Uthibitisho: Mwigulu Nchemba ni majina bandia ila vyeti ni vya kweli

Dhana ya kwamba atang'oka kwa hii issue haitowezekana. Nadhani tuendelee na maisha yetu tu maana hata yule Diamond siyo jina lake halisi lakini sisikii mtu akiuliza
mkuu umetisha, watakuelewa wachache sana...leo kazi yangu ni kutoa shikamoo tu
shikamoo great thinker
 
"Kwakuwa miaka hiyo kurudia shule ya msingi ilikuwa hairuhusiwi" hapo ndio kwenye kosa na forgery imeanzia hapo, mana hii kama kweli ni lazima afanye forgery ya cheti cha kuzaliwa japo vyeti vyengine vya academic ni vyake....nahisi tu
 
cheti cha kuzaliwa alikipataje?
 
Mpaka atakapoletwa au kuonekana Mwigulu Lameck Nchemba original, huyu ndie ninayemtambua ni original.

Mwigulu kasema namna alivyoyapata majina yake. Kinawashinda nini kuanzia hapo ili kuupata ukweli.

Au ndo ile tabia ya KUZUSHA jambo bila utafiti mkiumbuliwa, mnaachana nalo mnadandia jingine, mfano, UKUTA, Prof. Lipumba saga, Mbowe Hotels saga, Jacqueline Ndalichako saga, Lema kutaja machache.
 
Watu mpaka sasa hamjamuelewa Pasco hebu msomeni mstarinkwa mstari muelewa anachoandika hamtetei mtuhapa bali ameleta uzi ila ameandika kwa mafumbo isionekane anamkandamiza muheshimiwa....
 
Mi hili sjalielewa vizuri ....ina maana watu wawili wanatumia majina yanayofanana huku kila mtu na vyeti vyake .....necta wanatakiwa wasaidie kuweka hili jambo vizuri linatoa taswira mbaya kwa mh...
 
MM nilifel shule ya msingi na jamaazangu ambo tulikuwa tunaongoza kutoka daras la kwanza wakafulu wasichana wa tano ambao hata kumi bora hawajawah kuingia wengi watoto wa waalimu na wengine wa matajir fulan pale kijijin kwe2 ilaa nashukuru mungu baba angu kanisomesha shule binafsi (R.I.P DAD) na nilifanikiwa kufika chuo kikuu ila wale wasichana wote walipiga zero form 4 kasoro 1 alifanikiwa kufika chuo sahv naamin sasa kumbe inawezekana kuna usanii mwingi kwenye matokeo ya shule ya msingi kuna watu wanafaulu ila kunauchakachuaji unafanyikaa ili watu fulanfulan wapate nafas na wale maskin wakose .MH nchemba kama alisomea jina la mtu aliyefaulu wakamficha mhusika akaenda yeye hapo anakosaa ilaa kama alichukua jina la mtu aliyekimbia shule akasomea yy na kufanya mtihan na kufaulu hana kosa hata kidogo kinachotakiwa sahv apige kazi 2
 
baiser kwa nini achukue jina la mtu darasa la saba una uhakika gani na matokeo ya chuo kama sio ya watu wengine fikiri zaidi ukifoji Elimu hata darasa la Nne zamani tulikua tunarudia ni kosa kabisa ni vile bongo tunaishi kwa mazoea ndio maana hata wewe ulimaliza chuo umetoa hayo mawazo Mkuu..
 
Wapo wengi wanao tumia majina ya kisukuma na maelezo Yao huwa Ni hayo hayo ya dactari wa kisukuma- Je wakati huo kulikua na madaktari wa kisukuma wangapi? JE Ni Kweli wakati huo alipo zaliwa kulikua na dactari wakisukuma? Tuendelee kutafakari
 
Pasco acha maneno ya ujanja ujanja yaaani unazunguka weeeeee Kama cheti feki....
 
Pamoja na hayo ila huyu dogo ni kwikwi when it comes to shule, UDSM kule dep. Ya uchumi kaacha jina kubwa sana ndo maana BOT wakambeba kama alivyo na hata masters wamemsomesha wao
Kwikwi ndiyo kiswakitarafa gani tena? Aarrrrrgh! Uhondo unautia uchungu! Kwanini!
 
Labda ni usalama wa taifa, hivyo hatakiwi kujulikana julikana hovyo!
 
Buku 7 leo zimekuhusu hilo halina ubishi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…