Uteuzi wa Afande Ramadhani Kingai kuwa DCI (Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai). Je, Rais Samia amepotoshwa?

Hao jamaa huwa wanafanya kazi kwa manufaa ya serikali ya CCM, ndio maana licha ya mabaya yao yote, bado hupewa vyeo na viongozi wa serikali ya CCM kwa sababu CCM ndio huwatuma kufanya ubaya kwa watanzania wenzao nao hukubali.

Ajabu zaidi huu uteuzi unafanyika katikati ya maridhiano ya kisanii, lakini kila mkiambiwa hawa jamaa hawapo serious hamtaki kuelewa.
 
Raia gani hao unaowazungumzia? mliomba huruma ya Rais ya kazi gani kama Mbowe alionewa? upuuzi mtupu na huna ulijualo.
 
Kama tunaamini urais ni taasisi basi hakuna haja ya kuwa na wasiwasi juu ya teuzi za rais. Naamini vetting ya kutosha hufanyika kabla rais hajaamua kutangaza uteuzi.

Na pia rais hawezi kuendesha mambo yake kwa kutegemea matakwa ya individuals. Taratibu zinazingatiwa.
 
Raia gani hao unaowazungumzia? mliomba huruma ya Rais ya kazi gani kama Mbowe alionewa? upuuzi mtupu na huna ulijualo.
Huruma aliomba nani? na aliyesema mahakama zetu zinafanya kazi kwa huruma ni nani? kwa sheria ipi?

Kama kwa ule ushahidi uliokuwa unatolewa kwenye ile kesi ya Mbowe na Kingai na wenzake bado unaamini Mbowe alihurumiwa utakuwa una mtindio wa ubongo.
 
IMETHIBITISHWA Mahakamani huyo Ramadhani Kingai HAJUI hata namna ya utekekezaji wa GPO.
Na kama mtoto wa Primary alikuwa akiomba kwenda maliwato kujisidia kila akipigwa swali gumu.

Huyu ndiyo Mkuu wa Upelelezi.

What a joke!
 
Wewe ndio una faili lake mpaka ujue hafai? Cv yake umeisoma?
 
Uteuzi huu hauligawi Taifa, labda unagawa akili zako wewe na Saccos yako
 
Huyu mpumbafu Kingai aliyemponza Lt Denis Urio kufukizwa kazi?

Au Kuna Vingai wengi huko idara ya polisi?
 
Ndo mjue sasa aliyowahi kuyafanya mkamchukia hakujiamulia ilikuwa ni amri.

Ninyi huku nje ndo mnamuona mchafu ila wanaomjua vizuri huko ndani wanaona anafaa kwa nafasi aliyopewa.

Hii inanifundisha kuwa zile tuhuma hazikuwa zake kuna pahali zilipaswa kuelekezwa yeye alikuwa anatekeleza alichotumwa.
 
Kuna mambo mawili nimeona
1.Ama anapewa uteuzi kuwa ni mtoto wa Magufuli kikazi.
2.Au ameandaliwa zengwe aje kutumbuliwa kila kitu kinawezekana.
 
Kwa kweli inakatisha tamaa pale ambapo waovu wanapopewa mamlaka.

Kwa mambo kama haya, ni vigumu kuamini kuwa eti tumeamua kujenga Taifa ambalo viongozi wanatakiwa kuwa ni watu walio na dhamira na maadili ya kutenda haki kwa makundi yote.
 
Hata angeteuliwa nani ungesikia kelele tu kuna haja rais akiwa anataka kufanya teuzi awe anawahusisha,wabongo bhana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…