Uteuzi wa Afande Ramadhani Kingai kuwa DCI (Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai). Je, Rais Samia amepotoshwa?

Uteuzi wa Afande Ramadhani Kingai kuwa DCI (Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai). Je, Rais Samia amepotoshwa?

Ni huyu aliyekuwa anahusishwa na utekaji na yale mambo ya wasiojulikana, naona sasa nchi inahitaji mafia ili watu waheshimiane, serikali inajiona untouchable
Nasubiri kuona utaifanya nini serikali
 
Huyu yupo vizuri sana,

Yupo very straight kwenye mambo yake hana longo longo.

Nadhani wengi wanaopiga kelele hapa ni mambo ya kisiasa tu ila kiuweledi yupo vizuri.
DCI asiyejua PGO hafai kabisa
 
Kwanini kama Taifa tunarudia makosa ya kuteua watu wenye makando kando kama Afande Ramadhani Kingai? Huyu mtu kwa sasa anafahamika na kila Raia kwa matendo yake yaliyojidhihirisha pale Mahakamani wakati wa kesi ya Mbowe

Je, tunasubiri afanye ukatili na unyama wa kiasi gani kwenye hili Taifa?

Tulishajifunza wakati wa JPM umuhimu wa vetting ya viongozi kwa yaliyotokea. Je, bado tunaendelea kujifunza.

Afande Kingai hakupaswa kupewa nafasi ya DCI hata kidogo, Imani ya Raia kwa huyu mtu ni ndogo sana, Wakati wa kesi ya Mbowe huyu alihusishwa na utesaji na utekaji, Na hata majibu yake mahakamani alijichanganya sana kuhusu kuwahamisha watuhumiwa tokea kituo kimoja cha polisi kwenda kingine na malengo yake kuhusu utesaji

Uteuzi wa Afande Ramadhani Kingai kuwa Mkurugenzi wa makosa ya jinai unaligawa Taifa ambalo Rais Samia alikuwa anafanya jitihada za kuliunganisha kwa maridhiano

Kwenye kesi ya Mbowe pale mahakamani, Afande Kingai alikuwa shahidi mkuu upande wa jamhuri na ushahidi wake alioutoa pale mahakamani wa kuwanunulia watuhumiwa Mo energy ikawa mwanzo wa watu kuamini huyu Bwana ameshiriki Katika kesi ya mchongo kuanzia kudraft mpaka kupeleka mahakamani.

Afande Kingai alishindwa kujibu maswali ya mawakili wa utetezi hata moja na hata maswali yaliyohusiana na kitendea kazi chake ya General Orders of police (PGO) alionekana haelewi pale Mahakama ya uhujumu Uchumi.

Ushahidi wa Afande Kingai ambaye alikuwa Shahidi mkuu ulileta mkanganyiko pale Mahakama ya Uhujumu Uchumi na ndio ukawa mwanzo wa watu kufahamu siri ya kesi ya akina Mbowe pamoja na Kikosi kazi maalum kilichojumuisha Afande Goodluck

Maswali ya kujiuliza sisi kama Raia wa nchi hii:

Unawezaje kumpa mtu nafasi ya DCI wakati umma wa Watanzania wanafahamu huyu mtu amechafuka?

Je, huu ndio mwanzo wa watu kubambikiwa kesi za mauaji hapa nchini?

Je, uteuzi huu Bwana Kingai sio ni mwanzo wa kufumua madonda ambayo Rais Samia alishaanza kuyaponya?

Moja ya watu kuzidi kudai Katiba Mpya ni kutokana na uteuzi wa watu aina ya Afande Kingai, Tungekuwa na tume maalum ya kuchuja na kuteua aina ya watu kama Afande Kingai kama Rasimu ya Jaji Warioba alivyopendekeza tusingekuwa na utata.
Huu ndio utopolo mtupu.
Ndio maana madai ya KATIBA MPYA ni muhimu. Nafasi kama hizi zinatakiwa kuombwa kama ada ya ufahamu na uelewa hata akiteuliwa!
Na isitoshe nafasi hizi zinatakiwa kupitishwa bungeni na wahusika kwenda kujieleza Kwa Nini anaona anafaa kwenye hiyo nafasi na atafanya Nini? Yawepo maswali yenye tija sio ya kubeA
 
Matahira bhana!Mkiambiwa kuwa CCM haifai hamsikii,ninyi ni kukomaa tu na Samia.🐒🐒🐒
 
CCM ina laana,badala ya kuteua watu wenye weledi kama hawa, unateua Mapaka!🐒🐒🐒
 
Mbowe kashaingizwa chaka kwa maridhiano ya mchongo.
 
Kwanini kama Taifa tunarudia makosa ya kuteua watu wenye makando kando kama Afande Ramadhani Kingai? Huyu mtu kwa sasa anafahamika na kila Raia kwa matendo yake yaliyojidhihirisha pale Mahakamani wakati wa kesi ya Mbowe

Je, tunasubiri afanye ukatili na unyama wa kiasi gani kwenye hili Taifa?

Tulishajifunza wakati wa JPM umuhimu wa vetting ya viongozi kwa yaliyotokea. Je, bado tunaendelea kujifunza.

Afande Kingai hakupaswa kupewa nafasi ya DCI hata kidogo, Imani ya Raia kwa huyu mtu ni ndogo sana, Wakati wa kesi ya Mbowe huyu alihusishwa na utesaji na utekaji, Na hata majibu yake mahakamani alijichanganya sana kuhusu kuwahamisha watuhumiwa tokea kituo kimoja cha polisi kwenda kingine na malengo yake kuhusu utesaji

Uteuzi wa Afande Ramadhani Kingai kuwa Mkurugenzi wa makosa ya jinai unaligawa Taifa ambalo Rais Samia alikuwa anafanya jitihada za kuliunganisha kwa maridhiano

Kwenye kesi ya Mbowe pale mahakamani, Afande Kingai alikuwa shahidi mkuu upande wa jamhuri na ushahidi wake alioutoa pale mahakamani wa kuwanunulia watuhumiwa Mo energy ikawa mwanzo wa watu kuamini huyu Bwana ameshiriki Katika kesi ya mchongo kuanzia kudraft mpaka kupeleka mahakamani.

Afande Kingai alishindwa kujibu maswali ya mawakili wa utetezi hata moja na hata maswali yaliyohusiana na kitendea kazi chake ya General Orders of police (PGO) alionekana haelewi pale Mahakama ya uhujumu Uchumi.

Ushahidi wa Afande Kingai ambaye alikuwa Shahidi mkuu ulileta mkanganyiko pale Mahakama ya Uhujumu Uchumi na ndio ukawa mwanzo wa watu kufahamu siri ya kesi ya akina Mbowe pamoja na Kikosi kazi maalum kilichojumuisha Afande Goodluck

Maswali ya kujiuliza sisi kama Raia wa nchi hii:

Unawezaje kumpa mtu nafasi ya DCI wakati umma wa Watanzania wanafahamu huyu mtu amechafuka?

Je, huu ndio mwanzo wa watu kubambikiwa kesi za mauaji hapa nchini?

Je, uteuzi huu Bwana Kingai sio ni mwanzo wa kufumua madonda ambayo Rais Samia alishaanza kuyaponya?

Moja ya watu kuzidi kudai Katiba Mpya ni kutokana na uteuzi wa watu aina ya Afande Kingai, Tungekuwa na tume maalum ya kuchuja na kuteua aina ya watu kama Afande Kingai kama Rasimu ya Jaji Warioba alivyopendekeza tusingekuwa na utata.
Mtoa mada huna hoja. Je hayo aliyoyafanya kingai je ni maamuzi yake binafsi au ni maelekezo, juu yake yuko IGP na viongozi wengine kwanini hujajiuliza hill kabla ya kumlaumu.
 
Unawezaje kumpa mtu nafasi ya DCI wakati umma wa Watanzania wanafahamu huyu mtu amechafuka?

Je, huu ndio mwanzo wa watu kubambikiwa kesi za mauaji hapa nchini?
Binafsi naliwaza kwa sauti kuu, nahisi aqngekuja mbele ya jamii ili aseme kitu ili aweze kuaminika na umma.
 
MH Rais mama yetu Samia Suluhu Hassan kwakweli japo jeshi Zima la polisi limekuwa bovu Sanaa lakini Kuna wachache ambao Wana hofu ya Mungu, na Taasisi kubwa na ya muhimu kama hili jeshi halitakiwi kuwa na kiongozi asiyetoa Haki au Mwongo.

Kama mama una nia kweli ya kulirekebisha watu kama KINGAI hawakupaswa kupewa ofisi kubwa maana kwa UONGO na uonevu aliowafanyia watu akiwa ngazi za chini akiwa Ngazi uliyompa atakuwa mbaya zaidi.

Sio polisi mwenye maadili hasa msingiziaji mporaji wa haki za watu mtesaji ana damu kwenye vganja vyake.

Jiepushe nae, HAWEZI kutenda Haki tunakuomba Unda na kulisuka upya Hili jeshi lililopoteza maana ya jeshi la kusimamia Haki.

Kwa hili nasema WAMBURA SAWA LAKINI SIO KINGAI, HAPANA.
Wacha watu wakule maisha

Pambana na wewe
 
Waliomshauri Amiri Jeshi Mkuu Kumteuwa Camilius Wambura kuwa IGP na Ramadhani Kingai kuwa DCI hakika jicho lao limelega ipasavyo.

Wambura ni muadilifu sana, ana nidhamu , ni msikivu/mfuatiliaji wa shida za watendaji wa chini yaani hata awe ni Constable atafuatilia na haki itatendeka, pia ni mtu mwenye ushirikiano mzuri sana na vyombo vingine/ kimsingi ana busara sana. Lakini kubwa kuliko yote ni mtendaji mahiri/hardworking.

Kuhusu CP Ramadhan Kingai jamaa yupo Kikazi sana na ni mtu anayejali na kuheshimu Misingi ya kazi. Mtendaji Mzuri, mfuatiliaji yaani sio mtu wakufanya jambo bila kujiridhisha uhalisia wake, anazingatia sana Nidhamu ya Kijeshi. Ni mtu anayefikika na msikivu(Approachable). Kiufupi jamaa akili yake imetulia vizuri. Kingai ni hazina na ninampongeza aliyemshauri Rais.

Kuhusu CP Liberatus Saba's aliyeteuliwa kuongoza mambo ya Fedha na Logistics siwezi kumzungumzia lakini inasemekana JAMAA NI MSAFI SANA na MUADILIFU

Kuhusu CP Awadhi aliyeteuliwa kuwa Mkurugenzi wa Operation kwa kweli jamaa Kazi anaiweza sana na sio mtu wa ofisini tu bali pia ni mtu wa field kwa sana. Yeye ni mtu anayependa kuona sheria zilizowekwa zinafuatwa kama zilivyoandikwa na hana cha kuangalia excuse za mazingira nk nk.

Japo hapa inaweza kutafsiriwa kama NI AINA YA KIONGOZI ALIYE RIGID, Mfano sheria inakataza eneo fulani dereva kuendesha speed ya 50 hivyo akikukamata unaendesha 70 hata kama unamuwahisha mgonjwa Muhimbili kuokoa maisha yeye anaweza kukung'ang'ania tu.

Kwa hiyo ni Mtu wa kunyoosha haswa yeye anachoangalia ni utaratibu, yaani hata itokee amekukabidhi chupa ya maji halafu ukayanywa pengine ulihitaji kumeza dawa kuponya kichwa chako yeye atakukomalia kuwa ulitakiwa upate ruhusa na sio kujiamlia.

Na vilevile inasemekana ni Mtu ambaye hana mahusiano mazuri na vyombo vingine vya Ulinzi na Usalama japo hapa binafsi sijajua ni kwanini na kivipi.

Kimsingi jamaa katika kazi ni jembe hasa. Hayo mengine nadhani anaweza kushauriwa kulingana na unyeti wa Madaraka aliyopewa sasa.
 
Wakati huku Tanzania akina Kingai walipandiswa cheo, huko Kenya ambako kuna Rais wa watu hali ni Tofauti.
 
Back
Top Bottom