Muungano anaweza mteua mteule wa Rais wa Zanzibar? Hii imekaaje?
Jamaa yuko fiti,Yusuph Mwenda..Mhasibu Mahiri (ADA,CPA-T),PGD Tax Management,MBA,LLB Laws…Diwani,Mayor-Kinondoni…Auditor,Zakayo🔥
Hayo ni makaratasi tu yenye maandishi ya kitaaluma. Hakuna cha umahiri wala nini?Yusuph Mwenda..Mhasibu Mahiri (ADA,CPA-T),PGD Tax Management,MBA,LLB Laws…Diwani,Mayor-Kinondoni…Auditor,Zakayo🔥