Uthubutu wake, Kukabiliana Kwake na Umakini wake dhidi ya Janga la 'CORONA' lamfanya Rais Dkt. Magufuli akubalike kama 'Malaika' nchini Uganda

Uthubutu wake, Kukabiliana Kwake na Umakini wake dhidi ya Janga la 'CORONA' lamfanya Rais Dkt. Magufuli akubalike kama 'Malaika' nchini Uganda

Jpm anampenda Mungu. Na hiki ndicho kinampa sifa kubwa Tanzania na duniani kwa ujumla
Mungu yupi unayemzungumzia hapa? Maana yeye JPM aliomba kuwa malaika mkuu akapewa, na sasa na yeye anajiona ni mungu.
 
Watanzania najua baadhi yetu tunaweza ama tukawa hatujui 'Thamani' ya Rais Dkt. Magufuli au 'Umuhimu' wake Kwetu ila itoshe tu kusema kwamba pamoja na kwamba 'Kibinadamu' anaweza akawa na 'Mapungufu' yake kama niliyonayo Mimi GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE ila kwa Tanzania 'Kumpata' Kiongozi kama Yeye ( JPM ) ni kama vile Mwenyezi Mungu 'ametupendelea' sana tu.

Leo asubuhi kupitia Kipindi cha BBC News ( Africa ) kinachoruka Kuanzia Saa 1 na Nusu hadi Saa 2 Kamili ( Redioni ) nilibahatika kuwasikia Viongozi mbalimbali wa 'Kidini' na Wananchi kadhaa ( waliowawakilisha ) Wenzao ( Waganda ) katika 'Mjadala' mkubwa uliokuwa 'Mezani' wa Janga la CORONA na namna nzima ya 'Kukabiliana' nalo.

Mazunguzo ya 'Kimjadala' yalikuwa ni mengi na yenye 'Tija' na 'Mantiki' ila katika kila 'Mzungumzaji' aliyekuwa akichangia wote walikuwa 'wakimpongeza' sana Rais wa Tanzania Dkt. Magufuli kwa 'Kupambana' Kwake juu ya Janga la CORONA huku 'wakimshutumu' wazi wazi Rais wao Mzee Museveni kuwa 'ameshindwa' na kwamba kazidiwa mbali na Rais Magufuli.

Mwishoni kabisa Wote 'walisikika' wakisema kuwa laiti kungekuwa kuna uwezekano wa 'Kukopana' Marais hata kwa muda fulani tu basi kwa 'Taabu' ambazo wanazipitia sasa 'Waganda' na Maisha magumu 'waliyonayo' tokea Janga hili la CORONA lianze huku 'wakizuiwa' Kufanya Shughuli zao mbalimbali za 'Kiuchumi' basi wangetuomba Watanzania 'tuwakopeshe' Rais wetu huyu Dkt. Magufuli.

Kwa 'Kuhitimisha' Kwao tu Viongozi hao wa 'Dini' na Wananchi wa Uganda 'wamemtaka' Rais wao Mzee Museveni 'ayaige' mengi ya Rais Wetu JPM.

Nami GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE ninamalizia pia kwa kusema hebu Watanzania 'tujivunie' mno Rais Magufuli na 'tumsaidie' pale anapokosea.
Be Serious Mkuu, Sifa za kijinga! Eti maombi yamezuia korona! and he is trumpeting it to the world, making us all look like fools!
 
-Mkuu GENTAMYCINE kwenye suala la Corona kweli JPM alilimudu vema kwanza kuliongoza taifa katika kumwomba Mungu na pili Kulikuza Jina la Mungu kuliko haka kaugonjwa na hapo ndipo tuliposikiwa na Mungu. Wale wote wanaofahamu kisa cha Nchi ya Ninawi Yona 3:1-10 wataelewa kuwa JPM ametuvusha hapa.

-Issue inakuja je kipengele hichi tu inatosha mtu kuwa na sifa ya kuwaa Rais....JPM ni mbaguzi sana kwenye majimbo ambayo hawajamchagua pamoja na lugha nzuri ninayosikia kinywani mwake kuwa maendeleo hayana chama....lakini ukweli mikoa na maeneo ambayo JPM hawakumchagua 2015 hakuna uhusiano mzuri na eneo hilo.
 
Ishu ya corona tumebebwa na Hali ya kitropical sababu ya joto
Kenya, uganda, dubai hamna joto ee.... Remember kipind cha corona tanzania ilikuwa ni kipind cha mvua na baridi then ikaja baridi kali....
Kuna sehemu kama mbeya, iringa na njombe huwa kuna baridi muda mwingi mbona hawakufa
Tumpe ongera zake alitutoa uwoga na kutushawishi tumwombe Mungu...
 
Corona ipo Tanzania,ukienda Vatican upo,ukienda Israel upo tofauti ni kwamba huku kwetu hatutoi taarifa.
 
Wakati wa coona si nilisikia alikimbilia Gbadolite?🙄🙄🙄🙄🙄🙄🙄🙄🙄
 
Mkuu ugonjwa haufichiki asee... Corona ni highly contagious na killing disease bro ugonjwa huo haufichiki kabisa
Tuwe tuna appreciate japo kidogo..

Kwahiyo hakuna Corona Tanzania ?.
 
Jpm anampenda Mungu. Na hiki ndicho kinampa sifa kubwa Tanzania na duniani kwa ujumla
'Huwezi kumpenda Mungu ambaye humwoni wakati humpendi jirani yako unayemwona' imeandikwa kwenye Biblia ndo Amri kubwa kuliko zote
 
Kenya, uganda, dubai hamna joto ee.... Remember kipind cha corona tanzania ilikuwa ni kipind cha mvua na baridi then ikaja baridi kali....
Kuna sehemu kama mbeya, iringa na njombe huwa kuna baridi muda mwingi mbona hawakufa
Tumpe ongera zake alitutoa uwoga na kutushawishi tumwombe Mungu...

Kama Hakuna corona why watu wamekufa kwa corona
 
Back
Top Bottom