Uthibitisho: Mwigulu Nchemba ni majina bandia ila vyeti ni vya kweli

Uthibitisho: Mwigulu Nchemba ni majina bandia ila vyeti ni vya kweli

Dhana ya kwamba atang'oka kwa hii issue haitowezekana. Nadhani tuendelee na maisha yetu tu maana hata yule Diamond siyo jina lake halisi lakini sisikii mtu akiuliza
mkuu umetisha, watakuelewa wachache sana...leo kazi yangu ni kutoa shikamoo tu
shikamoo great thinker
 
Mtaumiza vichwa sana. Ukweli ni kwamba Lameck Madelu Mkumbo alifanya mtihana wa darasa la saba akashindwa.

Baada ya kushindwa darasa la saba mara ya kwanza, Lameck Madelu Mkumbo akaamua kurudia shule ya msingi. Kwakuwa miaka hiyo kurudia shule ya msingi ilikuwa hairuhusiwi, ndipo Lameck Madelu Mkumbo, akachukua jina la Mwigulu Nchemba, kijana wa kisukuma aliyekuwa ameacha shule wakati huo akiwa darasa la tano.

Hivyo Lameck Madelu Mkumbo akasoma darasa la tano kwa kutumia jina la Mwigulu Nchemba hadi darasa la saba na akafaulu mtihani kwa jina hilo la Mwigulu Nchemba.

Hivyo Mwigulu Nchemba aka Lameck Madelu Mkumbo hakuiba cheti cha mtu bali alisoma kwa kutumia jina la mtu mwingine aliyekuwa ameacha shule wakati huo kwasababu zake.
"Kwakuwa miaka hiyo kurudia shule ya msingi ilikuwa hairuhusiwi" hapo ndio kwenye kosa na forgery imeanzia hapo, mana hii kama kweli ni lazima afanye forgery ya cheti cha kuzaliwa japo vyeti vyengine vya academic ni vyake....nahisi tu
 
Mkuu Isanga Family, kuna issues mbili zinazojitegemea. Uhakiki wa vyeti bandia ndio hoja iliyopo mezani na sio uhakiki wa majina.

Jina la Mwigulu Mchemba ndilo jina bandia, lakini aliyesoma ndio huyo Mwigulu, aliyehudhuria darasani ndiye huyo Mwigulu, mwenye akili ndani ya kicwa chake, ndio huyo Mwigulu, aliyehitimu, ndio huyo Mwigulu, hivyo vyeti vyake vyote ni bonafide genuine, na jina pia ni lake ila ni just a given name. Hakuna jinao yoyote kwa mtu yoyote kutmia jina lolote, popote.

Pasco
cheti cha kuzaliwa alikipataje?
 
Mwigulu kapiga sana chenga kwenye majibu yake na kuacha maswali kadhaa. Maana inatia shaka kwamba hiyo zamani yake mtu akirudi shule kutoka machungani, unaweza kutumia jina la nesi basi ukapata usajili. Kuna walakini bado hapo. Yupo Mwigulu mwenye jina hili.
Mpaka atakapoletwa au kuonekana Mwigulu Lameck Nchemba original, huyu ndie ninayemtambua ni original.

Mwigulu kasema namna alivyoyapata majina yake. Kinawashinda nini kuanzia hapo ili kuupata ukweli.

Au ndo ile tabia ya KUZUSHA jambo bila utafiti mkiumbuliwa, mnaachana nalo mnadandia jingine, mfano, UKUTA, Prof. Lipumba saga, Mbowe Hotels saga, Jacqueline Ndalichako saga, Lema kutaja machache.
 
Watu mpaka sasa hamjamuelewa Pasco hebu msomeni mstarinkwa mstari muelewa anachoandika hamtetei mtuhapa bali ameleta uzi ila ameandika kwa mafumbo isionekane anamkandamiza muheshimiwa....
 
Mi hili sjalielewa vizuri ....ina maana watu wawili wanatumia majina yanayofanana huku kila mtu na vyeti vyake .....necta wanatakiwa wasaidie kuweka hili jambo vizuri linatoa taswira mbaya kwa mh...
 
pasco eti tena veryfied user humu hawezi kudanganya kama amedanganya kwenye vyeti atashindwa kudanganya Jamii Forum hili nalo linahitaji Elimu kujua kwa mtu aliesoma shule na akafauru vizuri hawezi kutetea majina feki na vyeti bandia kwamba kimoja kipo sahihi kimoja hakipo sahihi..
MM nilifel shule ya msingi na jamaazangu ambo tulikuwa tunaongoza kutoka daras la kwanza wakafulu wasichana wa tano ambao hata kumi bora hawajawah kuingia wengi watoto wa waalimu na wengine wa matajir fulan pale kijijin kwe2 ilaa nashukuru mungu baba angu kanisomesha shule binafsi (R.I.P DAD) na nilifanikiwa kufika chuo kikuu ila wale wasichana wote walipiga zero form 4 kasoro 1 alifanikiwa kufika chuo sahv naamin sasa kumbe inawezekana kuna usanii mwingi kwenye matokeo ya shule ya msingi kuna watu wanafaulu ila kunauchakachuaji unafanyikaa ili watu fulanfulan wapate nafas na wale maskin wakose .MH nchemba kama alisomea jina la mtu aliyefaulu wakamficha mhusika akaenda yeye hapo anakosaa ilaa kama alichukua jina la mtu aliyekimbia shule akasomea yy na kufanya mtihan na kufaulu hana kosa hata kidogo kinachotakiwa sahv apige kazi 2
 
baiser kwa nini achukue jina la mtu darasa la saba una uhakika gani na matokeo ya chuo kama sio ya watu wengine fikiri zaidi ukifoji Elimu hata darasa la Nne zamani tulikua tunarudia ni kosa kabisa ni vile bongo tunaishi kwa mazoea ndio maana hata wewe ulimaliza chuo umetoa hayo mawazo Mkuu..
 
Wapo wengi wanao tumia majina ya kisukuma na maelezo Yao huwa Ni hayo hayo ya dactari wa kisukuma- Je wakati huo kulikua na madaktari wa kisukuma wangapi? JE Ni Kweli wakati huo alipo zaliwa kulikua na dactari wakisukuma? Tuendelee kutafakari
 
Mkuu Samari, alichoeleza humu Mwigulu ndio ukweli wake, usitake kumlisha maneno kwa kulazimishwa ukweli unaotuka wewe!, kuna kweli za aina tatu,
1. Ukweli unaosemwa kuwa ni kweli -spoken truth
2. Ukweli unaotakiwa kuwa ni ukweli-the purported truth
3. Ukweli halisi - the real and plain truth.

Kati ya kweli hizi, ni ukweli halisi tuu ndio utasimama mpaka mwisho, ukweli unaosemwa kuwa ni kweli unaweza kuwa ni uongo unasemwa na kuitwa ni kweli, ukweli unaotakiwa ni ule ukweli unaohitajika, ili uwe ukweli mfano miongini mwa sifa za rais, lazima awe ni Mtanzania, akitokea kijana wa banyamulenge kule mipakani, na anautaka urais, na akaupata, then hata ukweli ukiibua kuwa sio Mtanzania, ukweli unaotakiwa kuwa ni kusemwa ni Mtanzania.

Pasco
Pasco acha maneno ya ujanja ujanja yaaani unazunguka weeeeee Kama cheti feki....
 
1477144526150.jpg

Mambo haya tutayaona sana...
 
Pamoja na hayo ila huyu dogo ni kwikwi when it comes to shule, UDSM kule dep. Ya uchumi kaacha jina kubwa sana ndo maana BOT wakambeba kama alivyo na hata masters wamemsomesha wao
Kwikwi ndiyo kiswakitarafa gani tena? Aarrrrrgh! Uhondo unautia uchungu! Kwanini!
 
Labda ni usalama wa taifa, hivyo hatakiwi kujulikana julikana hovyo!
 
Wanabodi,
Katika zoezi la kusaka vyeti bandia, kuna watu wanashindwa kutofautisha kati ya vyeti bandia na majina bandia.

Cheti bandia ni cheti ambacho ama hakipo kabisa hivyo kimetengezwa cheti fake kwa forgery ama ni cheti cha kweli lakini anayekitumia sii mwenyewe mwenye cheti halisi, hivyo kufoji cheti cha mtu mwingine, hili ni kosa kubwa la jinai na huu ni wizi!.

Jina bandia ni kutumia majina ya kuunga unga ambayo sio majina yako halisi, lakini aliyeingia darasani kusoma ni wewe, aliyehitimu ni wewe, hivyo hicho cheti ulichokipata ni cheti halali na sio cheti bandia ila jina ndilo jina bandia.

Nimesoma utetezi wa Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba kuhusu tuhuma za kuwa na cheti bandia, nimejiridhisha kabisa tena pasi shaka kuwa vyeti vya Mhe. Mwingulu Nchemba sio vyeti fake ila majina ya Mwigulu Nchemba ndilo jina bandia.

Sio kila jina bandia ni forgery, kuna majina bandia yanayoitwa Nick Names sio forgery bali ni just given names. Given names hizo zinapokuwa registered kwenye vyeti, vyeti hivyo ni halali ila jina la mwenye cheti ndilo jina bandia ambalo halina kosa lolote kisheria.

Uthibitisho huu ni kufuatia utetezi huu wa Mhe. Mwingulu Nchemba umethibitisha jina la Mwigulu Nchemba ni jina bandia la mtu halisi aitwae mwenye given name ya Lameck Madelu Mkumbo ambaye hata majina hayo,hakuna jina lolote la wazazi wake wala jina la ukoo wake, kama anavyojieleza yeye mwenyewe.


Mkuu Mhe. Mwigulu, kwa vile hili bandiko nimelikutia page 33, na sijaweza kusoma mabandiko yate ya nyuma, hivyo siwezi kujua kama ulijibu haya, ila kwanza kwa heshma na taadhima, nakupongeza sana kujitokeza kujibu tuhuma, ila very unfortunately, majibu yako, hayajitoshelezi kabisa!, hakuna kitu chochote ulichojibu hapa, you leave more questions than answers and there is something fishy!.

Majina yana formula ya majina, na hayawezi kuijiibukia tuu hivi hivi, na formula hiyo ni universal, dunia nzima.

Jina lina given name, yaani jina ulilopewa wewe, hili given name linaweza kuwa moja au hata kumi, haijalishi, kwenye given name, ni lile jina unaloitwa, liwe la utoto, ubatizo, etc, Kiingeza linaitwa fast name!.

Jina la pili, ni lazima liwe ni jina la kwanza la mzazi wako, na hapa hakuna excuse, kama mwanzo kwenye given name, umetumia jina la nyumbani, la kilugha, then jina la pili lazima liwe jina la ubatizo, ukitangulia na jina la ubatizo, then jina la pili au liwe ni jina la kwanza, la mzazi wako, au ukitumia fast name ya majina mawili yote ya kwako, then jina la tatu ni lazima liwe ni jina la kwanza la mzazi wako!, na jina la nne ni lazima liwe ni jina la ukoo wenu yaani sir name.

Kwenye majina yako, sijaweza kuona jina la mzazi na jina la ukoo, huwezi kutumia majina yote ya given name bila jina la mzazi na jina la ukoo!.

Naomba wenye acess na immigration, fatulieni DN ya Mhe. Mwigulu Mchemba muone imeandikwaje, kwa sababu bila jina la mzazi na jina la ukoo mtu huwezi kupata passport kwa majina ya kuokotezwa!.

This is the begining of opening a pandora box, we have to reach to the bottom of this, ila asante sana kujitokeza na kujibu, kwa sababu uwongo, ukisemwa sana na kuachwa kurudiwa rudiwa bila kukanushwa hugeuka kuwa ni ukweli.

Kwa kuwasaidia wengine wasio jua, hakuna kosa lolote la jinai kujiita jina lolote la bandia na kuitumia popote.

Japo jina la Mwigulu Nchemba ni jina bandia ila vyeti vyake vyote ni vyeti halali.

Kutumia jina bandia, given name sio kosa kisheria na hakuna jinai yoyote! .

Hata mimi Pasco wa JF naweza kuisajili kama Mashokolokubangashe na nikatambulika kama Mashokolokubangashe na vyeti vyangu vyote vikasomeka Mashokolokubangashe na nikawa sijafanya kosa lolote la jinai, ila ikitokea kwenye ujazaji wa fomu zozote za kisheria kama hati ya kusafiria au cheti cha kuzaliwa lazima nitaonyesha majina halisi ya wazazi wangu, na ikitokea kule nako nimejiorodhesha jina la Mashokolokubangashe kuwa ni moja ya majina ya wazazi wangu, then hivyo inageuka forgery, cheating na ni kosa la jinai.

Hivyo natoa wito kwako wanaomtuhumu Mwigulu kudanga wapate uthibitisho toka NIDA na Uhamiaji, watayaona majina halisi wazazi wa Mhe. Mwigulu Lameck Nchemba.

Finally, wewe mwana Ilboru mwenzangu, ujege mara moja moja humu jf sio mpaka tuu kuja kujibu tuhuma, na ile shule iliokufikisha hapo uikumbukege!.
NB. Tukilimaliza vizuri hili zoezi la vyeti bandia, tunaweza kuamua kuanzisha msako wa wenye majina bandia, na kisha hata kwenye asili za watumishi wa umma, maana kuna a very interesting story ya kijana mmoja wa kabila la Kihaya, mwenye jina la Katto.
Asante.
Pasco
Rejea, kati ya wagombea wote wa urais wa CCM, Mhe. Mwingulu, ndie aliye ni impress sana kuliko wote kwa kuwa the most genuine kumbe...
Mwigulu Lameck Nchemba, Is The Most Genuine So Far!-Can Make The Best President ...
Buku 7 leo zimekuhusu hilo halina ubishi
 
Back
Top Bottom