Uwepo wa Mungu unadhihirika kwa alama zake na viumbe vyake

Uwepo wa Mungu unadhihirika kwa alama zake na viumbe vyake

Dunia hii imepitia uongo/utapeli/propaganda kubwa sana na zikapita lakini uongo pekee uliodumu kwa muda mrefu ni huu:

Hebu fikiria; unaambiwa kuna MUNGU muweza wa yote yupo sahihi na hajawahi kukosea

Ameumba dunia kwa ajili yetu na ataiangamiza(jiulize akili za huyo Mungu anaewatakia maafa watu wake)

Alijua ataiangamiza dunia kabla hata hajaiumba lakini aliiumba hivyo hivyo ili aje kuiangamiza(kama vile hajielewi),

Ameumba moto wa jehanamu kwakuwa ametuumba tukosee ili atuchome moto japo alikua na uwezo wakutuumba tusiwe wakosefu ili atuumbie pepo tu tukale bata


Anajua tunacho hitaji lakini lazima tumuombe ili atupe, lakini hata tukimuomba hatupi tunavyotaka sisi maana tayari amekwisha tupangia kila mtu atampa nini, ataishije na atakufaje

Ndio muumba wa kila kitu(magonjwa, bangi, majini,umalaya,ukahaba, ulabu nk) na anaweza kudhibiti chochote lakini anamlaumu msaidizi wake muasi(Shetani) kuleta mambo hayo mabaya duniani (magonjwa nk) kwa watu wake aliyewaumba wakati yeye ndiye aliye mtupa msaidizi wake huyo huku duniani( inaelekea huyu hajiwezi mpaka awe na msaidizi mhuni,amuache tu amchanganyie habari)

Yaani yeye kashindwana naye huko mbinguni kaja kumtupa kwetu sisi viumbe dhaifu tupambane naye na tukishindwa tutachomwa moto milele, lakini anasisitiza anatupenda sana kama mtu anavyopenda na kujali mboni ya jicho lake


Hebu tafakari hili, kawaumba Adam na Hawa na wakati bado wageni duniani akawatupia Nyoka(Shetani) ili awarubuni, na kwa ugeni wao wakarubunika matokeo yake katupa adhabu ya shuruba watu wote hata ambao tulikua hatupo na hata ambao hawajazaliwa chamoto watakiona...... Not fair


Mungu muweza wa yote hayupo WAZI PASI NA SHAKA kwa watu wote kujua huyu ndio MUNGU badala yake Mungu ndio amekua sehemu kubwa ya mgawanyiko wa watu na kusababisha kuwa na imani za MIUNGU zaidi ya milioni dunia nzima

Na kibaya zaidi unatakiwa to blindly believe him, usihoji wala kuwa na shaka juu ya uwepo wake(ni laana na kufuru) vinginevyo moto wa milele unakuhusu


Yaani kuna mtoto wa fundi Kapenta mmoja huko Galilaya eti kafa kwa ajili ya dhambi za watu wote duniani.... Kweli jamani ?

Akaitwa neno. Neno huyo alikua Mungu, mtoto wa Mungu lakini Mungu huyu akajaribiwa na shetani na akapatikana. Shetani aliemuumba mwenyewe.

Mtoto huyu wa fundi kapenta, hakuandika kitabu chochote ila wahuni walio kuwa wanampinga ndio wakaja kuandika vitabu kuhusu dogo huyu na vinaitwa “Bibilia Neno la Mungu takatifu”

Mabilioni ya watu dunia kote wanakesha makanisani wakimlilia na kumuomba awape uponyaji, mali, waume/wake nk


Hebu fikiria huko Arabia kuna maamuma mmoja hajui kusoma wala kuandika alidai anashushiwa maagizo na Mungu kukata vichwa watu wote watakaopinga na kutokutii maagizo yake, “akashushiwa” aya za vitisho na neema kwa watakao tii, yaani ukifa unampigania Mungu unakwenda kupewa mabikra 72 kazi yako ni kuzagamua tu.

Mabilioni ya watu duniani wanasujudu mara 5 kwa siku na kushinda njaa mwezi kila mwaka ili wakale naye bata Peponi

Kwamba maisha yako hapa duniani ni ya mpito tu maisha yako yapo baada ya kufa

Unachotakiwa kufanya ni kumuamini na kufanya aliyoagiza ili ukale bata sana baada ya kufa


Badhi ya sababu za kutoamini uwepo wake hizo hapo mtoa mada. Zipinge tuone!
Habari ya Mungu muweza wa yote mjuzi wa yote na mwenye upendo ni illogical.

Inakuhitaji uwe mwendawazimu tu kukubaliana na mambo hayo.

Imani za kidini ni shambulio la akili.
 
Yaani aliyeanzisha mada anajua vyote anavyosema vimeshapingwa kwenye manyuzi kibao na ufafanuzi ushatolewa ila anataka na yeye aone raha ya kubishana na atheists. Mi nishasemaga ukiona mtu wa dini yupo kwenye hizi threads Imani yake imeshapungua by more than 50% coz up to that point ushajua vitabu vya dini ni vya watu tu na sio vya Mungu, argument za existence of Mungu wa dini nyingi no illogical na impossible to exist . Yaani humu ndani mtu anajikosha tu eti jua bahari sijui miwa...sukari serious.. Yaani waalimu wa geography na science walikuwa wanafundisha tenzi za rohoni class au..
Wapo humu kwa sababu wana personal conflict na imani zao mkuu.
 
Kwa nini swali lako linakuwa "aliye...?".

Huoni kuwa swali lako linalenga kwenye jibu unalolitaka tayari? Huoni swali yako lina bias, kasumba ya kwamba kuna "aliyeumba"?

Sayansi imeshaelezea vizuri kabisa jinsi jua lilivyotokea. Na maelezo hayo hayamuhutaji Mungu.

Wewe umesoma nini kuhusu maelezo ya kisayansi kuhusu jua lilivyotokea?

Tunasoma haya mambo au tunashangaa tu na kusema hii ni kazi ya Mungu?

Mbona vitu vyote vipo mtandaoni? Tatizo ni nini, ni hiki Kiingereza?


Formation​

The Sun formed about 4.6 billion years ago in a giant, spinning cloud of gas and dust called the solar nebula. As the nebula collapsed under its own gravity, it spun faster and flattened into a disk. Most of the nebula's material was pulled toward the center to form our Sun, which accounts for 99.8% of our solar system’s mass. Much of the remaining material formed the planets and other objects that now orbit the Sun. (The rest of the leftover gas and dust was blown away by the young Sun's early solar wind.)
hao wazungu wa NASA ni waongo waongo tuh sio kila kitu unameza utameza matango pori.
 
binafsi naamini MUNGU wangu mimi kaka mimi na hizo dini sjui Islamic au Christian sijui nini nishatoka huko sababu MUNGU wa hizo dini anaubaguzi kabisa.

Lakini MUNGU wangu mimi hana ubaguzi.

staki kukujibu maswali ya kuumiza kichwa saana...sababu bado najifuza hasa pia kupitia nondo zako.

Vipi kwanza ushalipa KODI ya nyumba mkuu?
Sorry,

Mungu wako?

Ulivyoandika tu inaonesha unamungu wako mmoja tu,

Sasa umejuaje kuwa Mungu wako ni mmoja na si wengi kama cyo mawazo yako bado kushikwa na mapokeo ya dini hizi za Kiabraham (zinazoamini katika mungu mmoja[monotheism] ) ambazo unazikataa hapa?
 
hao wazungu wa NASA ni waongo waongo tuh sio kila kitu unameza utameza matango pori.
Kwanza NASA si ya wazungu.

Pili, ukisema hawa ni waongo, onesha waongo katika hili, ukweli ni huu, uthibitisho ni huu.

Usipofanya hivyo, na wewe unaweza kuwa muongo katika kusema hao ni waongo.
 
Mungu Ni Omnipotent,yeye ndo mwanzo na mwisho,yeye hajaumbwa wala hajasababishwa kuwepo na chochote.
Vyote vimefanywa na yeye.
Kubali kataaa,Ulimwengu umeumbwa na Mungu.
Unaweza thibitisha huyo Mungu kuwa yupo kwa hakika na si imani tu ya kwamba yupo kaumba vitu vyote?

Mimi nikikwambia kuwa huu ulimwengu ni mwanzo na mwisho, haujaumbwa wala kusababishwa na chochote...
utanipinga vipi?
 
Sana tu. Mkuu sisi waislam tuna amini Qur'an ni zaidi hata ya hiyo sayansi kaa ujifunze kwanza mambo mengi katika maandiko yetu ya Qur'an yapo kisayansi
Umeshasema mna amini...

Unaelewa maana sahihi ya neno kuamini?

Unaelewa maana sahihi ya Saysnsi?

Ukielewa maana ya term hzo mbili utajiona kuwa wewe unamatatzo tu ya psychology.

Unapaswa kuwa tyar kwa psychotherapy.
 
Mkuu inatosha sasa maana mpaka nakuonea huruma Allah akusamehe hujuwi ulitendalo ishia hapo usizidi kukufuru.

Kama unaoana Qur'an sio maneno ya Allah direct bad tunga na wew Qur'an yako tuone, japo sura moja ukishindwa japo aya moja. Acha kukufuru
Huyo Allah ni mjinga sana.
لو أنزلناهذا القرءان علي جبل لرأيته خشعا متصد عا من خشية الله، وتلك الامثل نضربها للناس للعلهم يتفكرون

lau kama tungeiteremsha hii Qur'an juu ya milima, basi bila ya shaka ungeliona ukinyenyekea, ukipasukapasuka kwa kumuogopa mwenye zi mungu
Na hiyo mifano Tunawapigia watu ili Wafikiri.
 
Sana tu. Mkuu sisi waislam tuna amini Qur'an ni zaidi hata ya hiyo sayansi kaa ujifunze kwanza mambo mengi katika maandiko yetu ya Qur'an yapo kisayansi
Maandiko yenu ni zaidi ya SAYANSI

Halafu
Maandiko yenu yapo KISAYANSI

Wtf!!
 
Hivi mwanadamu ambaye Ni mavumbi tuuu anapata wapi ujasiri wa kusema hakuna Mungu.
Hata kama Ni ujuaji au kiburi tusifike huko.
God exists and will exist forever.
Amen
Kwanza kabisa mwanadamu siyo mavumbi,

Unaweza kuthibitisha huyo Mungu yupo na sio hadithi za uongo zilizotungwa na watu wajinga wajinga tu wasioelewa ulimwengu vzuri?

You need a psychotherapy rn
 
Sorry,

Mungu wako?

Ulivyoandika tu inaonesha unamungu wako mmoja tu,

Sasa umejuaje kuwa Mungu wako ni mmoja na si wengi kama cyo mawazo yako bado kushikwa na mapokeo ya dini hizi za Kiabraham (zinazoamini katika mungu mmoja[monotheism] ) ambazo unazikataa hapa?
Mkuu huyo MUNGU wangu ndio mkuu kabisa.

Hilo sitaki kulipinga kwa upande wangu.

Nilichokataa ni utumwa wa dini sababu dini zimeleta chuki kabisa.

Ukiwa na misimamo unaambiwa unakufuru asee..

Acha imani iwe ndani ya moyo wangu hiyo inatosha sana.
 
Uthibitisho;
للذي خلق سبع سموت طباقا ماتري في خلق الرحمن من تفوت فارجع البصر هل تري من فطور
Ambae ameumba mingu saba kwa tabaka hutaona tofauti yoyote katika uumbaji wake mwingi wa rehema basi rudisha jicho. Je, utaona ufa wowote?

Rudisha jicho lako mbinguni na tazama kwa makini. Je, pamoja na ukubwa wake na upana wake utaona humo mpasuko au ufa wowote?
Kwahyi wewe unatazama jicho lako mbinguni?

Mbinguni ni wapi na sisi tupatizame tuangalie kama kuna mpasuko ama ufa?
 
Kama vilivyo complex hivi vyote vyenye high order hivi ulivyovitaja, bahari,jua, watu, wanyama, ni lazima viwe vimeumbwa na higher intelligence, basi complexity haiwezi kutokea bila kuumbwa na higher intelligence.

Sasa, hapo hapo linakuja swali, kwa kanuni hiyo hiyo ya kwamba kilicho complex hakiwezi kuwepo tu, ni lazima kiwe kimeumbwa, hata Mungu wako naye atahitaji juwa aneumbwa, na aliyemuumba naye atahitaji kuwa na muumba, hivyo hivyo, bila mwisho.

Kwa hiyo, ukisema kuwa bahari, jua, watu ni lazima vimeumbwa, kwa sababu complexity haiwezi kutokea tu, kimsingi hapo unasema Mungu hayupo, labda hujaelewa tu kwamba unajenga hoja kwamba Mungu hayupo.

Ni hivi.

Ama, hivi vitu complex ni lazima viwe vimeumbwa, ama si lazima.

Kama si lazima viwe vimeumbwa, hapo Mungu hahitajiki, kwa sababu kama ulivyosema, unatumia dhana ya kwamba Mungu kaumba kudhihirisha Mungu yupo. Kama vitu hivi si lazima viwe vimeumbwa, basi Mungu hahitajiki.

Kama ni lazima viwe vimeumbwa, basi huyo unayemuita Mungu naye ni lazima awe kaumbwa, na kama ni lazima awe kaumbwa, huyo si Mungu.

Sijui hata kama una uwezo wa kuelewa hizi hoja.
Higher intelligence ndio nini? kuna ulazima gani wa kutumia maneno ya kizungu
 
Kuna jambo limenisukuma sana kuandika huu Uzi.

Mambo ambayo yanaendelea kuhusu uwepo wa mungu.

Kuna baadhi ya watu wa amini hakuna mungu nk.

Ni ingie kwenye point

Uwepo wa mungu una dhihirika kwa alama zake na viumbe vyake.

Hebu tutafakari kama hakuna mungu nani alieumba bahari, jua, mbingu, binadamu, wanyama hivi vitu vimetokea vipi kama hakuna alieviimba.

Leo hii hata ukimchukuwa mtoto mdogo wa miaka mitatu ukamuuliza nani kaumba mbingu atakujibu mungu.

Vipi mtu mzima mwenye akili timamu unashindwa kutambua hilo.

Yapo mambo mengi sana yana thibitisha uwepo wa mungu naweza kesha kuelezea kiufupi, Tufahamu mungu yupo na yeye ndo ametuumba sisi ili tumuabudu yeye tu.
Barikiwa sana
 
Kuwa na akili wewe kwani hiyo aya ili shuka kwa kingereza,
Mbona hujielewi weka aya kama ilivyo shuka kutoka kwa Allah
Duniani kuna watu wa lugha mbalimbali kuna waswahili, wafaransa, wafilipino, wahindi, wajerumani, waingereza, Wareno, wanyarwanda, warundi, wasudani,wakenya, waganda n.k

Kama Allah huyo aliumba watu wa lugha mbalimbali, Kwa nini huyo Allah ashushe Quran kwa lugha moja tu ya kiarabu?

Kwani huyo Allah alikuwa hajui kwamba aliumba watu wa lugha mbalimbali?

Au huyo Allah ana ongea kiarabu tu? Ilhali anajua kuna watu wa lugha mbalimbali.

Hivi huyo Allah ana jielewa kweli?
 
Mkuu huyo MUNGU wangu ndio mkuu kabisa.

Hilo sitaki kulipinga kwa upande wangu.

Nilichokataa ni utumwa wa dini sababu dini zimeleta chuki kabisa.

Ukiwa na misimamo unaambiwa unakufuru asee..

Acha imani iwe ndani ya moyo wangu hiyo inatosha sana.
Hujajibu ile core ya swali langu mkuu,

Unajuaje kama kuna Mungu mkuu na msaidizi?

Vipi kama Miungu wako 20 na wote ni wakuu na ndio walioumba ulimwengu huu?

Huoni kama utakuwa wrong kuamini Mungu mmoja tu?

By the way najua huwezi thibitisha kuwa Mungu wako huyo yupo,
Kwasababu hayupo.

Kama unabisha sema.

Imani haina kanuni, unaweza kuamini chochote tu, hata ndoo ukiamua.


Lengo langu kukuhoji maswali yale, ilikuwa ni kujaribu kukuonesha kuwa hata mawazo yako bado yamekamatwa na mazoea/ maisha uliyowahi kuyaishi katika dini yako uliyokuwepo.
Imani yako ya Mungu mmoja tyari imekuwa imeshikwa na Dini hizi hizi unazozikataa leo!!
 
Kwahyi wewe unatazama jicho lako mbinguni?

Mbinguni ni wapi na sisi tupatizame tuangalie kama kuna mpasuko ama ufa?
Aisee! Kwani ukitoka njee kwako ukatizama juu angani si ndo mbingu huko kwenye nyota.
 
Higher intelligence ndio nini? kuna ulazima gani wa kutumia maneno ya kizungu
Kizungu si lugha, na hakuna ulazima wa kusoma ninachoandika kama hupendi ninavyoandika.

Unaweza kuniweka katika ignore list usione kabisa ninachoandika ili siku nyingine usikutane na maandiko yangu ambayo nakuhakikishia yataendelea kuchanganya Kiingereza na Kiswahili hapa JF.

Hapo vipi?
 
Duniani kuna watu wa lugha mbalimbali kuna waswahili, wafaransa, wafilipino, wahindi, wajerumani, waingereza, Wareno, wanyarwanda, warundi, wasudani,wakenya, waganda n.k

Kama Allah huyo aliumba watu wa lugha mbalimbali, Kwa nini huyo Allah ashushe Quran kwa lugha moja tu ya kiarabu?

Kwani huyo Allah alikuwa hajui kwamba aliumba watu wa lugha mbalimbali?

Au huyo Allah ana ongea kiarabu tu? Ilhali anajua kuna watu wa lugha mbalimbali.

Hivi huyo Allah ana jielewa kweli?
Wewe ndo hujielewi unauliza vitu vya kijinga
Mfano mdogo Tanzania kuna makabila mangapi kwanini kila jamii isiongee lugha yake site twazungumza kiswahili litafakari hilo kwanza utapata jibu
Halafu mungu hapangiwi binaadam ni سمعنا وأعطعنا "Tumesikia na Tunatii"
 
Back
Top Bottom