Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Dunia imekuwa kama kijiji kutokana na uwezo mkubwa aliounyesha mwanadamu wa kugundua hata ambavyo vilifikirika kwamba haviwezekani
Elimu na ufahamu kuhusu mwili wa mwanadamu kuanzia kuumbwa tumboni kuzaliwa hadi kufa umetafitiwa na kunyumbulishwa kwa mapana yake na wengi wamepata elimu ya juu kabisa PhD kwenye hili eneo, lakini wakashishindwa kitu kimoja tuu!!! Uwezo wa kumuita marehemu na kuongea naye
Zamani kabla ya dini za kigeni hazijaja Africa tulikuwa kwa kiasi fulani tuna uwezo wa kuwaita marehemu kwa njia ya matambiko na kuwaomba hili au lile, lakini ikumbukwe kwamba hawakuja live bali dalili na ishara kadha zilionyesha uwepo wao na kukubali au kukataa ombi husika
Tumekuwa tunaondokewa na wapendwa wetu na watu tunaowahitaji mno katika maisha yetu, tumekuwa na vipindi vigumu kabisa ambapo tunawahamu na kuwahitaji japo wajitokeze kwa dakika chache tu lakini haikuwezekana kabisa
Mfu ni mfu na hatuna uwezo wowote iwe wa kimwili au wa kiroho kuweza kumuita na kuongea naye lolote, hii ni kwakuwa roho inapotengana na mwili hakuna tena huyo MTU bali kunatokea vitu vitatu visivyoweza kuungana tena na kutengeneza kitu kimoja. vitu hivyo ni roho mwili na nafsi, vitatu hivi ndio vinatengeneza MTU nje ya hapo kuna 'mwili wake', 'roho yake' au 'nafsi yake'
Watu wamejaribu kutoa shuhuda nyingi za kutokewa na marehemu, hili linawezekana kwasababu baada ya kifo kuna roho huwa zinawayawaya duniani, zipo tu na hizi ndizo ambazo hugeuka mizimu mizuri au mibaya
Wakati mmoja tu marehemu anaweza kusikia sauti ya mwanadamu na kuitii ni pale tu anapoandaliwa kwa safari yake ya mwisho kaburini, hasa kwenye ishu ya kumsafirisha au kumvalisha nguo
Nikiwa mtu ambaye nilidili na miili ya marehemu kwa miaka mitatu mfululizo nilikutana mara nyingi tu na hizi hali, marehemu hataki dharau ubishi au kufokewa nguo hata iwe inamtosha Siku hiyo itakataa mpaka mumbembeleza
Tuna wajuaji wengi Siku hizi wanaojifanya wametokewa na marehemu fulani na kumpa maagizo Fulani hizi kwa asilimia 90 ni story tu kwakuwa hatujakuwa na uwezo wa kuwaita au wao kututokea tu na uchafu wote huu tulionao
YalishindikanaSikia [HASHTAG]#Mshana[/HASHTAG] jr kuna technology wafanyakazi wa space x waliitafiti kuwa roho inavyotoka inawaje walifanya utafiti wa kufunga software fulan ambayo mtu akitoa roho inatoka na ile app so iyo app itakuwa inarudisha feedback nn kinaendelea huko roho ilipo sijuu matokeo yake yaliishia wapi
Hakuna ufundi mkubwa zaidi ya kumsogelea na kumwambia taratibu kile unachotaka kumwambia
Kumbuka hatakujibu wala kugeuka au kushtuka lakini akikubaliana na ombi lako utagundua tu tofauti
Kwa mfano kama mikono ilikuwa inakakamaa kwenye kumvalisha mikono hiyo hiyo hulainika
inakuwaje hiy mkuuKatika seance huongei na mtu aliyekufa. Unaingia katika trance,na mtu aliyekufa anaongea through you.
zaburi 146:4 Roho yake hutoka, naye hurudi ardhini; Siku hiyohiyo mawazo yake hupotea.
Muhubiri 9:5 Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa, lakini waliokufa hawajui jambo lolote kamwe, wala hawana thawabu tena, kwa sababu kumbukumbu lote kuwahusu limesahauliwa
huo ndio ukuweli wafu hawajui lolote na hawezi kuongea nasi... Wanaongea na wafu huwa wanadanganywa na roho waovu ambao huugiza sauti zao ndio maana pia tunapewa shauri hii
Kumbukumbu 18:10 Asipatikane miongoni mwenu mtu yeyote anayemteketeza motoni mwanawe au binti yake, mtu yeyote anayefanya uaguzi, mtu yeyote anayefanya uchawi, mtu yeyote anayetafuta ishara za ubashiri, mlozi, 11 mtu yeyote anayewafunga wenzake kwa uchawi, mtu yeyote anayetafuta ushauri kutoka kwa watu wanaowasiliana na roho, mpiga ramli, au mtu yeyote anayetafuta habari kuhusu wafu
Unajua kuna vitabu vimeandikwa wakati wa Giza kabla Yesu Kristo hajaleta tumaini kimoja wapo ni Muhubiri .zaburi 146:4 Roho yake hutoka, naye hurudi ardhini; Siku hiyohiyo mawazo yake hupotea.
Muhubiri 9:5 Kwa maana walio hai wanajua kwamba watakufa, lakini waliokufa hawajui jambo lolote kamwe, wala hawana thawabu tena, kwa sababu kumbukumbu lote kuwahusu limesahauliwa
huo ndio ukuweli wafu hawajui lolote na hawezi kuongea nasi... Wanaongea na wafu huwa wanadanganywa na roho waovu ambao huugiza sauti zao ndio maana pia tunapewa shauri hii
Kumbukumbu 18:10 Asipatikane miongoni mwenu mtu yeyote anayemteketeza motoni mwanawe au binti yake, mtu yeyote anayefanya uaguzi, mtu yeyote anayefanya uchawi, mtu yeyote anayetafuta ishara za ubashiri, mlozi, 11 mtu yeyote anayewafunga wenzake kwa uchawi, mtu yeyote anayetafuta ushauri kutoka kwa watu wanaowasiliana na roho, mpiga ramli, au mtu yeyote anayetafuta habari kuhusu wafu
Unajua kuna vitabu vimeandikwa wakati wa Giza kabla Yesu Kristo hajaleta tumaini kimoja wapo ni Muhubiri .
Kimeandikwa kwa hekima sana ila na watu ambao hawakujua maisha baada ya kifo nini kinatokea
Iko hivi sikuwa anakataa live bali wakati wa kumvisha kama ni koti shati au hata suruali kuna kiungo kimoja hukakamaa kwa mfano kama ni mkono haunyanyuki au haukunjiki, kama ni mguu unajipinda au unakuwa mzito kunyanyua
Hivi vitu vinafanyika kwa namna ya ajabu na ya kipekee kabisa
Vilevile kuna kukosea vifungo au zipu kujichanganya! Yani mnaanza kufunga kifungo cha kwanza vizuri kabisa mkifika mwisho aidha vimepishana au mmeruka matundu, tulishawahi kukosea vifungo Mara SABA
Ni mpaka nilipotumia elimu niliyojifunza kuongea na marehemu kwa upole na kwa kumbembeleza ndio mambo yakawa sawa, na pia ndani ya chumba husika kama yupo mtu alikuwa na ugomvi na marehemu hakuna kitakachokwenda sawa hapo mpaka yule mtu atoke
KWA WANAOTAKA KUMUITA MAREHEMU NA KUZUNGUMZANAE WATUMIE NJIA HII HAPA MASHARTI MUWE WATU 3 NA MUWASHE UDI WA KIJITI NA TAA MUTUMIE MISHUMAA MEUPE 3 TA YA KAWAIDA MUIZIME NA KUMUITA MAREHEMU KWA NJIA HIZI HAPA CHINI ANGALIA VIDEO HAPA CHINI.Dunia imekuwa kama kijiji kutokana na uwezo mkubwa aliounyesha mwanadamu wa kugundua hata ambavyo vilifikirika kwamba haviwezekani
Elimu na ufahamu kuhusu mwili wa mwanadamu kuanzia kuumbwa tumboni kuzaliwa hadi kufa umetafitiwa na kunyumbulishwa kwa mapana yake na wengi wamepata elimu ya juu kabisa PhD kwenye hili eneo, lakini wakashishindwa kitu kimoja tuu!!! Uwezo wa kumuita marehemu na kuongea naye
Zamani kabla ya dini za kigeni hazijaja Africa tulikuwa kwa kiasi fulani tuna uwezo wa kuwaita marehemu kwa njia ya matambiko na kuwaomba hili au lile, lakini ikumbukwe kwamba hawakuja live bali dalili na ishara kadha zilionyesha uwepo wao na kukubali au kukataa ombi husika
Tumekuwa tunaondokewa na wapendwa wetu na watu tunaowahitaji mno katika maisha yetu, tumekuwa na vipindi vigumu kabisa ambapo tunawahamu na kuwahitaji japo wajitokeze kwa dakika chache tu lakini haikuwezekana kabisa
Mfu ni mfu na hatuna uwezo wowote iwe wa kimwili au wa kiroho kuweza kumuita na kuongea naye lolote, hii ni kwakuwa roho inapotengana na mwili hakuna tena huyo MTU bali kunatokea vitu vitatu visivyoweza kuungana tena na kutengeneza kitu kimoja. vitu hivyo ni roho mwili na nafsi, vitatu hivi ndio vinatengeneza MTU nje ya hapo kuna 'mwili wake', 'roho yake' au 'nafsi yake'
Watu wamejaribu kutoa shuhuda nyingi za kutokewa na marehemu, hili linawezekana kwasababu baada ya kifo kuna roho huwa zinawayawaya duniani, zipo tu na hizi ndizo ambazo hugeuka mizimu mizuri au mibaya
Wakati mmoja tu marehemu anaweza kusikia sauti ya mwanadamu na kuitii ni pale tu anapoandaliwa kwa safari yake ya mwisho kaburini, hasa kwenye ishu ya kumsafirisha au kumvalisha nguo
Nikiwa mtu ambaye nilidili na miili ya marehemu kwa miaka mitatu mfululizo nilikutana mara nyingi tu na hizi hali, marehemu hataki dharau ubishi au kufokewa nguo hata iwe inamtosha Siku hiyo itakataa mpaka mumbembeleza
Tuna wajuaji wengi Siku hizi wanaojifanya wametokewa na marehemu fulani na kumpa maagizo Fulani hizi kwa asilimia 90 ni story tu kwakuwa hatujakuwa na uwezo wa kuwaita au wao kututokea tu na uchafu wote huu tulionao
Jamaa muongo sana wewe, Mimi najua maiti zinavyovalishwa wala hakuna kibembelezana wala kugomeanaIko hivi sikuwa anakataa live bali wakati wa kumvisha kama ni koti shati au hata suruali kuna kiungo kimoja hukakamaa kwa mfano kama ni mkono haunyanyuki au haukunjiki, kama ni mguu unajipinda au unakuwa mzito kunyanyua
Hivi vitu vinafanyika kwa namna ya ajabu na ya kipekee kabisa
Vilevile kuna kukosea vifungo au zipu kujichanganya! Yani mnaanza kufunga kifungo cha kwanza vizuri kabisa mkifika mwisho aidha vimepishana au mmeruka matundu, tulishawahi kukosea vifungo Mara SABA
Ni mpaka nilipotumia elimu niliyojifunza kuongea na marehemu kwa upole na kwa kumbembeleza ndio mambo yakawa sawa, na pia ndani ya chumba husika kama yupo mtu alikuwa na ugomvi na marehemu hakuna kitakachokwenda sawa hapo mpaka yule mtu atoke
Jamaa muongo sana wewe, Mimi najua maiti zinavyovalishwa wala hakuna kibembelezana wala kugomeana
Kiungo kikikakamaa kinalazimishwa na kinakubali
Sent using Jamii Forums mobile app