Uwe makini zaidi unapotaka kununua gari kwa watu hawa

Uwe makini zaidi unapotaka kununua gari kwa watu hawa

Status
Not open for further replies.

illegal migrant

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2013
Posts
1,277
Reaction score
1,121
Wengi tunataka magari ya bei nafuu, hii hupelekea kujikuta tuko tayari kununua gari bila kufanya uchunguzi wa kina, baada ya kujiridhisha kuwa gari unalotaka kununua lipo katika hali inayokuridhisha, ni.

Ni muhimu kujua gari hilo liliingiaje nchini, hapa nazungumzia documents. Watumishi huwa ni rahisi kupata magari utakuta labda minadani huko walijiuzia magari, na wale wengine wanaojimilikisha magari yaliyokamatwa na kutelekezwa, na wale wenye misamaha ya kodi, unaweza kudhani kwamba sababu mtu huyu ni mtumishi basi ninaweza kumuamini, ukaishia kutoa hela zako ambazo ulitafuta kwa taabu, baada ya kulipia gari kuna hatua nyingine muhimu ambayo ni kuhamisha umiliki.

Ndipo unaweza kugundua kuwa umeuziwa gari ambalo huwezi kulimiliki, pengine kumbukumbu/taarifa zisiwepo mamlaka ya forodha (Hii ni kwa magari mengi yaliyoibiwa nchi za jirani na kutelekezwa) wakati wa kuyauza yanatengenezewa kadi ya “Haraka” ushauri unapotaka kununua gari hususani kutoka kwa kundi tajwa usiseme tu “ngoja nikamlete fundi wangu” ni Bora pia ukaenda na kadi mamlaka ya forodha kujua gari hilo liliingiaje nchini (kumbuka sisi hatuna viwanda vya magari), angalia pia liliingiaje kwa matumizi gani, pia limepita kwa wamiliki wangapi na kama jina la muuzaji ndiyo jina la mmiliki, pia kama lina msamaha wowote wa kodi. Yote haya ni ili kujiridhisha usije ukanunua gari ambalo huwezi kulimiliki.
 
Hii imemtokea rafik yangu saiv anatembea na gari haina card
 
20220124_212306.jpg


Hawa jamaa wana ofisi zao Posta, wanadai wanaagiza magari unalipia nusu kisha gari ikifika unamalizia.

Binafsi nimeagiza gari miezi tisa kila nikipiga simu naambiwa boss hayupo, nikienda ofisini naambiwa boss katoka.

Nimewaandikia barua wamenijibu kwa kunipa masharti mapya ambayo kwenye mkataba wa awali haukuwepo mwishowe wananiambia niende popote.

Sasa mimi nitaenda huko popote na nitawaletea mrejesho kutoka huko popote. Sambazieni watu wasije wakapigwa hela, ni ngumu kwa sasa.
 
View attachment 2094407
Hawa jamaa wana ofisi zao posta..wanadai wana agiza magari unalipia nusu kisha gari ikifika unamalizia....binafsi nimeagiza gari miezi ya tisa kila nikipiga simu naambiwa boss hayupo nikienda ofisini naambiwa boss katoka nimewaandikia barua wamenijibu kwa kunipa masharti mapya ambayo kwenye mkataba wa awali haukuwepo mwishowe wananiambia niende popote...sasa mimi ntaenda huko popote na nitawaterea mrejesho kutoka huko popote ....sambazieni watu wasije wakapigwa hela ni ngumu kwa sasa
Mali ya mwanaume haipotei mkuu pambania
 
Mkuu pole, nadhani ungetoa details kwamba uliagiza gari gani na lini, hiyo pesa ya awali uliwapa kwa njia gani?? Na mlisainishana wakati unawapa hiyo pesa?? Una nakala yako ya malipo??

Kuna wahuni kama hao mwaka jana June walimfanyia hivyo ndugu yangu, baada ya kumzungusha sana akanipa hiyo taarifa, nikamwambia nitumie tu tiketi ya Ndege nije Dar kutoka Dodoma akatuma, tuliwaibukia saa 4 asubuhi ofisini kwao, kuingia ofisini kwa Boss tu nilichomoa mkwaju, nikakoki nikapiga risasi moja chupa kubwa ya Maji ilikuwa mezani pembeni ya huyo jamaa Mkurugenzi.

Nikamwambia nakuua rudisha pesa ya huyu jamaa hapa, alihamisha pesa palepale kutoka kwenye CRDB yake Account kuja kwa jamaa ndani ya dakika 2, ofisini kulikuwa kuna AC lakini tulitoka pale jamaa shati lote limeloa jasho, wahuni na matapeli kama hao ni ku-deal nao kihuni tu
 
Mkuu pole, nadhani ungetoa details kwamba uliagiza gari gani na lini,hiyo pesa ya awali uliwapa kwa njia gani??na mlisainishana wakati unawapa hiyo pesa??una nalala yako ya malipo?...
Kuna mkataba na nililipia Bank kama unaweza kazi njoo pm maana wanaonekana ni wahuni sasa tu deal nao kihuni tu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom