Uwezo wa kuongea na wafu: Elimu Iliyoshindikana duniani

Uwezo wa kuongea na wafu: Elimu Iliyoshindikana duniani

Mkuu Mshana.

Tanga twaamini sana matambiko na hiyo ndiyo jadi yetu si wabondei, wazigua wasambaa na hata wasegeju.

Hata baadhi ya makabila mengine wana taratibu zao za kutambika.

Wakati naishi Ireland niliwahi kuona wenzetu wazungu wa kabila la Irish wale wanaoitwa Gipsy wao wanakwenda kwenye makaburi ya waliotangulia na kutumia siku nzima kushehereka kwa kunywa pombe pamoja na kucheza muziki kwenye eneo hilo.

Haya matukio ya jadi hizi yapo sehemu nyingi duniani na watu hupita wakifanya mambo haya waziwazi.

Lakini je, ni vizuri kila siku kusafisha kaburi kwa mazungumzo na roho ya marehemu au inahitajika kipindi maalum kila mwaka?

Ikiwa ni roho tu basi twaweza kuzungumza nayo mahali popote tulipo bila kwenda kaburini.

Je, jadi yaweza kuachwa bila madhara?

Au wewe waonaje kwenye hili?

Maana mimi nimekuwa mzito sana kwenda Potwe miaka hii.
Roho unaweza kuongea nayo popote lakini ni vema kwenda pale jumba lake ambako ni makaburini ni ishara ya heshima upendo na kujali
Si vizuri kwenda kufanya usafi kila mara ni Kama usumbufu kwao
Mengine hayana shida
 
Mimi nakubaliana na wewe katika hili.Ni kweli kabisa unayosema maana nimewahi kusikia hivi kutoka kwa bibi yangu akinihadithia mikasa aliyoiona kwa macho yake.
Pia marehemu babu yangu amewahi kufanya hivi pale alipoingia adui yake katika chumba alichokua anaoshewa.
Kwahili ni dhahiri marehemu hua wanasikia.
Hata shetani hugeuka na kuwa malaika wa nuru.
 
Ha ha ha haaaaa....wakuu lakini chini si wapo waheshimiwa wamepumzika kwa amani?
Huko Kinondoni na Msata ambapo ukikuta mtu tu kasimama nywele na mwili vinasisimka nani aende!!
Kile kituo cha kinondoni makaburini ikifika muda fulani abiria wenyewe hawaaminiani.
Hahahaaaaaa!
 
Wewe unaamini biblia wengine hatuamini,unaongea as if kila Mtu humu ni muumini wa biblia .Sio lazima kila usichokubaliana nacho kwa muktadha wa imani yako ukiite ushetani.biblia ni kitabu cha juzi,kulikua na maisha pia kabda ya biblia after all hii mada sio ya kidini bali ni nyie ndio mnataka kuharibu somo,biblia this biblia that.Akili zinazunguka kwenye vitabu vya dini tu ndiyo maana wengi mnashindwa kujifunza.Be open minded ,jifunze jinsi ya kujifunza na kuheshimu kile ambacho unahisi kinaenda tafauti na imani yako.
Sio ugonvi
Misozwe ni wapi
 
Hakuna Kazi yoyote huko kuzimu, na lolote mkono wako ulipendalo ulitende ukiwa Hai maana huko kuzimu hakuna shauri lolote
 
Dunia imekuwa kama kijiji kutokana na uwezo mkubwa aliounyesha mwanadamu wa kugundua hata ambavyo vilifikirika kwamba haviwezekani

Elimu na ufahamu kuhusu mwili wa mwanadamu kuanzia kuumbwa tumboni kuzaliwa hadi kufa umetafitiwa na kunyumbulishwa kwa mapana yake na wengi wamepata elimu ya juu kabisa PhD kwenye hili eneo, lakini wakashishindwa kitu kimoja tuu!!! Uwezo wa kumuita marehemu na kuongea naye

Zamani kabla ya dini za kigeni hazijaja Africa tulikuwa kwa kiasi fulani tuna uwezo wa kuwaita marehemu kwa njia ya matambiko na kuwaomba hili au lile, lakini ikumbukwe kwamba hawakuja live bali dalili na ishara kadha zilionyesha uwepo wao na kukubali au kukataa ombi husika

Tumekuwa tunaondokewa na wapendwa wetu na watu tunaowahitaji mno katika maisha yetu, tumekuwa na vipindi vigumu kabisa ambapo tunawahamu na kuwahitaji japo wajitokeze kwa dakika chache tu lakini haikuwezekana kabisa

Mfu ni mfu na hatuna uwezo wowote iwe wa kimwili au wa kiroho kuweza kumuita na kuongea naye lolote, hii ni kwakuwa roho inapotengana na mwili hakuna tena huyo MTU bali kunatokea vitu vitatu visivyoweza kuungana tena na kutengeneza kitu kimoja. vitu hivyo ni roho mwili na nafsi, vitatu hivi ndio vinatengeneza MTU nje ya hapo kuna 'mwili wake', 'roho yake' au 'nafsi yake'

Watu wamejaribu kutoa shuhuda nyingi za kutokewa na marehemu, hili linawezekana kwasababu baada ya kifo kuna roho huwa zinawayawaya duniani, zipo tu na hizi ndizo ambazo hugeuka mizimu mizuri au mibaya

Wakati mmoja tu marehemu anaweza kusikia sauti ya mwanadamu na kuitii ni pale tu anapoandaliwa kwa safari yake ya mwisho kaburini, hasa kwenye ishu ya kumsafirisha au kumvalisha nguo

Nikiwa mtu ambaye nilidili na miili ya marehemu kwa miaka mitatu mfululizo nilikutana mara nyingi tu na hizi hali, marehemu hataki dharau ubishi au kufokewa nguo hata iwe inamtosha Siku hiyo itakataa mpaka mumbembeleza

Tuna wajuaji wengi Siku hizi wanaojifanya wametokewa na marehemu fulani na kumpa maagizo Fulani hizi kwa asilimia 90 ni story tu kwakuwa hatujakuwa na uwezo wa kuwaita au wao kututokea tu na uchafu wote huu tulionao
Ngoja niongee na Mzee nyerere
 
Dunia imekuwa kama kijiji kutokana na uwezo mkubwa aliounyesha mwanadamu wa kugundua hata ambavyo vilifikirika kwamba haviwezekani

Elimu na ufahamu kuhusu mwili wa mwanadamu kuanzia kuumbwa tumboni kuzaliwa hadi kufa umetafitiwa na kunyumbulishwa kwa mapana yake na wengi wamepata elimu ya juu kabisa PhD kwenye hili eneo, lakini wakashishindwa kitu kimoja tuu!!! Uwezo wa kumuita marehemu na kuongea naye

Zamani kabla ya dini za kigeni hazijaja Africa tulikuwa kwa kiasi fulani tuna uwezo wa kuwaita marehemu kwa njia ya matambiko na kuwaomba hili au lile, lakini ikumbukwe kwamba hawakuja live bali dalili na ishara kadha zilionyesha uwepo wao na kukubali au kukataa ombi husika

Tumekuwa tunaondokewa na wapendwa wetu na watu tunaowahitaji mno katika maisha yetu, tumekuwa na vipindi vigumu kabisa ambapo tunawahamu na kuwahitaji japo wajitokeze kwa dakika chache tu lakini haikuwezekana kabisa

Mfu ni mfu na hatuna uwezo wowote iwe wa kimwili au wa kiroho kuweza kumuita na kuongea naye lolote, hii ni kwakuwa roho inapotengana na mwili hakuna tena huyo MTU bali kunatokea vitu vitatu visivyoweza kuungana tena na kutengeneza kitu kimoja. vitu hivyo ni roho mwili na nafsi, vitatu hivi ndio vinatengeneza MTU nje ya hapo kuna 'mwili wake', 'roho yake' au 'nafsi yake'

Watu wamejaribu kutoa shuhuda nyingi za kutokewa na marehemu, hili linawezekana kwasababu baada ya kifo kuna roho huwa zinawayawaya duniani, zipo tu na hizi ndizo ambazo hugeuka mizimu mizuri au mibaya

Wakati mmoja tu marehemu anaweza kusikia sauti ya mwanadamu na kuitii ni pale tu anapoandaliwa kwa safari yake ya mwisho kaburini, hasa kwenye ishu ya kumsafirisha au kumvalisha nguo

Nikiwa mtu ambaye nilidili na miili ya marehemu kwa miaka mitatu mfululizo nilikutana mara nyingi tu na hizi hali, marehemu hataki dharau ubishi au kufokewa nguo hata iwe inamtosha Siku hiyo itakataa mpaka mumbembeleza

Tuna wajuaji wengi Siku hizi wanaojifanya wametokewa na marehemu fulani na kumpa maagizo Fulani hizi kwa asilimia 90 ni story tu kwakuwa hatujakuwa na uwezo wa kuwaita au wao kututokea tu na uchafu wote huu tulionao
Uzi murua kabisa ndg mshana jr,hongera na ninashukuru sana kupitia eneo hili.
NISHAKUTANA NA VINGI ILA HIKI NI CHA KARIBUNI TU.
Hapa nyumbani kwetu tulikuwa na mpangaji(mwanamke) ambaye alipanga kwa kitambo kidogo.Alikuwa akiishi na mtoto(umri kati ya miaka 13) wa ndg yake lakin baadae wakahamia kwny nyumba yao mpya.
Walipohama niliweza kukutana mara kadhaa na mama huyo na kumsalimiana nae na mara moja moja sana nilikutana na yule mtoto.
.......HISIA MBAYA.....
Siku moja asubuh kama saa tatu asubuh nilitoka nyumban kuelekea mjini nikiwaza pia nipitie nmsalim yule mama pia nkakumbuka kuwa yule mtoto sjamuona muda kidogo...hivyo nikawa na shauku ya kutaka kumwona yule mtoto,nikiwa njian hali ya ajabu ikaanza kunijia. nkaanza kutojisikia amani,kuhisi roho kama inanichomoka,mara kama kuna mtu ananifata na upepo kunizongazonga hivi(eneo hilo pia kuna majeneza yalikuwa yaktengezwa na kuuzwa)....nliendelea na safar nkafika kwa yule mama kwel nkamsalm nkapiga soga kidogo afu nkaondoka...umbali wa dakika tatu tu toka ofisini kwa yule mama nkakutana na yule mtoto moyo ulishtuka kiasi(sikujua kwa nn),nkasalim,nakumsihi ajitahid na masomo....tukaachana yy akielekea ofisini kwa yule mama....
.......MSIBA SIKU YA PILI YAKE....
Asubuhi saa 2 tulipokea habar za msiba za mtoto yule maana tairi la semitrela lilichomoka na kumkuta yy wakati akivuka barabara anavoenda shule...ni yy tu ndo lilimkuta tairi lile...
......SIKU TATU BAADAE...
Siku hiyo niliota ndoto nko nyumbani pale ndani ya banda la kuku.Nilitazama nje ya banda hilo nkamwona mtoto yule,nakumbuka sikuwa nasikia sauti ya kitu chochote...ulikuwa ni utulivu mwanana sana...mtoto yule alikuwa akitabasam.(moyoni mwangu nkakumbuka kuwa yule ni alishafariki).Sjui nilijuaje ila tu nakumbuka nilimwambia kimoyonimoyoni UPUMZIKE KWA AMANI,naye alitikisa kichwa kwa ishara ya kukubali..akapotea...
SIJAMUOTA TENA MPAKA LEO.
Mungu ampumzishe kwa amani.Amen
 
Uzi murua kabisa ndg mshana jr,hongera na ninashukuru sana kupitia eneo hili.
NISHAKUTANA NA VINGI ILA HIKI NI CHA KARIBUNI TU.
Hapa nyumbani kwetu tulikuwa na mpangaji(mwanamke) ambaye alipanga kwa kitambo kidogo.Alikuwa akiishi na mtoto(umri kati ya miaka 13) wa ndg yake lakin baadae wakahamia kwny nyumba yao mpya.
Walipohama niliweza kukutana mara kadhaa na mama huyo na kumsalimiana nae na mara moja moja sana nilikutana na yule mtoto.
.......HISIA MBAYA.....
Siku moja asubuh kama saa tatu asubuh nilitoka nyumban kuelekea mjini nikiwaza pia nipitie nmsalim yule mama pia nkakumbuka kuwa yule mtoto sjamuona muda kidogo...hivyo nikawa na shauku ya kutaka kumwona yule mtoto,nikiwa njian hali ya ajabu ikaanza kunijia. nkaanza kutojisikia amani,kuhisi roho kama inanichomoka,mara kama kuna mtu ananifata na upepo kunizongazonga hivi(eneo hilo pia kuna majeneza yalikuwa yaktengezwa na kuuzwa)....nliendelea na safar nkafika kwa yule mama kwel nkamsalm nkapiga soga kidogo afu nkaondoka...umbali wa dakika tatu tu toka ofisini kwa yule mama nkakutana na yule mtoto moyo ulishtuka kiasi(sikujua kwa nn),nkasalim,nakumsihi ajitahid na masomo....tukaachana yy akielekea ofisini kwa yule mama....
.......MSIBA SIKU YA PILI YAKE....
Asubuhi saa 2 tulipokea habar za msiba za mtoto yule maana tairi la semitrela lilichomoka na kumkuta yy wakati akivuka barabara anavoenda shule...ni yy tu ndo lilimkuta tairi lile...
......SIKU TATU BAADAE...
Siku hiyo niliota ndoto nko nyumbani pale ndani ya banda la kuku.Nilitazama nje ya banda hilo nkamwona mtoto yule,nakumbuka sikuwa nasikia sauti ya kitu chochote...ulikuwa ni utulivu mwanana sana...mtoto yule alikuwa akitabasam.(moyoni mwangu nkakumbuka kuwa yule ni alishafariki).Sjui nilijuaje ila tu nakumbuka nilimwambia kimoyonimoyoni UPUMZIKE KWA AMANI,naye alitikisa kichwa kwa ishara ya kukubali..akapotea...
SIJAMUOTA TENA MPAKA LEO.
Mungu ampumzishe kwa amani.Amen
Duu nimeisoma gizani nikapata hali fulani ya kusisimka, ile amani uliyokosa ina ishara fulani kiroho na baada kufa alirudi ili muagane nawe ukafanya hivyo
Mawasiliano ya kiroho huja kwa namna ya kipekee kabisa na yasiyoweza kuidhibiti hata kidogo
 
Duu nimeisoma gizani nikapata hali fulani ya kusisimka, ile amani uliyokosa ina ishara fulani kiroho na baada kufa alirudi ili muagane nawe ukafanya hivyo
Mawasiliano ya kiroho huja kwa namna ya kipekee kabisa na yasiyoweza kuidhibiti hata kidogo
Mungu yupo ndg..kumtafuta tu ndo gharama ambayo binadam anahis hawez kughalimia.
 
Iko hivi sikuwa anakataa live bali wakati wa kumvisha kama ni koti shati au hata suruali kuna kiungo kimoja hukakamaa kwa mfano kama ni mkono haunyanyuki au haukunjiki, kama ni mguu unajipinda au unakuwa mzito kunyanyua
Hivi vitu vinafanyika kwa namna ya ajabu na ya kipekee kabisa

Vilevile kuna kukosea vifungo au zipu kujichanganya! Yani mnaanza kufunga kifungo cha kwanza vizuri kabisa mkifika mwisho aidha vimepishana au mmeruka matundu, tulishawahi kukosea vifungo Mara SABA
Ni mpaka nilipotumia elimu niliyojifunza kuongea na marehemu kwa upole na kwa kumbembeleza ndio mambo yakawa sawa, na pia ndani ya chumba husika kama yupo mtu alikuwa na ugomvi na marehemu hakuna kitakachokwenda sawa hapo mpaka yule mtu atoke[/QUOTE

Mshana jr huyu mlizika akiwa hai bs Kama anakunja mguu atakuwa alikuwa anwaelewa kabsa mlichokua mnafanya
 
Dunia imekuwa kama kijiji kutokana na uwezo mkubwa aliounyesha mwanadamu wa kugundua hata ambavyo vilifikirika kwamba haviwezekani

Elimu na ufahamu kuhusu mwili wa mwanadamu kuanzia kuumbwa tumboni kuzaliwa hadi kufa umetafitiwa na kunyumbulishwa kwa mapana yake na wengi wamepata elimu ya juu kabisa PhD kwenye hili eneo, lakini wakashishindwa kitu kimoja tuu!!! Uwezo wa kumuita marehemu na kuongea naye

Zamani kabla ya dini za kigeni hazijaja Africa tulikuwa kwa kiasi fulani tuna uwezo wa kuwaita marehemu kwa njia ya matambiko na kuwaomba hili au lile, lakini ikumbukwe kwamba hawakuja live bali dalili na ishara kadha zilionyesha uwepo wao na kukubali au kukataa ombi husika

Tumekuwa tunaondokewa na wapendwa wetu na watu tunaowahitaji mno katika maisha yetu, tumekuwa na vipindi vigumu kabisa ambapo tunawahamu na kuwahitaji japo wajitokeze kwa dakika chache tu lakini haikuwezekana kabisa

Mfu ni mfu na hatuna uwezo wowote iwe wa kimwili au wa kiroho kuweza kumuita na kuongea naye lolote, hii ni kwakuwa roho inapotengana na mwili hakuna tena huyo MTU bali kunatokea vitu vitatu visivyoweza kuungana tena na kutengeneza kitu kimoja. vitu hivyo ni roho mwili na nafsi, vitatu hivi ndio vinatengeneza MTU nje ya hapo kuna 'mwili wake', 'roho yake' au 'nafsi yake'

Watu wamejaribu kutoa shuhuda nyingi za kutokewa na marehemu, hili linawezekana kwasababu baada ya kifo kuna roho huwa zinawayawaya duniani, zipo tu na hizi ndizo ambazo hugeuka mizimu mizuri au mibaya

Wakati mmoja tu marehemu anaweza kusikia sauti ya mwanadamu na kuitii ni pale tu anapoandaliwa kwa safari yake ya mwisho kaburini, hasa kwenye ishu ya kumsafirisha au kumvalisha nguo

Nikiwa mtu ambaye nilidili na miili ya marehemu kwa miaka mitatu mfululizo nilikutana mara nyingi tu na hizi hali, marehemu hataki dharau ubishi au kufokewa nguo hata iwe inamtosha Siku hiyo itakataa mpaka mumbembeleza

Tuna wajuaji wengi Siku hizi wanaojifanya wametokewa na marehemu fulani na kumpa maagizo Fulani hizi kwa asilimia 90 ni story tu kwakuwa hatujakuwa na uwezo wa kuwaita au wao kututokea tu na uchafu wote huu tulionao
Mkuu kuna tukio nimelishuhudia mwenyewe la MAREHEMU kuitwa akajitokeza kwenye kioo na kuanza kuulizwa maswali huku anajibu, Hiko hivi pale mwanza maeneo ya Kisesa kwenye rada ya Jeshi kuna mganga mmoja aliishi akijulikana kama Fikili, alikuwa mzaliwa wa Sumbawanga kwa histolia wanadai alikuwa moto mkali sana ila mi sikumwona, alikuwa anatoa mali za kijerumani( maficho kwa wanaojua). Huyu bwana wazazi wake wapo na aliyekuwa msaidizi wake yupo anaitwa Mangi wanadai kwenye kutoa mali hizi za mjerumani hakuwahi kuuza hata kidogo alikuwa ameyaifadhi ndani mpaka alipoanza kuumwa akamwambia nzee wake kuwa hizi mali atazificha hapohapo nyumbani ila hakuna mtu wakuziona labda mungu ashuke. Ila akampatia chupa tatu za dawa baba yake akidai ni zakutolea mzigo huo na akamwachia CD yamaelekezo ila baada ya kifo chake kama miaka miwili hivi ile nyumba ya yule mzee alimokuwa ameifadhi zile dawa ilianguka kwa kimbunga bahati mbaya wakati wakuokoa watu zile dawa zikapotea ila CD na kidaftali vikabaki, baadaye yule mzee umaskini ulipompiga akakumbuka mali za mwanaye ila sasa hana dawa zakutolea mzigo ndo akaanza kuangaika kwa watu wengi waganga,mapadre hata watu wa madini bila mafanikio. Sasa siku moja nilienda kupima kiwanja kwa mtu kule Tarime nikiwa na machine moja inaitwa Rover Cii treasure hunting scanner yule boss akaniomba niende mwanza kupima eneo la huyo mzee. Baada ya kwenda nikascan eneo mashine ikaonesha kuna dhahabu ndani ya nyumba sebuleni kama 1.5m depth. Kwa kushilikiana na yule mzee na mjukuu wake tukabomoa sakafu na kufukua ile point cha ajabu nikakuta ka shimo chini hapohapo ka ulefu huohuo uliopimwa na machine, ila ndani kuna jiwe moja la mviringo kubwa tu kama ndoo ya lita ishirini ila si dhahabu bali jiwe aina ya basalt kwa wanaolewa, basi yule mzee akashauli nimsaidie kutafuta mtu mwenye dawa za Kijerumani ndo anaweza kuondoa giza ilo 'kwa maneno yake lakini' Nilipomtaalifu boss akadai kuna mkenya anaitwa Kaizer ana mafuta ya kaizali, basi akaenda Nairobi kumleta.Baada ya siku kadha alikuja na mbaba huyo mwenye dawa iyo ya kijerumani baada ya kumpatia maelezo akadai inabidi amwite MAREHEMU either aje kwa sauti au kupitia kioo hiki tu cha kujiangalia au apitie kichwa cha babaye au mamaye aongee na kutoa maelekezo. Baada ya kuojiana washilika wakadai kioo ili kila mtu amwone kama ni yeye au la! Basi akasema kazi itafanyika kati ya xaa 9 na 11 alfajili, akaagiza mzee wake aweke mawe natatu juu ya kabuli la mwanaye na akaomba mishumaa sita mweupe, yote yakafanyika mda ulipofika akawasha mishumaa akajipaka hayo mafuta akaweka hicho kioo kidogo mbele huku wote tukiangalia kile kioo. Basi akaanza kuamlisha MAREHEMU ajitokeze aongee na wazazi wake kwa kumtaja jina. Maajabu kama dakika 5 alianza kuonekana mtu kwenye kioo amevalishwa sanda mpaka mama yake akaanza kulia kwamba mwanangu karudi. MAREHEMU akauliza baba mbona hunanisumbua wakati nimepumzika? Mzee wake akaanza kumwongelesha kifipa nakumbuka neno moja TULEBE wakajibishana kwa muda huku sauti ikitoka kwenye kile kioo ambacho hakina spika maana nilikinunua mimi dukan! Baada ya muda MAREHEMU akadai babayake afanye tambiko la ukoo wao ataoneshwa mali ilipo ila kuitoa mpaka apate mafuta ya" KAMPUMA" kwa wanaojua maan mimi sijui ni nini.Baadaye akaomba amechoka wamwache apumzike, mpaka leo shida imekuwa kupata iyo KAMPUMA maana nayo ni jambo gumu sana.
 
[emoji15] [emoji15] [emoji15]
223501_10151503712304796_1939411903_n.jpg
 
Back
Top Bottom