Uwekezaji wa vyumba vya kupanga, mrejesho wa uwekezaji

Uwekezaji wa vyumba vya kupanga, mrejesho wa uwekezaji

Yeah, na hiyo bagamoyo kuanzia gari za Arusha na Tanga zianze kupita kule basi ndio imezidi kuwa ghari, mapinga zamani ilikua viwanja bei chee ila sasa hivi sidhani kama hata viwanja venyewe vipo pale😅😅😅
Kwisha habari nilienda huko kuonyeshwa kiwanja cha 5M kwa 500M² kilikuwa huko ndanindani nilijilaumu kuchelwa kuchukua hatua mapema😭😭😭
 
Bora viwanja vya kibaha ila ile miinuko ya kibamba,Bonyokwa,Maramba mawili na Kinyerezi siwezi kutoa hata mia mbovu kununua kiwanja maeneo hayo🙌🙌🙌
Ni kama goba tu, goba kuna maeneo ni hatari au salasala kule kinzudi🤣🤣🤣🤣
 
Ukiweka pesa utt usisahau na inflation rate ya mwaka ni bora awekeze kwa real estate ambapo thaman yake inaongezeka kila mwaka. Utt unaweka pesa kwa muda ukisubir cha kufanya.
Kwa structure ya nyumba aliyojenga, UTT bado ungekuwa uwekezaji mzuri kwake. Kwa maoni yangu. Service ya nyumba baada ya kuondoka kwa wapangaji huwa ni kubwa sana, wapangaji wengi wa units ni wapangaji shikizi ambao wanajiandaa kujenga nyumba zao. Wabongo si wastaarabu inapokuwa kwenye kuondoka, labda pawepo na mkataba mkali unaemlazimisha afanye service ya nyumba wakati wa kuhama.
 
Ni kama goba tu, goba kuna maeneo ni hatari au salasala kule kinzudi🤣🤣🤣🤣
Yaani nikipitaga Goba najisemeaa hiii mimi bora nikakae huko kibaha au Mapinga aridhi imenyooka.

Ni mara kumi nikae huko pembezoni alafu ninunue kivits 1KR engine cc990.Nikifanye kibodaboda changu cha kujia mjini kati.

Maeneo hayo ya muinuko yana ujenzi wake sio hivyo vichuguu watz walivyootesha, chakukera kabisa ni ukosefu wa mitaa na mpangilio😬😬😬😬
 
Ukiweka pesa utt usisahau na inflation rate ya mwaka ni bora awekeze kwa real estate ambapo thaman yake inaongezeka kila mwaka. Utt unaweka pesa kwa muda ukisubir cha kufanya.
Kuweka pesa utt labda kama huna shida ya kufanya biashara yoyote ila utt sio biz ni kutunza tu fedha coz pale hakuna scaling yoyote mtu anaweza akifanya, kule weka zako faida au fedha ambayo huna kwa kuipeleka.
 
Yaani nikipitaga Goba najisemeaa hiii mimi bora nikakae huko kibaha au Mapinga aridhi imenyooka.

Ni mara kumi nikae huko pembezoni alafu ninunue kivits 1KR engine cc990.Nikifanye kibodaboda changu cha kujia mjini kati.

Maeneo hayo ya muinuko yana ujenzi wake sio hivyo vichuguu watz walivyootesha chakukera kabisa ni ukosefu wa mitaa na mpangilio😬😬😬😬
Kabisa, yale maeneo kujenga huwa ni gharama hatari😂😂😂... Hata hivyo waliojenga kule wapewe maua yao, maana kwanza ule msingi pale chini tu unaweza ukasimamisha nyumba yako huko vikindu🤣🤣
 
Kwa structure ya nyumba aliyojenga, UTT bado ungekuwa uwekezaji mzuri kwake. Kwa maoni yangu. Service ya nyumba baada ya kuondoka kwa wapangaji huwa ni kubwa sana, wapangaji wengi wa units ni wapangaji shikizi ambao wanajiandaa kujenga nyumba zao. Wabongo si wastaarabu inapokuwa kwenye kuondoka, labda pawepo na mkataba mkali unaemlazimisha afanye service ya nyumba wakati wa kuhama.
Mimi naamini kwenye kuwa na multiple sources of income mkuu.Hata huko UTT ninayo account ambayo natupia huko vijisenti,hiyo haimaanishi nisifanye harakati zingine. Haiwezekani hela yote niiweke tu UTT.
Plus, kinachotakiwa kwenye hii biashara kwanza ni usimamizi wa karibu na kuweka mikataba mikali, ambayo ndicho nilichofanya. Wakati nakabidhi funguo mpangaji, tunakabidhiana kwa picha kabisa hali ya ndani ya vyumba ilivyo (milango, rangi, holder za mapazia, etc), na hizo picha zimehifadhiwa pamoja na mkataba, anapoondoka tunalinganisha, kama kuna uharibifu anarekebisha kabisa.
 
Aisee ni kweli kabisa watu tulikua tunapazarau ila Sasa pamekua town
Kibaha ni eneo mujarab sana, hasa ukipata eneo karibu na barabara kubwa ile. Kama hili eneo nililojenga, hadi kufika Morogoro road kwa boda ni buku tu, ukiamua kutembea ni dakika 7-10.
Na pia viwanda viko vingi sana, mji unakua kwa kasi sana.
 
Yaani haya mambo ya real estate ukipata sehemu nzuri, Kila siku kichwa kitakuwa kinawaza namna ya kujenga tena na tena. Hii sekta ina utamu wa ajabu na addiction.
Ina addiction mbaya sana. Mimi hapa tu nimeanza kuwaza nizikusanye tena, nizichimbie😂😂
 
Kibaha ni eneo mujarab sana, hasa ukipata eneo karibu na barabara kubwa ile. Kama hili eneo nililojenga, hadi kufika Morogoro road kwa boda ni buku tu, ukiamua kutembea ni dakika 7-10.
Na pia viwanda viko vingi sana, mji unakua kwa kasi sana.
Maeneo huko yanasimamia ngapi hapo karibu yako
 
Eneo dogo kabisa la 20 by 20 linasimama 5m, ukilia sanaaaa ukaonewa huruma mwisho kabisa 4.5m, hapo umkute muuzaji ana shida.
🤝Hapo sawa vipi udongo ni kichanga au mfinyanzi.

Mimi haya ambayo sio ya serikali napenda kununua kwa wenyeji hawa madalali kama Maboss kwenzi huwa siwaamini kabisa😄😄😄
 
🤝Hapo sawa vipi udongo ni kichanga au mfinyanzi.

Mimi haya ambayo sio ya serikali napenda kununua kwa wenyeji hawa madalali kama Maboss kwenzi huwa siwaamini kabisa😄😄😄
Kibaha ni CBD waache watu waendelee kushangaa shangaa.
 
Udongo ni tifutifu, pia ardhi ni tambarare, ujenzi wa huku haugharimu sana kwa sababu udongo wake ni mzuri, ba hakuna milima!
Miembeni huko ngoja nitafute weekend moja nije kupaona.

📌📌Mkuu usisite kutuwekea fursa za wauzaji wa viwanja kama watakuwepo hiyo bei ni ya kizalendo kabisa😄😄😄 hapo unaunga viwili au vitatu unamaliza kazi🤝💪
 
Kibaha ni CBD waache watu waendelee kushangaa shangaa.
Watu watakuja kushtuka too late😂😂
Mji unaendelea kwa spidi kubwa sana ule. Yaani kama hayo maeneo niliyopiga hizi mijengo, mahitaji ni makubwa sana ya makazi.
Wanaouza maeneo makubwa makubwa sasa hivi ni wale ambao walikamata maeneo kipindi hicho, sasa hivi wameyagawanya, wanayapiga bei tu kwa raha zao (wengi ni wazee wazee- wastaafu).
 
Watu watakuja kushtuka too late😂😂
Mji unaendelea kwa spidi kubwa sana ule. Yaani kama hayo maeneo niliyopiga hizi mijengo, mahitaji ni makubwa sana ya makazi.
Wanaouza maeneo makubwa makubwa sasa hivi ni wale ambao walikamata maeneo kipindi hicho, sasa hivi wameyagawanya, wanayapiga bei tu kwa raha zao (wengi ni wazee wazee- wastaafu).
Vipi we upo upande wa miembe Saba sekondari
 
Back
Top Bottom