UTEUZI: Rais Samia ateua Majaji wa Mahakama Kuu

UTEUZI: Rais Samia ateua Majaji wa Mahakama Kuu

Kwa

Ukiangalia list ya wateule wote 22 utagundua kwamba zaidi ya asilimia 80 ya wateule wote kwa nafasi za ujaji wametokea mahakama na baadhi kwenye ofisi za wanasheria wa serikali.

Lakini mahakama kuu inasikiliza mashauri yenye wigo mpana zaidi mfano land tribunal, commercial, labour, tax nk.

Ningetarajia ili kukuza specialization uteuzi ungefanyika pia kupitia tribunals ambazo rufaa huenda mahakama kuu mfano CMA for labour cases, land tribunals for land matters FCC for commercial matters, tax nk. Wafanya maamuzi kwenye vyombo hivyo ambao ndio wanaozijua kiueledi sheria husika ndio wangepaswa kuwa promoted kwenye nafasi za ujaji ili kujenga jurisprudence (specialization).

Kutokufanya hivyo ni kuendelea kutengeneza mazingira ya mahakama kuu na mahakama ya rufaa kutokufanya kazi kiueledi hadi kufikia kutoa maamuzi kinzani (kama ilivyo kwa maamuzi mengi ya kesi za kazi yanavyoamuliwa kinyume na msingi uliowekwa na sheria husika)

Mfano jaji mteule mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka kumi kwenye uanasheria serikalini aende kuamua rufaa za mashauri ya kazi inayotokea CMA ambako ni purely labour laws tena kwa sasa hivi isiyohusisha serikali hawezi kuwa sawa na ambaye angetoka CMA.

Aidha maamuzi hayo yanademoralize utendaji kazi wa hizi tribunals na kuondoa misingi ambayo sheria ilimaanisha na kutengeneza ustawi katika secta husika

Ni rai yangu kwamba kabla ya uteuzi wa majaji, kigezo kinachohusu, specialization, uzoefu kwenye specialization, uweledi kwenye specialization vingezingatiwa ili kupromote high court yenye wabobezi na kuondoa mazoea ya kila jaji anaweza kufanya kesi yoyote.

Pia nashauri hizi tribunals zitazamwe kwa jicho la kipekee, si tu katika uteuzi wa majaji bali pia kwenye mabadiliko na marekebisho ya sheria husika.

Naomba kuwasilisha
Umenena vyema mkuu. Tatizo la nchi yetu uteuzi huangalia sana obedience/allegiance kwa mamlaka badala ya professionalism.
 
Umenena vyema mkuu. Tatizo la nchi yetu uteuzi huangalia sana obedience/allegiance kwa mamlaka badala ya professionalism.
Naamini haipaswi kuwa hivi hasa kwa tasnia nyeti kama ya sheria kwa sababu tusipoangalia hili mapema tunaweza kujikuta ni watu wa kutunga sheria na kuzitungua kila mara tofauti na nchi nyingine.
 
Kazi zigawiwe kwa uwezo na si jinsia, kabila, dini, kanda
 
tusisahau kuhesabiwa siku ya jumanne Agosi 23.
Sensa kwa maendeleo yako na kizazi chako.
 
Naamini haipaswi kuwa hivi hasa kwa tasnia nyeti kama ya sheria kwa sababu tusipoangalia hili mapema tunaweza kujikuta ni watu wa kutunga sheria na kuzitungua kila mara tofauti na nchi nyingine.
Sasa we niambie majaji walioendesha kesi ya mbowe? Yaani utafikiri vikao vya mahojiano ktk kamati kuu ya CCM.
 
Hakuna jaji hapo, sifa kuu lazima uwe mwanachama wa chama cha huyo anayekuteua. Hao ni majaji wa kimkakati.
 
V8 22 hizo zinunuliwe haraka wapewe ma Jaji wapya !! Kila V8 moja ni Mil 330. Mafuta kwa siku lita 30 sawa na Tshs 50 sawa na 145,000.
 
Back
Top Bottom