Utoto bwana,acheni tu

Utoto bwana,acheni tu

Sisi dawati letu lilikua mnakaa wa5
Ogomvi ulikua ni huo tu kwamba dawati letu hatutaki wasichana halafu sasa wewe msichana ndio mwalimu kakupanga hapo
Ndio wanakusukuma mpaka uanguke na wewe ukianguka unaita mob lako la wasichana[emoji23] mnawasukuma basi mnaeza kusukumana hata nusu ya darasa
Hiyo ya kusukuma hujaeleza vizuri. Mnakaa watu wawili upande mmoja na wawili nusu nyingine. Unakuta mna bifu mnafukuzana, toka-sitoki na ndo mnaanza kusukumana. Siku zote waliokaa ukutani ndo wanashinda
 
Mi nlivokuwa chalii nlivaa boksi kichwan nkatoboa matundu 2 machoni nkawa nachek magar yaliyopakiwa bar na barabaran then natoa upepo matair mwenyw akitoka huyo nshakimbia najificha kweny uchochoro bas bwana eehh namwangalia mjuba anahaingaika na tairi haina upepo mimi naskia raha balaa...siku moja nkafuliwa jiwe la mgongo dah nliskia kama mgongo umepigwa rungu nlikimbia balaa
 
Ukimi kufika kwenye matundu ya pua hiaya ni matango pori
 
Kuvua nguo zote kisha kuvaa nylon (Rambo) kisha naingia misele[emoji861]
 
Kuna sisimizi mkubwa ilikiwa tumeaminishwa ukimkuta, unamuimbia na kumtemea mate unaomba unachotaka, mimi kila nikimuona namuimbia habari za ubwabwa tuu!

Pia kuna wale wadudu wakati tukiwa wadogo tunatamani maziwa, basi tunawachukua tunawaumisha kwenye maziwa! Wakikung'ata waumwa haswa tumaziwa tunavimba basi kwa akili za kitoto unahisi yameota!
 
Kuna sisimizi mkubwa ilikiwa tumeaminishwa ukimkuta, unamuimbia na kumtemea mate unaomba unachotaka, mimi kila nikimuona namuimbia habari za ubwabwa tuu!

Pia kuna wale wadudu wakati tukiwa wadogo tunatamani maziwa, basi tunawachukua tunawaumisha kwenye maziwa! Wakikung'ata waumwa haswa tumaziwa tunavimba basi kwa akili za kitoto unahisi yameota!
Wale wadudu wana kasi sana kwenye maji na wanateleza balaa
 
Utoto bwana mda wa kula tulikua tunapakuliwa kwenye senia sababu ya uvivu wa kutokula nikila pekeyangu basi tukimaliza kusali naanza na nyama yangu nikimaliza nalilia za wenzangu wakininyima watagombezwa kwamba hawaoni me mdogo wanipe wakigoma bmkubwa atanipa hata yake ilimradi tu

Mda wa kuoga nachuka mda mrefu bafuni nikiskia miguu ya mtu anakuja namwagamwaga maji ovyo ilimradi ujue naoga ila nikitoka bafuni miguu tu ndoimeloana maji sehemu nyingine ya mwili kavu nilipewa mikwaju sikumoja na bmkubwa ikawa ndo mwisho wa hiyo tabia


Cc Kingsmann
 
Fitna zimeanza zamani ukipewa 100 ukatoe sadaka unachange sh 10 kumi unanunua ice cream sadaka unatoa Sh 50..
Tuliosoma kayumba kama umekaa dawati wanaume wa4 msichana ndio wewe wanakusukuma mpaka uanguke[emoji3] na wewe unaita wasichana wenzio mnawasukuma mpaka waanguke yani nusu saa nzima mpaka mwalimu aje
Kaka zangu waliniambiaga ukila kichwa cha samaki utakua na akili kama za samaki mpaka leo sili[emoji3]
ha ha ha.. wengine tuliambiwa ukila miguu ya kuku unakua unazurura sana
 
Back
Top Bottom