Uwekezaji wa vyumba vya kupanga, mrejesho wa uwekezaji

Uwekezaji wa vyumba vya kupanga, mrejesho wa uwekezaji

TheCrocodile hongera sana mkuu kwa hii hatua. Umejipata. Wewe sasa umeingia daraja la Kati la uchumi wa Tanzania.

Vipi ungepiga kodi 200k kwa mwezi usingepata wapangaji?
Asante sana mkuu. Kwa 200k ingekua parefu sana. Nilivyoset hapo ndo nimeanza, si unajua kodi huwa haishuki siku zote, inapanda tu juu. Kwa survey niliyofanya ya hayo maeneo, 150k ni kiwango cha juu kabisa (matawi ya juu). Ila with time, labda wakati na review kodi mwaka unaofuata labda inaweza fika huko!
 
Karibu sana mkuu. Naona hii kitu ni nzuri kama ukiwa na hela zako unataka kuzichimbia, na unataka return ya muda mrefu kido
IMG_20250219_175545_1.jpg

Next project zipange hivi mkuu.
 
Well done mkuu.....
Hapo maanayake ndani ya miaka mitano na nusu utakua umesha rudisha gharama za ujenzi, then unaanza kula faida polepole
Iwapo kutakua hamna maintenance kama mpangaji kaondoka inarudi. But hapo kuna operation cost zitakuja baada ya miaka miwili.

Pia bado anajenga ukuta. Akimaliza ataweka geti. Akimaliza wapangaji watataka paving.

So real return unakuja kuipata kuanzia miaka 8-10...
 
Wakuu mko vizuri?

Kuna kipindi nilileta thread humu ya kujaribu kupata ideas ya namna ya kuiwekeza shs milioni 64 niliyokua nimei save, kwenye link hii hapa.
Nimekuja hapa kuleta mrejesho wa namna nilivyotumia ile pesa. Ule mzigo wote niliuchimbia kwenye ujenzi wa vyumba vya kupanga wakuu. Vyumba hivi nimejenga maeneo ya Kibaha hapo (karibu na Miembe 7), na nimejenga kwa style ya chumba chenye choo ndani (self-contained) + sebule yake. Nimejenga jumla ya units 8 (zikiwa zimeunganika).
Maeneo hayo niliyojenga uhitaji wa makazi ni mkubwa sana. Nimezijenga katika style ya unit nne nne (majengo mawili, kila moja unit nne). Jumla ya gharama nimetumia sio chini ya shilingi milioni 76 kukamilisha kila kitu hapo (hii ni kabla ya kuweka fence).
Tangia wakati nanyanyua boma, watu wengi sana walikua wanaulizia kila mara. Sasa hivi nimemaliza, nimeweka na fence pia (ujenzi wa fence unaendelea-bado mageti).
Tayari nimeanza kula kodi wakuu, hadi sasa unit zote 8 zimeshaingia wapangaji, nimeanza kula kodi kuanzia mwezi huu wa pili. Napangisha kwa gharama ya 150,000 kwa mwezi kwa kila unit. Nawashukuru wote ambao mlinipa ideas na mawazo mbalimbali wakuu. Mbarikiwe sana!

Nimeweka picha chache hapa chini kwa uelewa zaidi.
Hongera fanya sherehe ya uzinduzi Wana JF tuje tuserebuke na kuombea!
 
Asante sana mkuu. Kwa 200k ingekua parefu sana. Nilivyoset hapo ndo nimeanza, si unajua kodi huwa haishuki siku zote, inapanda tu juu. Kwa survey niliyofanya ya hayo maeneo, 150k ni kiwango cha juu kabisa (matawi ya juu). Ila with time, labda wakati na review kodi mwaka unaofuata labda inaweza fika huko!
Kwa Dodoma kama maneno ya Ilazo, Kisasa ungelamba hiyo200k!
 
Back
Top Bottom