Uwanja wa Entebe kuchukuliwa na China kwa ajili ya Mkopo, Mashabiki wa Bagamoyo kaeni mkao wa kula

Hivi sisi wenyewe hatuna uwezo wa kuijenga hiyo banadari ya bagamoyo kama kweli tuna uhitaji nayo?
Na kwa nini tujenge bandari mpya ilihali tulizonazo(Dar,Tanga na Mtwara) hatujaziutilize ipasavyo?
 
Hivi sisi wenyewe hatuna uwezo wa kuijenga hiyo banadari ya bagamoyo kama kweli tuna uhitaji nayo?
Na kwa nini tujenge bandari mpya ilihali tulizonazo(Dar,Tanga na Mtwara) hatujaziutilize ipasavyo?
Hapo panamwagwa pesa nyingi sana i think..tungekuwa na uwezo tungejikongoja kama kwenye sgr na mwawa la umeme.
 

wakati Ghana wakipigania mikataba iwekwe wazi, sisi tupo comfortable kumegewa vidokezo vya mikataba tena hata kwa politicians ambao dhamira zao huwa na interest zisizoaminika
 
Wabunge wote kuanzia Ndugai wamehongwa
 
Hapo panamwagwa pesa nyingi sana i think..tungekuwa na uwezo tungejikongoja kama kwenye sgr na mwawa la umeme.
Kwani Bandari ya Dar Es Salaam haifanyi kazi?
 
KWA TUNAVYOJIJUA WATANZANIA HILI NALO LITAPITA NA BANDARI ITAJENGWA NA HAKUNA TUTAKACHOKIFANYA.....

CCM WAMEIFANYA HII NCHI NI KAMA SHAMBA LAO NA WATOTO WAO......

INGAWA WATANZANIA WAMESHINDWA KUJISIMAMIA LAKINI IPO SIKU MUNGU ATASIMAMA NA WATANZANIA KWANI KAMWE HAWEZI KUACHA DHURUMA NA UONEVU VIENDELEE MACHONI MWAKE.........
 
Bungeni atajadili nani?

Babu Tale!!!!
 
Magufuli alikupa huo mkataba ukausoma?
Alikuwa mkweli kiasi gani?
Maneno na mawazo yake ni msaafu?
 
China inaimaliza Afrika kwa tamaa za viongozi, mradi wa Bagamoyo hata waipambe vipi mwisho wake ni kilio tu!

Wachina wanajua udhaifu wa mtu mweusi, ndio maana ni rahisi mno kuweka ndoano na mwafrika kuimeza!

Hatuna uwezo wa kufikiria nchi kuliko familia na matumbo yetu.

Siku kizazi cha viongozi wenye ugonjwa wa ubinafsi kitaisha ndio Afrika itapata maendeleo ya kweli.

Ni mradi gani huu wenye konakona, mara mikataba ni ya hovyo, kiongozi mwingine anauzindua, mwingine anasema hakukuwepo na mkataba wowote uliokwisha sainiwa!

Hii ni dharau kubwa kwa wananchi, mtu akichaguliwa kushika nafasi anaona waliomchagua hawana akili na uwezo wa kufikiri.

Tamaa ikizidi hupofusha macho.
 
Mchina anakopa, kwa umaskini upi alionao?
 
Lijadiliwe kweupe tu watanzani hatuna shida sisi tutaridhika tu hata kama tunapelekwa chaka
Kama huna shida subiri tu ijengwe, mjadala wa nini na huna shida hata kama unapelekwa chaka? Ukipelekwa chaka kwako ni sawa, usipopelekwa kwako ni sawa sasa unataka mjadala wa kazi gani?

Halafu usipende kusema sisi sema mimi mtanzania sina shida.
 
Nafikiri kiingereza hakijamnyookea sana mleta mada
Ni wapi waliposema uwanja huo unachukuliwa?
Kwa maelezo bado Uganda hawajashindwa kulipa deni, wanacholakamika ni kubanwa kwenye mapato na matumiz (budget) jambo ambalo nafikiri liliwekwa kusaidia urejeshaji salama wa mkopo ukizingatia akili ya waafrika.

Hoja kwamba wakishindwa uwanja utawekwa chini ya Uchina mpaka deni liishe, sioni mantiki ya kulalamika, hata Wewe ukiweka bond nyumba ukishindwa kulipa inauzwa. Ukikopa lipa
 
Meko alishamaliza hii kitu.....maana naona wazee wa legacy mnahangaika sana.
 

Attachments

  • VID-20211126-WA0012.mp4
    6.8 MB



ila hawa Exim bank ya china mbona kwenye masoo ya namna hii kama vile hawakosi.. hivi ile ya zambia kuchukiwa na china pia hawakuwepo? .. na kuna issue ya ufisadi humu tz kama niliwasikiaga ?
 
Mnatufanya wote hatujui uchumi eeh! Yaani mtu aje kwako, akushauri mjenge nyumba kiwanjani kwako, we ukope na ye akope halafu useme Hakuna hata mia ya mkopo wa aliyekuja kuungana nawe?? Yaani China anakupenda kuliko unavyojipenda?

Hii miladi huja kwa sura nzuri nzuri ila ni wizi wa kalamu tu na mzigo wa kulipa uyawaumiza wananchi wa chini.

Matokeo Yake mafuta juu, Vifaa vya ujenzi juu, tozo za wizi wizi nk Vyote hivyo ni mzigo kwa mwananchi!
 
Kama huna shida subiri tu ijengwe, mjadala wa nini na huna shida hata kama unapelekwa chaka? Ukipelekwa chaka kwako ni sawa, usipopelekwa kwako ni sawa sasa unataka mjadala wa kazi gani?

Halafu usipende kusema sisi sema mimi mtanzania sina shida.
Hata ningesema 'mimi sina shida', kwa hulka yako hii ungesema sipaswi kuchangia chochote nikae kimya

Nimezunguza hivyo kwa maana

kwakuwa najua kinga zipatikanazo kwa watu hao na kipi ambacho siwezi kufanya wala kukibadili kwa wakati huu wala wewe na yeyote yule

Ila nafahamu kuwa mabiliko yapo karibu,na ni wakati kidogo mambo yatakua mambo kwakuwa mbegu ilipandwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…