Uwekezaji nyumba za kupanga

Kwamba ni ngumu kupangisha chumba cha master bedroom kwa laki moja??????
halafu nani kakuambia Mimi nazungumzia maeneo ya huko kibamba ulipopanga boss,

Uko vyumba Kodi zake si za kawaida tu Kama mbagala
Nilikuwa nataka location ambayo unasemea mradi wako una shine , ili nijue bei za kiwanja huko,
Kibamba na mbezi nimetoa mfano , huko ndioo unaweza kujenga property za 70 mil ,za staili unayosemea ukijumlisha na bei ya kiwanja ,
Maeneo yote uliyosemea kwenye post yako pale juu sio cheap , unless uwe na kiwanja cha kupewa
 
Sawa mkuu, haya we tuache sisi tuzike pesa, we mjanja subiri uje kujenga nyumba ya ndoto zako,

Sisi tutaendelea kuzika milioni sitini ardhini, makusanyo kwa mwaka milioni 7,
 
dizaini yako wengi uja kujuta baadae sanaa,
 
Yaan hata Mimi zamani nilikuwa na ujinga na ujuaji Kama wako
 
Mpe idea mkuu tuko hapa kujenga na si kubomoa
Dunia itampa Idea mkuu,

Mi mwaka 2000 nilikuwa mjuaji nikaingia kwenye biashara ya daladala, Tena mahesabu ya kwenye daftari na u-much know ndio uliniingiza uko, nilijuta,dunia ilinifunza
 
Wengi somo la kuandaa business plan lime kuwa gumu sana.

Ideas zipo nyingi tatizo ni katika analysis.
 
Sawa mkuu, haya we tuache sisi tuzike pesa, we mjanja subiri uje kujenga nyumba ya ndoto zako,

Sisi tutaendelea kuzika milioni sitini ardhini, makusanyo kwa mwaka milioni 7,
Wala tusitiane unyonge na visasi,, hatujuani na hii ni forum tu
60 millions unazika ili upate faida ya 7 millions kwa mwaka , ambayo kuna uwezekano hata kodi hujalipa , ni matumizi mabaya sana ya pesa zako .
 
dizaini yako wengi uja kujuta baadae sanaa,
Mbona unaniombea mabalaa ? We mganga?? Hahaaa
Vijumba hapa mjini nnavyo tu halafu wala sio big deal usimuize kichwa , nyumba yangu ya kwanza ilikuwa 2007 , sitakwambia nna ngapi miji hapa

Mjadala ulikuwa unaspend nini na kupata faida ipi ,
 
Binafsi mm nilishindwa stick na biashara moja...
Yaan itakuletea umaskini tu!..siwezi kbs
Huyu jamaa yeye anamilik malori ya mizigo, so hiyo miaka aliyotumia n sahihi, anayajua balaaa utadhan aliyatengeneza yeye, i think kuna watu pale swiden yanapotengenezwa Hawana uelewa alionao yeye kwenye products zao hizo hizo
 
Wala tusitiane unyonge na visasi,, hatujuani na hii ni forum tu
60 millions unazika ili upate faida ya 7 millions kwa mwaka , ambayo kuna uwezekano hata kodi hujalipa , ni matumizi mabaya sana ya pesa zako .
Aya binti, baki na unachokiamini,
tunasubiria wewe uje kujenga hekalu lako uwe unalipia na Kodi,

hata sisi pia tulikuwa na ujuaji Kama wewe, enzi izo Rafki yako akijenga", unamuambia Mimi siwezi kujenga kibanda Kama iko, nataka nije kujenga bongeee la sefucontina nikiwa na pesa ya pamoja,tena wiki tu nahamia"!
 
Huyu jamaa yeye anamilik malori ya mizigo, so hiyo miaka aliyotumia n sahihi, anayajua balaaa utadhan aliyatengeneza yeye, i think kuna watu pale swiden yanapotengenezwa Hawana uelewa alionao yeye kwenye products zao hizo hizo
Nice.....
 
Lodge hata mie naifikiria sana kama retirement plan yangu baada ya kuhangaika sana ,

Tatizo wife !! Na ulokole wake , anazingua kweli na project za kutengeneza dhambi
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Real estate huwa inafanywa na developers ambazo huwa ni kampuni zenye mitaji mikubwa na ambao hujenga makazi mengi yaani estates kisha kuziuza nyumba aidha kwa cash au mortgage kwa ushirikiano na mabenki mfano mzuri wa sekta hii inavyofanyika ni hapo 254.

Hii ya kibongo bongo kwamba mtu binafsi anamtaji mdogo anajenga nyumba moja au 2 kupangisha hailipi sababu hata hao developer wakubwa wanapata faida kwa kuuza na sio kupangisha. Tatizo nchi haina sheria zinazowabana developers, sababu huko kwingine developer lazima aweke miundombinu yote ikiwemo maji safi na taka, barabarabza mtaa n.k

Kwa mazingira yetu italipa tu kama una kiwanja kwenye eneo zuri (prime location) ambapo unaweza kutoza kodi kubwa, kinyume na hapo ni kuweka mtaji tu au pesa kuzihifadh lakini sio kupata faida.
 
Dunia itampa Idea mkuu,

Mi mwaka 2000 nilikuwa mjuaji nikaingia kwenye biashara ya daladala, Tena mahesabu ya kwenye daftari na u-much know ndio uliniingiza uko, nilijuta,dunia ilinifunza
Swala la kufeli wewe biashara haimaanishi kuwa kila mtu atafeli ,
Dala dala hata mimi siwezi fanya , ila haimaanishi kwamba watu hawapati faida huko.

Halafu again , hii ni mitandao tu, hatujuani usiweke kinyongo na sononi hadi ukatoa ya moyoni kwa t blj kama vile tunajuana .

Leo tu unaniita mchuuza mayai ya kware , mara nimeajiriwa na wala hunijui , yaani kwa maandishi tu unanikadiria hivyo , ukinijua uhalisia wangu itakuwaje?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…